Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2024
Sheria hii itaanza kutumika kwenye tarehe itakayoteuliwa na Waziri kwa notisi kwenye Gazeti la Serikali.
AI-assisted research synopsis — verify against the official legal text below.
- Jurisdiction
- Tanzania
- Instrument
- Act or statute
- Citation
- Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2024
- Version
- Undated source snapshot
- Language
- sw
- Official source
- View official record ↗
Statute overview
About this statute
Sheria hii itaanza kutumika kwenye tarehe itakayoteuliwa na Waziri kwa notisi kwenye Gazeti la Serikali. This section says the law applies in Tanzania Mainland and Tanzania Zanzibar for presidential and parliamentary elections, and in Tanzania Mainland for councilor elections. Sehemu hii inaeleza maana ya maneno na istilahi mbalimbali zinazotumika katika Sheria hii. Tume inaweza kuandaa au kutoa kanuni, maelekezo na notisi; zitaonekana kuwa halali zikisainiwa na Mwenyekiti wa Tume au Mkurugenzi wa Uchaguzi. Tume lazima igawanye kila jimbo katika maeneo ya uchaguzi na ichapishe notisi ya kuyataja katika Gazeti la Serikali. Inaweza pia kubadili idadi na maeneo ya uchaguzi na kutangaza mabadiliko au mabadiliko ya eneo baada ya mipaka kubadilishwa.
Search within this statute
Search all stored provisions in this version.
Legal text
Provisions of Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2024
Showing 169 of 169
- 1 Verify source ↗
2. Matumizi
AI-assisted research summary: Sheria hii itaanza kutumika kwenye tarehe itakayoteuliwa na Waziri kwa notisi kwenye Gazeti la Serikali.
1. Sheria hii itajulikana kama Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2024, na itaanza kutumika katika tarehe ambayo Waziri atateua kwa notisi katika Gazeti la Serikali. Matumizi Tafsiri - 2 Verify source ↗
Matumizi
AI-assisted research summary: This section says the law applies in Tanzania Mainland and Tanzania Zanzibar for presidential and parliamentary elections, and in Tanzania Mainland for councilor elections.
2. Sheria hii itatumika Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar kwa Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano, na kwa uchaguzi wa Madiwani kwa Tanzania Bara. - 3 Verify source ↗
4. Kanuni, maelekezo na notisi
AI-assisted research summary: Sehemu hii inaeleza maana ya maneno na istilahi mbalimbali zinazotumika katika Sheria hii.
3.-(1) Katika Sheria hii, isipokuwa kama muktadha utahitaji vinginevyo- “afisa mwandikishaji” maana yake ni mtu aliyeteuliwa chini ya kifungu cha 7 na inajumuisha afisa mwandikishaji msaidizi; 10 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Sura ya 258 “chama cha siasa” maana yake ni chama cha siasa kilichosajiliwa chini ya Sheria ya Vyama vya Siasa; “Daftari” maana yake ni Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililoanzishwa chini ya kifungu cha 12; “Daftari la Awali la Wapiga Kura” maana yake ni daftari lililoanzishwa chini ya kifungu cha 11; “dhamana ya gharama” maana yake ni kiasi cha fedha kinacholipwa mahakamani na mlalamikaji kabla shauri lake halijapangwa kusikilizwa; “Diwani” maana yake ni diwani aliyechaguliwa katika kata na inajumuisha madiwani wanawake wa viti maalumu; “elimu ya mpiga kura” maana yake ni usambazaji wa taarifa zinazohusiana na mchakato na taratibu za uchaguzi; “eneo la uchaguzi” maana yake- jimbo (a) kwa uchaguzi wa Mbunge, ni eneo au iliyogawanywa kwa sehemu ya mujibu wa kifungu cha 5(1), (2) na (3); na (b) kwa uchaguzi wa Diwani, ni kata iliyotangazwa kwa mujibu wa kifungu cha 5(4); “Halmashauri” maana yake- Sura ya 287 na 288 (a) kuhusiana na wilaya, halmashauri ya wilaya; (b) kuhusiana na jiji, halmashauri ya jiji; (c) kuhusiana na manispaa, halmashauri ya manispaa; (d) kuhusiana na mji, halmashauri ya mji; iliyoanzishwa au kuchukuliwa kuanzishwa chini ya Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji); “Jaji” maana yake ni Jaji wa Mahakama ya Rufani au Mahakama Kuu; “jimbo” maana yake ni jimbo la uchaguzi kwa madhumuni ya uchaguzi wa Mbunge; “kadi ya mpiga kura” maana yake ni kadi iliyotolewa chini ya masharti ya Sheria hii ikithibitisha 11 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Sura ya 287 na 288 Sura ya 287 na 288 kwamba mtu aliyetajwa katika kadi hiyo ameandikishwa kuwa mpiga kura; “kata” maana yake ni mgawanyo wa mamlaka katika mamlaka za serikali za mitaa kwa mujibu wa masharti ya Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji); “Katiba” maana yake ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977; “kipindi cha kampeni” kuhusu uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, maana yake ni kipindi chote kuanzia mara baada ya siku ya uteuzi mpaka siku kabla ya siku ya uchaguzi; “kituo cha kupigia kura” maana yake ni kituo kilichobainishwa chini ya masharti ya kifungu cha 69; “kufunga upigaji kura” maana yake ni muda wa mwisho wa kupiga kura katika kituo cha kupigia kura kuhusiana na uchaguzi wowote; “mamlaka ya serikali za mitaa” maana yake ni mamlaka ya Wilaya iliyoanzishwa chini ya Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) au mamlaka ya Mji iliyoanzishwa chini ya Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji); “Mbunge” maana yake ni Mbunge wa jimbo na inajumuisha Wabunge wanawake wa viti maalumu; “mgombea” maana yake ni mtu anayegombea katika uchaguzi wa Rais au Wabunge au Madiwani; “Mgombea wa Urais” maana yake ni mtu aliyeteuliwa na chama cha siasa kugombea kiti cha Rais; “mjumbe” maana yake ni diwani aliyechaguliwa katika mamlaka ya serikali za mitaa na inajumuisha madiwani wanawake viti maalumu; “mkazi wa kawaida” maana yake ni mtu anayeishi kwa muda mrefu au mfupi katika eneo la uchaguzi kwa madhumuni ya makazi kama sehemu ya utaratibu wa kawaida wa maisha yake kwa wakati huo: 12 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Sheria Na. 2 ya 2024 Isipokuwa kwamba- (a) mtu hatahesabiwa kuwa mkazi wa kawaida katika eneo la uchaguzi kwa sababu anamiliki au kuhodhi nyumba ya kuishi katika eneo hilo; (b) mbunge wa jimbo hataacha kuwa mkazi wa kawaida katika jimbo husika, ikiwa sababu ya kutokuwepo kwake katika eneo la jimbo inahusiana na utekelezaji wa majukumu yake; na (c) mtu ambaye ni mgonjwa katika taasisi yoyote inayotoa huduma ya matibabu kwa wagonjwa au ambaye amefungwa gerezani au yuko chini ya ulinzi mwengine kisheria mahali popote, hatachukuliwa kwa sababu hiyo kuwa mkazi wa kawaida katika eneo husika; “Mkurugenzi wa Uchaguzi” maana yake ni mtu aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi kwa mujibu wa masharti ya Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na itajumuisha mtu ambaye kwa kipindi hicho anatekeleza ya Mkurugenzi wa yoyote majukumu Uchaguzi; “mpiga kura” maana yake ni mtu yeyote mwenye sifa za kupiga kura katika uchaguzi kwa mujibu wa masharti ya Sheria hii; “msimamizi msaidizi wa kituo” maana yake ni mtu aliyeteuliwa kuwa msimamizi msaidizi wa kituo cha kupigia kura chini ya masharti ya kifungu cha 76(b); “msimamizi wa kituo” maana yake ni mtu aliyeteuliwa chini ya masharti ya kifungu cha 76(c) kuwa msimamizi mkuu wa kituo cha kupigia kura; “msimamizi wa uchaguzi” maana yake ni mtu aliyeteuliwa chini ya kifungu cha 6 na inajumuisha msimamizi msaidizi wa uchaguzi; “mwangalizi” maana yake ni mwangalizi wa ndani au wa kimataifa aliyesajiliwa na Tume; “Mwenyekiti” maana yake ni Mwenyekiti aliyeteuliwa 13 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Sheria Na. 2 ya 2024 chini ya Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na inajumuisha Makamu Mwenyekiti au mtu yeyote kwa wakati huo atakayekuwa anatekeleza majukumu ya Mwenyekiti; “mtendaji wa uchaguzi” inajumuisha mratibu wa uchaguzi wa mkoa, msimamizi wa uchaguzi, msimamizi msaidizi wa uchaguzi, afisa uchaguzi, msimamizi wa kituo, msimamizi msaidizi wa kituo, mratibu wa uandikishaji mkoa, afisa mwandikishaji msaidizi, mwandishi msaidizi, mwendeshaji wa kifaa cha bayometriki, karani mwongozaji yeyote atakayeteuliwa kwa ajili ya kutekeleza majukumu ya Tume; na mtu mwingine mwandikishaji, afisa “Sheria” maana yake ni Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani; “sifa” au “kuwa na sifa” maana yake ni- (a) inapotumika kwa mtu anayedai kuwa na sifa za kuandikishwa kuwa mpiga kura, ana sifa zinazostahili au sifa za kuwa mpiga kura; (b) inapotumika kwa mtu anayedai kuwa na sifa za kuwa mgombea wa uchaguzi wa kiti cha Rais, ana sifa au anastahili kuwa mgombea wa kiti cha Rais; (c) inapotumika kwa mtu anayedai kuwa anastahili kuwa mgombea katika uchaguzi wa Mbunge, ana sifa au anastahili kuwa jimbo mgombea wa ubunge katika linalohusika; (d) inapotumika kwa mtu anayedai kuwa anastahili kuwa mgombea katika uchaguzi wa diwani, ana sifa au anastahili kuwa mgombea wa uchaguzi katika uchaguzi wa diwani katika kata husika; “siku ya uchaguzi” maana yake ni siku iliyopangwa chini ya kifungu cha 68 au siku yoyote mbadala wa siku hiyo kwa mujibu wa masharti ya kifungu hicho; 14 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 “siku ya uteuzi” maana yake ni siku iliyopangwa kuwa siku ya uteuzi wa wagombea; “Tume” maana yake ni Tume Huru ya Taifa ya iliyoanzishwa kwa mujibu wa Uchaguzi Katiba; “uchaguzi” maana yake- (a) iwapo ni kumchagua Rais, ni uchaguzi wa Rais; (b) iwapo ni kumchagua Mbunge, ni uchaguzi wa Mbunge na utajumuisha uchaguzi mdogo; na (c) iwapo ni kumchagua Diwani, ni uchaguzi wa Diwani na utajumuisha uchaguzi mdogo; “uchaguzi unaoshindaniwa” maana yake ni uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mbunge katika jimbo au Diwani katika kata ambapo kuna wagombea zaidi ya nafasi zilizo wazi; “Uchaguzi wa Rais” maana yake ni uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano; “uteuzi” maana yake ni uteuzi wa wagombea kwa ajili ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani na utajumuisha uteuzi wa wabunge na madiwani wanawake wa viti maalumu; “wakala wa kuhesabu kura” maana yake ni mtu aliyeteuliwa kuwa wakala wa kuhesabu kura chini ya masharti ya kifungu cha 91; “wakala wa upigaji kura” maana yake ni mtu aliyeteuliwa kuwa wakala wa upigaji kura chini ya masharti ya kifungu cha 77; na “Waziri” maana yake ni Waziri mwenye dhamana ya masuala ya uchaguzi.
Part
sehemu ya
- 4 Verify source ↗
Kanuni, maelekezo na notisi
AI-assisted research summary: Tume inaweza kuandaa au kutoa kanuni, maelekezo na notisi; zitaonekana kuwa halali zikisainiwa na Mwenyekiti wa Tume au Mkurugenzi wa Uchaguzi.
4. Kanuni, maelekezo na notisi zote ambazo Tume ina mamlaka ya kuandaa au kutoa zitachukuliwa kuwa zimeandaliwa au zimetolewa kihalali endapo zitaandaliwa au zitatolewa zikiwa na saini ya Mwenyekiti wa Tume au Mkurugenzi wa Uchaguzi. 15 Kanuni, maelekezo na notisi Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Maeneo ya uchaguzi - 5 Verify source ↗
Maeneo ya uchaguzi
AI-assisted research summary: Tume lazima igawanye kila jimbo katika maeneo ya uchaguzi na ichapishe notisi ya kuyataja katika Gazeti la Serikali. Inaweza pia kubadili idadi na maeneo ya uchaguzi na kutangaza mabadiliko au mabadiliko ya eneo baada ya mipaka kubadilishwa.
5.-(1) Tume itagawa kila jimbo katika maeneo ya uchaguzi na itachapisha notisi katika Gazeti la Serikali, itakayoainisha maeneo hayo ya uchaguzi. ya jimbo (2) Endapo mipaka lolote itabadilishwa kwa mujibu wa Ibara ya 74(6)(c) ya Katiba au kwa mazingira yoyote ambayo Tume itaona inafaa, Tume inaweza kubadili idadi na maeneo ya uchaguzi ndani ya jimbo na baada ya mabadiliko hayo, Tume itachapisha notisi katika Gazeti la Serikali itakayoainisha mabadiliko. Sura ya 287 na 288 Uteuzi wa wasimamizi wa uchaguzi na watendaji wengine (3) Endapo kutokana na kuanzishwa kwa jimbo au mabadiliko katika mipaka ya jimbo, eneo ambalo lilikuwa ni eneo la uchaguzi katika jimbo moja lote lipo katika jimbo lingine, Tume inaweza kutangaza kuwa eneo hilo litakoma kuwa eneo la uchaguzi katika jimbo lililotajwa awali na kuwa eneo la uchaguzi katika jimbo lililopo. (4) Endapo Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa ataanzisha kata kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) au Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji), kata hiyo itakuwa ni kata kwa madhumuni ya uchaguzi wa madiwani chini ya Sheria hii. - 6 Verify source ↗
Uteuzi wa wasimamizi wa uchaguzi na watendaji wengine
AI-assisted research summary: Tume inaweza kuteua wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi, na wasimamizi hao lazima waape siri na kutoa tamko la kujitoa au kutokuwa mwanachama wa chama cha siasa kabla ya kuanza kazi.
6.-(1) Tume inaweza kumteua mtumishi wa umma mwandamizi kuwa msimamizi wa uchaguzi kwa madhumuni ya kuendesha uchaguzi katika jimbo au kata na msimamizi huyo wa uchaguzi anaweza kuwa msimamizi wa uchaguzi kwa jimbo au kata zaidi ya moja. (2) Tume inaweza kuteua mtu kutoka miongoni mwa watumishi wa umma, kwa jina au nafasi aliyonayo katika ofisi, kuwa msimamizi msaidizi wa uchaguzi kwa madhumuni ya kuendesha uchaguzi katika jimbo au kata. (3) Kwa madhumuni ya vifungu vidogo vya (1) na (2), mtu atakuwa na sifa ya kuteuliwa kuwa msimamizi wa uchaguzi au msimamizi msaidizi wa uchaguzi endapo katika miaka mitano kabla ya uchaguzi husika- 16 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 (a) hajawahi kutiwa hatiani katika shauri la nidhamu au kosa jinai na kuadhibiwa kwa kifungo kinachozidi miezi sita; na lolote la (b) hajawahi kuwa kiongozi wa chama cha siasa. (4) Tume itatangaza majina ya watu walioteuliwa kuwa wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali. (5) Bila kuathiri masharti mengine ya Sheria hii, Tume inaweza kumteua mtu yeyote kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu ya Tume yanayohusiana na mchakato wa uchaguzi. (6) Msimamizi wa uchaguzi, kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 76 na maelekezo ya Mkurugenzi wa Uchaguzi, anaweza kuteua watendaji kwa idadi inayohitajika kwa madhumuni ya kuendesha uchaguzi katika jimbo au kata. (7) Kila msimamizi wa uchaguzi na msimamizi msaidizi wa uchaguzi, kabla ya kuanza kutekeleza majukumu ya ofisi hiyo, ataapa kiapo cha kutunza siri na kutoa tamko la kujitoa au kutokuwa mwanachama wa chama cha siasa, mbele ya Hakimu kwa kutumia fomu itakayoainishwa. - 7 Verify source ↗
Maafisa waandikishaji
AI-assisted research summary: Watawala fulani wa serikali ya mtaa na wilaya ni maafisa waandikishaji wa wapiga kura, na Tume inaweza kuwateua wengine kwa nafasi hiyo; maafisa waandikishaji na watendaji wanaoteuliwa lazima waape kiapo cha siri na kutoa tamko kuhusu uanachama wa chama cha siasa.
7.-(1) Kwa madhumuni ya uandikishaji wa wapiga kura chini ya Sheria hii, kila Mkurugenzi wa Jiji, Mkurugenzi wa Manispaa, Mkurugenzi wa Mji na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya atakuwa ni afisa mwandikishaji kwa madhumuni ya kuandikisha wapiga kura katika jimbo au kata na anaweza kuwa afisa mwandikishaji wa jimbo zaidi ya moja. (2) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (1), Tume inaweza kuteua mtu kwa kuzingatia nafasi aliyonayo katika ofisi au kwa jina kutoka miongoni mwa watumishi wa umma kuwa mratibu wa uandikishaji wa mkoa au afisa mwandikishaji msaidizi kwa ajili ya kuandikisha wapiga kura kama itakavyoona inafaa. 17 Maafisa waandikishaji Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 (3) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (1), pale ambapo mazingira yanahitaji na kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, Tume inaweza kuteua mtu yeyote kutoka katika ofisi ya umma kwa jina au kwa kuzingatia nafasi aliyonayo katika ofisi kuwa afisa mwandikishaji katika jimbo au kata yoyote badala ya yule aliyetajwa katika kifungu kidogo cha (1) na endapo mtu huyo anateuliwa, Mkurugenzi wa Jiji, Mkurugenzi wa Manispaa, Mkurugenzi wa Mji au Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya atakoma kuwa afisa mwandikishaji katika jimbo au kata husika. (4) Afisa mwandikishaji, kwa kuzingatia maelekezo ya Mkurugenzi wa Uchaguzi, anaweza kuteua idadi ya watendaji kama watakavyohitajika kwa madhumuni ya kuandikisha wapiga kura katika jimbo au kata. (5) Watendaji watakaoteuliwa na afisa mwandikishaji chini ya kifungu kidogo cha (4) wataapa kiapo cha kutunza siri na kutoa tamko la kujitoa au kutokuwa wanachama wa chama cha siasa, mbele ya afisa mwandikishaji kwa kutumia fomu itakayoainishwa. (6) Kila mratibu wa uandikishaji wa mkoa, afisa mwandikishaji au afisa mwandikishaji msaidizi kabla ya kuanza kutekeleza majukumu ya ofisi hiyo, wataapa kiapo cha kutunza siri na kutoa tamko la kujitoa au kutokuwa wanachama wa chama cha siasa, mbele ya Hakimu kwa kutumia fomu itakayoainishwa. (7) Afisa mwandikishaji atawajibika katika masuala yote yanayohusu uandikishaji wa wapiga kura katika eneo la mamlaka yake. - 8 Verify source ↗
Uteuzi wa waratibu wa uchaguzi
AI-assisted research summary: Wakati wa uchaguzi, Tume inaweza kumteua mratibu wa uchaguzi wa mkoa. Pia, mtu mwenye wadhifa katika ofisi ya umma akihitajika na mamlaka husika, lazima asaidi au atekeleze jukumu lingine ili kuwezesha uendeshaji wa uchaguzi.
8.-(1) Wakati wa uchaguzi, Tume inaweza kumteua mtu kwa kuzingatia nafasi aliyonayo katika ofisi au kwa jina kwa kila mkoa, kuwa mratibu wa uchaguzi wa mkoa kwa ajili ya kuratibu taarifa, upatikanaji wa vifaa, rasilimali na masuala mengine muhimu kwa ajili ya kuendesha uchaguzi kwa ufanisi katika majimbo ya uchaguzi na kata katika mkoa 18 Uteuzi wa waratibu wa uchaguzi Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 husika. (2) Mtu yeyote mwenye wadhifa katika ofisi ya umma, atakapohitajika na Tume, Mkurugenzi wa Uchaguzi, msimamizi wa uchaguzi, msimamizi msaidizi wa uchaguzi au mratibu wa uchaguzi wa mkoa, atasaidia au atatekeleza jukumu lingine lolote kama itakavyohitajika kwa madhumuni ya kuwezesha uendeshaji wa uchaguzi. SURA YA PILI UANDIKISHAJI WA WAPIGA KURA SEHEMU YA KWANZA SIFA NA KUKOSA SIFA ZA KUANDIKISHWA KUWA MPIGA KURA NA KUPIGA KURA Sifa za kuandikishwa
Part
SEHEMU YA KWANZA
- 9 Verify source ↗
Sifa za kuandikishwa
AI-assisted research summary: Some Tanzanian citizens aged 18 or older, and not disqualified under this law or another law, are entitled to be registered as voters.
9.-(1) Mtu yeyote ambaye ni raia wa Tanzania aliyetimiza umri wa miaka kumi na nane na ambaye hajapoteza sifa chini ya Sheria hii au sheria nyingine yoyote, atastahili kuandikishwa kuwa mpiga kura chini ya masharti ya Sheria hii. (2) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (1), na kwa kuzingatia uthibitisho wa umri, Mtanzania yeyote ambaye hajapoteza sifa chini ya Sheria hii au sheria nyingine yoyote, ambaye wakati au kabla ya tarehe ya uchaguzi atakuwa ametimiza umri wa miaka kumi na nane, atastahili kuandikishwa kuwa mpiga kura chini ya Sheria hii. Kukosa sifa za kuandikishwa - 10 Verify source ↗
Kukosa sifa za kuandikishwa
AI-assisted research summary: Mtu hana sifa ya kuandikishwa kuwa mpiga kura ikiwa ana kiapo kwa nchi nyingine, hana akili timamu kwa uthibitisho wa sheria, amehukumiwa kwa kosa lenye adhabu ya kifo au kifungo kinachozidi miezi sita, au amepoteza sifa chini ya sheria za uchaguzi.
