Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ya Mwaka 2023
Sheria inaanza kutumika tarehe itakayoteuliwa na Waziri kupitia tangazo katika Gazeti la Serikali, na Waziri anaweza pia kuteua tarehe tofauti kwa Sehemu au vifungu vyake.
AI-assisted research synopsis — verify against the official legal text below.
- Jurisdiction
- Tanzania
- Instrument
- Act or statute
- Citation
- Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ya Mwaka 2023
- Version
- Undated source snapshot
- Language
- sw
- Official source
- View official record ↗
Statute overview
About this statute
Sheria inaanza kutumika tarehe itakayoteuliwa na Waziri kupitia tangazo katika Gazeti la Serikali, na Waziri anaweza pia kuteua tarehe tofauti kwa Sehemu au vifungu vyake. This provision says the Act applies in Tanzania Bara. This section defines many terms used in the Act. The provision states the law’s objectives for health insurance for all. Health insurance is mandatory, everyone must join a health insurance scheme, employers must contribute for their employees, and certain foreign visitors must also join.
Search within this statute
Search all stored provisions in this version.
Legal text
Provisions of Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ya Mwaka 2023
Showing 71 of 71
- 1
AI-assisted research summary: Sheria inaanza kutumika tarehe itakayoteuliwa na Waziri kupitia tangazo katika Gazeti la Serikali, na Waziri anaweza pia kuteua tarehe tofauti kwa Sehemu au vifungu vyake.
1.-(1) Sheria hii itajulikana kama Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ya Mwaka 2023 na itaanza kutumika kwa tarehe ambayo Waziri, kwa tangazo litakalochapishwa kwenye Gazeti la Serikali, atateua. (2) Wakati wa utekelezaji wa masharti ya kifungu kidogo cha (1), Waziri anaweza kuteua tarehe tofauti ya kuanza kutumika kwa masharti ya Sehemu au vifungu vya Sheria hii kwa kadiri atakavyoona inafaa. Matumizi - 2
AI-assisted research summary: This provision says the Act applies in Tanzania Bara.
2. Sheria hii itatumika Tanzania Bara. 5 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 Tafsiri Sura ya 197 Sura ya 135 - 3
AI-assisted research summary: This section defines many terms used in the Act.
3. Katika Sheria hii, isipokuwa kama muktadha utahitaji vinginevyo- “Benki” maana yake ni Benki Kuu ya Tanzania iliyoanzishwa kwa Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania; “bima ya afya kwa wote” maana yake ni utaratibu ulioidhinishwa kwa mujibu wa Sheria hii unaowezesha kila mwananchi kupata huduma za afya kupitia bima ya afya bila kikwazo cha fedha pindi anapozihitaji huduma hizo; “Divisheni” ina maana kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Hifadhi ya Jamii; “kitita cha bima ya afya cha jamii” maana yake ni kitita cha mafao kilichoanzishwa kwa mujibu wa kifungu cha 15; “kitita cha huduma za ziada” maana yake ni kitita cha huduma za afya zaidi ya kitita cha mafao ya huduma muhimu kinachotolewa na skimu ya bima ya afya; “kitita cha mafao” maana yake ni huduma za afya zinazotolewa kwa mnufaika wa skimu ya bima ya afya; “kitita cha mafao ya huduma muhimu” maana yake ni kitita cha mafao kilicho anzishwa kwa mujibu wa kifungu cha 14; “kitita maalum cha mafao” maana yake ni kitita cha mafao kitakachoanzishwa chini ya kifungu cha 8(2); “kituo cha huduma za afya” inajumuisha kliniki, zahanati, kituo cha afya, hospitali, maabara, duka la dawa au kituo kingine chochote kinachotoa huduma za afya; “kituo cha huduma za afya kilichoingia mkataba” maana yake kituo cha kutolea huduma za afya kilichoingia makubaliano na skimu kuwahudumia wanufaika kwa mujibu wa Sheria hii; “kiwango cha mchango” maana yake ni kiwango kutoka katika mshahara au chanzo kingine chochote kitakacholipwa katika skimu ya bima ya afya na mwanachama au kwa niaba ya mwanachama; “kiwango cha uchangiaji” maana yake ni kiasi cha fedha kinacholipwa kwa lengo la kuwa mwanachama kwa mujibu wa Sheria hii; 6 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 Sura ya 394 Sura ya 54 “Mamlaka” maana yake ni Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania iliyoanzishwa kwa Sheria ya Bima; “mkazi” ina maana kama ilivyotafsiriwa katika Sheria ya Uhamiaji; “mnufaika” maana yake ni mtu anayestahili kupata mafao ya matibabu chini ya Sheria hii; “mshahara” kwa madhumuni ya: (a) mtumishi wa umma, maana yake ni mshahara usiojumuisha malipo ya ziada, stahiki, na posho; (b) mwajiriwa wa sekta binafsi, maana yake ni mshahara unaojumuisha stahiki zote za kisheria zinazolipwa kama sehemu ya mshahara wa mwajiriwa; “mtegemezi” maana yake ni- (a) mzazi wa mwanachama au mzazi wa mwenza wa mwanachama; (b) mtoto wa mwanachama wa kuzaa, kuasili au wa kambo aliye na umri chini ya miaka ishirini na moja; au (c) ndugu wa damu wa mwanachama aliye na umri wa chini ya miaka ishirini na moja; “mtoa huduma” inajumuisha kituo cha kutolea huduma za afya na skimu ya bima ya afya chini ya Sheria hii. “mtu aliyejiajiri” maana yake ni mtu anayefanya kazi asiye katika uhusiano wa mwajiri na mwajiriwa; “mtu asiye na uwezo” maana yake ni mtu anayeishi kwa kipato kilicho chini ya mstari unaopima kiwango cha umaskini kama inavyofafanuliwa na mamlaka husika; “mwajiri” ina maana kama ilivyotafsiriwa katika Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini; “mwajiriwa” ina maana kama ilivyotafsiriwa katika Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini; “mwanachama” maana yake ni mtu yeyote aliyesajiliwa katika skimu chini ya Sheria hii na anachangia ama yeye mwenyewe au kupitia kwa Serikali; “ndugu wa damu” maana yake ni kaka au dada wa kuzaliwa wa mwanachama na aliye chini ya umri wa miaka ishirini na moja; 7 Sura ya 366 Sura ya 366 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 Sura ya 357 “raia” ina maana kama ilivyotafsiriwa katika Sheria ya Uraia; “sekta isiyo rasmi” maana yake ni sekta inayojumuisha wafanyakazi wanaofanya kazi zisizo rasmi na ambao hawana mikataba ya ajira au mikataba mingine yoyote tafsiri ya neno “mwajiriwa” na inajumuisha mtu asiyejihusisha na aina yoyote ya uzalishaji; iliyoelezewa katika “sekta rasmi” maana yake ni sekta inayojumuisha kazi zilizorasimishwa na kufanywa kwa mikataba ambapo mikataba hiyo imeainisha mishahara au ujira na muda maalum wa kazi; “sekta rasmi binafsi” inajumuisha wafanyakazi katika mashirika au taasisi isipokuwa watumishi wa sekta ya umma; “sekta ya umma” maana yake ni sekta inayojumuisha watumishi wa umma pamoja na wafanyakazi katika mashirika au taasisi binafsi ambayo Serikali inamiliki angalau asilimia thelathini ya hisa; “skimu ya bima ya afya” maana yake ni bima ya afya ya umma au kampuni binafsi inayotoa huduma za bima ya afya chini ya Sheria hii; “skimu ya bima ya afya binafsi” maana yake ni bima ya afya iliyoanzishwa au kutambuliwa chini ya Sheria hii; “skimu ya bima ya afya ya umma” maana yake ni bima ya afya iliyoanzishwa au kutambuliwa chini ya Sheria hii; “Waziri” maana yake ni Waziri mwenye dhamana na masuala ya afya; na “Wizara” maana yake ni Wizara yenye dhamana ya masuala ya afya. - 4
AI-assisted research summary: The provision states the law’s objectives for health insurance for all.
4. Malengo ya Sheria hii yatakuwa- (a) kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wote kupitia mfumo wa bima ya afya; na (b) kuweka mfumo wa ushiriki katika skimu za bima ya afya kwa raia na wakazi wote. 8 Malengo Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 SEHEMU YA PILI MFUMO WA BIMA YA AFYA KWA WOTE Ulazima wa bima ya afya wote.