10.-(1) Mtu hatakuwa na sifa ya kuandikishwa au hataandikishwa kuwa mpiga kura chini ya Sheria hii ikiwa- (a) yuko chini ya kiapo cha utii kwa nchi nyingine tofauti na Tanzania; (b) katika sheria yoyote inayotumika Tanzania, imethibitika kuwa hana akili timamu au amewekwa kizuizini kama mhalifu mwenye ugonjwa wa akili au amewekwa kuzuizini kwa ridhaa ya Rais; (c) ametiwa hatiani kwa kosa ambalo adhabu 19 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 yake ni kifo au anatumikia kifungo kwa kosa ambalo adhabu yake inazidi miezi sita au kama iliyotolewa na mahakama ilivyobadilishwa yenye dhamana; au na mamlaka (d) amepoteza sifa za kuandikishwa kuwa mpiga kura chini ya masharti ya Sheria hii inayotumika au sheria nyingine yoyote kuhusu makosa yanayohusiana na uchaguzi wowote. (2) Kwa madhumuni ya aya (c) ya kifungu kidogo cha (1)- (a) adhabu mbili au zaidi zinazopaswa kutumikiwa kwa kufuatana zitachukuliwa iwapo hakuna kuwa ni adhabu tofauti adhabu moja kati ya hizo inayozidi miezi sita, na endapo mojawapo ya adhabu hizo inazidi miezi sita, zitahesabika kuwa ni adhabu moja; na (b) hakuna kitakachozingatiwa kwa adhabu ya kifungo iliyotolewa kama mbadala wa, au kwa ukiukwaji wa malipo ya faini. (3) Endapo mtu yeyote aliyeandikishwa chini ya Sheria hii atapoteza sifa za kuandikishwa kuwa mpiga kura, jina lake litafutwa katika Daftari: Isipokuwa kwamba, jina halitafutwa katika Daftari, ila kwa mujibu wa masharti ya Sehemu ya Tatu na Nne ya Sura hii au kwa taarifa ya mahakama kuwa mtu huyo ametiwa hatiani kwa vitendo vinavyomsababisha kupoteza sifa za kuandikishwa au kupiga kura. (4) Mtu hataandikishwa kuwa mpiga kura katika jimbo au kata zaidi ya moja au katika eneo la uchaguzi zaidi ya moja katika jimbo au kata. - 11 Verify source ↗
Daftari la Awali la Wapiga Kura
AI-assisted research summary: Tume lazima itunge Daftari la Awali la Wapiga Kura kwa ajili ya Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
11.-(1) Kwa madhumuni ya utayarishaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, Tume itaandaa Daftari la Awali la Wapiga Kura. (2) Daftari la Awali la Wapiga Kura litatumika kwa ajili ya- 20 Daftari la Awali la Wapiga Kura Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Daftari la Kudumu la Wapiga Kura (a) uwekaji wazi ili kukaguliwa na umma; (b) marekebisho yanayohusu kubadilika kwa makazi au taarifa nyingine zozote za mpiga kura; (c) uwekaji pingamizi dhidi ya uandikishwaji wa mpiga kura yeyote; (d) kuingiza au kufuta jina la mpiga kura katika Daftari; na (e) kufanya masahihisho au marekebisho kama itakavyohitajika chini ya Sheria hii. - 12 Verify source ↗
Daftari la Kudumu la Wapiga Kura
AI-assisted research summary: Sehemu hii inaweka Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kumpa Mkurugenzi wa Uchaguzi jukumu la kuliweka, kulitunza na kuliboresha.
12.-(1) Kwa kuzingatia kifungu hiki na kwa madhumuni ya Sheria hii, kutakuwa na Daftari la Kudumu la Wapiga Kura la Jamhuri ya Muungano ambalo litakuwa katika sehemu, sura au mgawanyo mwingine kama Tume itakavyoamua. (2) Mkurugenzi wa Uchaguzi ataweka, atatunza na kuboresha Daftari lililoanzishwa chini ya kifungu kidogo cha (1). (3) Daftari litakuwa na majina ya watu wote ambao wameandikishwa kuwa wapiga kura katika eneo la uchaguzi. (4) Daftari litaonesha bayana kwa kila mpiga kura aliyeandikishwa, namba ya kadi ya mpiga kura iliyotolewa, hali ya ulemavu, ikiwa ipo, jinsi na anwani ya makazi ya kawaida ya mpiga kura na taarifa nyingine kama Tume itakavyoelekeza. (5) Tume itasimamia utunzaji wa Daftari lililoanzishwa chini ya kifungu kidogo cha (1). (6) Mkurugenzi wa Uchaguzi anaweza kutoa maelekezo kwa afisa afisa mwandikishaji mwandikishaji msaidizi kuhusu masuala yanayohusu uandikishaji wa wapiga kura, yaliyomo katika Daftari au masuala mengine yanayohusiana na hayo. au Uandikishaji wa wapiga kura Tanzania Zanzibar - 13 Verify source ↗
Uandikishaji wa wapiga kura Tanzania Zanzibar
AI-assisted research summary: Tume lazima imwandikishe mtu yeyote aliye Tanzania Zanzibar na anayestahili kuandikishwa kuwa mpiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Rais.
13.-(1) Bila kujali masharti ya kifungu cha 12 na kwa madhumuni ya uendeshaji wa uchaguzi wa Rais na Wabunge kwa upande wa Tanzania Zanzibar, sheria inayohusu uandikishaji wa wapiga kura na daftari la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi katika 21 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Mahali pa kupigia kura na kukosa sifa za kupiga kura la Wawakilishi la Zanzibar, pamoja na Baraza mabadiliko yatakayofaa, itakuwa ndiyo sheria ya uandikishaji wa wapiga kura na daftari la wapiga kura Tanzania Zanzibar kwa madhumuni ya Sheria hii. (2) Tume itamwandikisha mtu yeyote aliyepo Tanzania Zanzibar ambaye anastahili kuandikishwa kuwa mpiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano. - 14 Verify source ↗
Mahali pa kupigia kura na kukosa sifa za kupiga kura
AI-assisted research summary: Registered voters may vote in their constituency and assigned polling station, but polling officials must verify identity before allowing a vote.
14.-(1) Kwa kuzingatia masharti ya Sheria hii, mtu aliyeandikishwa kuwa mpiga kura katika eneo la uchaguzi atastahili kupiga kura katika lolote uchaguzi wowote katika eneo hilo la uchaguzi na mtu huyo atastahili kupiga kura katika kituo cha kupigia kura alichopangiwa katika eneo hilo la uchaguzi. (2) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (1), msimamizi wa kituo au msimamizi msaidizi wa kituo chochote cha kupigia kura hatamruhusu mtu yeyote kupiga kura katika kituo hicho cha kupigia kura isipokuwa kama mtu huyo atamthibitishia msimamizi wa kituo au, kwa kadiri itakavyokuwa, msimamizi msaidizi wa kituo, kuwa yeye ndiye mpiga kura kama kadi ya mpiga kura anavyodai kwa kuonesha iliyotolewa kwake au uthibitisho mwingine wa utambulisho wake kama Mkurugenzi wa Uchaguzi atakavyoelekeza kwa wakati huo kuwa ni uthibitisho wa kutosha wa utambulisho wa mtu anayedai kuwa anastahili kupiga kura. (3) Mtu aliyeandikishwa kuwa mpiga kura chini ya Sheria hii hatastahili kupiga kura katika uchaguzi wowote ikiwa mazingira yatajitokeza kuhusiana na mtu huyo ambayo, kama asingekuwa ameandikishwa, yangesababisha mtu huyo kupoteza sifa za kuandikishwa chini ya Sheria hii. (4) Bila kujali masharti mengine ya Sheria hii, Mkurugenzi wa Uchaguzi yeyote aliyeidhinishwa kwa niaba yake anaweza, kwa hati aliyoisaini, kumuidhinisha mpiga kura aliyeandikishwa ambaye ni mgombea wa uchaguzi katika jimbo au kata, kupiga kura kwenye uchaguzi wa jimbo au kata au mtu 22 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 hiyo katika kituo kilichoainishwa kwenye hati hiyo, iwe mgombea huyo ameandikishwa au hajaandikishwa kuwa mpiga kura kwenye kituo hicho cha kupigia kura. (5) Bila kujali masharti mengine yoyote ya Sheria hii, endapo mpiga kura aliyeandikishwa katika eneo la uchaguzi ataajiriwa kuwa msimamizi wa uchaguzi, msimamizi wa kituo, msimamizi msaidizi wa kituo, karani mwongozaji, mlinzi wa kituo au katika wadhifa mwingine wowote katika kituo cha kupigia kura katika eneo hilo la uchaguzi tofauti na kituo cha kupigia kura alichopangiwa, Mkurugenzi wa Uchaguzi au mtu mwingine yeyote aliyeidhinishwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi anaweza, kupitia hati aliyoisaini, kumuidhinisha mpiga kura huyo kupiga kura katika kituo kingine chochote cha kupigia kura katika eneo hilo la uchaguzi, na kituo hicho, kwa madhumuni ya Sheria hii, kitachukuliwa kuwa kituo cha kupigia kura alichopangiwa mpiga kura huyo. (6) Mtu ambaye anatumikia adhabu ya kifungo anaweza, kwa kuzingatia masharti ya Sheria hii, kuandikishwa kuwa mpiga kura au kupiga kura katika sheria uchaguzi inayosimamia kifungo cha mtu huyo: ataruhusiwa iwapo kwa tu Kubadili jina Isipokuwa kwamba, hakuna chochote katika kifungu hiki kidogo kitakachotafsiriwa kumuidhinisha mtu huyo kupiga kura katika kituo chochote tofauti na kituo alichopangiwa. - 15 Verify source ↗
Kubadili jina
AI-assisted research summary: A registered voter whose name changes after registration may vote using the registered name, if they still meet voting qualifications under section 14.
15. Mtu aliyeandikishwa kuwa mpiga kura ambaye jina lake limebadilika kutokana na ndoa au kwa sababu nyingine yoyote baada ya kuandikishwa, iwapo hajapoteza sifa za kupiga kura chini ya kifungu cha 14, atastahili kupiga kura kwa jina ambalo ameandikishwa. 23 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Muda wa uandikishaji Wakala wa uandikishaji SEHEMU YA PILI UANDIKISHAJI WA WAPIGA KURA - 32 Verify source ↗
Uteuzi wa wagombea wa kiti cha Rais na Makamu wa Rais
AI-assisted research summary: A registered political party intending to contest the presidential election must submit the names of its presidential and vice-presidential candidates to the Commission.
32. Kila unapofanyika uchaguzi wa Rais, kila chama cha siasa kilichosajiliwa na kinachokusudia kushiriki katika uchaguzi wa Rais kitawasilisha kwa Tume jina la mgombea wa kiti cha Rais na jina la mgombea wa nafasi ya Makamu wa Rais wa chama hicho. Idadi ya wadhamini Uteuzi wa mgombea wa kiti cha Rais - 33 Verify source ↗
34. Uteuzi wa mgombea wa kiti cha Rais
AI-assisted research summary: A person can be nominated as a valid presidential candidate only if they are sponsored in writing by registered voter sponsors meeting the stated regional minimums, and those sponsors are to be verified by the relevant District Election Supervisor.
33.-(1) Ili kuweza kuteuliwa kuwa mgombea halali wa kiti cha Rais, mtu anapaswa kudhaminiwa kwa maandishi na wadhamini walioandikishwa kuwa wapiga kura kwa madhumuni ya uchaguzi chini ya Sheria hii wasiopungua mia mbili kwa kila mkoa, angalau kwa mikoa kumi ya Jamhuri ya Muungano, kati ya hiyo angalau mikoa miwili kutoka Tanzania Zanzibar. (2) Kwa kuzingatia masharti ya kifungu kidogo cha (1), wadhamini wa mgombea wa nafasi ya kiti cha Rais na nafasi ya Makamu wa Rais watathibitishwa na Msimamizi wa Uchaguzi wa jimbo ambalo wadhamini husika wameandikishwa. - 34 Verify source ↗
Uteuzi wa mgombea wa kiti cha Rais
AI-assisted research summary: Section 34 requires presidential candidates to file nomination forms by the deadline and with the required attachments, and limits each person to sponsoring only one presidential candidate unless a stated exception applies.
34.-(1) Tume itatoa fomu za uteuzi kwa mgombea wa kiti cha Rais aliyependekezwa na chama cha siasa au mpiga kura aliyeidhinishwa na chama cha siasa kadiri itakavyoelekezwa na Tume. kwa maandishi idadi kwa na (2) Kila mgombea wa kiti cha Rais atawasilisha fomu za uteuzi kwa utaratibu na mahali kadiri Tume itakavyoelekeza, si zaidi ya saa kumi kamili alasiri ya 37 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 siku ya uteuzi. (3) Fomu za uteuzi zitawasilishwa zikiwa na maelezo yafuatayo: (a) jina, jinsi, hali ya ulemavu, ikiwa ipo na anwani ya mgombea wa kiti cha Rais na cha Makamu wa Rais ambaye atakuwa ni mgombea mwenza; (b) tamko la mgombea kwamba yupo tayari na ana sifa za kuwa mgombea katika uchaguzi; (c) kiapo cha mgombea wa kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano kitakachojazwa na kusainiwa mbele ya Jaji; (d) majina na anwani za wadhamini; (e) namba za kadi za kupigia kura za wadhamini; na (f) uthibitisho wa msimamizi wa uchaguzi kuhusu wadhamini kutoka katika jimbo husika: Isipokuwa kwamba, ikiwa Tume itaona kuna sababu za msingi za mgombea kushindwa kuwasilisha mwenyewe fomu za uteuzi, kiongozi wa chama kilichomteua anaweza kuwasilisha fomu hizo kwa niaba yake. (4) Kila fomu ya uteuzi itaambatishwa na- (a) idadi ya picha za mgombea kama Tume itakavyoelekeza, zilizopigwa si zaidi ya miezi mitatu kabla ya siku ya uteuzi; na (b) taarifa binafsi yoyote inayomhusu mgombea kama itakavyohitajika kutolewa itakayokuwa na kanuni kwa namna imeelekezwa. (5) Endapo, kwa vyovyote vile fomu ya uteuzi haijaambatishwa na nyaraka zilizoainishwa katika (4), uteuzi wa mgombea kifungu kidogo cha utachukuliwa kuwa ni batili: Isipokuwa kwamba, Tume, katika mazingira yoyote mahususi na kama itaona kuna sababu ya kufanya hivyo, inaweza kuelekeza kuwa fomu ya uteuzi ikubaliwe kuwa halali bila kujali kuwa fomu ikiwa hiyo haikuambatishwa na nyaraka zozote 38 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 nyaraka zinazohusika zitawasilishwa kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi ndani ya muda mwingine kama ambavyo Tume inaweza kuruhusu. (6) Kwa madhumuni ya Sehemu hii, “siku ya uteuzi” maana yake ni siku iliyotangazwa na Tume kuwa siku ya mwisho ya kupokea majina ya watu wenye nia ya kugombea kiti cha Rais. (7) Tume, mapema iwezekanavyo itabandika nakala ya fomu ya uteuzi katika sehemu ya wazi inayoonekana nje ya ofisi yake. (8) Mtu hatamdhamini mgombea zaidi ya mmoja wa kiti cha Rais na iwapo msimamizi wa uchaguzi ametoa hati chini ya kifungu kidogo cha (3)(f) kwa ajili ya udhamini wa mgombea mmoja, atakataa kutoa hati ya udhamini wa mtu huyo kwa mgombea mwingine katika uchaguzi mmoja: Isipokuwa kwamba, mtu hatazuiwa kusaini fomu ya uteuzi kwa sababu tu amekwisha saini fomu ya mgombea aliyefariki au aliyejitoa kabla ya kuwasilisha fomu ya uteuzi ya mwanzo. (9) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (8), iwapo mdhamini atamdhamini mgombea zaidi ya mmoja katika uchaguzi mmoja na hati zimetolewa chini ya kifungu kidogo cha (3)(f) kwa ajili ya uandikishwaji wa mtu huyo, udhamini wa wagombea wote wawili utakuwa ni halali. yeyote (10) Mtu kujua anamdhamini mgombea zaidi ya mmoja anatenda kosa, na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyozidi shilingi laki mbili. ambaye kwa (11) Endapo msimamizi wa uchaguzi ataridhika kuwa mtu yeyote ametenda kosa chini ya kifungu kidogo cha (10), kwa amri iliyotolewa kwa idhini yake anaweza kufifilisha kosa na kuamuru mtu huyo kulipa kiasi cha fedha: Isipokuwa kwamba- (a) kiasi cha fedha hakitazidi kiasi cha juu cha faini iliyowekwa kwa kosa hilo; (b) mamlaka yaliyotolewa na kifungu hiki kidogo yatatumika kama mtu atakiri kwa maandishi 39 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kuwa ametenda kosa; na (c) msimamizi wa uchaguzi atatoa stakabadhi ya malipo kwa mtu aliyetoa kiasi hicho cha fedha. (12) Msimamizi wa uchaguzi, atakapoombwa na mgombea, au kwa niaba yake, kutoa hati kuhusu mdhamini aliyeandikishwa katika eneo la uchaguzi analohudumu, atatoa hati hiyo ipasavyo. (13) Endapo baada ya siku ya uteuzi, jina la mtu aliyemdhamini mgombea litafutwa katika Daftari katika eneo la uchaguzi husika, kufutwa huko hakutabatilisha udhamini wa mgombea. - 35 Verify source ↗
Dhamana
AI-assisted research summary: Mtu anayetaka kugombea urais lazima aweke dhamana katika ofisi ya Tume wakati wa kuwasilisha fomu za uteuzi, kwa kiasi kitakachoainishwa na kanuni.
35.-(1) Wakati wa kuwasilisha fomu za uteuzi kwa mujibu wa masharti mengine ya Sehemu hii, kila mgombea wa kiti cha Rais ataweka dhamana katika ofisi ya Tume ya kiasi cha fedha kitakachoainishwa katika kanuni. (2) Dhamana itakayowekwa na mgombea itataifishwa kwa Serikali ikiwa- Dhamana (b) idadi ya kura (a) mgombea wa kiti cha Rais atajitoa kugombea baada ya siku ya uteuzi; au alizopata baada ya kuhesabiwa katika uchaguzi ni chini ya moja ya kumi ya kura zote halali zilizopigwa, dhamana isipokuwa mgombea atafariki kabla ya uchaguzi. haitataifishwa kama hiyo (3) Endapo dhamana iliyowekwa haitataifishwa chini ya masharti ya kifungu kidogo cha (2), mapema iwezekanavyo baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa, dhamana hiyo itarejeshwa kwa mgombea wa kiti cha Rais au kulipwa kwa mwakilishi wake wa kisheria. Kukataa uteuzi wa mgombea wa kiti cha Rais Sura ya 278 - 36 Verify source ↗
Kukataa uteuzi wa mgombea wa kiti cha Rais
AI-assisted research summary: Tume inaweza kukataa kumteua mtu kuwa mgombea wa kiti cha Rais katika siku ya uteuzi ikiwa inaridhika kuwa mtu huyo ameondolewa sifa za kushiriki kwenye mchakato wa uteuzi chini ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi.
36. Tume inaweza, katika siku ya uteuzi, kukataa kumteua mtu kuwa mgombea wa kiti cha Rais iwapo itajiridhisha kuwa mtu huyo ameondolewa sifa za kushiriki katika mchakato wa uteuzi na Msajili wa Vyama vya Siasa kwa mujibu wa masharti ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi. 40 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Pingamizi dhidi ya uteuzi wa mgombea wa kiti cha Rais na Makamu wa Rais - 37 Verify source ↗
Pingamizi dhidi ya uteuzi wa mgombea wa kiti cha Rais na Makamu
AI-assisted research summary: Pingamizi dhidi ya uteuzi wa mgombea wa Rais au Makamu wa Rais linaweza kuwasilishwa kwa sababu zilizoelezwa, lakini lazima liwasilishwe kwa Tume ndani ya muda uliowekwa.
37.-(1) Pingamizi linaweza kuwekwa dhidi ya fomu ya uteuzi wa mgombea wa kiti cha Rais na Makamu wa Rais kutokana na sababu zote au yoyote kati ya sababu zifuatazo: (a) taarifa zilizotolewa kuhusu mgombea Sura ya 278 hazitoshelezi kumtambulisha; (b) fomu ya uteuzi haikidhi au haikuwasilishwa kwa mujibu wa masharti ya Sehemu hii; (c) ni dhahiri kutokana na yaliyomo kwenye fomu ya uteuzi kwamba mgombea hana sifa za kugombea; (d) masharti yaliyoainishwa katika kifungu cha 34(2) cha Sheria hii hayakutimizwa; na (e) masharti ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi hayakutimizwa. (2) Pingamizi dhidi ya fomu ya uteuzi halitakubaliwa isipokuwa kama limewasilishwa kwa Tume si zaidi ya saa kumi kamili alasiri ya siku inayofuatia siku ya uteuzi. (3) Pingamizi linaweza kuwekwa na mgombea mwingine, Msajili wa Vyama vya Siasa au isipokuwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, pingamizi chini ya kifungu kidogo cha (1)(e) ambalo linaweza kuwekwa na Msajili wa Vyama vya Siasa pekee, na litawekwa kwa maandishi na kusainiwa na mweka pingamizi na kubainisha sababu za pingamizi. (4) Tume, kabla ya kuamua juu ya uhalali wa pingamizi lolote na bila kuchelewa- (a) itamtaarifu mtu aliyewekewa pingamizi; na (b) itampa mtu huyo nafasi ya kusikilizwa. (5) Endapo Tume itatoa uamuzi kuhusiana na pingamizi lolote chini ya kifungu kidogo cha (3), itamjulisha kwa maandishi mgombea anayehusika kuhusu uamuzi na sababu za uamuzi huo. (6) Uamuzi wa Tume chini ya kifungu hiki utakuwa ni wa mwisho na hautahojiwa na mahakama yoyote. (7) Bila kujali masharti yoyote ya kifungu hiki, 41 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Mgombea pekee wa kiti cha Rais Kujitoa ugombea endapo Msajili wa Vyama vya Siasa ataweka pingamizi chini ya kifungu kidogo cha (3), pingamizi hilo litawasilishwa ndani ya siku kumi na nne baada ya siku ya uteuzi. - 38 Verify source ↗
Mgombea pekee wa kiti cha Rais
AI-assisted research summary: If there is only one valid nominated presidential candidate, the Commission must declare that person the sole candidate. That candidate is then put to a yes/no vote and is elected President only if they get more valid votes than all valid votes cast. If they do not, the Commission must announce another nomination day by Gazette notice.
38.-(1) Endapo kutakuwa na mgombea mmoja halali wa kiti cha Rais aliyeteuliwa, Tume itamtangaza mgombea huyo kuwa mgombea pekee wa kiti cha Rais. (2) Mgombea wa kiti cha Rais aliyetangazwa chini ya kifungu kidogo cha (1) atapigiwa kura ya ndio au hapana na atakuwa amechaguliwa kihalali kuwa Rais endapo atapata kura nyingi zaidi ya kura zote halali zilizopigwa. (3) Endapo mgombea pekee wa kiti cha Rais atashindwa kupata kura nyingi zaidi kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (2), Tume itatangaza siku nyingine ya uteuzi kwa ajili ya uchaguzi wa Rais kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali. - 39 Verify source ↗
Kujitoa ugombea
AI-assisted research summary: Mgombea wa urais anaweza kujitoa kwa taarifa ya maandishi iliyosainiwa na kuwasilishwa mwenyewe Tume, pamoja na nakala kwa Katibu Mkuu wa chama, kabla ya saa kumi kamili alasiri siku ya uteuzi.
39.-(1) Mgombea wa kiti cha Rais anaweza kujitoa ugombea kwa kutoa taarifa ya maandishi aliyoisaini na kuiwasilisha yeye mwenyewe Tume na nakala kwa Katibu Mkuu wa chama kilichomdhamini kabla ya saa kumi kamili alasiri siku ya uteuzi. (2) Kila taarifa ya kujitoa chini ya kifungu kidogo cha (1) itaambatishwa na tamko katika fomu itakayoainishwa, ambalo litajazwa na kusainiwa na mgombea mbele ya Jaji. (3) Kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (1), endapo mgombea atajitoa kugombea baada ya saa kumi kamili alasiri ya siku ya uteuzi, chama chake hakitaruhusiwa kuweka mgombea mwingine mbadala na dhamana iliyotolewa na mgombea itataifishwa. Kifo au kukosekana kwa wagombea - 40 Verify source ↗
Kifo au kukosekana kwa wagombea
AI-assisted research summary: The Commission must arrange a new nomination day, and in one case a new election day, if no valid candidate is nominated or if a presidential or vice-presidential candidate dies before the election ends.
40.-(1) Endapo- (a) baada ya saa kumi kamili alasiri ya siku ya uteuzi hakuna mgombea halali aliyeteuliwa, Tume, mapema iwezekanavyo kupitia notisi katika Gazeti la Serikali, itapanga siku 42 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 nyingine ya uteuzi; au (b) muda wowote baada ya saa kumi kamili alasiri ya siku ya uteuzi na kabla ya kumalizika kwa uchaguzi, mgombea yeyote wa kiti cha Rais au Makamu wa Rais atafariki, Tume, mapema iwezekanavyo kupitia notisi katika Gazeti la Serikali, itateua siku nyingine ya uteuzi si zaidi ya siku kumi na nne baada ya tarehe ya kifo ili kutoa muda kwa siasa kinachohusika kuteua mgombea mwingine wa kiti cha Rais au Makamu wa Rais, kadiri itakavyokuwa. chama cha (2) Endapo siku nyingine ya uteuzi itapangwa chini ya kifungu hiki, Tume itapanga siku nyingine ya uchaguzi wa Rais na taratibu husika zitaanza upya, isipokuwa kwamba hakutakuwa na uteuzi mpya utakaohitajika kwa wagombea wengine wa kiti cha Rais kama wapo. SEHEMU YA PILI TARATIBU ZA UCHAGUZI WA URAIS NA SIFA ZA MGOMBEA Siku ya uchaguzi wa Rais - 48 Verify source ↗
Sifa za wagombea katika uchaguzi wa ubunge
AI-assisted research summary: A person is not qualified to be a parliamentary election candidate or to be elected unless they meet the qualifications for election as a Member of Parliament under Article 67 of the Constitution.
48. Mtu hatakuwa na sifa ya kuwa mgombea katika uchaguzi wa Ubunge au kuchaguliwa kuwa isipokuwa kama atakuwa na sifa za Mbunge kuchaguliwa kuwa Mbunge kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 67 ya Katiba. Siku ya uteuzi SEHEMU YA PILI UTEUZI WA WAGOMBEA jimbo au - 56 Verify source ↗
Uchaguzi wa madiwani
AI-assisted research summary: Councilor elections are held every five years after the last election and whenever a new council is established, unless the new council’s establishment did not change parliamentary constituency boundaries.
56.-(1) Kutafanyika uchaguzi wa madiwani katika mamlaka za serikali za mitaa kila mwaka wa tano baada ya uchaguzi wa madiwani uliopita, na wakati wowote Halmashauri mpya inapoanzishwa. (2) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (1), uchaguzi wa madiwani hautafanyika pale ambapo uanzishwaji wa Hamashauri mpya haujabadilisha mipaka ya majimbo ya ubunge. (3) Uchaguzi wa madiwani wa mamlaka za serikali za mitaa utafanyika katika kila kata au kadiri itakavyokuwa, kwa kata ya mamlaka ya serikali za mitaa katika tarehe itakayotangazwa na Tume kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali. (4) Notisi itakayotolewa chini ya kifungu hiki itaainisha siku na saa ambayo wasimamizi wa uchaguzi wanaweza kupokea fomu za uteuzi wa wagombea wa uchaguzi katika kata yoyote ambayo notisi hiyo inahusika. (5) Uendeshaji wa kila uchaguzi utakuwa kwa mujibu wa maelekezo na usimamizi wa Tume katika eneo ambalo uchaguzi unafanyika. - 57 Verify source ↗
Uchaguzi mdogo
AI-assisted research summary: Tume lazima itangaze kiti cha diwani kuwa wazi ikipata taarifa ya maandishi kutoka kwa Waziri wa Serikali za Mitaa, na lazima iendeshe uchaguzi mdogo angalau mara mbili kwa mwaka kwa nafasi wazi za kata.
57.-(1) Tume itatangaza kiti cha diwani kuwa wazi mara itakapotaarifiwa kwa maandishi na Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa kuwa- (a) mjumbe amefariki au amejiuzulu; (b) mjumbe, kwa mujibu wa masharti ya au chini ya Sheria hii au Sheria nyingine yoyote, ameondolewa au ametangazwa kuwa hana uwezo wa kuwa au kuendelea kuwa mjumbe; (c) uchaguzi wa mjumbe umetangazwa kuwa batili; 54 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 (d) kiti cha mjumbe kinachukuliwa kuwa wazi chini ya Sheria hii; au (e) mjumbe amekoma kuwa mwanachama wa chama cha siasa ambacho kilimdhamini mjumbe huyo kuwa mgombea. (2) Kwa madhumuni ya kujaza nafasi wazi zilizojitokeza kwenye kata mbalimbali katika kalenda ya mwaka, Tume itaendesha uchaguzi mdogo angalau mara mbili kwa kila mwaka katika tarehe ambazo Tume itaainisha kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali. (3) Notisi chini ya kifungu hiki itaainisha siku na saa ambayo wasimamizi wa uchaguzi wanaweza kupokea fomu za uteuzi wa wagombea wa uchaguzi katika kata ambayo nafasi wazi imetokea. Uwakilishi katika kata na muda wa madiwani kuwa madarakani na - 58 Verify source ↗
Uwakilishi katika kata na muda wa madiwani kuwa madarakani
AI-assisted research summary: Each ward gets one elected councillor. A councillor normally serves five years, with special rules for by-elections and vacancies near the end of a term.
58.-(1) Kutakuwa diwani mmoja aliyechaguliwa kwa kila kata ambapo eneo la halmashauri limegawanywa, na kila diwani baada ya tarehe inayofuata tarehe ambayo matokeo ya uchaguzi yatathibitishwa na msimamizi wa uchaguzi, atakuwa mjumbe aliyechaguliwa kuwa mjumbe wa halmashauri ambayo amechaguliwa. cha (2) Kwa kuzingatia masharti ya Sheria hii, kipindi kwa mjumbe kuwa madarakani aliyechaguliwa katika halmashauri kitakuwa ni miaka mitano isipokuwa mjumbe aliyechaguliwa katika uchaguzi mdogo atakuwa madarakani kwa muda uliosalia wa kipindi cha madaraka cha mjumbe aliyetangulia. (3) Endapo nafasi wazi itatokea ndani ya miezi kumi na mbili kabla ya tarehe ya kawaida ya kumalizika kwa muda wa mjumbe ambaye nafasi yake iko wazi, uteuzi au uchaguzi hautafanyika kujaza nafasi hiyo, isipokuwa nafasi hiyo itajazwa katika uteuzi au uchaguzi wa madiwani utakaofuata. 55 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 SEHEMU YA PILI SIFA ZA WAGOMBEA UDIWANI Sifa za mgombea - 68 Verify source ↗
Wagombea walioteuliwa na siku ya uchaguzi
AI-assisted research summary: The Commission must set election dates within specified time limits after nominations, and it may change a scheduled election day in limited cases.
68.-(1) Endapo wagombea watateuliwa kwa ajili ya uchaguzi tofauti na uchaguzi mdogo katika jimbo au kata, Tume, kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, itapanga si chini ya siku sitini na si zaidi ya siku tisini baada ya siku ya uteuzi kwa ajili ya uchaguzi katika jimbo au kata: Isipokuwa kwamba, endapo kuna chaguzi mbili au zaidi zinazoshindaniwa wakati wa uchaguzi wa Wabunge au Madiwani, Tume inaweza kupanga siku tofauti za uchaguzi kwa majimbo au kata tofauti. (2) Endapo wagombea watateuliwa kwa ajili ya uchaguzi mdogo katika jimbo au kata, Tume, kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, itapanga si zaidi ya siku thelathini baada ya siku ya uteuzi kwa ajili ya uchaguzi katika jimbo au kata. (3) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (1) na (2), Tume inaweza, kwa sababu ya msingi au kutokana na kutokea tukio ambalo litazuia uchaguzi kufanyika, kutengua siku ya uchaguzi iliyopangwa awali na kupanga siku nyingine ya uchaguzi. (4) Endapo uchaguzi utaahirishwa chini ya kifungu kidogo cha (3), muda, utaratibu na namna ya upigaji kura utakaofuata utakuwa kama siku ya mwanzo ya kupiga kura. - 69 Verify source ↗
Tangazo la uchaguzi
AI-assisted research summary: Msimamizi wa uchaguzi lazima atoe tangazo la uchaguzi unaoshindaniwa katika jimbo au kata angalau siku nane kabla ya uchaguzi, na Tume inaweza kuagiza vinginevyo kuhusu muda wa kupiga kura.
69.-(1) Endapo kuna uchaguzi unaoshindaniwa, msimamizi wa uchaguzi, kabla au ifikapo siku nane kabla ya siku ya uchaguzi, atatoa tangazo katika jimbo au kata kwa namna atakavyoona inafaa kuhusu mambo yafuatayo: (a) siku na muda wa kuanza na kufunga upigaji kura, kwa kuzingatia masharti ya kifungu 64 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kidogo cha (3); (b) anwani ya kituo au vituo vya kupigia kura; (c) katika kila eneo la uchaguzi ambalo kuna vituo viwili au zaidi vya kupigia kura, wapiga kura waliopangwa kwa kila kituo cha kupigia kura; na (d) jina kamili la mgombea, picha zilizopigwa karibuni, finyanzo au nembo ya chama cha siasa kinachomdhamini mgombea, ikiwa ipo. (2) Siku iliyopangwa kwa ajili ya kupiga kura kwa mujibu wa masharti ya kifungu kidogo cha (1)(a) katika eneo lolote la uchaguzi, inaweza kutofautiana na siku iliyopangwa kwa eneo lingine la uchaguzi katika jimbo au kata hiyo: Isipokuwa kwamba- (a) siku ya uchaguzi katika jimbo itakuwa ni siku ya kupiga kura kwa angalau eneo moja la uchaguzi katika jimbo au kata hiyo; (b) siku moja tu ndiyo itakayopangwa kuwa siku ya kupiga kura kwa kila eneo la uchaguzi; na (c) siku ya mwisho iliyopangwa kwa ajili ya kupiga kura katika eneo lolote la uchaguzi katika jimbo au kata yoyote, itakuwa si zaidi ya muda huo baada ya siku ya uchaguzi katika jimbo au kata hiyo kama Tume itakavyopanga. (3) Kwa madhumuni ya kifungu kidogo cha (1)(a), muda wa kuanza kupiga kura utakuwa saa mbili kamili asubuhi na muda wa kufungwa kwa upigaji kura utakuwa ni saa kumi na mbili kamili jioni, isipokuwa kama Tume itaelekeza vinginevyo. SEHEMU YA PILI KUJITOA, KIFO AU KUTOKUWEPO KWA WAGOMBEA Kujitoa au kukoma kwa ugombea - 114 Verify source ↗
Makosa yanayohusu uandikishaji
AI-assisted research summary: Mtu hapaswi kutoa taarifa za uongo au kufanya vitendo vingine vilivyotajwa kuhusu uandikishaji na kadi ya mpiga kura; pia kuna adhabu kwa kushindwa kurudisha kadi au tamko ukitakiwa, na kwa kuzuia maafisa wa uchaguzi kutekeleza majukumu yao.
114.-(1) Mtu ambaye- (a) kwa madhumuni ya kutaka kuandikishwa yeye mwenyewe au mtu mwingine yeyote au kupata kadi ya mpiga kura, kutoka kwa afisa mwandikishaji au kutoka kwa mtu mwingine yeyote ambaye ana wajibu juu ya maombi ya kuandikishwa au kutoa kadi ya mpiga kura, atatoa taarifa yoyote ya uongo kuhusu ombi lake mwenyewe au kwa niaba ya mtu mwingine kuandikishwa au kupewa kadi ya mpiga kura; (b) kwa kujua au akiwa na sababu ya kuamini kuwa ameandikishwa katika eneo la uchaguzi, anaomba kuandikishwa bila kuzingatia matakwa ya kifungu cha 25, na bila kueleza kwa afisa mwandikishaji kuhusu uandikishwaji wake wa awali katika eneo lingine la uchaguzi; wakati (c) anaomba kuandikishwa katika eneo la ameshaomba uchaguzi kuandikishwa katika eneo la uchaguzi na maombi yake ya awali hayajaamuliwa kwa kusubiri uchunguzi wowote kuhusu sifa za mwombaji au kuondolewa; lingine (d) baada ya kupewa kadi ya mpiga kura, 96 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 anaomba kupewa yeye binafsi kadi mpya ya mpiga kura kinyume cha mazingira yaliyowekwa katika kifungu cha 19, 20 au 21 na bila kueleza kwa afisa mwandikishaji mazingira ambayo maombi yamefanywa au ambayo haamini kwamba ni ya kweli kulingana na hali halisi; lolote anatoa kujua, lililoainishwa katika kifungu cha 22 ambalo ni la uongo, au ambalo haamini kuwa ni la kweli kulingana na hali halisi; tamko (e) kwa (f) ananunua au anaiba kadi yoyote ya mpiga kura ili aonekane kuwa ni mpiga kura aliyeandikishwa kihalali; au (g) ananunua, anauza, anaiba, anafuta au kwa namna yoyote anaharibu kadi ya mpiga kura ili kumzuia mpiga kura yeyote asimpigie kura mgombea wa chama fulani cha siasa au kwa madhumuni ya kufanya kura nyingi zaidi zipigwe kwa mgombea wa chama fulani cha siasa, anatenda kosa na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi laki moja na isiyozidi shilingi laki tatu au kutumikia kifungo kwa kipindi kisichopungua miezi sita na kisichozidi miaka miwili au vyote kwa pamoja. (2) Mtu ambaye jina lake limefutwa katika Daftari na ametakiwa na afisa mwandikishaji kurudisha kadi ya mpiga kura iliyotolewa kwake au kutoa na kuwasilisha kwa afisa mwandikishaji tamko lililoainishwa katika kifungu cha 22 katika muda ulioainishwa na afisa mwandikishaji bila sababu za msingi, ama harudishi kadi hiyo wala hatoi na kuwasilisha tamko hilo katika muda ulioainishwa, anatenda kosa na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi elfu hamsini na isiyozidi shilingi laki moja. (3) Mtu ambaye kwa namna yoyote anamzuia au anajaribu kumzuia msimamizi wa kituo, msimamizi msaidizi wa kituo, msimamizi wa uchaguzi au 97 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Kutumia wadhifa kushawishi watu wengine ili wasiombe kuteuliwa Mwenendo usiofaa wa mtendaji wa uchaguzi msimamizi msaidizi wa uchaguzi katika kutekeleza majukumu yake au kutekeleza mamlaka yake chini ya Sheria hii anatenda kosa na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi laki moja na isiyozidi shilingi laki tatu. - 115 Verify source ↗
Kutumia wadhifa kushawishi watu wengine ili wasiombe
AI-assisted research summary: A person holding office or a post must not use that position to discourage someone from applying for appointment or to persuade an appointed person to withdraw candidacy.
115.-(1) Mtu mwenye madaraka katika ofisi au mwenye dhamana katika ofisi ambaye, katika kutekeleza majukumu ya ofisi hiyo au wadhifa huo, anatoa maelezo yoyote au anafanya kitendo chochote kwa nia ya kumkatisha tamaa mtu mwingine yeyote kuomba kuteuliwa chini ya Sheria hii au anamshawishi mtu yeyote ambaye ameteuliwa kujitoa ugombea wake, anatenda kosa, na akitiwa hatiani, atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi laki moja na isiyozidi shilingi laki tatu au kifungo kwa kipindi kisichopungua miezi mitatu na kisichozidi miezi kumi na mbili au vyote kwa pamoja. (2) Mashtaka hayatafunguliwa dhidi ya mtu yeyote kwa kosa lolote kinyume na kifungu hiki bila kupata idhini ya Mkurugenzi wa Mashtaka. (3) Katika kifungu hiki “ofisi” na “wadhifa” ina inajumuisha ofisi katika utumishi wa maana na Jamhuri ya Muungano na ofisi nyingine yoyote au wadhifa ambao aliyeshika ana nafasi yenye ushawishi kwa mgombea fulani au mgombea mtarajiwa. - 116 Verify source ↗
Mwenendo usiofaa wa mtendaji wa uchaguzi
AI-assisted research summary: A returning/election officer who knowingly or intentionally does, or fails to do, something about the election process that causes the result to be annulled commits an offence and may be fined, imprisoned, or both.
116.-(1) Mtendaji wa uchaguzi ambaye kwa kujua au kwa makusudi anafanya au anaacha kufanya kitu chochote kinachohusu mchakato wa uchaguzi na kikasababisha matokeo ya uchaguzi kubatilishwa, anatenda kosa na akitiwa hatiani, atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi laki tano na isiyozidi shilingi milioni moja au atatumikia kifungo kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja na kisichozidi miaka miwili au vyote kwa pamoja. (2) Endapo katika la uchaguzi Mahakama inaamua kwamba mtendaji wa uchaguzi amefanya au ameacha kufanya kitu chochote kuhusu mchakato wa uchaguzi ambacho kimesababisha shauri 98 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kuharibika kwa mchakato wa uchaguzi, Mahakama itathibitisha uamuzi huo kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. (3) Endapo shtaka limefunguliwa kwa kosa lililo chini ya kifungu hiki, hati iliyotolewa chini ya kifungu kidogo cha (2) itakuwa ni uthibitisho wa mwisho wa kile kilichomo ndani yake. (4) Kwa madhumuni ya kuondoa shaka, hati iliyotolewa chini ya kifungu kidogo cha (2) haitazuia upande wa mashtaka kuitisha ushahidi zaidi ili kuthibitisha shtaka. (5) Masharti ya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai au Sheria ya Ushahidi yatatumika kwa kuzingatia maboresho katika uendeshaji wa kesi itakayofunguliwa chini ya kifungu hiki. yatakayohitajika - 117 Verify source ↗
Kufidia hasara
AI-assisted research summary: For an election officer who causes the government loss, cost, or damage through an act or omission in the election process, the Public Officials Debt Recovery Act applies with necessary modifications.
117. Bila kujali masharti ya kifungu cha 116, masharti ya Sheria ya Urejeshaji wa Madeni ya Maafisa wa Umma yatatumika kwa kuzingatia maboresho yatakayohitajika kwa mtendaji wa uchaguzi ambaye ameisababishia Serikali hasara, gharama au uharibifu kutokana na kutenda au kutokutenda kwake katika mchakato wa uchaguzi. - 118 Verify source ↗
Tafsiri ya mtendaji wa uchaguzi
AI-assisted research summary: For sections 116 and 117, “mtendaji wa uchaguzi” includes several election officers and any other person appointed to carry out the Commission’s functions.
118. Kwa madhumuni ya kifungu cha 116 na 117, mtendaji wa uchaguzi inajumuisha mratibu wa uchaguzi wa Mkoa, msimamizi wa uchaguzi, msimamizi afisa anayeshughulikia uchaguzi, msimamizi wa kituo, msimamizi msaidizi wa kituo na mtu mwingine yeyote atakayeteuliwa kwa ajili ya kutekeleza majukumu ya Tume. uchaguzi, msaidizi wa - 119 Verify source ↗
Makosa yanayohusu Daftari na kadi ya mpiga kura
AI-assisted research summary: Inaweka kosa kwa mtu kughushi, kufuta au kuharibu Daftari la wapiga kura au kadi ya mpiga kura, na pia kwa kushikilia kadi ya mpiga kura ya mtu mwingine na kukataa kuirudisha inapohitajika.
119.-(1) Mtu ambaye- (a) anaghushi au kwa udanganyifu anafuta au anaharibu Daftari lolote la wapiga kura; au kwa anatengeneza udanganyifu anaharibu kadi yoyote ya mpiga kura au nakala rasmi ya kadi ya (b) anaghushi, au 99 Sura ya 20 Sura ya 6 Kufidia hasara Sura ya 76 Tafsiri ya mtendaji wa uchaguzi Makosa yanayohusu Daftari na kadi ya mpiga kura Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 mpiga kura au alama yoyote rasmi katika kadi ya mpiga kura, anatenda kosa na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi laki mbili na isiyozidi kipindi shilingi kisichopungua miaka miwili na kisichozidi miaka minne au vyote kwa pamoja. kifungo tano kwa laki au (2) Mtu ambaye anamiliki au anayo katika usimamizi wake kadi yoyote ya mpiga kura ambayo imetolewa kwa mtu mwingine yeyote na ambaye anakataa au anazembea bila sababu ya msingi kurudisha kadi hiyo kwa mtu ambaye alipewa, itakapohitajika na mtu huyo au afisa mwandikishaji, anatenda kosa na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi laki moja na isiyozidi shilingi laki tatu au kifungo kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja na kisichozidi miaka miwili au vyote kwa pamoja. Mwenendo usiofaa wa maafisa waandikishaji - 120 Verify source ↗
Mwenendo usiofaa wa maafisa waandikishaji
AI-assisted research summary: Afisa mwandikishaji anayejua kufanya au kuacha kufanya jambo kuhusu uandikishaji na kuvuruga mchakato wa uandikishaji anatenda kosa, na anaweza kuadhibiwa kwa faini au kifungo kulingana na aina ya afisa.
120.-(1) Afisa mwandikishaji yeyote ambaye kwa kujua anafanya au anaacha kufanya kitu chochote kuhusu uandikishaji na hivyo kuvuruga mchakato wa uandikishaji, anatenda kosa na akitiwa hatiani- (a) ikiwa ni afisa aliyeainishwa chini ya kifungu kidogo cha (2)(a), atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi laki tano na isiyozidi shilingi milioni moja au kifungo kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja na kisichozidi miaka miwili, au vyote kwa pamoja; (b) ikiwa ni afisa aliyeainishwa chini ya kifungu kidogo cha (2)(b), atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi laki mbili na isiyozidi shilingi laki tano au kifungo kwa kipindi kisichopungua miezi sita na kisichozidi mwaka mmoja au vyote kwa pamoja. (2) Kwa madhumuni ya kifungu hiki, afisa mwandikishaji inajumuisha- (a) afisa mwandikishaji na afisa mwandikishaji 100 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Makosa yanayohusu fomu za uteuzi au karatasi za kura msadizi; na (b) mwandishi msaidizi. - 121 Verify source ↗
Makosa yanayohusu fomu za uteuzi au karatasi za kura
AI-assisted research summary: This section criminalizes forgery, unauthorized handling, and false statements involving nomination forms, ballot papers, ballot boxes, and related election materials, with fines and possible imprisonment.