Part
SEHEMU YA PILI
- 5
AI-assisted research summary: Health insurance is mandatory, everyone must join a health insurance scheme, employers must contribute for their employees, and certain foreign visitors must also join.
5.-(1) Bima ya afya itakuwa ni ya lazima kwa watu (2) Kwa kuzingatia masharti ya Sheria hii, kila mtu anapaswa kujiunga na skimu ya bima ya afya ili kuhakikisha anapata huduma za afya. (3) Kila mwajiri atatakiwa kumchangia mwajiriwa wake katika skimu ya bima ya afya kiwango cha uchangiaji kwa kuzingatia masharti ya Sheria hii. (4) Wageni wote wenye umri wa miaka kumi na nane au zaidi wanaoingia nchini na kukaa zaidi ya siku thelathini ambao hawana bima ya afya inayotambulika nchini watapaswa kujiunga na bima ya afya kwa mujibu wa Sheria hii. Mfumo wa bima ya afya - 6
AI-assisted research summary: The universal health insurance system includes employers and employees in the public and formal private sectors, people in the informal sector, health insurance schemes, people without means, health service delivery facilities, and the Authority.
6. Mfumo wa bima ya afya kwa wote utajumuisha- (a) waajiri na waajiriwa katika sekta ya umma na sekta rasmi binafsi; (b) watu walioko katika sekta isiyo rasmi; (c) skimu za bima ya afya; (d) watu wasio na uwezo; (e) vituo vya kutolea huduma za afya; na (f) Mamlaka. Udhibiti wa mfumo wa bima ya afya - 7 Verify source ↗
Jina na kuanza kutumika
AI-assisted research summary: Mamlaka ya Udhibiti wa bima ndiyo mamlaka ya kusimamia huduma za bima ya afya, na ina majukumu kadhaa ya usajili, uangalizi, miongozo, ukaguzi, na utoaji wa taarifa.
7.-(1) Mamlaka ya Udhibiti wa bima iliyoanzishwa chini ya Sheria ya Bima itakuwa ndiyo mamlaka ya udhibiti wa huduma za bima ya afya. (2) Kwa madhumuni ya kuhakikisha ufanisi wa utekelezaji wa mfumo wa bima ya afya kwa wote, Mamlaka itakuwa na wajibu wa- (a) kusajili skimu za bima ya afya; (b) kuhakikisha bima za afya zinatoa kitita cha mafao ya huduma muhimu kwa mujibu wa Sheria hii; (c) kuhakikisha huduma za bima zinazotolewa zinaendana na viwango vya michango; (d) kutoa miongozo ya malipo kwa watoa huduma; 9 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 (e) kutoa miongozo ya uendeshaji wenye ufanisi na tija katika usimamizi wa skimu za bima ya afya; (f) kuhakikisha kuwa skimu ya bima ya afya ina ukwasi na akiba kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa; (g) kutunza kanzidata ya vituo vya kutolea huduma za afya vilivyoingia mikataba na skimu za bima ya afya; (h) kufanya ukaguzi wa skimu za bima ya afya; (i) kuweka miongozo kuhusu usajili wa wanachama katika skimu za bima ya afya; (j) kuomba au kuitisha taarifa yoyote itakayoihitaji; (k) kufanya la tafiti na uvumbuzi kwa kuendeleza ufanisi na uendelevu wa mfumo wa bima ya afya kwa wote”; na lengo (l) kutekeleza jukumu lingine lolote kwa madhumuni ya utekelezaji bora wa Sheria hii. (3) Kila mwaka wa fedha au kwa kadiri itakavyohitajika, Mamlaka itawasilisha kwa Divisheni na nakala kwa Wizara, taarifa kuhusu udhibiti wa huduma za bima ya afya. SEHEMU YA TATU SKIMU ZA BIMA YA AFYA Skimu ya bima ya afya ya umma Sura ya 395
Part
SEHEMU YA TATU
- 8
AI-assisted research summary: Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya unatambuliwa kama skimu ya bima ya afya ya umma kwa madhumuni ya Sheria hii.
8.-(1) Kwa madhumuni ya Sheria hii, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ulioanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya utatambulika kama skimu ya bima ya afya ya umma. (2) Waziri kwa kushauriana na Mamlaka na kwa kuzingatia utaratibu utakaoainishwa katika kanuni, anaweza kuboresha skimu ya bima ya afya ya umma ikiwemo kuanzisha kitita maalum cha mafao kulingana na uhitaji kwa lengo la kufikia bima ya afya kwa wote. Skimu ya bima ya afya binafsi - 9
AI-assisted research summary: A person may be eligible to register as a private health insurance scheme after meeting the conditions set by regulations under the Act.
9.-(1) Mtu atakuwa na sifa ya kusajiliwa kuwa skimu ya bima ya afya ya binafsi baada ya kutimiza masharti kama yatakavyoainishwa katika kanuni chini ya Sheria hii. 10 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 Sura ya 394 (2) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (1), kampuni au chombo kilichoidhinishwa chini ya Sheria ya Bima kutoa bima ya afya, kabla ya kuanza kutumika kwa Sheria hii, kitaendelea kutoa huduma kama skimu ya bima ya afya binafsi baada ya kutimiza masharti ya Sheria hii. Zuio la kuendesha skimu ya bima ya afya - 10
AI-assisted research summary: A person may not operate a health insurance scheme unless the Authority has issued a registration certificate, and health insurance schemes must carry out the duties set out in this Act.
10.-(1) Isipokuwa kama imeelezwa vinginevyo katika Sheria hii, mtu hataendesha skimu ya bima ya afya isipokuwa kama amepewa cheti cha usajili na Mamlaka kwa mujibu wa Sheria hii. (2) Kila skimu ya bima ya afya itatatekeleza kama kuzingatia masharti yake majukumu yalivyoainishwa katika Sheria hii. kwa Utunzaji wa rejesta Kufuta usajili wa skimu ya bima ya afya - 11
AI-assisted research summary: Mamlaka lazima itunze rejesta ya skimu za bima ya afya zilizosajiliwa na pia skimu nyingine za bima ya afya zilizokuwepo kabla ya sheria hii kuanza kutumika.
11. Mamlaka itatunza rejesta ya skimu za bima ya afya zilizosajiliwa kwa mujibu wa Sheria hii na skimu nyingine za bima ya afya zilizokuwepo kabla ya kuanza kutumika kwa Sheria hii. - 12 Verify source ↗
Skimu ya bima ya afya ya umma
AI-assisted research summary: Mamlaka inaweza kufuta usajili wa skimu ya bima ya afya kwa masharti fulani, lakini lazima itoe notisi ya angalau siku 90 kabla ya kufanya hivyo.
12.-(1) Mamlaka inaweza kufuta usajili wa skimu ya bima ya afya iwapo- (a) Sheria iliyoanzisha skimu ya bima ya afya ya umma imefutwa; (b) skimu ya bima ya afya imekiuka masharti ya Sheria hii, kanuni au miongozo chini ya Sheria hii; (c) skimu ya bima ya afya imesitisha kutoa huduma za bima au imefilisika; (d) skimu ya bima ya afya imeomba kufutiwa usajili na Mamlaka imeridhia maombi hayo; au (e) skimu ya bima ya afya imepoteza sifa za kusajiliwa kwa mujibu wa Sheria hii. (2) Mamlaka, kabla ya kufuta usajili wa skimu ya bima ya afya, itatoa notisi ya angalau siku tisini ya kusudio lake la kufanya hivyo ikiitaka skimu ya bima ya afya kutoa sababu kwanini Mamlaka isifute usajili wa skimu hiyo. (3) Skimu ya bima ya afya, baada ya kupokea notisi iliyotolewa chini ya kifungu kidogo cha (2)- 11 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 (a) itasitisha usajili wa wanachama wapya kuanzia tarehe ya kupokea notisi ya kufuta usajili hadi itakapoelekezwa vinginevyo na Mamlaka; na (b) itaendelea, chini ya uangalizi wa Mamlaka, kutoa huduma kwa wanachama na kulipa vituo vilivyoingia mikataba na skimu hiyo. (4) Mamlaka, kwa namna itakavyoainishwa katika kanuni, itaweka utaratibu utakaohakikisha kuwa wanachama hawaathiriki na kufutwa kwa skimu. SEHEMU YA NNE VITITA VYA MAFAO (a) Kitita cha Mafao ya Huduma Muhimu
Part
SEHEMU YA NNE
- 13
AI-assisted research summary: Health insurance scheme members and beneficiaries have a right to the essential benefits package, which generally applies for one year from registration; some contributors keep it until its expiry, and additional services may be available under the scheme plan.