121.-(1) Mtu ambaye- (a) anaghushi au kwa udanganyifu anafuta au anaharibu fomu ya uteuzi au karatasi ya kura au anawasilisha kwa msimamizi wa uchaguzi fomu ya uteuzi akijua kuwa fomu hiyo imeghushiwa; (b) anaghushi au anatengeneza au kwa udanganyifu anaharibu karatasi yoyote ya kura au alama rasmi katika karatasi yoyote ya kura; (c) akiwa ni msimamizi wa uchaguzi au msimamizi wa kituo kwa kujua au kwa uzembe, anashindwa kuweka alama rasmi katika karatasi ya kura; (d) bila kuwa na mamlaka stahiki, anasambaza karatasi za kura kwa mtu yeyote; (e) kwa udanganyifu anaweka ndani ya sanduku la kura karatasi yoyote tofauti na karatasi ya kura iliyoidhinishwa kisheria kuwekwa humo; (f) bila kuwa na mamlaka stahiki, anatoa nje ya kituo chochote cha kupigia kura karatasi ya kura au anakutwa na karatasi ya kura nje ya kituo cha kupigia kura; au (g) bila kuwa na mamlaka stahiki, anaharibu, anachukua, au vinginevyo anafungua anazuia sanduku la kura au kifurushi cha karatasi za kura kinachotumika kwa ajili ya uchaguzi, anatenda kosa na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi elfu hamsini na isiyozidi shilingi laki tatu au kifungo kisichopungua miezi sita na kisichozidi miaka miwili au vyote kwa pamoja. (2) Mtu ambaye kwa madhumuni ya kuteuliwa yeye mwenyewe au mtu mwingine yeyote, kuwa mgombea, kwa kujua, anatoa maelezo ya uongo kuhusu uteuzi katika fomu ya uteuzi, fomu ya maelezo 101 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 binafsi au tamko la kisheria lililowasilishwa kwa msimamizi wa uchaguzi, anatenda kosa na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi elfu hamsini na isiyozidi shilingi laki tatu au kifungo kwa kipindi kisichopungua miezi sita na kisichozidi miezi kumi na mbili au vyote kwa pamoja. shtaka (3) Katika lolote kuhusu kosa linalohusiana na fomu ya uteuzi, sanduku la kura, kishina cha karatasi ya kura, vifaa vya kuwekea alama na vitu vingine vinavyotumika katika uchaguzi, vitu vilivyomo katika karatasi hizo, masanduku, zana na vitu vinaweza kuelezwa kuwa katika miliki ya msimamizi wa uchaguzi kwa uchaguzi huo. Matangazo ya uongo ya kujitoa Vishawishi vya rushwa kwa ajili ya kujitoa - 122 Verify source ↗
Matangazo ya uongo ya kujitoa
AI-assisted research summary: Mtu anayejua na kueneza taarifa za kujitoa kwa mgombea ili kumsaidia mgombea mwingine kushinda uchaguzi anatenda kosa na akihukumiwa anaweza kufungwa kwa angalau miezi 6 na hadi miaka 2.
122. Mtu ambaye kwa kujua, kwa kutamka, kuchapisha au kutangaza, anatangaza maelezo yoyote ya kujitoa kwa mgombea yeyote kwa madhumuni ya kumsaidia mgombea mwingine kushinda uchaguzi, anatenda kosa la kitendo haramu na akitiwa hatiani atatumikia kifungo kwa kipindi kisichopungua miezi sita na kisichozidi miaka miwili. - 123 Verify source ↗
Vishawishi vya rushwa kwa ajili ya kujitoa
AI-assisted research summary: Kumsababisha au kumshawishi mtu kujitoa kuwa mgombea kwa malipo au ahadi ya malipo ni kosa la rushwa, na mtu anayejitoa kwa sababu hiyo pia anatenda kosa.
123. Mtu atakayemshawishi au kumsababishia mtu mwingine kujitoa kuwa mgombea katika uchaguzi kwa malipo au kwa ahadi ya malipo na mtu yeyote ambaye atajitoa kutokana na vishawishi au ahadi hizo, anatenda kosa la kitendo cha rushwa na iwapo atatiwa hatiani atatumikia kifungo kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja na kisichozidi miaka mitano. SEHEMU YA PILI MAKOSA MENGINEYO YA UCHAGUZI Makosa mengineyo - 137 Verify source ↗
Kupinga matokeo ya uchaguzi kwa njia ya shauri la uchaguzi
AI-assisted research summary: Section 137 says when a parliamentary election may be declared void on election petition, and when it will not be void despite corrupt or unlawful acts by an agent.
137.-(1) Kwa mujibu wa ukomo uliowekwa na Ibara ya 41(7) ya Katiba, masharti ya kifungu hiki yatatumika kwa uchaguzi wa Mbunge. (2) Uchaguzi wa Mbunge utatangazwa kuwa batili kwa shauri la uchaguzi na si kwa sababu nyingine isipokuwa zifuatazo zimethibitishwa kwa kiwango cha kuiridhisha Mahakama Kuu: mojawapo sababu ya (a) kwamba, wakati wa kampeni za uchaguzi, maelezo yaliyotolewa na mgombea, au kwa niaba yake na kwa ufahamu wake na ridhaa au idhini yake, kwa nia ya kutumia hoja za ukabila, rangi au udini au tofauti zinazohusu uchaguzi au kuhusu yeyote kati ya wagombea au iwapo wagombea si wa jinsi moja, kwa nia ya kutumia tofauti hizo; (b) kutozingatia masharti ya Sheria hii kuhusu uchaguzi, iwapo itajitokeza kuwa uchaguzi haukufanyika taratibu zilizowekwa katika masharti hayo na kuwa kutozingatia huko kumeathiri matokeo ya uchaguzi; au kuzingatia kwa (c) kwamba mgombea wakati wa kuchaguliwa sifa ya kwake hakuwa mtu mwenye kuchaguliwa kama Mbunge. (3) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (2), pale ambapo wakati wa usikilizaji wa shauri la uchaguzi kuhusu uchaguzi chini ya Sheria hii, Mahakama Kuu ikibaini kuwa kitendo cha rushwa au kitendo haramu kuhusu uchaguzi kimetendwa na au kwa ufahamu na ridhaa au idhini ya wakala yeyote wa mgombea na Mahakama Kuu ikibaini zaidi, baada ya kumpa Mwanasheria Mkuu wa Serikali au mwakilishi wake nafasi ya kusikilizwa, kwamba mgombea ameithibitishia Mahakama Kuu kwamba- 108 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 (a) hakuna kitendo cha rushwa au kitendo haramu na mgombea mwenyewe au kwa ufahamu na ridhaa au idhini ya mgombea huyo; kilichotendwa (b) mgombea alichukua hatua zote zinazostahili kuzuia kufanyika kwa kitendo chochote cha rushwa au kitendo haramu katika uchaguzi huo; na (c) kwa hali nyingine yoyote uchaguzi haukuwa na kitendo cha rushwa au kitendo haramu kwa upande wa mgombea na wakala wake, ikiwa Mahakama Kuu itaamua hivyo, kuchaguliwa kwa mgombea huyo hakutakuwa batili kwa sababu ya kitendo chochote. - 138 Verify source ↗
Makosa yanayotendwa na watendaji wa uchaguzi
AI-assisted research summary: If an election-related bribery, gift, corruption, or other unlawful act is proven to have been knowingly committed or continued by a commission member, commission officer, or a person acting under the commission’s directions, conviction can lead to imprisonment of up to five years.
138. Endapo katika uchaguzi imethibitika kuwa kosa lolote la hongo, takrima, kitendo cha rushwa au kitendo haramu lilitendwa kwa kujua au kuendelezwa na mjumbe au afisa wa Tume au na mtu anayetekeleza majukumu kwa maelekezo ya Tume, mjumbe au afisa au mtu huyo mwingine akitiwa hatiani atatumikia kifungo kwa kipindi kisichozidi miaka mitano. Makosa yanayotendwa na watendaji wa uchaguzi SEHEMU YA PILI UTARATIBU NA MAMLAKA YA MAHAKAMA KUU Mashauri yanayosikilizwa na Mahakama Kuu
Part
SEHEMU YA PILI
- 16 Verify source ↗
Muda wa uandikishaji
AI-assisted research summary: Tume must arrange voter registration and updates in each constituency area, and eligible unregistered people may go to the registration service in the relevant area.
16.-(1) Tume itakuwa na jukumu la kupanga muda wa kuandikisha na kuboresha taarifa za wapiga kura katika kila eneo la uchaguzi ndani ya jimbo au kata. (2) Mtu anayestahili kuandikishwa kuwa mpiga kura katika eneo lolote la uchaguzi na ambaye hajaandikishwa, anaweza kwenda yeye mwenyewe katika ambalo huduma ya uandikishaji inapatikana katika eneo la uchaguzi linalohusika. eneo (3) Bila kujali masharti mengine yoyote ya kifungu hiki yanayoelekeza vinginevyo, itakuwa halali kwa Tume kuelekeza kuwa uandikishaji wa wapiga kura katika maeneo yote au eneo lolote la uchaguzi katika jimbo au kata iliyoainishwa katika maelekezo hayo, usitishwe kwa kipindi ambacho Tume inaweza kuelekeza iwapo, kwa maoni ya Tume, itaona inafaa kusitisha uandikishaji wa wapiga kura. (4) Endapo maelekezo chini ya kifungu kidogo cha (3) yametolewa kuhusiana na eneo lolote la uchaguzi, hakutakuwa na uandikishaji wa wapiga kura utakaofanyika katika eneo hilo la uchaguzi kwa kipindi kilichoainishwa katika maelekezo hayo. (5) Kwa madhumuni ya kifungu hiki, uboreshaji wa Daftari utakuwa mara mbili kati ya kipindi kinachoanza mara baada ya uchaguzi mkuu na kabla ya siku ya uteuzi. - 17 Verify source ↗
Wakala wa uandikishaji
AI-assisted research summary: Chama cha siasa kinaweza kuteua wakala wa uandikishaji kwa kila kituo cha uandikishaji, lakini lazima kiwajulishe maafisa wa uandikishaji kwa maandishi ndani ya siku 7 kabla ya uandikishaji kuanza (au mapema zaidi kama Tume itaruhusu).
17.-(1) Chama cha siasa kinaweza kumteua mtu mmoja kuwa wakala wa uandikishaji kwa kila kituo cha uandikishaji katika jimbo au kata, kwa madhumuni ya- (a) kuwatambua watu wenye sifa za kuandikishwa; na (b) kumsaidia mwandishi msaidizi kutekeleza ipasavyo sheria na taratibu zinazohusu mwenendo wa uandikishaji wa wapiga kura bila kuingilia majukumu yake. 24 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 (2) Kwa madhumuni ya kifungu kidogo cha (1), kila chama cha siasa, kupitia taarifa ya maandishi, kitamtaarifu afisa mwandikishaji kuhusu uteuzi ndani ya muda wa siku saba kabla ya tarehe iliyopangwa kuanza uandikishaji wa wapiga kura au ndani ya kipindi kifupi kama Tume itakavyoruhusu. (3) Taarifa itakayotolewa chini ya kifungu kidogo cha (2) itaainisha jina la wakala aliyeteuliwa na jina na anwani ya kituo cha uandikishaji ambacho wakala huyo amepangiwa. (4) Chama cha siasa kinaweza, katika taarifa iliyotolewa chini ya kifungu kidogo cha (2), kumteua wakala mbadala wa uandikishaji anayeweza kuwepo na kutekeleza ama kwa muda wa kudumu au muda mfupi majukumu yoyote ya wakala wa uandikishaji wakati ambapo wakala wa uandikishaji hayupo katika kituo cha uandikishaji. (5) Endapo wakala wa uandikishaji atafariki au ipasavyo, atashindwa kutekeleza majukumu yake chama cha siasa kinachohusika kinaweza kumteua wakala mwingine wa uandikishaji badala yake, na mapema iwezekanavyo kitatoa taarifa ya maandishi kwa afisa mwandikishaji kuhusu jina na anwani ya wakala wa uandikishaji aliyeteuliwa na kituo cha uandikishaji ambacho amepangiwa. (6) Mwandishi msaidizi, kwa kusaidiwa na kushirikiana na wakala wa uandikishaji, mapema iwezekanavyo malalamiko atashughulikia yatakayotolewa na mtu yeyote mwenye nia ya kuandikishwa mbele ya wakala katika kituo cha uandikishaji. (7) Kila wakala wa uandikishaji na wakala mbadala wa uandikishaji kabla ya kuanza kutekeleza majukumu yake ataapa kiapo cha kutunza siri mbele ya afisa mwandikishaji. Kadi ya mpiga kura - 18 Verify source ↗
Kadi ya mpiga kura
AI-assisted research summary: A person who applies to register as a voter and proves eligibility to the registration officer, or another authorized officer, must be registered in that electoral area and then issued a voter card as specified.
18.-(1) Endapo mtu ataomba kuandikishwa kuwa mpiga kura kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 16, mtu huyo, kama atamthibitishia afisa mwandikishaji au afisa mwingine yeyote mwenye 25 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 jukumu la kuandikisha wapiga kura kwa wakati huo kuwa ana sifa za kuandikishwa kuwa mpiga kura katika eneo la uchaguzi lililo katika mamlaka ya afisa mwandikishaji au afisa mwingine, ataandikishwa kuwa mpiga kura katika eneo hilo la uchaguzi na baada ya kuandikishwa atapewa kadi ya mpiga kura kwa namna itakavyoainishwa. (2) Tume inaweza kumtaka mtu yeyote anayeomba kuandikishwa kuwa mpiga kura kujaza fomu kama itakavyoainishwa. (3) Bila kujali masharti ya kifungu hiki, Tume inaweza kuweka utaratibu wa kuwaandikisha wapiga kura walioandikishwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa. - 19 Verify source ↗
Kubadili makazi
AI-assisted research summary: A registered voter who becomes a usual resident in another electoral area may apply for re-registration there, and the registration officer must register them and issue a new voter card if the conditions are met.
19.-(1) Endapo mpiga kura aliyeandikishwa katika eneo moja la uchaguzi anakuwa mkazi wa kawaida katika eneo lingine la uchaguzi, mpiga kura huyo anaweza, kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 14, kuomba kwa afisa mwandikishaji, mwandishi msaidizi au mtendaji mwingine yeyote kama itakavyoelekezwa na Tume kwa madhumuni ya uandikishaji wa wapiga kura katika eneo la uchaguzi ambalo mtu huyo atakuwa mkazi wa kawaida, na afisa mwandikishaji, mwandishi msaidizi au mtendaji mwingine yeyote kama itakavyoelekezwa na Tume kwa madhumuni ya uandikishaji wa wapiga kura- (a) baada ya kujiridhisha kuwa mwombaji- Kubadili makazi (i) ana sifa za kuandikishwa; na (ii) ni mkazi wa kawaida wa eneo la anafanya ambalo uchaguzi maombi; na (b) baada ya mwombaji kurejesha kadi yake ya kupigia kura au baada ya mwombaji kumthibitishia mwandikishaji, afisa mwandishi msaidizi au mtendaji mwingine yeyote kama itakavyoelekezwa na Tume kwa madhumuni ya uandikishaji wa wapiga kura kuwa kadi ya mpiga kura imepotea au imeharibika, 26 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 fomu atamuandikisha mwombaji iliyoainishwa kwa ajili ya eneo la uchaguzi na kumpa kadi nyingine ya mpiga kura. katika huyo (2) Endapo afisa mwandikishaji, mwandishi msaidizi au mtendaji mwingine yeyote kama itakavyoelekezwa na Tume kwa madhumuni ya uandikishaji wa wapiga atamwandikisha mwombaji chini ya kifungu hiki, afisa mwandikishaji, mwandishi msaidizi au mtendaji huyo ataifuta mara moja kadi ya mpiga kura iliyorudishwa na mwombaji. kura (3) Bila kujali masharti ya kifungu cha 18(1) au kifungu kidogo cha (1) cha kifungu hiki, iwapo kwa sababu ya- (a) mabadiliko yoyote ya jina la jimbo au kata; (b) mabadiliko yoyote ya idadi ya majimbo au kata; au (c) mabadiliko yoyote ya mipaka au maeneo ya jimbo au kata moja au zaidi, jimbo au kata ikawa sehemu ya jimbo au kata nyingine au eneo la uchaguzi la jimbo au kata moja ikawa eneo la uchaguzi au sehemu ya eneo la uchaguzi la jimbo au kata nyingine, mabadiliko hayo hayatamlazimu mpiga kura ambaye jina lake liko katika Daftari lolote lililoathirika na mabadiliko hayo kuomba kuhamishwa jina lake katika isipokuwa Mkurugenzi wa Daftari atafanya Uchaguzi, marekebisho kadiri utekelezaji wa itakavyohitajika ya mabadiliko kuhamishwa yamefanywa na mpiga kura anayehusika kwa mujibu wa masharti ya Sheria hii. linalostahili, mapema ya mabadiliko kuwezesha kwamba maombi iwezekanavyo, hayo hayo kana ili Kupotea, kufutika au kuharibika kwa kadi ya mpiga kura - 20 Verify source ↗
Kupotea, kufutika au kuharibika kwa kadi ya mpiga kura
AI-assisted research summary: Ikiwa kadi ya mpiga kura imepotea, imefutika au imeharibika, mwenye kadi anaweza kuomba kadi mpya, na afisa husika anaweza kuitoa ikiwa maombi ni sahihi na mwombaji bado anastahili kuandikishwa.
20.-(1) Endapo kadi ya mpiga kura iliyotolewa kwa mtu yeyote imepotea, imefutika au imeharibika, mtu ambaye kadi hiyo ilitolewa kwake anaweza kuomba yeye mwenyewe kwa afisa mwandikishaji, mwandishi msaidizi au mtendaji mwingine yeyote kama itakavyoelekezwa na Tume kwa madhumuni ya uandikishaji wa wapiga kura kupewa kadi mpya ya 27 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Marekebisho ya taarifa mpiga kura. (2) Baada ya maombi hayo kufanyika, afisa mwandikishaji, mwandishi msaidizi au mtendaji mwingine yeyote kama itakavyoelekezwa na Tume kwa madhumuni ya uandikishaji wa wapiga kura ikiwa atajiridhisha kuwa maombi yamefanywa ipasavyo na kwamba mwombaji bado ana sifa za kuandikishwa, atampa mwombaji kadi mpya ya mpiga kura na iwapo maombi yatafanyika kutokana na kuharibika au kufutika kwa kadi ya mpiga kura, mwombaji atarudisha kadi hiyo iliyoharibika au iliyofutika. - 21 Verify source ↗
Marekebisho ya taarifa
AI-assisted research summary: Mtu anaweza kuomba kadi mpya ya mpiga kura ikiwa taarifa zake zinahitaji kurekebishwa kwa sababu ya mabadiliko ya jina au hali nyingine inayomwathiri, lakini si kwa mabadiliko ya makazi kati ya maeneo ya uchaguzi.
21.-(1) Endapo taarifa zozote zilizopo katika kadi ya mpiga kura au Daftari la Awali la Wapiga Kura zitahitaji kufanyiwa marekebisho kwa sababu ya kubadilika kwa jina au mabadiliko mengine yoyote katika mazingira ambayo yatamuathiri mtu ambaye kadi ya mpiga kura imetolewa kwake tofauti na mabadiliko ya makazi kutoka eneo moja la uchaguzi kwenda lingine, mtu ambaye kadi ya mpiga kura imetolewa kwake anaweza kuomba kadi mpya ya mpiga kura. (2) Baada ya kupokea maombi na kujiridhisha kuwa maombi yamefanywa ipasavyo na kwamba mwombaji bado ana sifa ya kuandikishwa, afisa mwandikishaji, mwandishi msaidizi au mtendaji mwingine yeyote kama itakavyoelekezwa na Tume kwa madhumuni ya uandikishaji wa wapiga kura atamwandikisha fomu mwombaji itakayoainishwa na kumpa kadi nyingine ya mpiga kura: katika Isipokuwa kwamba, kadi mpya ya mpiga kura haitatolewa chini ya kifungu hiki hadi mwombaji- (a) atakapowasilisha nyaraka inayotambulika sheria, endapo ni kwa mujibu wa mabadiliko ya jina; na (b) atakaporejesha kadi yake ya mpiga kura au afisa atakapomthibitishia mwandikishaji, mwandishi msaidizi au kama mtendaji mwingine yeyote 28 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 na kwa itakavyoelekezwa madhumuni ya uandikishaji wa wapiga kura kuwa kadi hiyo imepotea au imeharibika. Tume Tamko kuhusu kupotea au kuharibika kwa kadi ya mpiga kura Kukataliwa kwa maombi - 22 Verify source ↗
Tamko kuhusu kupotea au kuharibika kwa kadi ya mpiga ya kura
AI-assisted research summary: A person seeking a replacement for a lost or damaged voter card may be required to give a statement about the loss or damage, and the application may be refused if the statement is not given.
22. Endapo, chini ya masharti ya Sehemu hii, maombi yamefanywa kwa afisa mwandikishaji, mwandishi msaidizi au mtendaji mwingine yeyote kama itakavyoelekezwa na Tume kwa madhumuni ya uandikishaji wa wapiga kura na mtu ambaye anadai kuwa kadi iliyotolewa kwake imepotea au imeharibika, afisa mwandikishaji, mwandishi msaidizi au mtendaji mwingine yeyote kama itakavyoelekezwa na Tume kwa madhumuni ya uandikishaji wa wapiga kura fomu atamtaka mwombaji kutoa iliyoainishwa kuhusu kupotea au kuharibika huko, na bila kuathiri mamlaka ya kukataa maombi hayo kwa sababu nyinginezo, afisa mwandikishaji, mwandishi msaidizi au mtendaji mwingine yeyote kama itakavyoelekezwa na Tume kwa madhumuni ya uandikishaji wa wapiga kura, anaweza kukataa maombi hayo isipokuwa kama mwombaji atatoa tamko hilo. tamko katika - 23 Verify source ↗
Kukataliwa kwa maombi
AI-assisted research summary: If an application is refused, the applicant can ask for written reasons and may seek review and appeal within set time limits.
23.-(1) Endapo mwandishi msaidizi au mtendaji mwingine yeyote kama itakavyoelekezwa na Tume kwa madhumuni ya uandikishaji wa wapiga kura atakataa maombi yaliyotolewa chini ya masharti ya Sehemu hii, pale mwombaji atakapohitaji, atatoa maelezo ya maandishi kwa mwombaji akiainisha sababu za kukataa maombi katika fomu iliyoainishwa, na endapo mwombaji hataridhika na kukataliwa huko anaweza kuwasilisha maombi ya mapitio kwa afisa mwandikishaji ndani ya siku saba baada ya kupokea maelezo hayo. (2) Afisa mwandikishaji atatoa uamuzi wa maombi ya mapitio ndani ya siku kumi na nne baada ya kupokea maombi hayo. (3) Endapo mwombaji hataridhika na uamuzi wa afisa mwandikishaji, anaweza kukata rufaa katika 29 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Mahakama ya Mwanzo dhidi ya kukataliwa huko ndani ya siku kumi na nne baada ya kutolewa kwa uamuzi. (4) Mahakama ya Mwanzo itatoa uamuzi wa rufaa ndani ya siku kumi na nne tangu siku rufaa ilipowasilishwa. SEHEMU YA TATU PINGAMIZI DHIDI YA UANDIKISHAJI AU KUENDELEA KUANDIKISHWA Ukaguzi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura Kuingizwa kwa jina katika Daftari la Awali la Wapiga Kura - 41 Verify source ↗
Siku ya uchaguzi wa Rais
AI-assisted research summary: Tume ya Uchaguzi lazima ipange siku ya uchaguzi wa Rais, na inaweza pia kupanga siku tofauti kwa majimbo tofauti au kubatilisha na kuweka siku nyingine kwa kuzingatia masharti ya kifungu hiki.
41.-(1) Tume itapanga siku ambayo kwa mujibu wa Sheria hii itajulikana kama siku ya uchaguzi wa Rais, kwa ajili ya kupiga kura katika kila jimbo kwa ajili ya uchaguzi wa Rais. (2) Kwa kuzingatia masharti ya kifungu hiki, Tume inaweza kupanga siku tofauti za uchaguzi wa Rais katika majimbo tofauti na inaweza kutengua siku ya uchaguzi wa Rais na kupanga siku nyingine ya uchaguzi wa Rais. (3) Tume itapanga siku ya uchaguzi wa Rais- (a) ikiwa uchaguzi wa Rais unafanyika kwa sababu ya kuvunjwa kwa Bunge tofauti na ibara mazingira yaliyoainishwa katika ndogo ya (2)(b), (c), (d) au (e) ya ibara ya 38 ya Katiba- (i) kwa kila jimbo ambalo kuna 43 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 uchaguzi wa Wabunge, siku itakayopangwa kuwa siku ya uchaguzi wa Wabunge; siku jimbo (ii) kwa kila lingine zisizopungua lolote, arobaini zisizozidi na hamsini baada ya siku ya uteuzi; (b) ikiwa ni uchaguzi wa Rais ambao aya (a) ya kifungu kidogo hiki haitumiki, kwa kila jimbo, siku zisizopungua arobaini na zisizozidi hamsini baada ya uteuzi wa wagombea wa kiti cha Rais. (4) Siku tofauti zinaweza kupangwa chini ya kifungu kidogo cha (3)(a)(ii) au (b) kwa majimbo tofauti. (5) Kwa madhumuni ya kifungu kidogo cha (3), jimbo ambalo uchaguzi wa Wabunge unaanza upya, litachukuliwa kuwa ni jimbo ambalo hakuna uchaguzi wa Wabunge. - 42 Verify source ↗
Watu wanaostahili kupiga kura katika uchaguzi wa Rais
AI-assisted research summary: Watu walioandikishwa kuwa wapiga kura wana haki ya kupiga kura katika uchaguzi wa Rais.
42.-(1) Kila mtu aliyeandikishwa kuwa mpiga kura chini ya Sheria hii atastahili kupiga kura katika uchaguzi wa Rais. (2) Kwa kuzingatia masharti ya kifungu kidogo cha (3), mpiga kura aliyeandikishwa anaweza kupiga kura- Watu wanaostahili kupiga kura katika uchaguzi wa Rais (a) katika ya uchaguzi wa Rais siku iliyopangwa jimbo kwa alilojiandikisha kuwa mpiga kura; na ajili ya (b) katika kituo cha alichopangiwa katika eneo aliloandikishwa. kupigia kura la uchaguzi (3) Tume inaweza kutoa maelekezo na kuweka masharti ambayo mtu anaweza, katika siku ya uchaguzi wa Rais, kuruhusiwa kupiga kura katika kituo cha kupigia kura tofauti na kile alichopangiwa. Sifa za mgombea katika uchaguzi wa Rais - 43 Verify source ↗
Sifa za mgombea katika uchaguzi wa Rais
AI-assisted research summary: A person is not qualified to be a presidential election candidate unless they meet the qualifications for being elected President under Article 39 of the Constitution.
43. Mtu hatakuwa na sifa ya kuwa mgombea wa uchaguzi wa Rais isipokuwa kama ana sifa za 44 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kuchaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 39 ya Katiba. Matumizi ya Sura ya Sita Majumuisho ya kura katika uchaguzi wa Rais - 44 Verify source ↗
Matumizi ya Sura ya Sita
AI-assisted research summary: Uchaguzi wa Rais katika kila jimbo ufanywe kwa utaratibu ule ule wa uchaguzi wa ubunge, na masharti ya Sura ya Sita ya Sheria hii yatumike pamoja na maboresho yanayohitajika.
44. Kura ya uchaguzi wa Rais katika kila jimbo itapigwa kwa utaratibu kama ilivyo katika uchaguzi wa ubunge na masharti ya Sura ya Sita ya Sheria hii yatatumika maboresho yatakayohitajika. kuzingatia kwa - 45 Verify source ↗
Majumuisho ya kura katika uchaguzi wa Rais
AI-assisted research summary: Section 45 sets out who may be present at the vote tallying centre and how the election officer must count, post, prepare, and distribute presidential results.
45.-(1) Watu wafuatao wataruhusiwa kuwepo katika kituo cha majumuisho ya kura- (a) mjumbe wa Tume; (b) Mkurugenzi wa Uchaguzi; (c) Katibu Mkuu wa chama cha siasa au mwakilishi wake kwa barua; (d) afisa wa Tume; (e) mgombea; (f) wakala wa kuhesabu kura; (g) afisa wa polisi au mtu mwingine anayehusika na usalama wa mahali pa kuhesabia kura; (h) mwangalizi wa uchaguzi aliyeidhinishwa kwa maandishi na Tume; au (i) mtu mwingine atakayeruhusiwa na Tume. (2) Baada ya taarifa zote za matokeo na masanduku ya kura yenye karatasi za kura kuhusu uchaguzi wa Rais kupokelewa kutoka katika vituo vya kupigia kura katika jimbo, msimamizi wa uchaguzi, baada ya kuamua uhalali wa kura zote zenye mgogoro, atajumlisha- (a) kura zote zilizopigwa katika jimbo la uchaguzi; (b) kura alizopigiwa kila mgombea; na (c) kura zilizokataliwa. (3) Msimamizi wa uchaguzi, baada ya kujumuisha matokeo ya kura za Rais katika jimbo, atabandika matokeo hayo katika sehemu ya wazi na inayoonekana. (4) Kwa kuzingatia kifungu kidogo cha (3), msimamizi wa uchaguzi ataandaa na kuwasilisha kwa 45 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Tume, taarifa ya matokeo ya awali ya uchaguzi wa Rais katika jimbo. (5) Msimamizi wa uchaguzi atathibitisha na kutoa nakala ya taarifa ya matokeo kwa kila wakala au wagombea wa kiti cha Rais, kama wapo. (6) Tume inaweza kuelekeza kwamba, msimamizi wa uchaguzi, baada ya kuandaa taarifa ya matokeo chini ya kifungu kidogo cha (3), abandike nakala ya taarifa hiyo katika sehemu ya wazi inayoonekana. (7) Endapo kuna shaka yoyote kuhusu usahihi katika kujumlisha kura za Rais katika jimbo lolote, Tume inaweza kuelekeza kurudiwa kujumlishwa kwa idadi ya kura za matokeo ya awali kutoka baadhi au vituo vyote vya kupigia kura katika jimbo. kupokea matokeo ya yaliyowasilishwa chini ya kifungu kidogo cha (4), Tume itatangaza matokeo ya uchaguzi wa Rais kwa jimbo husika. Baada (8) Marudio ya upigaji kura (9) Kwa kuzingatia kifungu kidogo cha (3), Tume, baada ya kujumlisha kura zote zilizowasilishwa na kila msimamizi wa uchaguzi kwa mujibu wa itatangaza matokeo ya kifungu kidogo cha (4), uchaguzi wa Rais ya nchi nzima. (10) Mgombea yeyote wa kiti cha Rais atatangazwa kuwa amechaguliwa kuwa Rais iwapo amepata kura halali nyingi zaidi kuliko mgombea mwingine yeyote. - 46 Verify source ↗
Marudio ya upigaji kura
AI-assisted research summary: If no presidential candidate gets the most valid votes in the first count, the Commission must set a later rerun election date by Gazette notice, within 40 days after polling day.
46.-(1) Endapo katika upigaji kura wa awali hakuna mgombea wa kiti cha Rais aliyepata kura nyingi zaidi kati ya kura halali zilizopigwa, Tume, kwa notisi katika Gazeti la Serikali, itapanga siku nyingine itakayofaa isiyozidi siku arobaini baada ya siku ya uchaguzi, kwa ajili ya marudio ya upigaji kura katika uchaguzi wa Rais. (2) Endapo kutatokea kufungana kwa kura za wagombea waliopata kura nyingi zaidi, wagombea wa kiti cha Rais waliofungana ndio watakuwa wagombea pekee katika uchaguzi wa marudio. 46 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Uchaguzi wa Rais kuchukuliwa kuwa uchaguzi wa Makamu wa Rais - 47 Verify source ↗
Uchaguzi wa Rais kuchukuliwa kuwa uchaguzi wa Makamu wa
AI-assisted research summary: If the presidential candidate is declared elected, the running mate is treated as elected Vice President.
47. Endapo mgombea wa kiti cha Rais atatangazwa kuwa amechaguliwa, mgombea mwenza atachukuliwa kuwa amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais. SURA YA NNE UCHAGUZI WA WABUNGE SEHEMU YA KWANZA SIFA ZA MGOMBEA UBUNGE Sifa za wagombea katika uchaguzi wa ubunge - 49 Verify source ↗
Siku ya uteuzi
AI-assisted research summary: Kifungu hiki kinaweka tarehe za siku ya uteuzi kwa uchaguzi wa Wabunge na kinampa Tume uwezo wa kupanga, kubadili, na kutoa taarifa za siku hiyo.
49.-(1) Endapo uchaguzi wa Wabunge ikiwa uchaguzi huo utafanyika katika umesitishwa na taratibu za uchaguzi kutakiwa kuanza upya, Tume, kwa notisi katika Gazeti la Serikali, itapanga siku ya uteuzi kwa ajili ya uchaguzi wa Wabunge: Isipokuwa kwamba- (a) iwapo uchaguzi wa Wabunge utafanyika baada ya kuvunjwa kwa Bunge, siku ya uteuzi kwa jimbo lolote itakuwa si chini ya siku tano na si zaidi ya siku ishirini na tano baada ya kuvunjwa kwa Bunge; (b) iwapo uchaguzi mdogo utafanyika, siku ya uteuzi itakuwa si chini ya siku ishirini na si zaidi ya siku hamsini baada ya kutokea kwa tukio ambalo ndiyo sababu ya uchaguzi kufanyika. (2) Endapo Mbunge atajiuzulu, kufariki au vinginevyo ataachia ofisi kwa sababu nyingine tofauti 47 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 na zilizo chini ya kifungu cha 142, Spika atamtaarifu kwa maandishi Mwenyekiti wa Tume, na kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, atatangaza kuwepo kwa nafasi wazi ya Ubunge. (3) Tume inaweza kupanga siku tofauti za uteuzi kwa ajili ya majimbo tofauti, na inaweza kutengua siku yoyote ya uteuzi iliyopangwa na kupanga siku nyingine ya uteuzi: Isipokuwa kwamba, siku hiyo nyingine iliyopangwa kuwa siku ya uteuzi kwa ajili ya uchaguzi wa Ubunge itakuwa ndani ya kipindi kilichoainishwa chini ya kivuo cha kifungu kidogo cha (1). (4) Tume itatoa taarifa ya siku ya uteuzi angalau siku saba, na iwapo uchaguzi wa Ubunge utafanyika pale ambapo Rais ametoa taarifa ya kusudio la kuvunja Bunge, taarifa ya siku ya uteuzi inaweza kutolewa kabla ya kuvunjwa kwa Bunge. (5) Endapo uchaguzi mdogo unatakiwa tarehe ya kuvunjwa kwa Bunge kufanyika na imetangazwa au imejulikana kwa mujibu wa matukio yaliyoainishwa katika Ibara ya 90(3) ya Katiba, uchaguzi mdogo hautafanyika katika muda wowote wakati wa kipindi cha miezi kumi na mbili mara tu baada ya tarehe ya kuvunjwa kwa Bunge. - 50 Verify source ↗
Uteuzi wa wagombea ubunge
AI-assisted research summary: A parliamentary candidate must be sponsored by at least 25 registered voters in the constituency area and must file signed nomination forms on time with the required attachments.
50.-(1) Ili kuweza kuteuliwa kuwa mgombea halali wa uchaguzi wa Wabunge, mtu atapaswa kudhaminiwa na wadhamini wasiopungua ishirini na tano ambao ni wapiga kura walioandikishwa katika maeneo ya uchaguzi ndani ya jimbo ambalo mtu huyo ni mgombea. kwa maandishi (2) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (1), Tume inaweza, katika siku ya uteuzi, kukataa kumteua mtu kuwa mgombea iwapo itajiridhisha kuwa mtu huyo ameondolewa sifa za kushiriki katika mchakato wa uteuzi na Msajili wa Vyama vya Siasa kwa mujibu wa masharti ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi. (3) Uteuzi utafanyika kwa kutumia fomu itakayoainishwa ambayo itazingatia matumizi ya watu 48 Uteuzi wa wagombea ubunge Sura ya 278 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 wenye mahitaji maalumu, itakayosainiwa na mgombea na wadhamini na itakuwa na taarifa zifuatazo: (a) jina, jinsi, hali ya ulemavu, ikiwa ipo, anwani na kazi ya mgombea; (b) majina na anwani za wadhamini na namba za kadi zao za kupigia kura; (c) tamko la mgombea kwamba yupo tayari na ana sifa za kuwa mgombea katika uchaguzi; (d) uthibitisho wa msimamizi wa uchaguzi wadhamini ambalo jimbo katika wameandikishwa; na (e) kiapo cha mgombea kitakachojazwa na kusainiwa na mgombea mbele ya hakimu na kitakachoonesha sifa za mgombea na kuwa hajapoteza sifa kwa ajili ya uchaguzi. (4) Kila fomu ya uteuzi itaambatishwa na- (a) idadi ya picha za mgombea kama Tume itakavyoelekeza, zilizopigwa si zaidi ya miezi mitatu kabla ya siku ya uteuzi; na (b) taarifa binafsi yoyote inayomhusu mgombea kama itakavyohitajika kutolewa na kanuni kwa namna itakayokuwa imeelekezwa. (5) Endapo, kwa vyovyote vile fomu ya uteuzi haijaambatishwa na nyaraka zilizoainishwa katika (4), uteuzi wa mgombea kifungu kidogo cha utachukuliwa kuwa ni batili: Isipokuwa kwamba, Tume, katika mazingira maalumu na kama itaona kuna sababu ya kufanya inaweza kuelekeza kuwa fomu ya uteuzi hivyo, ikubaliwe kuwa halali bila kujali kuwa fomu hiyo haikuambatishwa na nyaraka zozote ikiwa nyaraka zinazohusika zitawasilishwa kwa msimamizi wa uchaguzi ndani ya muda mwingine kama ambavyo Tume inaweza kuruhusu. (6) Msimamizi wa uchaguzi atatoa fomu za uteuzi kwa mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa au mpiga kura aliyeidhinishwa na chama cha siasa kwa maandishi na atampa idadi ya fomu za uteuzi kama itakavyoelekezwa na Tume. 49 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 (7) Kila mgombea atawasilisha fomu za uteuzi zilizosainiwa kama ilivyoainishwa chini ya kifungu hiki, katika ofisi ya msimamizi wa uchaguzi si zaidi ya saa kumi kamili alasiri ya siku ya uteuzi: Isipokuwa kwamba, ikiwa Tume itaona zipo sababu za msingi za mgombea mwenyewe kushindwa kuwasilisha chama kilichomdhamini anaweza kuwasilisha fomu hizo kwa niaba yake. hizo, kiongozi wa fomu (8) Msimamizi wa uchaguzi, mapema iwezekanavyo atabandika nakala ya fomu ya uteuzi katika sehemu ya wazi inayoonekana nje ya ofisi yake. (9) Mtu hatamdhamini mgombea zaidi ya mmoja kwa uchaguzi mmoja na iwapo msimamizi wa uchaguzi ametoa hati chini ya kifungu kidogo cha (3)(d) kwa ajili ya udhamini wa mgombea mmoja, atakataa kutoa hati ya udhamini wa mtu huyo kwa mgombea mwingine katika uchaguzi mmoja: Isipokuwa kwamba, mtu hatazuiwa kusaini fomu ya uteuzi kwa sababu tu amekwisha saini fomu ya mgombea aliyefariki au aliyejitoa kabla ya kuwasilisha fomu ya uteuzi ya mwanzo. (10) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (9), iwapo mdhamini atamdhamini mgombea zaidi ya mmoja katika uchaguzi mmoja na hati zimetolewa chini ya kifungu kidogo cha (3)(d) kwa ajili ya uandikishwaji wa mtu huyo, udhamini wa wagombea wote wawili utakuwa ni halali. (11) Mtu yeyote atakayemdhamini mgombea zaidi ya mmoja anatenda kosa, na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyozidi shilingi laki mbili. (12) Endapo msimamizi wa uchaguzi ataridhika kuwa mtu yeyote ametenda kosa chini ya kifungu kidogo cha (11), kwa amri iliyotolewa kwa idhini yake anaweza kufifilisha kosa na kuamuru mtu huyo kulipa kiasi cha fedha: Isipokuwa kwamba- (a) kiasi cha fedha hakitazidi kiasi cha juu cha faini iliyowekwa kwa kosa hilo; (b) mamlaka yaliyotolewa na kifungu hiki 50 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kidogo yatatumika kama mtu atakiri kwa maandishi kuwa ametenda kosa; na (c) msimamizi wa uchaguzi atatoa stakabadhi ya malipo kwa mtu aliyetoa kiasi hicho cha fedha. (13) Msimamizi wa uchaguzi, atakapoombwa na mgombea au mtu mwingine kwa niaba yake, kutoa hati kuhusu mdhamini aliyeandikishwa katika eneo la uchaguzi analohudumu, atatoa hati hiyo ipasavyo. (14) Endapo baada ya siku ya uteuzi, jina la mtu aliyemdhamini mgombea litafutwa katika Daftari la uchaguzi husika, kufutwa huko katika eneo hakutabatilisha udhamini wa mgombea. - 51 Verify source ↗
Dhamana
AI-assisted research summary: Mgombea lazima aweke dhamana ya kiasi kitakachoainishwa anaporudisha fomu ya uteuzi, na msimamizi wa uchaguzi arejeshe dhamana hiyo mapema iwezekanavyo baada ya matokeo ikiwa haitataifishwa.
51.-(1) Wakati wa kurudisha fomu ya uteuzi kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 50, mgombea ataweka dhamana kwa msimamizi wa uchaguzi ya kiasi cha fedha kitakachoainishwa. (2) Dhamana ya mgombea anayepingwa itataifishwa kwa Serikali ikiwa atajiondoa kugombea baada ya siku ya uteuzi au ikiwa idadi ya kura alizopigiwa katika uchaguzi ni chini ya moja ya kumi ya kura zote zilizohesabiwa katika jimbo ambalo alikuwa ni mgombea, isipokuwa dhamana hiyo haitataifishwa ikiwa mgombea atafariki. Dhamana (3) Endapo dhamana ya mgombea haitataifishwa chini ya masharti ya kifungu kidogo cha (2), mapema iwezekanavyo baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi, msimamizi wa uchaguzi atamrejeshea mgombea au mwakilishi wake wa kisheria kama itakavyokuwa. Mgombea kuteuliwa kwa jimbo moja tu - 52 Verify source ↗
Mgombea kuteuliwa kwa jimbo moja tu
AI-assisted research summary: A person may not be nominated as a candidate in more than one constituency or for any other elected office under this Act.
52. Mtu hatateuliwa kuwa mgombea wa uchaguzi katika jimbo zaidi ya moja au nafasi nyingine yoyote ya kuchaguliwa chini ya Sheria hii. Pingamizi na uamuzi juu ya uhalali wa fomu ya uteuzi - 53 Verify source ↗
Pingamizi na uamuzi juu ya uhalali wa fomu ya uteuzi
AI-assisted research summary: Section 53 allows objections to a nomination form on listed grounds and sets who may object and by when.
53.-(1) Pingamizi linaweza kuwekwa dhidi ya fomu ya uteuzi kutokana na sababu zote au yoyote kati ya sababu zifuatazo: (a) taarifa zilizotolewa kuhusu mgombea 51 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 hazitoshelezi kumtambulisha; (b) fomu ya uteuzi haikidhi au haikuwasilishwa kwa mujibu wa masharti ya Sehemu hii; (c) ni dhahiri kutokana na taarifa zilizomo katika fomu ya uteuzi kwamba mgombea hana sifa za kugombea; (d) masharti yaliyoainishwa katika kifungu cha 50(3) hayajazingatiwa; na Sura ya 278 (e) masharti ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi hayajazingatiwa. (2) Pingamizi dhidi ya fomu ya uteuzi halitakubaliwa isipokuwa kama limewasilishwa kwa msimamizi wa uchaguzi si zaidi ya saa kumi kamili alasiri ya siku inayofuatia siku ya uteuzi. (3) Pingamizi linaweza kuwekwa na mgombea mwingine ndani ya jimbo, Msajili wa Vyama vya Siasa au Mwanasheria Mkuu wa Serikali, isipokuwa kwa pingamizi chini ya kifungu kidogo cha (1)(e) ambalo linaweza kuwekwa na Msajili wa Vyama vya Siasa pekee, na litawekwa kwa maandishi na kusainiwa na mweka pingamizi, na litabainisha sababu za pingamizi. (4) Msimamizi wa uchaguzi, kabla ya kuamua juu ya uhalali wa pingamizi lolote na bila kuchelewa- (a) atamtaarifu mtu aliyewekewa pingamizi; na (b) atampa mtu huyo nafasi ya kusikilizwa. (5) Endapo msimamizi wa uchaguzi atatoa uamuzi kuhusiana na pingamizi lolote chini ya kifungu kidogo cha (4), atamjulisha kwa maandishi mgombea anayehusika kuhusu uamuzi na sababu za uamuzi huo. (6) Mgombea yeyote ambaye hataridhika na uamuzi wa msimamizi wa uchaguzi kuhusu uhalali wa pingamizi, kwa kuzingatia utaratibu na ndani ya muda utakaoainishwa na Tume, anaweza kukata rufaa kwa Tume, na uamuzi wa Tume utakuwa ni wa mwisho na hautahojiwa na mahakama yoyote, isipokuwa kwa njia ya mashauri ya uchaguzi yatakayowasilishwa kwa mujibu wa masharti ya Sura ya Nane kutokana na sababu moja au nyinginezo zilizoainishwa katika Sura hiyo. (7) Bila kujali masharti yoyote ya kifungu hiki, 52 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 endapo Msajili wa Vyama vya Siasa ataweka pingamizi chini ya kifungu kidogo cha (3), pingamizi hilo litawasilishwa ndani ya siku kumi na nne baada ya siku ya uteuzi. Mgombea pekee nafasi ya ubunge au kukosekana kwa mgombea - 54 Verify source ↗
Mgombea pekee nafasi ya ubunge au kukosekana kwa mgombea
AI-assisted research summary: Akikuwa na mgombea mmoja halali wa ubunge, msimamizi wa uchaguzi lazima amtangaze kuwa mgombea pekee; kura ya ndiyo au hapana itapigwa, na kama hapati kura za ndiyo za kutosha, Tume itapanga siku nyingine ya uteuzi na upigaji kura ndani ya siku 40.