13.-(1) Mwanachama au mnufaika wa skimu ya bima ya afya atakuwa na haki ya kupata kitita cha mafao ya huduma muhimu, kama hitaji la msingi, kama ambavyo itaainishwa chini ya Sheria hii. (2) Kitita cha mafao ya huduma muhimu kitatumika kwa kipindi cha mwaka mmoja tangu tarehe ambayo mwanachama atasajiliwa kujiunga na Bima ya Afya: Isipokuwa kwamba, kitita cha mafao ya huduma muhimu kwa mwanachama anayechangia kwa mujibu wa kifungu cha 23(1) kitaendelea kutumika hadi kufikia ukomo wake kwa kuzingatia masharti ya kifungu 28(2) cha Sheria hii. (1), (3) Bila kuathiri kifungu kidogo cha mwanachama au mnufaika wa skimu ya bima ya afya, anaweza, kwa kutegemea mpango wa skimu husika, kupata kitita cha huduma za ziada. Kitita cha mafao ya huduma muhimu Huduma za kitita cha mafao ya huduma muhimu - 14 Verify source ↗
Kitita cha mafao ya huduma muhimu
AI-assisted research summary: Kila skimu ya bima ya afya lazima itoe kitita cha mafao ya huduma muhimu kwa wanachama na wanufaika wake. Waziri anaweza pia kurekebisha, kuboresha au kufuta Sehemu A ya Jedwali kwa Amri ya Gazeti la Serikali, lakini mabadiliko yanapaswa kuzingatia matokeo ya tathmini ya uhai na uendelevu wa skimu.
14.-(1) Kitita cha mafao ya huduma muhimu kitajumuisha huduma za afya zitakazopatikana kuanzia ngazi ya zahanati hadi hospitali za Taifa. (2) Kila skimu ya bima ya afya itatoa kitita cha mafao ya huduma muhimu kwa wanachama na wanufaika wake kama hitaji la msingi. 12 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 Kitita cha bima ya afya cha jamii (3) Huduma zitakazotolewa katika kitita cha mafao ya huduma muhimu zitakuwa kama zilivyoorodheshwa katika Sehemu A ya Jedwali la Sheria hii. (4) Waziri, kwa Amri itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, anaweza kurekebisha, kuboresha au kufuta Sehemu A ya Jedwali la Sheria hii: Isipokuwa kwamba, mabadiliko ya kitita cha mafao ya huduma muhimu yatazingatia matokeo ya tathmini ya uhai na uendelevu wa skimu za bima ya afya. (b) Kitita cha Bima ya Afya cha Jamii - 15
AI-assisted research summary: People without any health insurance under this Act must have the community health insurance package.
15.-(1) Kwa madhumuni ya kufikia bima ya afya kwa wote, kutakuwa na kitita cha bima ya afya cha jamii chini ya skimu ya bima ya afya ya umma kitakachojumuisha huduma za afya zitakazotolewa katika vituo vya kutolea huduma za afya. (2) Mtu ambaye hatokuwa na bima ya afya yoyote chini ya Sheria hii, atapaswa kuwa na kitita cha bima ya afya ya Jamii. (3) Huduma zitakazotolewa chini ya kifungu kidogo cha (1) zitakuwa kama ilivyoorodheshwa katika Sehemu B ya Jedwali la Sheria hii. (4) Waziri, kwa Amri itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, anaweza kurekebisha, kuboresha au kufuta Sehemu B ya Jedwali la Sheria hii. Akaunti ya kitita cha bima ya afya cha jamii - 16
AI-assisted research summary: The public health insurance scheme must open a special community health insurance account and use the money for health insurance services and operating costs, with operating costs capped at 15% of members’ contributions.
16.-(1) Skimu ya bima ya afya ya umma itafungua akaunti maalumu ya kitita cha bima ya afya cha jamii ambapo fedha kutoka katika vyanzo vifuatavyo itawekwa: (a) michango ya wanachama; (b) fedha zitakazotengwa na Bunge; (c) vyanzo vingine vitakavyotengwa na Serikali; (d) misaada na zawadi kutoka kwa wadau mbalimbali ndani na nje ya nchi; (e) fedha kutoka chanzo kingine chochote ambacho ni halali. (2) Fedha katika akaunti maalumu chini ya kifungu hiki zitatumika kwa ajili ya huduma za bima ya afya kwa 13 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 wanufaika wa kitita cha bima ya afya cha jamii pamoja na gharama za uendeshaji wake: Isipokuwa kwamba, gharama za uendeshaji wa akaunti maalumu hazitazidi asilimia 15 ya michango ya wanachama. Usimamizi na uendeshaji wa kitita cha bima ya afya cha jamii - 17 Verify source ↗
Kitita cha bima ya afya cha jamii
AI-assisted research summary: Waziri anaweza kutunga kanuni za kuweka utaratibu wa usimamizi na uendeshaji wa kitita cha bima ya afya ya jamii, baada ya kushauriana na Waziri wa serikali za mitaa.
17. Waziri, kwa kushauriana na Waziri mwenye dhamana na masuala ya serikali za mitaa, anaweza kutunga kanuni kwa ajili ya kuweka utaratibu wa usimamizi na uendeshaji wa kitita cha bima ya afya cha jamii. (c) Kitita cha Huduma za Ziada Kitita cha huduma za ziada - 18 Verify source ↗
Kitita cha huduma za ziada
AI-assisted research summary: Skimu ya bima ya afya inaweza kutoa huduma za ziada kwa wanufaika wake, na Mamlaka inasimamia ushindani katika utoaji wa vitita hivyo ili kuhakikisha huduma bora.
18.-(1) Skimu ya bima ya afya inaweza kutoa huduma ya ziada ya kitita cha mafao ya huduma muhimu kwa wanufaika wake na michango kuhusiana na kitita cha huduma za ziada itakuwa kwa kuzingatia miongozo itakayotolewa na Mamlaka. (2) Mamlaka itasimamia ushindani katika utoaji wa vitita vya huduma za ziada wa skimu za bima ya afya kwa madhumuni ya kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora. SEHEMU YA TANO UANACHAMA NA UCHANGIAJI KATIKA SKIMU YA BIMA YA AFYA Uanachama
Part
SEHEMU YA TANO
- 19 Verify source ↗
Uanachama
AI-assisted research summary: People in the formal private sector or the informal sector must join a health insurance scheme.
19.-(1) Uanachama katika skimu ya bima ya afya utajumuisha watu wafuatao: (a) watu wote ambao kabla ya kuanza kutumika kwa Sheria hii walikuwa wanachama wa skimu ya bima ya afya kama ilivyoainishwa katika Sheria zinazosimamia skimu husika; (b) watu wote ambao katika tarehe ya kuanza kutumika kwa Sheria hii watakuwa wametimiza umri wa miaka ishirini na moja; (c) watu wote ambao, kwa tarehe ya kuanza kutumika kwa Sheria hii, watakuwa chini ya umri wa miaka ishirini na moja lakini wanasifa za kusajiliwa kuwa wanachama kwa mujibu wa Sheria hii au Sheria nyingine yoyote; 14 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 (d) watu wote walioajiriwa katika sekta binafsi au ya umma; (e) watu wote waliojiajiri; (f) watu wasio na uwezo; na (g) makundi mengine ya watu kadri itakavyoainishwa na Waziri katika kanuni. (2) Mtu kutoka sekta rasmi binafsi au sekta isiyo rasmi atajiunga na skimu ya bima ya afya yoyote. Wanufaika - 20 Verify source ↗
Wanufaika
AI-assisted research summary: Mwanachama anaweza kusajili mwenza wake na wategemezi wasiozidi wanne kama wanufaika.