54.-(1) Endapo kutakuwa na mgombea mmoja halali wa nafasi ya ubunge aliyeteuliwa, msimamizi wa uchaguzi atamtangaza mgombea huyo kuwa mgombea pekee wa nafasi ya ubunge. ya nafasi (2) Mgombea wa ubunge aliyetangazwa chini ya kifungu kidogo cha (1) atapigiwa kura ya ndio au hapana na atakuwa amechaguliwa kihalali kuwa Mbunge endapo atapata kura nyingi za ndiyo kati ya kura zote halali zilizopigwa. (3) Endapo mgombea pekee wa kiti cha ubunge atashindwa kupata idadi ya kura zinazohitajika kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (2), msimamizi wa uchaguzi ataitaarifu Tume kuhusu matokeo hayo na Tume, kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, itapanga siku nyingine ya uteuzi na upigaji kura itakayofaa sio zaidi ya siku arobaini baada ya siku ya uchaguzi. (4) Ikiwa msimamizi wa uchaguzi ataamua kuwa hakuna mgombea aliyeteuliwa kihalali kwa ajili ya kiti cha ubunge katika jimbo, msimamizi wa uchaguzi ataitaarifu Tume. - 55 Verify source ↗
Picha
AI-assisted research summary: Wagombea lazima watambuliwe kwa kutumia picha iliyoidhinishwa na msimamizi wa uchaguzi, na picha zinazooneshwa wakati wa kampeni ziwe chini ya usimamizi wake.
55.-(1) Kwa madhumuni ya kuwasaidia wapiga kura kumtambua mgombea wakati wa kupiga kura, kila mgombea atatambuliwa kwa kutumia picha ya mgombea ambayo imeidhinishwa na msimamizi wa uchaguzi. (2) Picha ya mgombea itakayooneshwa wakati wa kampeni za uchaguzi itakuwa chini ya usimamizi wa msimamizi wa uchaguzi. Picha 53 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 SURA YA TANO UCHAGUZI WA MADIWANI SEHEMU YA KWANZA KUENDESHA UCHAGUZI NA MUDA WA KUWEPO MADARAKANI KWA MADIWANI Uchaguzi wa madiwani Uchaguzi mdogo - 59 Verify source ↗
Sifa za mgombea
AI-assisted research summary: A person may be chosen as a candidate for a councillor election only if the person meets the listed qualifications.
59.-(1) Mtu atachaguliwa kuwa mgombea ikiwa ana sifa za katika uchaguzi wa udiwani kuchaguliwa. (2) Mtu atakuwa na sifa za kuchaguliwa ikiwa atatimiza masharti yafuatayo: Sura ya 258 Kukosa sifa ya uteuzi (a) ni raia wa Jamhuri ya Muungano; (b) ametimiza umri wa miaka ishirini na moja; (c) hajapoteza sifa za kuchaguliwa chini ya masharti ya kifungu cha 60; (d) ni mkazi wa kawaida ndani ya eneo la mamlaka ya serikali za mitaa; (e) anajua kusoma na kuandika kwa lugha ya Kiswahili au Kiingereza; (f) ni mwanachama na amedhaminiwa na chama cha siasa kilichosajiliwa chini ya Sheria ya Vyama vya Siasa; na (g) ana kipato halali kinachomwezesha kuishi. - 60 Verify source ↗
Kukosa sifa ya uteuzi
AI-assisted research summary: Mtu hana sifa ya kuteuliwa katika uchaguzi ikiwa anakidhi mojawapo ya sababu zilizoorodheshwa, kama uraia/kiapo kwa nchi nyingine, kutokuwa timamu kiakili, hukumu fulani, au kushindwa kutangaza maslahi katika mkataba wa serikali za mitaa.
60.-(1) Mtu atakosa sifa ya kuteuliwa katika uchaguzi- (a) ikiwa ana kiapo cha utii kwa nchi nyingine tofauti na Jamhuri ya Muungano; (b) ikiwa katika sheria yoyote inayotumika imethibitika kuwa hana akili Tanzania timamu; (c) ikiwa ametiwa hatiani kwa kosa la kukwepa kulipa kodi ndani ya kipindi cha miaka mitano kabla ya uchaguzi; (d) endapo amehukumiwa adhabu ya kifo na au kifungo mahakama kutumikia amehukumiwa kinachozidi miezi sita gerezani; ya Tanzania yoyote Sura ya 361 (e) endapo yupo kizuizini chini ya amri iliyotolewa chini ya Sheria ya Uwekaji Kizuizini kwa Usalama na amekuwa kizuizini chini ya amri hiyo kwa kipindi kinachozidi miezi sita; 56 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Sura ya 380 (f) endapo ameondolewa nchini, kwa mujibu wa masharti ya Sheria ya Uhamisho wa Wahalifu kwa amri iliyotolewa chini ya Sheria hiyo ambayo inaendelea kwa kipindi kinachozidi miezi sita; (g) iwapo ni sehemu ya, au ni mbia katika shirika, au ni meneja wa kampuni ambayo ni sehemu ya mkataba wowote unaoendelea na mamlaka ya serikali za mitaa ambayo anataka kuchaguliwa na hajatangaza katika magazeti yanayochapishwa kwa lugha ya ya Kiingereza lugha na Kiswahili yanayosambazwa ndani la eneo mamlaka inayohusika, taarifa inayoelezea aina ya mkataba na maslahi yake au maslahi ya shirika au kampuni katika mkataba; ya (h) ikiwa amepoteza sifa za kuwa mjumbe wa mamlaka ya serikali za mitaa kwa Sheria hii au chini ya sheria nyingine yoyote; (i) ikiwa amepoteza sifa za kuandikishwa kuwa mpiga kura chini ya Sheria hii au amepoteza sifa ya kupiga kura katika uchaguzi wowote chini ya Sheria hii au chini ya sheria nyingine yoyote inayohusu makosa ya uchaguzi; na (j) kwa kuzingatia upekee na ukomo kama Rais anavyoweza kuelekeza, kwa amri itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, iwapo anashikilia au anakaimu nafasi katika ofisi yoyote au uteuzi katika utumishi wa Jamhuri ya Muungano au mamlaka za serikali za mitaa. (2) Kwa madhumuni ya kifungu kidogo cha (1)(d)- (a) adhabu mbili au zaidi zinazopaswa kutumikiwa kwa kufuatana zitachukuliwa kuwa ni adhabu tofauti, na iwapo adhabu zote hazizidi miezi sita zitachukuliwa kuwa ni adhabu moja; na 57 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Siku ya uteuzi Uteuzi wa mgombea (b) adhabu ya kifungo iliyotolewa kama mbadala wa kulipa faini au kwa kushindwa kulipa faini haitazingatiwa. SEHEMU YA TATU UTEUZI WA WAGOMBEA UDIWANI - 70 Verify source ↗
Kujitoa au kukoma kwa ugombea
AI-assisted research summary: Mgombea anaweza kujitoa kwa kutoa na kuwasilisha taarifa ya maandishi iliyosainiwa kabla ya saa kumi kamili alasiri siku ya uteuzi.
70.-(1) Mgombea anaweza kujitoa ugombea kwa kutoa taarifa ya maandishi aliyoisaini na kuiwasilisha yeye mwenyewe kwa msimamizi wa 65 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 na chama uchaguzi kilichomdhamini kabla ya saa kumi kamili alasiri siku ya uteuzi. nakala tawi kwa la Kufariki kwa mgombea Kutokuwepo kwa wagombea (2) Kila taarifa ya kujitoa chini ya kifungu kidogo cha (1) itaambatishwa na tamko katika fomu itakayoainishwa, ambalo litajazwa na kusainiwa na mgombea mbele ya hakimu. (3) Kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (1), endapo mgombea atajitoa kugombea baada ya saa kumi kamili alasiri ya siku ya uteuzi, chama chake hakitaruhusiwa kuweka mgombea mwingine mbadala na dhamana iliyotolewa na mgombea itataifishwa. - 71 Verify source ↗
Kufariki kwa mgombea
AI-assisted research summary: If a candidate dies after 10:00 p.m. on nomination day and before polls close, the election supervisor must stop the election in that constituency or ward. The Commission must then set a new suitable date within 30 days and restart the nomination and election process, subject to the proviso for already validly nominated candidates.
71.-(1) Endapo baada ya saa kumi kamili alasiri ya siku ya uteuzi na kabla ya kufunga kupiga kura kwenye uchaguzi, mgombea katika jimbo au kata atafariki, msimamizi wa uchaguzi, baada ya kujiridhisha na taarifa ya kifo atasitisha uchaguzi katika jimbo au kata. (2) Ikitokea msimamizi wa uchaguzi amesitisha uchaguzi kwa mujibu wa masharti ya kifungu kidogo (1), Tume, kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, itapanga siku nyingine muafaka si zaidi ya siku thelathini baada ya kusitishwa huko kwa ajili ya uteuzi wa wagombea wa uchaguzi katika jimbo au kata na taratibu za uchaguzi katika jimbo au kata hiyo zitaanza upya: Isipokuwa kwamba, uteuzi mpya hautafanyika kuhusiana na mgombea mwingine yeyote aliyeteuliwa kihalali katika uteuzi uliopita na kila mgombea atachukuliwa kuwa ameteuliwa kihalali isipokuwa kama atatoa taarifa ya kujitoa. - 72 Verify source ↗
Kutokuwepo kwa wagombea
AI-assisted research summary: If there are no candidates after nomination day in a constituency or ward, the Commission must suspend the election and set a new nomination day within 30 days; campaign and election procedures restart.
72. Endapo baada ya siku ya uteuzi kwa sababu ya kifo, kujitoa au kwa sababu nyingine yoyote, hakuna wagombea katika jimbo au kata, Tume, kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, itasitisha uchaguzi na kupanga siku nyingine isiyozidi siku thelathini baada ya kusitishwa huko, kwa ajili ya uteuzi wa wagombea wa uchaguzi katika jimbo au kata 66 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Kampeni za uchaguzi na taratibu za uchaguzi katika jimbo au kata hiyo zitaanza upya. SEHEMU YA TATU KAMPENI ZA UCHAGUZI - 124 Verify source ↗
Makosa mengineyo
AI-assisted research summary: Mtu anayetoa ushahidi au maelezo ya uongo kwa makusudi katika tamko chini ya kifungu cha 87 anatenda kosa na anaweza kupewa faini, kifungo, au vyote kwa pamoja akitiwa hatiani.
124. Mtu ambaye kwa kukusudia anatoa ushahidi wa uongo au anatoa maelezo ya uongo katika tamko lililotolewa chini ya kifungu cha 87, anatenda kosa na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi elfu hamsini na isiyozidi shilingi laki moja au kifungo kisichopungua miezi sita na kisichozidi miezi kumi na mbili au vyote kwa pamoja. 102 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Utunzaji siri katika chaguzi - 125 Verify source ↗
Utunzaji siri katika chaguzi
AI-assisted research summary: Watu fulani waliopo kwenye kituo cha kupigia kura au wakati wa kuhesabu kura lazima waape kutunza siri na wakatazwe kufichua au kutafuta taarifa fulani za upigaji kura; ukiukaji ni kosa linaloleta faini au kifungo.
125.-(1) Kila afisa, karani, mkalimani, mgombea na wakala aliyeidhinishwa kuwepo kwenye kituo cha kupigia kura au wakati wa kuhesabu kura, isipokuwa kama ameapa kiapo cha kutunza siri chini ya masharti mengine yoyote ya Sheria hii, kabla ya kuhudhuria, atapaswa kuapa kiapo cha kutunza siri kwa namna iliyoainishwa. (2) Msimamizi wa uchaguzi atakuwa na mamlaka ya kusimamia viapo vyote vinavyotakiwa kutolewa chini ya masharti ya kifungu kidogo cha (1). (3) Kila afisa, karani, mkalimani, mgombea na wakala atakayekuwepo katika kituo cha kupigia kura, atatunza na kusaidia kutunza siri ya upigaji kura katika kituo hicho na hatatoa kwa mtu yeyote, isipokuwa kwa madhumuni yaliyoidhinishwa kisheria, taarifa yoyote kuhusu jina au namba ya mpiga kura aliyeomba au ambaye hajaomba karatasi ya kura au aliyepiga kura katika kituo au kuhusu alama rasmi. (4) Afisa, karani, mkalimani, mgombea, wakala au mtu mwingine yeyote, hatapata au kujaribu kupata katika kituo cha kupigia kura taarifa za mgombea kutoka kwa mtu yeyote aliye katika kituo hicho ambaye anakaribia kupiga kura au ameshapiga kura, au kufanya mawasiliano muda wowote na mtu yeyote, kuhusu taarifa zozote zilizopatikana katika kituo cha kupigia kura kuhusu mgombea ambaye mtu yeyote katika kituo hicho anakusudia kumpigia au amempigia kura. (5) Kila afisa, karani, mkalimani, mgombea au wakala ambaye atakuwepo wakati wa kuhesabu kura atatunza na kusaidia utunzaji wa siri za upigaji kura na hatathibitisha au kutoa taarifa yoyote aliyoipata wakati wa kuhesabu kura kwa mgombea ambaye kura yoyote imepigwa kwake na karatasi yoyote ya kura. (6) Mtu isipokuwa msimamizi wa kituo anayehudumu kwa madhumuni yaliyoainishwa na Sheria hii, au mtu anayemsaidia mtu asiyeweza kupiga kura na anayehudumu kwa madhumuni hayo, hatawasiliana au kujaribu kuwasiliana na mtu yeyote 103 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Kosa la hongo, takrima au kurubuni Sura ya 329 Adhabu ya kujifanya mtu mwingine Sura ya 16 Kupoteza sifa kwa kuhukumiwa kwa kosa la kitendo cha rushwa au kitendo haramu Watu wanaodaiwa kuwa na hatia ya ushawishi mbaya baada ya mtu huyo kupokea karatasi ya kura na kabla hajaweka karatasi hiyo ndani ya sanduku la kura. (7) Mtu atakayekiuka masharti ya kifungu hiki anatenda kosa na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi laki moja na isiyozidi shilingi laki tatu au atatumikia kifungo kwa kipindi kisichopungua miezi sita na kisichozidi miezi kumi na mbili au vyote kwa pamoja. - 126 Verify source ↗
Kosa la hongo, takrima au kurubuni
AI-assisted research summary: A person who gives a bribe, gift, or inducement commits a corruption offence and, if convicted, will be punished under the Anti-Corruption law.
126. Mtu ambaye anatenda kosa la kutoa hongo, takrima au kurubuni, anatenda kosa la kitendo cha rushwa na akitiwa hatiani ataadhibiwa kwa mujibu wa Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa. - 127 Verify source ↗
Adhabu ya kujifanya mtu mwingine
AI-assisted research summary: Mtu anayejifanya mtu mwingine, au anayesaidia, kushiriki, kushauri, au kuwezesha kosa hilo, anatenda kosa na akipatikana na hatia ataadhibiwa kwa mujibu wa Sheria ya Kanuni za Adhabu.
127. Mtu ambaye anatenda kosa la kujifanya mtu mwingine au kusaidia kufanya kosa hilo, kushiriki kutenda kosa, kushauri au kuwezesha kutendeka kwa kosa la kujifanya mtu mwingine, anatenda kosa na akitiwa hatiani ataadhibiwa kwa mujibu wa Sheria ya Kanuni za Adhabu. - 128 Verify source ↗
Kupoteza sifa kwa kuhukumiwa kwa kosa la kitendo cha rushwa au
AI-assisted research summary: A person convicted of bribery or an unlawful act, whose conviction has not been overturned, loses eligibility to be registered as a voter for five years and cannot be registered or vote in any election under this Act or any other law.
128. Mtu atakayetiwa hatiani kwa kitendo cha rushwa au kitendo haramu na ambaye hukumu yake haijatenguliwa na mahakama yenye mamlaka pamoja na adhabu nyingine yoyote, atapoteza sifa ya kuandikishwa kuwa mpiga kura kwa kipindi cha miaka mitano tangu tarehe aliyopatikana na hatia na hataweza kuandikishwa kuwa mpiga kura au kupiga kura katika uchaguzi wowote chini ya Sheria hii au sheria nyingine yoyote. - 129 Verify source ↗
Watu wanaodaiwa kuwa na hatia ya ushawishi mbaya
AI-assisted research summary: A person commits an offence if they use threats, force, restraint, harm, or trickery to make a voter vote, not vote, or stop them voting freely.
129. Mtu ambaye kwa dhahiri au kwa kificho, yeye mwenyewe au mtu mwingine kwa niaba yake, anatumia au kutishia kutumia nguvu, vurugu au kizuizi, au anasababisha au anatishia kusababisha yeye mwenyewe au mtu mwingine yeyote, jeraha la mwili au la kiroho, uharibifu, madhara, au hasara kwa au dhidi ya mpiga kura yeyote, kwa ajili ya kumshawishi au kumlazimisha mpiga kura huyo kupiga kura au kuacha kupiga kura, au ikiwa mpiga kura huyo 104 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 amepiga kura au ameacha kupiga kura katika uchaguzi wowote au ambaye, kwa kumteka nyara, vitisho au hila ya aina yoyote, kumkwamisha au kumzuia kutumia uhuru wa kupiga kura mpiga kura yeyote ama kupiga au kuacha kupiga kura katika uchaguzi wowote, anatenda kosa la ushawishi mbaya kwa maana ya Sheria hii. Hongo, rushwa na ushawishi mbaya kwa wajumbe na maafisa wa Tume Hatia kwa kujifanya mtu mwingine itakavyokuwa, - 130 Verify source ↗
Hongo, rushwa na ushawishi mbaya kwa wajumbe na maafisa wa
AI-assisted research summary: Mtu yeyote hapaswi kutoa hongo, rushwa au ushawishi mbaya kwa mjumbe au afisa wa Tume ili kumsaidia mgombea katika uchaguzi, au kwa nia ya kubagua ili kumpendelea mgombea.
130. Endapo mtu yeyote anatenda kitendo chochote ambacho ni hongo, rushwa au ushawishi mbaya kwa mjumbe au afisa wa Tume aliyerejewa katika Sheria hii kwa nia ya kwamba mjumbe au afisa, kadiri kwa kumpendelea mgombea mmoja au wagombea wengine katika uchaguzi, au pale ambapo mjumbe huyo au afisa anatenda kitendo hicho kwa nia ya kubagua au baada ya kubagua ili kumpendelea mgombea mmoja au wengine, mtu huyo atachukuliwa, kwa mujibu wa mazingira ya kesi, kuwa ametenda kosa la rushwa, hongo au ushawishi mbaya. ubaguzi afanye - 131 Verify source ↗
Hatia kwa kujifanya mtu mwingine
AI-assisted research summary: Katika uchaguzi wowote, mtu haruhusiwi kuomba au kupiga kura kwa jina la mtu mwingine, au kutoa kadi ya mpiga kura ya mtu mwingine ili apewe karatasi ya kura.
131. Mtu ambaye katika uchaguzi wowote- (a) anaomba karatasi ya kura kwa jina la mtu mwingine au kwa kujua anapiga kura kwa jina la mtu mwingine, iwe jina hilo ni jina la mtu anayeishi au amefariki au mtu wa kufikirika; au (b) kwa madhumuni ya yeye kupewa mwenyewe karatasi ya kura, akiwa anafahamu, anatoa kadi ya mpiga kura iliyotolewa kwa mtu mwingine, anatenda kosa la kujifanya mtu mwingine kwa maana ya Sheria hii. Adhabu ya vitendo vya rushwa na vitendo haramu - 132 Verify source ↗
Adhabu ya vitendo vya rushwa na vitendo haramu
AI-assisted research summary: Mtu anayehusika na vitendo vilivyoelezwa hapa katika uchaguzi anaweza kutenda kosa la rushwa au kosa la kitendo haramu, na adhabu inaweza kujumuisha faini, kifungo, au vyote kwa pamoja.
132.-(1) Mtu ambaye- (a) anashawishi au anamtumia mtu mwingine kupiga kura katika uchaguzi wowote kwa kufahamu kuwa mtu huyo mwingine ameshapiga kura katika uchaguzi huo; au (b) kwa madhumuni ya kuwezesha kutolewa 105 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Sura ya 329 kwa karatasi yoyote ya kura kwa mtu mwingine yeyote au yeye mwenyewe, anatoa kadi yoyote ya mpiga kura iliyotolewa kwake au mtu mwingine wa au tatu kwa mtu huyo mwingine anashawishi, au anamwezesha mtu wa tatu kutoa kadi ya mtu huyo wa tatu kwa yeye mwenyewe au mtu huyo mwingine; au (c) anamshawishi mtu mwingine kupiga kura katika uchaguzi wowote huku akijua kwamba mtu huyo hastahili kupiga kura au amekatazwa na Sheria hii au sheria nyingine yoyote kupiga kura katika uchaguzi huo, anatenda kosa la kitendo cha rushwa na akitiwa hatiani ataadhibiwa kwa mujibu wa Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa. (2) Mtu ambaye- (a) anapiga kura katika uchaguzi wowote huku akijua kwamba hastahili kupiga kura au amekatazwa na Sheria hii au sheria nyingine yoyote kupiga kura katika uchaguzi huo; (b) anapiga kura au anajaribu kupiga kura katika uchaguzi wowote kwa kufahamu kuwa ameshapiga kura katika uchaguzi huo; au (c) kwa madhumuni ya kujipatia karatasi ya kura huku akijua anatoa kadi batili ya mpiga kura, anatenda kosa la kitendo haramu na akipatikana na hatia atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi elfu hamsini na isiyozidi shilingi laki mbili au kifungo kwa kipindi kisichopungua miezi mitatu na kisichozidi miezi kumi na mbili au vyote kwa pamoja. Kuingilia mikutano halali ya hadhara kuwa ni kitendo haramu - 133 Verify source ↗
Kuingilia mikutano halali ya hadhara kuwa ni kitendo haramu
AI-assisted research summary: Mtu haruhusiwi kufanya au kuchochea vurugu kwenye mkutano halali wa hadhara wa uchaguzi ili kuzuia shughuli zilizopangwa kufanyika.
133. Mtu ambaye, katika mkutano halali wa hadhara unaofanyika kwa ajili ya uchaguzi wa mtu yeyote kati ya siku ya kutoa notisi ya siku ya uteuzi na siku ambayo matokeo ya uchaguzi yatatangazwa, 106 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Vitendo vinavyokatazwa siku ya uchaguzi anafanya au anachochea wengine kufanya vurugu kwa madhumuni ya kuzuia shughuli ambazo zimepangwa kufanyika katika mkutano ulioitishwa, anatenda kosa na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi elfu hamsini na isiyozidi shilingi laki mbili au kifungo kwa kipindi kisichopungua miezi sita na kisichozidi miezi kumi na mbili au vyote kwa pamoja. - 134 Verify source ↗
Vitendo vinavyokatazwa siku ya uchaguzi
AI-assisted research summary: A person must not hold a meeting on voting day or within the voting premises or 300 metres of them, and must not wear or display items showing support for a candidate.