20. Mwanachama anaweza kusajili watu wafuatao kama wanufaika: (a) mwenza wa mwanachama; na (b) wategemezi wasiozidi wanne. Wigo wa upatikanaji wa huduma za afya - 21 Verify source ↗
Wigo wa upatikanaji wa huduma za afya
AI-assisted research summary: Mwanachama au mnufaika anaweza kupata huduma za afya katika kituo chochote cha afya kilicho na mkataba na skimu ya bima ya afya, kwa kuzingatia miongozo ya Wizara na miongozo ya rufaa.
21. Mwanachama au mnufaika anaweza kupata huduma za afya mahala popote katika kituo cha kutolea huduma za afya kilichoingia mkataba na skimu ya bima ya afya kwa ajili ya utoaji wa huduma za afya kwa kuzingatia miongozo ya Wizara ikiwemo miongozo ya rufaa. Usajili wa wanachama katika skimu ya bima ya afya Viwango vya uchangiaji - 22
AI-assisted research summary: Mwajiri wa sekta ya umma au sekta rasmi binafsi lazima asajili mwajiriwa katika skimu ya bima ya afya ndani ya siku 30 kutoka tarehe ya kuanza kwa mkataba wa ajira, kwa kufuata utaratibu wa kanuni.
22.-(1) Kwa kuzingatia utaratibu utakaoainishwa katika kanuni, mwajiri katika sekta ya umma na sekta rasmi binafsi atapaswa kumsajili mwajiriwa katika skimu ya bima ya afya ndani ya siku thelathini kutoka tarehe ya kuanza kwa mkataba wa ajira. (2) Kila raia au mkazi aliye katika sekta rasmi na isiyo rasmi atasajiliwa katika skimu ya bima ya afya kwa utaratibu utakaoanishwa katika kanuni. - 23
AI-assisted research summary: Waajiri wa sekta ya umma na sekta rasmi binafsi lazima wawasilishe kiwango cha mchango katika skimu ya bima ya afya ya umma; waajiri wa sekta rasmi binafsi pia wanaweza kumsajili mwajiriwa kwenye bima ya afya ya binafsi baada ya kuidhinishwa na Mamlaka.
23.- (1) Kwa madhumuni ya upatikanaji wa kitita cha mafao ya huduma muhimu katika skimu ya bima ya afya ya umma, kila mwajiri katika sekta ya umma na sekta rasmi binafsi atawasilisha katika skimu hiyo kiwango cha mchango kwa kuzingatia Sheria inayosimamia skimu ya bima ya afya ya umma. (2) Bila kuathiri masharti ya kifungu kidogo cha (1), mwajiri katika sekta rasmi binafsi anaweza kumsajili mwajiriwa wake katika skimu ya bima ya afya ya binafsi na 15 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 kuwasilisha kiwango cha uchangiaji kitakachopangwa na skimu hiyo baada ya kuidhinishwa na Mamlaka. (3) Waziri kwa kushauriana na Waziri mwenye dhamana ya masuala ya fedha, ataainisha viwango vya rasmi, kama uchangiaji kwa ajili ya sekta itakavyoainishwa katika kanuni, kwa kuzingatia tathmini ya uhai na uendelevu wa skimu za bima ya afya katika utoaji wa kitita cha mafao ya huduma muhimu. isiyo - 24 Verify source ↗
25. Mfuko wa kugharamia wasio na uwezo
AI-assisted research summary: Waziri lazima aweke utaratibu wa kutambua watu wasio na uwezo na atunze kanzidata yao; watu watakaotambuliwa wana haki ya kujumuishwa kwenye skimu ya bima ya afya kwa namna itakayoainishwa na kanuni.
24.-(1) Waziri, kwa kushirikiana na mamlaka zinazohusika, na kwa kupitia kanuni, ataweka utaratibu na namna ya utambuzi wa watu wasio na uwezo. (2) Watu watakaotambuliwa kama watu wasio na uwezo chini ya kifungu kidogo cha (1) watakuwa na haki ya kujumuishwa chini ya skimu ya bima ya afya kwa namna itakayoainishwa kwenye kanuni. (3) Waziri, kwa madhumuni ya Sheria hii, atatunza na kuhuisha kanzidata ya watu waliotambuliwa chini ya kifungu kidogo cha (1). Utambuzi na upatikanaji wa huduma kwa watu wasio na uwezo Mfuko wa kugharamia wasio na uwezo, nk. - 25 Verify source ↗
Mfuko wa kugharamia wasio na uwezo
AI-assisted research summary: A fund is established to finance health insurance for people who cannot afford it.
25.-(1) Kunaanzishwa mfuko kwa ajili ya kugharamia bima ya afya kwa watu wasio na uwezo. (2) Bila kuathiri kifungu kidogo cha (1), Mfuko unaweza kutumika kugharamia- (a) huduma za matibabu ya magonjwa sugu na ya muda mrefu; na (b) huduma za afya za dharura zitokanazo na ajali, kwa kuzingatia miongozo itakayotolewa na Wizara. (3) Kwa kuzingatia masharti ya sheria za fedha, fedha zinazolipwa katika Mfuko wa kugharamia bima ya afya kwa watu wasio na uwezo zitatatokana na vyanzo vifuatavyo- (a) mapato yatokanayo na miamala ya kielektroniki kwa kiwango kitakachoainishwa katika Sheria za fedha; (b) kwa namna itakavyopendekezwa na Waziri mwenye dhamana na masuala ya fedha- 16 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 (i) mapato yatokanayo na ushuru wa bidhaa kwenye bidhaa za vinywaji vyenye kaboni, vinywaji vyenye vileo na bidhaa za vipodozi; (ii) kodi kwenye michezo ya kubahatisha; na (iii) ada ya bima ya vyombo vya moto. (c) fedha zitakazotengwa na Bunge; (d) mapato yatakayotokana na uwekezaji wa Mfuko; na (e) zawadi na misaada kutoka kwa wadau mbalimbali; (4) Waziri kwa kushauriana na Waziri mwenye dhamana ya masuala ya fedha ataweka utaratibu wa usimamizi bora wa Mfuko. - 26
AI-assisted research summary: Mwenye kuendesha skimu ya bima ya afya binafsi lazima aweke benki kiasi cha fedha kilichowekwa na Sheria ya Bima kama sharti la usajili, na skimu lazima itunze akiba ya kutosha kwa angalau miaka miwili.
26.-(1) Mtu anayeendesha skimu ya bima ya afya binafsi, kama sharti la usajili, ataweka Benki kiwango cha fedha kilichoainishwa kwenye Sheria ya Bima. (2) Skimu ya bima ya afya itatunza akiba ya kiasi cha fedha kitakachotosheleza utolewaji wa huduma kwa wanachama wake kwa kipindi cha angalau miaka miwili, kwa namna itakavyoainishwa katika kanuni. (3) Amana inayorejewa katika kifungu kidogo cha (1) itadumu kwa kipindi chote cha uendeshaji wa skimu ya bima ya afya binafsi. Uwekaji wa amana Utambuzi wa uanachama ya- - 27
AI-assisted research summary: Health insurance scheme must establish procedures for member and beneficiary identification access and for verifying identification used by a health facility.
27. Skimu ya bima ya afya itaweka utaratibu kwa ajili (a) upatikanaji wa utambulisho kwa mwanachama na wanufaika wake; na (b) uhakiki wa utambulisho uliotolewa na huduma zinazotolewa na kituo cha kutolea huduma za afya. Ukomo wa uanachama - 28 Verify source ↗
Uwekaji wa amana
AI-assisted research summary: Uanachama wa skimu ya bima ya afya hukoma mwanaachama anapofariki au anapoacha kuchangia kwa muda unaotakiwa na kanuni; wategemezi wanaweza kuendelea kupata huduma katika hali fulani.
28.-(1) Uanachama katika skimu ya bima ya afya utakoma baada ya kutokea kwa kifo cha mwanachama au pale ambapo mwanachama ataacha kuchangia kwenye skimu ya bima ya afya kwa kipindi kitakachoainishwa kwenye kanuni. 17 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 Viwango vya udhibiti ubora vya skimu ya bima ya afya Udhibiti ubora wa watoa huduma za afya Ukwasi na uendelevu wa bima ya afya (2) Iwapo mwanachama anayechangia kupitia makato ya mshahara wake atafariki, atapata ulemavu wa kudumu au ataachishwa kazi, wategemezi wake wataendelea kunufaika na huduma kwa kipindi kitakachoinishwa katika kanuni. (3) Iwapo mwanachama anayechangia kwa utaratibu wa michango kwa mwaka atafariki, wategemezi wake wataendelea kunufaika na huduma kwa kipindi kilichosalia cha mkataba wa uanachama. SEHEMU YA SITA UDHIBITI UBORA
Part
SEHEMU YA SITA
- 29
AI-assisted research summary: Health insurance schemes must implement quality standards set by the Authority.
29. Skimu ya bima ya afya itatekeleza viwango vya ubora vitakavyoainishwa na Mamlaka. - 30 Verify source ↗
Viwango vya udhibiti ubora vya skimu ya bima ya afya
AI-assisted research summary: Wizara must ensure contracted health-insurance service facilities follow quality standards issued by the Ministry or under the Act.
30. Wizara itakuwa na jukumu la kuhakikisha kuwa vituo vya kutolea huduma vilivyoingia mikataba na skimu za bima ya afya vinatekeleza viwango vya ubora vilivyotolewa na Wizara au kwa mujibu wa Sheria. SEHEMU YA SABA MASHARTI MENGINEYO
Part
SEHEMU YA SABA
- 31
AI-assisted research summary: Skimu ya bima ya afya lazima ifanye tathmini ya uhai na uendelevu kila baada ya miaka mitatu au wakati wowote Mamlaka itakapoielekeza; taarifa iwasilishwe kwa Mamlaka na nakala ipelekwe kwa Waziri.
31.-(1) Skimu ya bima ya afya itatakiwa kufanya tathmini ya uhai na uendelevu kila baada ya miaka mitatu au wakati wowote kadiri imeelekezwa na Mamlaka kwa kumtumia mtathmini. itakavyokuwa (2) Taarifa ya tathmini itakayofanywa kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (1) itawasilishwa kwa Mamlaka na nakala kupelekwa kwa Waziri. (3) Mamlaka inaweza kuelekeza skimu ya bima ya afya kuchukua hatua kama itakavyohitajika kurekebisha upungufu ulioonekana katika taarifa ya tathmini ya uhai na uendelevu. 18 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 Uwekezaji wa skimu za bima ya afya - 32
AI-assisted research summary: Benki lazima izingatie miongozo iliyoshauriwa na Mamlaka kuhusu uwekezaji wa skimu za bima ya afya, na Benki pamoja na Mamlaka wanaweza kutoa miongozo, kufuatilia utekelezaji, na kuchunguza usimamizi wa fedha.
32.-(1) Uwekezaji wa skimu za bima ya afya itakayotolewa na Benki kwa utazingatia miongozo kushauriana na Mamlaka. (2) Kwa madhumuni ya kifungu kidogo cha (1), Benki, kwa kushirikiana na Mamlaka, itakuwa na mamlaka ya- (a) kutoa miongozo ya uwekezaji wa skimu za bima ya afya; (b) kufuatilia na kusimamia utekelezaji wa skimu za bima ya afya kwa wahusika wote chini ya Sheria hii; au (c) kuchunguza yote yanayohusiana na usimamizi wa fedha wa skimu za bima ya afya. kukagua masuala na Gharama za usimamizi na uendeshaji Malalamiko na usuluhishi wa migogoro Sura ya 394 Mamlaka ya kutunga kanuni - 33 Verify source ↗
34. Malalamiko na usuluhishi wa migogoro
AI-assisted research summary: Mamlaka inapaswa kutoa miongozo kuhusu ukomo wa juu wa gharama za uendeshaji wa skimu ya bima ya afya.
33. Mamlaka itatoa miongozo kuhusu ukomo wa juu wa gharama za uendeshaji wa skimu ya bima ya afya. - 34 Verify source ↗
Malalamiko na usuluhishi wa migogoro
AI-assisted research summary: Malalamiko na migogoro kati ya au dhidi ya skimu ya bima ya afya, kituo cha huduma za afya kilichoingia mkataba, mnufaika, mwajiri na mtu mwingine husika hushughulikiwa kwa utaratibu uliowekwa kwenye Sheria ya Bima.
34. Utaratibu wa kushughulikia malalamiko na utatuzi wa migogoro baina ya au dhidi ya skimu ya bima ya afya, kituo cha huduma za afya kilichoingia mkataba, mnufaika, mwajiri na mtu yeyote anayehusika utakua kama ulivyoainishwa kwenye Sheria ya Bima. - 35 Verify source ↗
Mamlaka ya kutunga kanuni
AI-assisted research summary: Waziri anaweza kutunga kanuni kuhusu usajili, mafao, madai, faini, na taratibu nyingine za utekelezaji wa Sheria hii.
35. Waziri anaweza kutengeneza kanuni zitakazoainisha- (a) utaratibu wa usajili wa skimu za bima ya afya; (b) kitita cha mafao, muda, masharti au wigo wa kitita cha mafao kwa kushirikiana na Mamlaka; (c) utaratibu wa kuboresha skimu ya bima ya afya ya umma ikiwemo kuanzisha kitita cha mafao maalum; (d) muda wa kuahirishwa kwa malipo yoyote ya madai wakati uchunguzi unaendelea; (e) utaratibu wa kusajiliwa kwenye skimu ya bima ya afya kwa watu wenye umri chini ya miaka ishirini na moja; 19 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 (f) utaratibu wa ulipaji wa faini zote au sehemu ya kama kuzingatia masharti faini kwa yatakavyoainishwa; (g) utaratibu wa utambuzi wa watu walio katika sekta isiyo rasmi na namna ya kuwasajilii katika skimu; (h) maelezo, taarifa, uthibitisho au ushahidi jambo utakaotolewa kwa suala linalojitokeza chini ya Sheria hii, ikiwemo suala lolote au jambo muhimu kuhusiana na malipo ya michango aliyolipa mwanachama au kuhusiana na mtu yeyote au uandaaji au uhalalishaji wa madai yoyote au maombi kwa ajili ya malipo ya mafao yoyote yanayotolewa chini ya Sheria hii; (i) utaratibu wa malipo kwa vituo vya kutolea lolote au huduma za afya; (j) hatua yoyote inayohitajika au kuruhusiwa kuchukuliwa chini ya Sheria hii, muda na namna ya kuchukua hatua hiyo, utaratibu utakaofuatwa na fomu zitakazotumika; (k) utambuzi na usajili wa watu wasio na uwezo kwa kushirikiana na mamlaka nyingine; (l) namna ya upatikanaji wa huduma za afya kwa watu wasio na uwezo; (m) utaratibu wa kuboresha kitita cha mafao katika skimu ya bima ya afya ya umma; na (n) suala lingine lolote kwa ajili ya utekelezaji bora wa masharti ya Sheria hii. - 36
AI-assisted research summary: A person who knowingly gives false information, causes false documents or statements to be produced, or fails to submit required documents without good reason commits an offence.