134.-(1) Mtu hatafanya mkutano siku ya kupiga kura au ndani ya jengo au eneo lolote ambamo upigaji kura katika uchaguzi unaendelea, au mahali popote ndani ya eneo la mita mia tatu ya eneo au jengo hilo, hatavaa au kuonesha kadi, picha au nembo nyingine yoyote inayoonesha kuunga mkono mgombea fulani katika uchaguzi. (2) Mtu anayekiuka kifungu hiki anatenda kosa na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi elfu hamsini na isiyozidi shilingi laki moja. Unyanyasaji na ukatili wa kijinsia katika uchaguzi - 135 Verify source ↗
Unyanyasaji na ukatili wa kijinsia katika uchaguzi
AI-assisted research summary: A person who sexually harasses or uses sexual violence against a candidate during election activities commits an offence and is punishable under the Electoral Code of Conduct if convicted.
135. Mtu ambaye, wakati wa shughuli za uchaguzi, anatenda kitendo cha unyanyasaji au ukatili wa kijinsia kwa mgombea, anatenda kosa na akitiwa hatiani kwa mujibu wa Kanuni za Maadili ya Uchaguzi ataadhibiwa kwa mujibu wa Kanuni hizo. Kuchafua matangazo - 136 Verify source ↗
Kuchafua matangazo
AI-assisted research summary: Mtu asiyekuwa na mamlaka halali haruhusiwi kuharibu, kukata, kuchafua au kuondoa tangazo au nyaraka zilizoandikwa kwa mujibu wa Sheria hii kwa ajili ya ukaguzi.
136. Mtu ambaye bila mamlaka halali, anaharibu, anakata, anachafua au anaondoa tangazo lolote ambalo limewekwa kwa mujibu wa Sheria hii au nyaraka yoyote ambayo imewekwa kwa ajili ya ukaguzi kwa kuzingatia masharti ya Sheria hii, anatenda kosa na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi elfu thelathini na isiyozidi shilingi au kifungo kwa kipindi kisichopungua mwezi mmoja na kisichozidi miezi sita au vyote kwa pamoja. laki moja 107 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 SURA YA NANE KUPINGA MATOKEO YA UCHAGUZI KWA NJIA YA SHAURI LA UCHAGUZI SEHEMU YA KWANZA SHAURI LA UCHAGUZI KUPINGA MATOKEO YA UBUNGE Kupinga matokeo ya uchaguzi kwa njia ya shauri la uchaguzi - 139 Verify source ↗
Mashauri yanayosikilizwa na Mahakama Kuu
AI-assisted research summary: Mahakama Kuu inasikiliza na kuamua mashauri ya uchaguzi wa ubunge, na inaweza kuamuru watu wanaohusishwa na uchaguzi kuhudhuria kama mashahidi.
139.-(1) Kila shauri la uchaguzi wa ubunge litasikilizwa na kuamuliwa na Mahakama Kuu, ambayo kwa mujibu wa masharti ya Sehemu hii itajulikana kama “Mahakama”. (2) Mashahidi wataitwa na kuapishwa kwa namna ambayo mazingira yataruhusu kama ilivyo katika shauri la mahakama inapotekeleza mamlaka yake ya mwanzo ya kuendesha mashauri ya madai na, bila ya kuathiri masharti ya sheria nyingine yoyote, watawajibishwa kwa adhabu sawa na ile ya kutoa ushahidi wa uongo au kutohudhuria. (3) Wakati wa usikilizaji wa shauri la uchaguzi chini ya Sheria hii, Mahakama kwa amri, inaweza kumuamuru mtu yeyote ambaye anaonekana kuhusika katika uchaguzi ambao unatajwa katika shauri 109 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kuhudhuria kama shahidi, na mtu yeyote atakayekataa kutii amri hiyo anatenda kosa la kuidharau mahakama na Mahakama inaweza kumhoji shahidi yeyote ambaye ameamriwa kuhudhuria au mdaawa yeyote katika shauri na baada ya kuhojiwa na Mahakama, shahidi huyo anaweza kudodoswa na au kwa niaba ya mlalamikaji, mlalamikiwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali au mwakilishi wake, kama yupo, au mtu yeyote kati yao. (4) Wakati wa usikilizaji wa shauri la uchaguzi, Mahakama itakuwa na mamlaka ya kumuamuru mtu yeyote ambaye anaonekana na Mahakama kuwa amehusika uchaguzi kushiriki unaolalamikiwa au ambaye ushahidi wake unaweza kuisaidia Mahakama kufikia uamuzi wa haki na wa usawa katika shauri lililo mbele yake kuhudhuria kama shahidi. katika au Shauri na taratibu za kuweka dhamana ya gharama - 140 Verify source ↗
Shauri na taratibu za kuweka dhamana ya gharama
AI-assisted research summary: Shauri la uchaguzi linaweza kuletwa na watu fulani, lakini mlalamikaji anaweza kulazimika kuweka dhamana ya gharama na kufuata muda maalum.
140.-(1) Shauri la uchaguzi linaweza kuwasilishwa na mmoja au zaidi ya watu wafuatao: (a) mtu aliyepiga kura kihalali au alikuwa na haki ya kupiga kura katika uchaguzi ambao shauri linahusika; (b) mtu anayedai kuwa alikuwa na haki ya kuteuliwa au kuchaguliwa katika uchaguzi huo; (c) mtu anayedai kuwa alikuwa mgombea katika uchaguzi huo; au (d) Mwanasheria Mkuu wa Serikali. (2) Msajili wa Mahakama hatapanga tarehe ya kusikilizwa kwa shauri lolote la uchaguzi isipokuwa kama mlalamikaji amelipa mahakamani, dhamana ya gharama, kiasi kisichozidi shilingi milioni tano kwa kila mlalamikiwa. (3) Mlalamikaji atatakiwa ndani ya siku kumi na nne baada ya kuwasilisha shauri, kuwasilisha maombi kwa ajili ya uamuzi wa kiasi kitakacholipwa kama dhamana ya gharama, na mahakama itaamua maombi hayo ndani ya siku kumi na nne zinazofuata baada ya tarehe ya kuwasilisha maombi kwa ajili ya 110 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 uamuzi wa kiasi kitakacholipwa kama dhamana ya gharama. (4) Endapo mtu yeyote ataunganishwa kama mlalamikiwa kwa mujibu wa amri ya Mahakama, mlalamikaji, ndani ya siku kumi na nne kutoka tarehe ambayo ikielekeza mtu huyo aunganishwe kuwa mlalamikiwa, atalipa mahakamani kiasi kingine kisichozidi shilingi milioni tatu, kama itakavyoelekezwa na Mahakama kuhusu mtu huyo. ilitolewa amri (5) Endapo kwa maombi yatakayofanywa na mlalamikaji, Mahakama itaridhika kuwa utekelezaji wa masharti ya kifungu kidogo cha (2) au (4) utasababisha ugumu kwa mlalamikaji, inaweza kuelekeza kuwa- (a) mlalamikaji atoe aina nyingine ya dhamana thamani yake haizidi shilingi ambayo milioni tano kama ambavyo Mahakama itaona inafaa; au (b) mlalamikaji asamehewe kulipa aina yoyote ya dhamana ya gharama. (6) Hakuna amri itakayotolewa chini ya kifungu kidogo cha (3), (4) na (5) mpaka nafasi imetolewa kwa mlalamikiwa, au, iwapo kuna walalamikiwa wawili au zaidi, kwa kila mlalamikiwa kujieleza kwa madhumuni hayo. (7) Endapo dhamana ya gharama haitalipwa mahakamani ndani ya siku kumi na nne kutoka tarehe ya uamuzi wa Mahakama kuhusu kiasi cha malipo ya dhamana ya gharama, hakuna mwenendo wa shauri la uchaguzi utakaoendelea kusikilizwa na shauri hilo litafutwa. ile kwa yoyote (8) Masharti ya kifungu kidogo cha (2) na (3) hayatatumika ikiwa namna Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni mlalamikaji au mmoja wa walalamikaji. (9) Kiasi cha fedha kilichowekwa kama dhamana ya gharama au salio la dhamana hiyo, iwapo mlalamikaji atashinda katika shauri au rufaa na iwapo hakuna amri iliyotolewa dhidi ya mlalamikaji kulipa gharama, kitarejeshwa kwa mlalamikaji mapema iwezekanavyo. 111 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Nafuu zinazoweza kuombwa Uthibitisho wa uhalali wa uchaguzi Taarifa ya Mahakama kuhusu vitendo vya rushwa au vitendo haramu - 141 Verify source ↗
Nafuu zinazoweza kuombwa
AI-assisted research summary: Mlalamikaji akileta shauri la uchaguzi anaweza kuomba nafuu zote au baadhi ya nafuu zilizoorodheshwa.
141. Katika kuwasilisha shauri la uchaguzi, mlalamikaji anaweza kuomba nafuu zote au yoyote kati ya nafuu zifuatazo anazoweza kustahili: (a) tamko kwamba uchaguzi ni batili; (b) tamko kwamba uteuzi wa mtu aliyechaguliwa haukuwa halali; au (c) endapo kiti kinadaiwa na mgombea ambaye hakushinda kwa madai kwamba alikuwa amepata kura nyingi halali, kufanyika kwa uchunguzi wa kura. - 142 Verify source ↗
Uthibitisho wa uhalali wa uchaguzi
AI-assisted research summary: Mahakama ikimaliza shauri au rufaa ya uchaguzi, lazima iamue kama uchaguzi wa Mbunge ni halali au batili na ithibitishe uamuzi huo kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi.
142.-(1) Mahakama, wakati wa kuhitimisha shauri au rufaa ya shauri la uchaguzi, itaamua iwapo uchaguzi wake Mbunge unalalamikiwa, aliteuliwa au alichaguliwa ipasavyo, au uchaguzi ni batili, na itathibitisha uamuzi huo kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi. ambaye uteuzi au (2) Baada ya uthibitisho uliofanyika chini ya kifungu kidogo cha (1), uchaguzi utathibitishwa au uchaguzi mdogo utafanyika, kadri itakavyohitajika, kwa mujibu wa uthibitisho. - 143 Verify source ↗
Taarifa ya Mahakama kuhusu vitendo vya rushwa au vitendo haramu
AI-assisted research summary: If the court finds a person guilty of a corrupt or unlawful act, the Director of Elections must remove that person’s name from the voter register and notify the relevant returning officer.
143.-(1) Endapo Mahakama inaamua kuwa mtu ana hatia kwa kitendo chochote cha rushwa au kitendo itathibitisha hivyo kwa Mkurugenzi wa haramu, Uchaguzi na kama mtu anayehusika ameandikishwa kuwa mpiga kura- (a) Mkurugenzi wa Uchaguzi atafuta jina lake katika Daftari ambalo ameandikishwa; na (b) Mkurugenzi wa Uchaguzi atamjulisha kwa maandishi msimamizi wa uchaguzi wa eneo la uchaguzi husika kuhusu kufutwa huko. (2) Wakati wa kuhitimisha usikilizaji wa shauri la uchaguzi au rufaa, Mahakama itathibitisha kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi- (a) iwapo kitendo chochote cha rushwa au kitendo chochote haramu kimethibitishwa kutendwa na mgombea au kwa uelewa na ridhaa au idhini ya mgombea yeyote katika 112 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 uchaguzi na aina ya kitendo hicho, kama kipo; na (b) majina na taarifa nyingine za watu wote, kama zipo, ambao wamethibitishwa kwa kiasi cha kuiridhisha Mahakama kuwa wana hatia ya kitendo chochote cha rushwa au kitendo haramu. (3) Kabla mtu yeyote, ambaye si mhusika katika shauri la uchaguzi wala si mgombea ambaye kwa niaba yake, nafasi inayogombewa katika shauri la uchaguzi, hajathibitishwa na Mahakama chini ya kifungu hiki, Mahakama itampa mtu huyo nafasi ya kusikilizwa na kutoa ushahidi wa kuonesha kwa nini asithibitishwe. (4) Endapo Mahakama inathibitisha kuwa kosa la kitendo cha rushwa au kitendo haramu kimetendwa na mtu yeyote, mtu huyo atawajibishwa kwa kuondolewa sifa kama vile katika tarehe hiyo ya hati la kitendo angekuwa ametiwa hatiani kwa kosa haramu. (5) Endapo Mahakama imethibitisha kuwa kitendo cha rushwa au kitendo haramu kimefanyika na mtu yeyote kwa uelewa na ridhaa au ruhusa ya mgombea, pamoja na matokeo mengine yoyote, mgombea atawajibishwa kwa kuondolewa sifa kama vile wakati wa tarehe ya hati, angekuwa ametiwa hatiani kwa kosa la kitendo cha rushwa au kitendo haramu. (6) Mkurugenzi wa Uchaguzi mapema iwezekanavyo- (a) ataagiza nakala ya uthibitisho iliyotolewa chini ya kifungu hiki kuchapishwa katika Gazeti la Serikali; (b) atafuta kwenye Daftari jina la mtu yeyote aliyeandikishwa katika kumbukumbu kuondolewa sifa ya kupiga kura katika uchaguzi; na anayeonekana (c) atamtaarifu kwa maandishi msimamizi wa uchaguzi wa eneo la uchaguzi linalohusika kuhusu kufutwa kwa jina la mtu huyo 113 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 ambaye ameandikishwa kuwa mpiga kura katika eneo hilo la uchaguzi. (7) Mara baada ya kujulishwa, msimamizi wa uchaguzi atachukua hatua zote kama itakavyolazimu kuhakikisha kuwa mtu anayehusika anarejesha kadi ya mpiga kura na nyaraka nyingine zozote zinazohusika kwa ajili ya kufutwa. - 144 Verify source ↗
Muda wa kuwasilisha na kuamuliwa kwa shauri la uchaguzi na rufaa
AI-assisted research summary: This section sets deadlines for election petitions and appeals, and lets the Chief Justice extend time in limited circumstances.
144.-(1) Kila shauri la uchaguzi litawasilishwa ndani ya siku thelathini kuanzia tarehe ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi na msimamizi wa uchaguzi. (2) Mahakama itasikiliza na kuamua shauri la uchaguzi ndani ya miezi sita kuanzia tarehe ya kuwasilisha shauri. (3) Upande wa shauri ambao hautaridhika na uamuzi wa Mahakama chini ya kifungu kidogo cha (2) unaweza kukata rufaa ndani ya siku arobaini na tano kutoka tarehe ya uamuzi. (4) Rufaa iliyowasilishwa kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (3) itasikilizwa na Mahakama ya Rufani. (5) Mahakama itasikiliza na kuamua rufaa ndani ya miezi sita kuanzia tarehe ya kuwasilisha rufaa. (6) Endapo hakuna uwezekano wa kuamuliwa kwa shauri la uchaguzi ndani ya kipindi cha miezi sita, Jaji Mkuu na kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, anaweza kuongeza muda kwa kipindi kingine kisichozidi miezi sita, kama atakavyoamua. - 145 Verify source ↗
Kura zinazoweza kuondolewa wakati wa uchunguzi
AI-assisted research summary: During an election petition hearing, certain votes must be removed in the investigation, including votes affected by bribery, personation, multiple voting, or disqualification; a registered voter’s vote is not to be removed merely because the voter lacked qualifications to be entered in the register, except as stated for multiple voting.
145.-(1) Wakati wa uchunguzi katika kusikiliza shauri la uchaguzi, kura zifuatazo zitaondolewa: (a) kura ya mtu yeyote tofauti na mgombea au ya mtendaji aliyepiga kura chini ya kifungu cha 14(4) ambaye jina lake halikuwemo katika Daftari la eneo la uchaguzi ambalo amepigia kura; Muda wa kuwasilisha na kuamuliwa kwa shauri la uchaguzi na rufaa Kura zinazoweza kuondolewa wakati wa uchunguzi (b) kura ya mtu yeyote ambaye kura yake au ilipatikana takrima hongo, kwa 114 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kushawishiwa; (c) kura ya mtu yeyote ambaye ametenda kosa au amesababisha kutendeka kwa kosa la kujifanya mtu mwingine katika uchaguzi; (d) kura ya mtu yeyote aliyethibitishwa kupiga kura zaidi ya mara moja katika uchaguzi huo isipokuwa kura ya kwanza iliyopigwa na mtu huyo kama kura hiyo ya kwanza inaweza kutambuliwa kiasi cha kuiridhisha Mahakama; (e) kura ya mtu yeyote ambaye, kwa sababu ya kutiwa hatiani kwa kosa la kitendo haramu au kwa sababu ya hati ya Mahakama au kwa sababu ya kutiwa hatiani kwa kosa la kukiuka Sheria hii au sheria nyingine yoyote aliondolewa sifa ya kupiga kura katika uchaguzi. (2) Kura ya mpiga kura aliyeandikishwa haitaondolewa, wakati wa uchunguzi kwa sababu mpiga kura huyo hakuwa na sifa za lake kuingizwa katika Daftari isipokuwa kwa sababu zilizoainishwa katika kifungu kidogo cha (1)(d). jina - 146 Verify source ↗
Kanuni za Mahakama
AI-assisted research summary: Jaji Mkuu anaweza, baada ya kushauriana na Tume, kutunga kanuni za mahakama kwa ajili ya taratibu na desturi za mashauri ya uchaguzi na maombi, na kuweka ada itakayolipwa.
146.-(1) Jaji Mkuu kwa kushauriana na Tume anaweza kutunga kanuni za ahakama kusimamia taratibu na desturi za kufuatwa na kuweka ada itakayolipwa kuhusu mashauri ya uchaguzi na maombi chini ya Sura hii. (2) Kanuni zitakazotungwa chini ya Sura hii zitachapishwa katika Gazeti la Serikali. Kanuni za Mahakama SEHEMU YA TATU SHAURI LA UCHAGUZI KUPINGA MATOKEO YA UDIWANI Kupinga matokeo ya uchaguzi kwa njia ya mashauri ya uchaguzi
Part
SEHEMU YA TATU
- 24 Verify source ↗
Ukaguzi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura
AI-assisted research summary: Anyone may inspect the Preliminary Voters Register on days directed by the registration officer or as decided by the Director of Elections.
24.-(1) Mtu yeyote anaweza kukagua Daftari la Awali la Wapiga Kura la eneo lolote la uchaguzi katika siku afisa mwandikishaji atakavyoelekeza au kwa kadiri itakavyoamuliwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi. na muda kama (2) Afisa mwandikishaji ataweka wazi Daftari la Awali la Wapiga Kura katika kila kata na, ikilazimu, namna anaweza itakavyoelekezwa na Tume. kufanya marekebisho kwa - 25 Verify source ↗
Kuingizwa kwa jina katika Daftari la Awali la Wapiga Kura
AI-assisted research summary: A registered voter with a valid voter card whose name is missing from the preliminary voter register may apply for correction, and the election authority must add the name if satisfied it should have been included.
25.-(1) Endapo mtu yeyote aliyeandikishwa kuwa mpiga kura na ana kadi halali ya mpiga kura kuhusiana na eneo la uchaguzi, amebaini, kufuatia ukaguzi uliofanyika kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 24, kuwa jina lake halionekani katika Daftari la Awali la Wapiga Kura katika eneo la uchaguzi, mtu huyo anaweza kuomba kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, na Mkurugenzi wa Uchaguzi, au kama itakavyokuwa, afisa mwandikishaji, iwapo ataridhika kuwa jina la mtu huyo lilipaswa kuwemo katika Daftari la Awali la Wapiga Kura katika eneo la uchaguzi, atafanya marekebisho au kusababisha kufanywa marekebisho katika Daftari la Awali la Wapiga Kura kwa kuingiza jina la mtu huyo. (2) Endapo Mkurugenzi wa Uchaguzi au afisa mwandikishaji atakataa kufanya marekebisho katika Daftari la Awali la Wapiga Kura ili kuingiza jina la mtu yeyote, mtu ambaye hataridhika na kukataliwa huko anaweza kupinga kukataliwa huko kwa mujibu 30 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Pingamizi Utaratibu wa kuweka pingamizi Uchunguzi na uamuzi wa afisa mwandikishaji wa vifungu vinavyofuata katika Sehemu hii. - 26 Verify source ↗
Pingamizi
AI-assisted research summary: A person listed in the preliminary voter register may object to keeping their own name or someone else’s name in the register if the person lacks qualification, has lost qualification, or has died.
26.-(1) Mtu ambaye jina lake lipo katika Daftari la Awali la Wapiga Kura la eneo lolote la uchaguzi anaweza kupinga kuendelea kuwemo kwa jina lake mwenyewe au jina la mtu mwingine yeyote katika Daftari la Awali la Wapiga Kura kwa sababu yeye au mtu huyo mwingine hana sifa au amepoteza sifa za kuandikishwa au mtu huyo mwingine amefariki. (2) Mtu anayeweka pingamizi chini ya kifungu hiki atajulikana kama “mweka pingamizi”. - 27 Verify source ↗
Utaratibu wa kuweka pingamizi
AI-assisted research summary: Pingamizi lazima liwekwe kwa kujaza nakala mbili za fomu na kuwasilishwa kwa afisa mwandikishaji ndani ya muda ulioainishwa, pamoja na dhamana ya kiasi kitakachoainishwa na Tume.
27.-(1) Kila pingamizi litawekwa kwa kujaza nakala mbili za fomu iliyoainishwa na litawasilishwa kwa afisa mwandikishaji ndani ya muda ulioainishwa. litawasilishwa likiambatishwa na malipo ya dhamana ya kiasi cha fedha kitakachoainishwa na Tume kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali. pingamizi, Kila (2) (3) Afisa mapema mwandikishaji, iwezekanavyo pingamizi kupokea ya lililowekwa kwa mujibu wa Sehemu hii, atapeleka taarifa ya pingamizi hilo kwa mtu aliyewekewa pingamizi: baada Isipokuwa kwamba, afisa mwandikishaji atapaswa kubandika taarifa ya pingamizi katika mbao za matangazo katika kituo cha uandikishaji endapo pingamizi limewekwa kwa sababu mtu ambaye jina lake limo katika Daftari la Awali la Wapiga Kura amefariki. - 28 Verify source ↗
Uchunguzi na uamuzi wa afisa mwandikishaji
AI-assisted research summary: Afisa mwandikishaji lazima achunguze pingamizi, awaarifu wahusika kwa maandishi angalau siku saba kabla, na atoe uamuzi ndani ya siku saba baada ya notisi ya uchunguzi.