36.-(1) Mtu yeyote ambaye- (a) kwa madhumuni ya kukwepa kulipa mchango wake au wa mtu yeyote mwingine kwa niaba yake, kwa kufahamu, akitoa taarifa zozote za uongo au kusababisha kutolewa kwa nyaraka au taarifa ambazo anaamini kuwa ni za uongo; (b) kwa madhumuni ya kunufaika au kufidiwa yeye binafsi au mtu yeyote mwingine, kwa kufahamu, akitoa taarifa zozote za uongo au kusababisha 20 Taarifa za uongo Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 kutolewa kwa nyaraka au anaamini kuwa ni za uongo; taarifa ambazo (c) anashindwa kuwasilisha nyaraka zinazohitajika chini ya Sheria hii pasipokuwa na sababu za msingi, anatenda kosa na akitiwa hatiani, atawajibika- (i) kwa kosa lililotendwa na mwanachama au mnufaika, kulipa faini isiyopungua shilingi laki tano na isiyozidi shilingi milioni tano au kutumikia kifungo kwa kipindi kisichopungua miezi sita na kisichozidi miezi kumi na mbili au vyote; (ii) kwa kosa lililotendwa na skimu ya bima ya afya, kulipa faini isiyopungua shilingi milioni kumi na isiyozidi shilingi milioni mia moja, na mahakama inaweza ikaamuru kulipwa hasara iliyosababishwa; na fidia kwa ya (iii) kwa kosa liliotendwa na kituo cha kutolea huduma za afya, kulipa faini isiyopungua shilingi milioni tano na isiyozidi shilingi milioni hamsini na mahakama inaweza ikaamuru kulipwa kwa fidia ya hasara iliyosababishwa; (2) Bila kuathiri masharti ya kifungu kidogo cha (1), Mamlaka- za cha kutolea huduma (a) inaweza kuifungia skimu ya bima ya afya au kituo afya kitakachobainika kutenda kosa chini ya kifungu hiki kwa kipindi kisichozidi miaka miwili; au (b) itaitaarifu mamlaka husika ya kitaaluma kuchukua hatua stahiki dhidi ya mwanataaluma anayetuhumiwa kukiuka masharti ya kifungu hiki. Kutojiunga na skimu ya bima ya afya - 37
AI-assisted research summary: Mtu anayeshindwa kujiunga na skimu ya bima ya afya ndani ya siku 21 tangu Sheria ianze, bila sababu za msingi, atalipa riba ya asilimia 10 ya kiwango cha uchangiaji kwa kila mwaka wa uchangiaji; Waziri anaweza kutoa msamaha kwa notisi ya Gazeti la Serikali.
37.-(1) Isipokuwa kwa wageni wanaoingia nchini ambao masharti mengine kuhusu adhabu katika Sheria hii yatatumika, mtu yeyote ambaye bila sababu za msingi atashindwa kujiunga na skimu ya bima ya afya ndani ya 21 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 tangu kuanza kutumika kwa Sheria, miaka mitatu atakapojiunga na bima ya afya, atalazimika kulipa riba ya asilimia 10 ya kiwango cha uchangiaji kwa kila mwaka wa uchangiaji. (2) Bila kujali kifungu kidogo cha (1), Waziri, kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali na kwa kuzingatia maslahi ya umma au kwasababu yoyote nyingine atakayoainisha katika notisi, anaweza kutoa msamaha wa ulipwaji wa riba kwa watu au kundi lolote lenye wajibu wa kujiunga na skimu ya bima ya afya chini ya Sheria hii. - 38 Verify source ↗
39. Makosa ya jumla
AI-assisted research summary: Mahakama inaweza kuamuru mshtakiwa alipe kiasi cha mchango unaodaiwa, faini, au gharama nyingine kwa skimu ya bima ya afya, na kiasi hicho kinaweza kudaiwa pia kwa madai ya haraka.
38.-(1) Mahakama inayosikiliza shauri dhidi ya mtu yoyote aliyeshtakiwa kwa kosa chini ya Sheria hii, bila kujali uwepo wa shauri lolote la madai, inaweza kuamuru mshtakiwa kuilipa skimu ya bima ya afya kiasi cha mchango kinachodaiwa pamoja na faini itakayotozwa au gharama nyingine yoyote, na kiasi kitakachoamriwa kinaweza kudaiwa na kulipwa kwa skimu. (2) Kiasi chochote kinachodaiwa na skimu ya bima ya afya kitakuwa ni deni kwa skimu na, bila kuathiri namna nyingine ya kudai, kiasi hicho kinaweza kudaiwa kwa njia ya madai ya haraka kwa mujibu wa kanuni ya XXXV ya Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Madai. - 39 Verify source ↗
Makosa ya jumla
AI-assisted research summary: A person who breaches any provision of the Act, where no specific penalty is set, commits an offence and may face a fine or imprisonment; companies or institutions face a fine.
39. Mtu anayekiuka masharti yoyote ya Sheria hii pale ambapo hakuna adhabu mahususi iliyowekwa, anatenda kosa na akitiwa hatiani, atawajibika- (a) iwapo ni mtu binafsi, kulipa faini isiyopungua shilingi laki tano na isiyozidi shilingi milioni tano au kutumikia kifungo kisichopungua miezi sita na kisichozidi miaka miwili au vyote; na (b) iwapo ni kampuni au taasisi, kulipa faini isiyopungua shilingi milioni kumi na iziyozidi shilingi milioni mia moja. Utaratibu wa madai ya skimu ya bima ya afya Sura ya 33 Makosa ya jumla Makosa yatendwayo na taasisi - 40 Verify source ↗
Makosa yatendwayo na taasisi
AI-assisted research summary: Kama kosa limetendwa na kampuni au taasisi, mkurugenzi, meneja au mbia anaweza kuwajibika kwa adhabu ya kosa hilo baada ya kuhukumiwa, isipokuwa akishawishi mahakama kuwa hakuwa na uelewa, idhini, au hatua za makusudi za kuzuia kosa hilo.
40. Endapo kosa limetendwa na kampuni au taasisi chini ya Sheria hii, mkurugenzi, meneja au mbia wa kampuni au taasisi hiyo atawajibika, ikiwa atatiwa hatiani, kwa adhabu iliyoainishwa kuhusiana na kosa hilo, isipokuwa 22 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 kama mkurugenzi, meneja au mbia huyo ataithibitishia mahakama kwa kiasi cha kuiridhisha kwamba kitendo kilichosababisha kosa hilo kufanyika kilifanyika pasipo yeye kuwa na uelewa, kutoa idhini au kuchukua hatua za makusudi kuzuia kosa hilo kutendeka. Mkinzano na sheria nyingine - 41 Verify source ↗
Mkinzano na sheria nyingine
AI-assisted research summary: Kama kuna mkinzano kati ya Sheria hii na sheria nyingine kuhusu bima ya afya, Sheria hii ndiyo itakayofuata.
41. Endapo kutakuwa na mkinzano baina ya masharti ya Sheria hii na masharti ya sheria nyingine yoyote kuhusiana na masuala ya bima ya afya, masharti ya Sheria hii yatapewa kipaumbele. SEHEMU YA NANE KUFUTWA KWA SHERIA NA MASHARTI YA MPITO Kufutwa kwa Sheria na masharti yanayoendelea Sura ya 409
Part
SEHEMU YA NANE
- 42 Verify source ↗
43. Masharti ya mpito
AI-assisted research summary: Sheria ya Mfuko wa Afya ya Jamii inafutwa, lakini baadhi ya kanuni, maelekezo, haki na mafao ya kabla ya kuanza kutumika kwa Sheria hii yanaendelea kutumika kwa muda fulani.
42.-(1) Sheria ya Mfuko wa Afya ya Jamii inafutwa. (2) Bila kujali kufutwa kwa Sheria chini ya kifungu kidogo cha (1)- (a) kanuni, amri, miongozo na sheria ndogo nyingine zilizotungwa chini ya Sheria ya Mfuko wa Afya ya Jamii na ambazo zilikuwa zinatumika kabla ya kuanza kutumika kwa Sheria hii, zitaendelea kutumika hadi zitakapofutwa; (b) maelekezo yote yaliyotolewa chini ya masharti ya Sheria ya Mfuko wa Afya ya Jamii yataendelea kuwa halali hadi hapo yatakapofutwa, kusitishwa au kukoma kutokana na sababu ya kuisha kwa muda wake; (c) mtu ambaye wakati wa kuanza kutumika kwa Sheria hii alikuwa akinufaika na mafao ya Mfuko wa Afya ya Jamii ataendelea kunufaika na mafao hayo hadi Waziri atakapoweka utaratibu wa kujiunga na kitita cha bima ya afya cha jamii kilichowekwa kwa mujibu wa Sheria hii; na (d) haki na afua ambazo, kabla ya kuanza kutumika kwa Sheria hii zilitolewa kwa 23 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 Masharti ya mpito mujibu wa Sheria ya Mfuko wa Afya ya Jamii, zitaendelea kuwepo kana kwamba zilitolewa chini ya Sheria hii hadi hapo zitakapofutwa kwa mujibu wa Sheria hii. - 43 Verify source ↗
Masharti ya mpito
AI-assisted research summary: There is a transitional period of up to 12 months, and the Ministry must coordinate winding up the Health Fund’s affairs before it ends. The Minister may extend the transitional period by up to 6 more months.
43.-(1) Kutakuwa na kipindi cha mpito kisichozidi miezi kumi na mbili, kitakachoanzia tarehe ya kuanza kutumika kwa Sheria hii. (2) Kwa kuzingatia Sheria hii na kabla kuisha kwa kipindi cha mpito, Wizara kwa kushirikiana na Wizara yenye dhamana na mamlaka za serikali za mitaa na mamlaka nyingine husika, itaratibu uhitimishwaji wa shughuli za Mfuko wa Afya ya Jamii ikiwa ni pamoja na utambuzi wa mali, madeni, madai, hatma ya mikataba iliyopo, mashauri yaliyopo na masuala mengine yanayohusiana na Mfuko wa Afya ya Jamii kwa namna itakavyoainishwa katika kanuni. (3) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (1), Waziri anaweza kuongeza muda wa kipindi cha mpito kwa kipindi kingine cha ziada kisichozidi miezi sita. SEHEMU YA TISA MAREKEBISHO YA SHERIA MBALIMBALI (a) Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Sura ya 395 Ufafanuzi Sura ya 395 Marekebisho ya kifungu cha 2
Part
SEHEMU YA TISA
- 44 Verify source ↗
45. Marekebisho ya kifungu cha 2
AI-assisted research summary: This subsection must be read together with the National Health Insurance Fund Act, which is called the “principal Act” here.
44. Sehemu Ndogo hii itasomwa pamoja na Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ambayo hapa itarejewa kama “Sheria Kuu”. - 45 Verify source ↗
Marekebisho ya kifungu cha 2
AI-assisted research summary: This provision amends section 2(1) by inserting the words “persons under formal private sector, students” between “Councillors,” and “retirees”.
45. Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 2(1) kwa kuongeza maneno “persons under formal private sector, students” kati ya maneno “Councillors,” na “retirees”. Marekebisho ya kifungu cha 3 - 46 Verify source ↗
Marekebisho ya kifungu cha 3
AI-assisted research summary: Section 3 is amended so that the definition of “Authority” is deleted and replaced with a reference to the Universal Health Insurance Act.
46. Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 3 kwa kufuta tafsiri ya neno “Authority” na badala yake kuweka tafsiri ifuatayo: 24 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 ““Authority” has the meaning ascribed to it under the Universal Health Insurance Act;”. Marekebisho ya kifungu cha 11 - 47 Verify source ↗
Marekebisho ya kifungu cha 11
AI-assisted research summary: This provision changes the text of section 11(1) by adding specified words after “Councilors” in paragraph (e), and it also repeals and rewrites sections 16 and 40.
47. Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu 11(1) kwa kuongeza maneno “persons under formal private sector, student and children” baada ya neno “Councilors” lililopo katika aya (e). kufutwa na kuandikwa upya kwa kifungu cha 16 Kufutwa na kuandikwa upya kwa kifungu cha 40 - 48
AI-assisted research summary: The principal law is amended by deleting section 16 and replacing it with a new section, but the new text is cut off here.
48. Sheria Kuu inarekebishwa kwa kufuta kifungu cha 16 na badala yake kuweka kifungu kifuatacho: “Benefit package - 16
AI-assisted research summary: The Fund must provide the standard benefit package, and it may also provide supplementary benefit packages, under the Universal Health Insurance Act.
16.-(1) The Fund shall provide the standard benefit package in accordance with the Universal Health Insurance Act. (2) Without prejudice to the provisions of subsection (1), the Fund may provide supplementary benefit packages in accordance with the Universal Health Insurance Act.”. - 49
AI-assisted research summary: This provision says section 40 is deleted and replaced with a new section, but the replacement text is only shown as “Appeal” in the source provided.
49. Sheria Kuu inarekebishwa kwa kufuta kifungu cha 40 na badala yake kuweka kifungu kifuatacho: “Appeal - 40 Verify source ↗
Makosa yatendwayo na taasisi
AI-assisted research summary: A person who is aggrieved by a scheme officer’s decision may appeal to the Ombudsman through the Authority.
40. A member or health care is aggrieved by any provider who decision of an officer of a scheme may appeal to the Ombudsman through the Authority in accordance with section 124(5) of the Insurance Act.”. Cap. 394 Kufutwa kwa vifungu vya 41 na 42 - 50 Verify source ↗
Kufutwa na kuandikwa upya kwa kifungu cha 16
AI-assisted research summary: This provision says the main law is amended by deleting sections 41 and 42.
50. Sheria ya Kuu inarekebishwa kwa kufuta vifungu vya 41 na 42. (b) Sheria ya Hifadhi ya Jamii, Sura ya 135 Ufafanuzi Sura ya 135 - 51 Verify source ↗
52. Marekebisho ya kifungu cha 61
AI-assisted research summary: This provision says it must be read together with the Social Security Act, and it identifies an amendment to section 61.
51. Sehemu Ndogo hii itasomwa pamoja na Sheria ya Hifadhi ya Jamii ambayo hapa itarejewa kama “Sheria Kuu”. 25 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 Marekebisho ya kifungu cha 61 - 52 Verify source ↗
Marekebisho ya kifungu cha 61
AI-assisted research summary: This section amends section 61(b)(ii) by replacing one phrase with another phrase naming the Tanzania Insurance Regulatory Authority under the Universal Health Insurance Act.
52. Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 61(b)(ii) kwa kufuta maneno “Ministry responsible for health matters” na badala yake kuweka maneno “Tanzania Insurance Regulatory Authority pursuant to the Universal Health Insurance Act.” (c) Sheria ya Bima, Sura ya 394 Ufafanuzi Sura ya 394 - 53 Verify source ↗
54. Marekebisho ya kifungu cha 6
AI-assisted research summary: Sehemu hii inasema isomwe pamoja na Sheria ya Bima na inaonyesha marekebisho ya kifungu cha 6.
53. Sehemu Ndogo hii itasomwa pamoja na Sheria ya Bima ambayo hapa itarejewa kama “Sheria Kuu”. Marekebisho ya kifungu cha 6 cha 6- - 54 Verify source ↗
Marekebisho ya kifungu cha 6
AI-assisted research summary: This provision amends section 6 by adding specified words to subsection (1) and subsection (2), including references to health insurance scheme members, employers, health service providers, and health insurance schemes.
54. Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu (a) katika kifungu kidogo cha (1), kwa kuongeza maneno “health insurance scheme members, employers, health service providers and health insurance schemes” baada ya neno “policy-holders”; (b) katika kifungu kidogo cha (2) kwa- (i) kuongeza maneno “health insurance scheme members, employers, health service providers and health insurance schemes” baada ya neno “policy- holder” lililopo mwishoni mwa aya (j); (ii) kuongeza aya mpya mara baada ya aya (k) kama ifuatavyo: “(l) package oversee and ensure quality the primary assurance of and benefit contribution in collaboration with the Ministry responsible for health matters; supervise and regulate funds, insurance and health care providers; companies rates (m) 26 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 (n) supervise the compliance of laws related with insurance;” na (iii) kubadilisha mpangalio wa aya (l) na (m) kuwa aya (o) na (p), mtawalia. Marekebisho ya kifungu cha 123 - 55 Verify source ↗
Marekebisho ya kifungu cha 123
AI-assisted research summary: This section amends section 123 and adds a new subsection allowing health insurance schemes, members, and health service providers to bring complaints or review applications to the Ombudsman.
55. Sheria Kuu inarekebishwa kwa- (a) kukifanya kifungu cha 123 kuwa kifungu cha 123(1); na (b) kuongeza mara baada ya kifungu kidogo cha (1) kifungu kidogo cha (2) kama ifuatavyo: “(2) Notwithstanding subsection (1)- (a) health insurance schemes may file to the Ombudsman complaints against a member of a health insurance scheme or a health service provider; and (b) a member of a health insurance scheme and health service provider may the ombudsman applications for review against the decision of a health insurance scheme.”. file to Marekebisho ya kifungu cha 124 - 56 Verify source ↗
Marekebisho ya kifungu cha 124
AI-assisted research summary: This section amends section 124 by adding a new subsection giving the Ombudsman jurisdiction over certain health insurance complaints.
56. Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 124 kwa kuongeza mara baada ya kifungu kidogo cha (4), kifungu kidogo cha (5) kama ifuatavyo: to “(5) Notwithstanding subsection (1), the Ombudsman shall have unlimited health jurisdiction insurance related complaints from a member of a health insurance scheme or a health service provider referred to it by the Authority.”. determine Marekebisho ya kifungu cha 126 - 57 Verify source ↗
Marekebisho ya kifungu cha 126
AI-assisted research summary: This provision amends section 126 by deleting and replacing subsection (2), which sets out the Tribunal’s membership and appointment method.
57. Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 126 kwa kufuta na kuandika upya kifungu kidogo cha (2) kama ifuatavyo- 27 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 “(2) The Tribunal shall be an adhoc forum consisting of five persons as follows: (a) three persons appointed by the Minister with adequate experience in insurance matters, provided that, one of the members shall be a law officer from the Attorney General; the Office of (b) two persons appointed by responsible the Minister in consultation with the Minister for health matters who shall be persons with adequate in health experience matters, provided that, consultation with the Minister responsible for health shall only be sought where a Tribunal is constituted to handle health insurance matters.”. (d) Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii, Sura ya 50 Ufafanuzi Sura ya 50 Marekebisho ya kifungu cha 21 Kufutwa na kuandikwa upya kifungu cha 41 - 58 Verify source ↗
59. Marekebisho ya kifungu cha 21
AI-assisted research summary: This subsection must be read together with the National Social Security Fund Act, which is called the “Principal Act” here.
58. Sehemu Ndogo hii itasomwa pamoja na Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii, ambayo hapa itarejewa kama “Sheria Kuu”. - 59 Verify source ↗
Marekebisho ya kifungu cha 21
AI-assisted research summary: Kifungu cha 21(1) kinarekebishwa kwa kufuta neno “insurance” katika aya (g).
59. Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 21(1) kwa kufuta neno “insurance” lililopo katika aya (g). - 60 Verify source ↗
61. Marekebisho ya kifungu cha 42
AI-assisted research summary: Section 60 amends section 41 by deleting it and rewriting it, but the replacement text is cut off after “Condition for medical benefit”.
60. Sheria Kuu inarekebishwa kwa kufuta kifungu cha 41 na kukiandika upya kama ifuatavyo: “Condition for medical benefit - 41 Verify source ↗
Mkinzano na sheria nyingine
AI-assisted research summary: Medical benefit is payable to a member, the member’s spouse, and four children if the member has contributed to the Fund for at least three months.
41. Medical benefit shall be paid to a member, the spouse and four children of the member if the member has contributed to the Fund for a minimum of three months, of which three months of contributions were paid to the Fund in the 28 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 three months immediately preceding the medical contingency.” Marekebisho ya kifungu cha 42 - 61 Verify source ↗
Marekebisho ya kifungu cha 42
AI-assisted research summary: This section amends section 42(1) by deleting the words “based on health insurance”.
61. Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 42(1) kwa kufuta maneno “based on health insurance”. (e) Sheria ya Mtoto, Sura ya 13 Ufafanuzi Sura ya 13 - 62 Verify source ↗
63. Marekebisho ya kifungu cha 8
AI-assisted research summary: This subsection must be read together with the Child Law, which is called the main law here.
62. Sehemu Ndogo hii itasomwa pamoja na Sheria ya Mtoto ambayo hapa itarejewa kama “Sheria Kuu”. Marekebisho ya kifungu cha 8 - 63 Verify source ↗
Marekebisho ya kifungu cha 8
AI-assisted research summary: A parent, guardian, or other person with custody of a child must enroll the child in a health insurance scheme.
63. Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 8 kwa kuongeza kifungu kidogo cha (7) kama ifuatavyo: “(7) For the purpose of ensuring attainment of the right of a child to medical care, a parent, guardian or any other person having custody of a child shall enroll the child with a health insurance scheme.”. (f) Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, Sura ya 366 Ufafanuzi Sura ya 366 - 64
AI-assisted research summary: This subsection must be read together with the Employment and Labour Relations Act, called the “Principal Act.”
64. Sehemu Ndogo hii itasomwa pamoja na Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ambayo hapa itarejewa kama “Sheria Kuu”. Kuongezwa kwa Sehemu Ndogo E
Part
Sehemu Ndogo E
- 65 Verify source ↗
Ufafanuzi
AI-assisted research summary: This section amends the law to add a new Sub-Part E on access to health insurance.
65. Sheria Kuu inarekebishwa kwa kuongeza mara baada ya kifungu cha 11 Sehemu Ndogo ya E kama ifuatavyo- “Sub-Part E- Access to health insurance Access to health insurance - 11A Verify source ↗
(1) Subject to the provisions of
AI-assisted research summary: An employer must register each employee with a health insurance scheme, subject to the Universal Health Insurance Act.
11A.-(1) Subject to the provisions of the Universal Health Insurance Act, the employer shall register his employee with a health insurance scheme. 29 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 (2) A person who contravenes the this section commits an provisons of offence.”. (g) Sheria ya Udhibiti wa Hospitali Binafsi, Sura ya 151 Ufafanuzi Sura ya 151 Marekebisho ya kifungu cha 7 - 66 Verify source ↗
67. Marekebisho ya kifungu cha 7
AI-assisted research summary: This provision says this subsection must be read together with the Private Hospitals Regulatory Act, which is called the Main Act here.
66. Sehemu Ndogo hii itasomwa pamoja na Sheria ya Udhibiti wa Hospitali Binafsi ambayo hapa itarejewa kama “Sheria Kuu”. - 67 Verify source ↗
Marekebisho ya kifungu cha 7
AI-assisted research summary: This section amends section 7(2) by adding a new paragraph, renumbering a paragraph, and changing the word “five” to “four” in the amended paragraph.
67. Sheria Kuu inarekebishwa katika kifungu cha 7(2)- (a) kwa kuongeza mara baada ya aya (b), aya ifuatayo- “(c) the Commissioner of Insurance or a person nominated on his behalf from the Tanzania Insurance Regulatory Authority;”; (b) kwa kubadilisha mpangilio wa aya (c) kuwa aya (d); na (c) katika aya (d) kama ilivyobadilishwa, kwa kufuta neno “five” na badala yake kuweka neno “four”. 30 Na. 13 Sheria ya Bima ya Afya Kwa Wote ya Mwaka 2023 _____ JEDWALI _____ Sehemu A (chini ya kifungu cha 14(3)) Huduma zitakazotolewa katika kitita cha huduma muhimu zitakuwa kama ifuatavyo- (a) uandikishaji na kumuona daktari; (b) vipimo vya uchunguzi tiba vya maabara, radiolojia na mionzi kwa ngazi husika; (c) huduma za kulazwa; (d) matibabu ikiwemo- (i) huduma za dawa zilizo katika orodha ya dawa muhimu ya Taifa inayotolewa na Wizara; (ii) huduma za matibabu ya macho, kinywa na meno; (iii) huduma za kujifungua; na (iv) huduma za upasuaji; (e) huduma za kibingwa na ubingwa bobezi; na (f) huduma nyinginezo kwa kadri zitakavyoainishwa na Waziri katika kanuni chini ya Sheria hii.” Sehemu B (chini ya kifungu cha 15(3)) Huduma za kitita cha bima ya afya ya jamii zitakuwa kama ifuatavyo- (a) uandikishaji na kumuona daktari; (b) vipimo vya uchunguzi tiba vya maabara, radiolojia na mionzi kwa ngazi husika; (c) huduma za kulazwa; na (d) matibabu ikiwemo- (i) huduma za dawa zilizo katika orodha ya dawa muhimu ya Taifa inayotolewa na Wizara; (ii) huduma za matibabu ya macho, kinywa na meno; (iii) huduma za kujifungua; na (iv) huduma za upasuaji; (e) huduma nyinginezo kwa kadri zitakavyoainishwa na Waziri katika kanuni chini ya Sheria hii.” Imepitishwa na Bunge tarehe 01 Novemba, 2023. NENELWA JOYCE MWIHAMBI Katibu wa Bunge 31
Provision text is displayed from LexChat’s stored statute record. Use the official source links to verify amendments, commencement, and current legal force.
Ask AI about this statute
Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ya Mwaka 2023
Sign in to ask AI about this statute
Sign in to start authenticated, citation-grounded statute research.
Sign in