28.-(1) Afisa mwandikishaji mapema iwezekanavyo atafanya uchunguzi wa wazi kuhusu mapingamizi yote yaliyowekwa ipasavyo, kwa kutoa taarifa ya maandishi kwa muda usiopungua siku saba kuhusu tarehe, muda na mahali ambapo uchunguzi huo utaanza kwa kila mweka pingamizi na mtu ambaye amewekewa pingamizi, na kwa kila uchunguzi huo wa wazi kila mtu atakayeonekana na afisa mwandikishaji kuwa ana maslahi au ameathirika na uchunguzi huo wa 31 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 wazi anaweza kufika na kusikilizwa ama yeye mwenyewe au kupitia mtu mwingine yeyote aliyeidhinishwa kwa maandishi na mtu ambaye ana maslahi au aliyeathirika. (2) Endapo pingamizi limewekwa dhidi ya kuendelea kuwepo au kutokuwepo kwa jina lolote katika Daftari la Wapiga Kura, afisa mwandikishaji atamuita mweka pingamizi au mtu yeyote aliyeidhinishwa kwa maandishi na mweka pingamizi kwa ajili ya kutoa uthibitisho wa awali wa sababu za pingamizi. la Awali (3) Endapo kwa maoni ya afisa mwandikishaji uthibitisho wa awali umetolewa, afisa mwandikishaji atahitaji uthibitisho wa sifa zilizopo za kuandikishwa kwa mtu aliyewekewa pingamizi na- (a) ikiwa sifa za mtu huyo hazijathibitika kiasi cha kumridhisha afisa mwandikishaji, afisa mwandikishaji atamtaarifu Mkurugenzi wa Uchaguzi kuhusu hali hiyo na Mkurugenzi wa Uchaguzi atafuta au ataelekeza kufutwa kwa jina la mtu huyo katika Daftari la Awali la Wapiga Kura; au au atabakiza, (b) ikiwa sifa za mtu huyo zitathibitishwa, afisa mwandikishaji atamtaarifu Mkurugenzi wa Uchaguzi kuhusu hali hiyo na Mkurugenzi kama wa Uchaguzi itakavyokuwa, ataingiza au ataelekeza kubakizwa au kuingizwa jina la mtu huyo katika Daftari la Awali la Wapiga Kura. (4) Endapo katika tarehe iliyopangwa kwa ajili ya uchunguzi wa pingamizi lolote, mweka pingamizi au mtu mwingine yeyote aliyeidhinishwa kwa maandishi kwa niaba ya mweka pingamizi, atashindwa na kushindwa kutoa kuhudhuria au atahudhuria uthibitisho wa afisa mwandikishaji, afisa mwandikishaji atalibakiza au la mtu huyo kuelekeza aliyewekewa pingamizi katika Daftari au, kama itakavyokuwa, kufanya marekebisho katika Daftari la Awali la Wapiga Kura ili kubakizwa kwa kumridhisha awali wa hatachukua hatua jina ya 32 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kubakiza jina la mtu aliyewekewa pingamizi katika Daftari la Awali la Wapiga Kura. (5) Endapo pingamizi linakataliwa na afisa mwandikishaji na kwa maoni yake, ataona pingamizi liliwekwa bila sababu za msingi, afisa mwandikishaji anaweza, kwa kadiri atakavyoona inafaa, kuagiza kwa maandishi kuwa mweka pingamizi amlipe mtu aliyewekewa pingamizi fidia ya kiasi cha fedha kama Tume itakavyoainisha kwa notisi itakayotolewa katika Gazeti la Serikali. (6) Kiasi chochote kitakachoagizwa kutolewa kama fidia chini ya kifungu hiki kitapatikana kama vile amri ya afisa mwandikishaji ni amri ya kukaza hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Mwanzo kwa ajili ya urejeshaji wa fedha. (7) Endapo pingamizi litakataliwa na afisa mwandikishaji na endapo kwa maoni yake ataona kuwa pingamizi liliwekwa bila sababu za msingi, dhamana ya kiasi cha fedha kilichowekwa na mweka pingamizi kwa kadiri Tume itakavyoainisha kwa notisi katika Gazeti la Serikali, itataifishwa kwa Serikali kwa amri ya afisa mwandikishaji, au ikiwa hakuna amri iliyotolewa, dhamana itarejeshwa. (8) Afisa mwandikishaji atatoa uamuzi kuhusu pingamizi lililowekwa chini ya Sehemu hii ndani ya siku saba tangu siku ya mwisho ya kutolewa kwa notisi ya uchunguzi. - 29 Verify source ↗
Mweka pingamizi au mtu aliyewekewa pingamizi anaweza kukata
AI-assisted research summary: Mweka pingamizi au mtu aliyewekewa pingamizi anaweza kukata rufaa Mahakama ya Mwanzo ndani ya siku saba dhidi ya uamuzi wa afisa mwandikishaji chini ya kifungu cha 28.
29.-(1) Endapo mweka pingamizi au mtu aliyewekewa pingamizi hataridhika na uamuzi wa afisa mwandikishaji chini ya kifungu cha 28, mweka pingamizi au mtu huyo anaweza, ndani ya siku saba tangu tarehe ya uamuzi huo kutolewa, kukata rufaa katika Mahakama ya Mwanzo. (2) Mahakama ya Mwanzo itatoa uamuzi wa rufaa ndani ya siku kumi na nne tangu siku rufaa ilipowasilishwa. 33 Mweka pingamizi au mtu aliyewekewa pingamizi anaweza kukata rufaa Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 SEHEMU YA NNE RUFAA NA KUONGEZWA AU KUFUTWA KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA Rufaa kwenda Mahakama ya Mwanzo - 61 Verify source ↗
Siku ya uteuzi
AI-assisted research summary: Tume must publish a notice and set a nomination day for ward councilor elections, may set different nomination days for different wards, and must give at least seven days’ notice.
61.-(1) Endapo uchaguzi wa diwani utafanyika katika kata, au ikiwa uchaguzi huo utasitishwa na taratibu za uchaguzi zitatakiwa kuanza upya, Tume, kwa notisi itakayochapisha katika Gazeti la Serikali, itapanga siku ya uteuzi kwa ajili ya uteuzi wa wagombea wa uchaguzi. (2) Tume inaweza kupanga siku tofauti za uteuzi kwa ajili ya kata tofauti na inaweza kutengua siku ya uteuzi iliyopangwa na kupanga siku nyingine kuwa siku ya uteuzi. (3) Tume itatoa taarifa ya angalau siku saba kwa ajili ya uteuzi. - 62 Verify source ↗
Uteuzi wa mgombea
AI-assisted research summary: A candidate in a ward must be sponsored in writing by at least 10 registered voters, and must submit the signed nomination forms by the stated deadline.
62.-(1) Ili mtu aweze kuteuliwa kihalali kuwa mgombea katika kata, ni lazima awe amedhaminiwa kwa maandishi na wapiga kura wasiopungua kumi walioandikishwa katika kata ambayo yeye ni mgombea. (2) Uteuzi utafanyika kwa kutumia fomu itakayoainishwa ambayo itazingatia matumizi ya watu wenye mahitaji maalumu, itakayosainiwa na mgombea na watu wanaomdhamini mgombea huyo na itakuwa na taarifa zifuatazo: (a) jina, jinsi, hali ya ulemavu, ikiwa ipo, anwani na kazi ya mgombea; (b) majina na anwani za wadhamini na namba za kadi zao za kupiga kura; (c) tamko la mgombea kuwa yupo tayari na ana sifa za kuwa mgombea katika uchaguzi; (d) uthibitisho wa msimamizi wa uchaguzi wadhamini ambayo kata katika wameandikishwa; na (e) kiapo cha mgombea kitakachojazwa na 58 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kusainiwa na mgombea mbele ya hakimu na kitakachoonesha sifa za mgombea na kuwa hajapoteza sifa kwa ajili ya uchaguzi. (3) Kila fomu ya uteuzi itaambatishwa na- (a) idadi ya picha za mgombea kama Tume itakavyoelekeza, zilizopigwa si zaidi ya miezi mitatu kabla ya siku ya uteuzi; na (b) taarifa binafsi zinazomhusu mgombea kama itakavyohitajika kutolewa na kanuni kwa namna itakayokuwa imeelekezwa. (4) Endapo, kwa vyovyote vile, fomu ya uteuzi haijaambatishwa na nyaraka zilizoainishwa katika kifungu kidogo cha (3), uteuzi wa mgombea utachukuliwa kuwa batili: Isipokuwa kwamba, Tume, katika mazingira yoyote mahsusi na kama itaona kuna sababu ya kufanya hivyo, inaweza kuelekeza kuwa fomu ya uteuzi ikubaliwe kuwa halali bila kujali kuwa fomu hiyo ya uteuzi haikuambatishwa na nyaraka zozote iwapo nyaraka zinazohusika zitawasilishwa kwa msimamizi wa uchaguzi ndani ya muda mwingine kama ambavyo Tume inaweza kuruhusu. (5) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (1), katika siku ya uteuzi, Tume inaweza kukataa kumteua mtu kuwa mgombea iwapo itaridhika kuwa mtu huyo ameondolewa kushiriki katika mchakato wa uteuzi na Msajili wa Vyama vya Siasa kwa mujibu wa masharti ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi. (6) Msimamizi wa uchaguzi atatoa fomu za uteuzi kwa mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa au mpiga kura aliyeidhinishwa na chama cha siasa kwa maandishi na atampa idadi ya fomu za uteuzi kama itakavyoelekezwa na Tume. (7) Kila mgombea atawasilisha fomu za uteuzi zilizosainiwa kama ilivyoainishwa chini ya kifungu hiki, katika ofisi ya msimamizi wa uchaguzi si zaidi ya saa kumi kamili alasiri ya siku ya uteuzi: Sura ya 278 Isipokuwa kwamba, ikiwa Tume itaona zipo sababu za msingi za mgombea mwenyewe kushindwa chama kuwasilisha hizo, kiongozi wa fomu 59 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kilichomdhamini anaweza kuwasilisha fomu hizo kwa niaba yake. (8) Msimamizi wa uchaguzi, mapema iwezekanavyo atabandika nakala ya fomu ya uteuzi katika sehemu ya wazi inayoonekana nje ya ofisi yake. (9) Mtu hatamdhamini mgombea zaidi ya mmoja kwa uchaguzi mmoja na iwapo msimamizi wa uchaguzi ametoa hati chini ya kifungu kidogo cha (4)(b) kwa ajili ya udhamini wa mgombea mmoja, atakataa kutoa hati ya udhamini wa mtu huyo kwa mgombea mwingine katika uchaguzi mmoja: Isipokuwa kwamba, mtu hatazuiwa kusaini fomu ya uteuzi kwa sababu tu amekwisha saini fomu ya mgombea aliyefariki au aliyejitoa kabla ya kuwasilisha fomu ya uteuzi ya mwanzo. (10) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (9), iwapo mdhamini atamdhamini mgombea zaidi ya mmoja katika uchaguzi mmoja na hati zimetolewa chini ya kifungu kidogo cha (2)(d) kwa ajili ya uandikishwaji wa mtu huyo, udhamini wa wagombea wote wawili utakuwa ni halali. (11) Mtu yeyote atakayemdhamini mgombea zaidi ya mmoja anatenda kosa, na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyozidi shilingi laki mbili. (12) Endapo msimamizi wa uchaguzi ataridhika kuwa mtu yeyote ametenda kosa chini ya kifungu kidogo cha (11), anaweza kufifilisha kosa na kuamuru mtu huyo kulipa kiasi cha fedha: Isipokuwa kwamba- (a) kiasi hicho cha fedha kitakachotozwa hakitakuwa zaidi ya kiasi cha juu cha faini iliyowekwa kwa kosa hilo; (b) mamlaka yaliyotolewa na kifungu hiki kidogo yatatumika kama mtu atakiri kwa maandishi kuwa ametenda kosa; na (c) msimamizi wa uchaguzi atatoa stakabadhi ya malipo kwa mtu aliyetoa kiasi hicho cha fedha. (13) Msimamizi wa uchaguzi, atakapoombwa na mgombea au mtu mwingine kwa niaba yake, kutoa 60 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Dhamana hati kuhusu mdhamini aliyeandikishwa katika eneo la uchaguzi analohudumu, atatoa hati hiyo ipasavyo. (14) Endapo baada ya siku ya awali ya uteuzi, jina la mtu aliyemdhamini mgombea litafutwa kutoka la kata husika, kufutwa huko katika Daftari hakutabatilisha udhamini wa mgombea huyo. - 63 Verify source ↗
Dhamana
AI-assisted research summary: A candidate must lodge a nomination deposit with the election supervisor when returning the nomination form.
63.-(1) Wakati wa kurudisha fomu ya uteuzi kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 62, mgombea ataweka dhamana kwa msimamizi wa uchaguzi ya kiasi cha fedha kitakachoainishwa. (2) Dhamana ya mgombea anayepingwa itataifishwa kwa Serikali ikiwa atajiondoa kugombea baada ya siku ya uteuzi au ikiwa idadi ya kura alizopigiwa katika uchaguzi ni chini ya moja ya kumi ya kura zote zilizohesabiwa katika kata ambayo alikuwa ni mgombea, isipokuwa dhamana hiyo haitataifishwa ikiwa mgombea atafariki. (3) Endapo dhamana ya mgombea haitataifishwa chini ya masharti ya kifungu kidogo cha (2), mapema iwezekanavyo baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi, msimamizi wa uchaguzi atamrejeshea mgombea au mwakilishi wake wa kisheria kama itakavyokuwa. Mgombea kuteuliwa kwa nafasi moja tu - 64 Verify source ↗
Mgombea kuteuliwa kwa nafasi moja tu
AI-assisted research summary: A person may not be nominated as a candidate in more than one ward election.
64. Mtu hatateuliwa kuwa mgombea wa uchaguzi katika kata zaidi ya moja. Pingamizi na uamuzi kuhusu uhalali wa fomu ya uteuzi - 65 Verify source ↗
Pingamizi na uamuzi kuhusu uhalali wa fomu ya uteuzi
AI-assisted research summary: This section allows objections to nomination forms, sets who may object and when, and requires the election supervisor to notify and hear the person objected to before deciding.
65.-(1) Pingamizi linaweza kuwekwa dhidi ya fomu ya uteuzi kutokana na sababu zote au yoyote kati ya sababu zifuatazo: (a) taarifa zilizotolewa kuhusu mgombea hazitoshelezi kumtambulisha; (b) fomu ya uteuzi haikidhi au haikuwasilishwa kwa mujibu wa masharti ya Sehemu hii; (c) ni dhahiri kwamba kutokana na taarifa zilizomo katika fomu ya uteuzi mgombea hana sifa za kugombea katika uchaguzi; (d) masharti yaliyowekwa katika kifungu cha 62(2) hayajazingatiwa; na 61 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Sura ya 278 (e) masharti ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi hayajazingatiwa. (2) Hakuna pingamizi dhidi ya fomu ya uteuzi litakalokubaliwa isipokuwa tu kama limewasilishwa kwa msimamizi wa uchaguzi au msimamizi msaidizi wa uchaguzi, si zaidi ya saa kumi kamili alasiri ya siku inayofuatia siku ya uteuzi. (3) Pingamizi linaweza kuwekwa na mgombea mwingine ndani ya jimbo, Msajili wa Vyama vya Siasa au Mwanasheria Mkuu wa Serikali, isipokuwa kwa pingamizi chini ya kifungu kidogo cha (1)(e) ambalo linaweza kuwekwa na Msajili wa Vyama vya Siasa pekee, na litawekwa kwa maandishi na kusainiwa na mweka pingamizi, na litabainisha sababu za pingamizi. (4) Msimamizi wa uchaguzi au msimamizi msaidizi wa uchaguzi kabla ya kuamua juu ya uhalali wa pingamizi lolote na bila kuchelewa- (a) atamtaarifu mtu aliyewekewa pingamizi; na (b) atampa mtu huyo nafasi ya kusikilizwa. (5) Endapo msimamizi msaidizi wa uchaguzi anatoa uamuzi kuhusiana na pingamizi lolote chini ya kifungu kidogo cha (4), atawasilisha uamuzi huo kwa msimamizi wa uchaguzi ambaye bila kuchelewa, atapitia uamuzi unaohusika, na anaweza kukubaliana au kutengua uamuzi wa msimamizi msaidizi wa uchaguzi. (6) Endapo msimamizi wa uchaguzi anatoa uamuzi kuhusiana na pingamizi lolote chini ya kifungu (5), atamjulisha mgombea kidogo cha anayehusika kuhusu uamuzi wake na sababu za uamuzi wake. (4) au (7) Mgombea yeyote ambaye hataridhika na uamuzi wa msimamizi wa uchaguzi kuhusu uhalali wa pingamizi, kwa kuzingatia utaratibu na ndani ya muda utakaoainishwa na Tume, anaweza kukata rufaa kwa Tume, na uamuzi wa Tume utakuwa ni wa mwisho na hautahojiwa na mahakama yoyote, isipokuwa kwa njia ya mashauri ya uchaguzi yatakayowasilishwa kwa mujibu wa masharti ya Sura ya Nane kutokana na 62 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Mgombea pekee nafasi ya udiwani Picha sababu moja au nyinginezo zilizoainishwa katika Sura hiyo. (8) Bila kujali masharti yoyote ya kifungu hiki, pingamizi lililowekwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, litawasilishwa ndani ya siku kumi na nne baada ya siku ya uteuzi. - 66 Verify source ↗
Mgombea pekee nafasi ya udiwani
AI-assisted research summary: A lone valid candidate for a ward councillor seat must be declared the sole candidate, and if that candidate does not get the required votes, the Commission must be notified and arrange another nomination and voting day within 40 days.
66.-(1) Endapo kutakuwa na mgombea mmoja halali wa kiti cha udiwani aliyeteuliwa, msimamizi msaidizi wa uchaguzi atamtangaza mgombea huyo kuwa mgombea pekee wa nafasi ya udiwani. (2) Mgombea udiwani aliyetangazwa chini ya kifungu kidogo cha (1) atakuwa amechaguliwa kihalali kuwa Diwani endapo atapata kura nyingi za ndiyo kati ya kura zote halali zilizopigwa. (3) Endapo mgombea pekee wa kiti cha udiwani atashindwa kupata idadi ya kura zinazohitajika kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (2), msimamizi msaidizi wa uchaguzi ataitaarifu Tume kuhusu matokeo hayo na Tume, kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, itapanga siku nyingine ya uteuzi na upigaji kura itakayofaa si zaidi ya siku arobaini baada ya siku ya uchaguzi. (4) Ikiwa msimamizi wa uchaguzi wa kata yoyote ataamua kuwa hakuna mgombea aliyeteuliwa kihalali kwa ajili ya uchaguzi katika kata hiyo, msimamizi wa uchaguzi ataitaarifu Tume. - 67 Verify source ↗
Picha
AI-assisted research summary: Wagombea hutambuliwa kwa kutumia picha iliyoidhinishwa na msimamizi wa uchaguzi.
67.-(1) Kwa madhumuni ya kuwasaidia wapiga kura kumtambua mgombea wakati wa kupiga kura, kila mgombea atatambuliwa kwa kutumia picha ya mgombea ambayo imeidhinishwa na msimamizi wa uchaguzi. (2) Picha ya mgombea itakayooneshwa wakati wa kampeni za uchaguzi itakuwa chini ya usimamizi wa msimamizi wa uchaguzi. 63 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 SURA YA SITA UCHAGUZI, UTARATIBU WA KUPIGA KURA NA UTEUZI WA WABUNGE NA MADIWANI WANAWAKE VITI MAALUMU Wagombea walioteuliwa na siku ya uchaguzi Tangazo la uchaguzi SEHEMU YA KWANZA SIKU YA UCHAGUZI - 73 Verify source ↗
Kampeni za uchaguzi
AI-assisted research summary: Katika uchaguzi unaoshindaniwa jimbo au kata, kampeni zitaendeshwa na mgombea, chama chake au wakala wake, na ratiba ya mikutano ya kampeni inapaswa kuwasilishwa; msimamizi wa uchaguzi pia anaweza kuratibu na kushauri mabadiliko ili kuepuka migongano.
73.-(1) Endapo kuna uchaguzi unaoshindaniwa jimbo au kata, kampeni za uchaguzi katika zitaendeshwa na mgombea, chama chake au wakala wake. (2) Mgombea, wakala wake au chama chake itakavyokuwa, atawasilisha kwa cha siasa, kadiri msimamizi wa uchaguzi mapendekezo ya ratiba inayoonesha mpangilio unaopendekezwa kufanya mikutano ya hadhara ya kampeni ya mgombea ikiainisha muda na mahali mikutano itakapofanyika. (3) Mgombea, wakala wake au chama cha siasa kwa idhini au ridhaa ya mgombea anaweza kuitisha na kuhutubia mkutano wowote wa hadhara katika jimbo au kata utakaofanyika kwa mujibu wa kifungu kidogo cha la kumwezesha mgombea kuchaguliwa au kuendesha kampeni za hadhara au nyumba kwa nyumba. (2), kwa lengo (4) Kwa madhumuni ya kuhakikisha amani na utulivu katika mikutano wakati wa kipindi cha kampeni, msimamizi wa uchaguzi ataitisha mkutano wa wagombea wote au mawakala wa vyama na kupitia ratiba za kampeni za wagombea wote na kama italazimu kuwashauri wagombea kufanya mabadiliko katika ratiba zao kwa lengo la kuepuka migongano ya mikutano. (5) Kila msimamizi wa uchaguzi atawasilisha nakala ya ratiba iliyoratibiwa kwa Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Polisi wa Wilaya katika jimbo au kata na ratiba hiyo itachukuliwa kuwa ni taarifa ya mikutano inayopendekezwa kwa madhumuni ya Sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Jeshi la Polisi na Huduma Saidizi. (6) Bila kujali kifungu kidogo cha (5), mikutano ya hadhara haitafanyika katika jimbo au kata 67 Sura ya 258 Sura ya 332 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Upatikanaji na wajibu wa vyombo vya habari vya umma kwa madhumuni ya kuwezesha kampeni za uchaguzi za mgombea katika siku yoyote ya uchaguzi au pale ambapo siku mpya ya uchaguzi imepangwa kwa mujibu wa kifungu cha 71(2), siku nyingine yoyote baada ya siku ya awali ya uchaguzi iliyopangwa. - 74 Verify source ↗
Upatikanaji na wajibu wa vyombo vya habari vya umma
AI-assisted research summary: Wagombea wa Rais na Makamu wa Rais na vyama vyao vya siasa wana haki ya kutumia redio na runinga za umma wakati wa kampeni, na Tume inaweza kupanga matumizi hayo. Vyombo vya habari vya Serikali vinavyoripoti uchaguzi lazima viwe na upendeleo wa kutokuwapo na ubaguzi.
74.-(1) Kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (2), wagombea wa nafasi ya kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano na vyama vya siasa vinavyoshiriki katika uchaguzi huo watakuwa na haki ya kutumia huduma ya vituo vya umma vya kurushia matangazo ya redio na runinga wakati wa kipindi cha kampeni za uchaguzi. (2) Baada ya kushauriana na wagombea, vyama vya siasa vinavyohusika na maafisa wanaohusika na vyombo vya habari vya umma, Tume itaratibu matumizi ya haki za matangazo chini ya kifungu hiki. (3) Kila chombo cha habari kinachomilikiwa na Serikali kinachochapisha taarifa kuhusu mchakato wa uchaguzi kitaongozwa na misingi ya kutokuwa na upendeleo namna kitakavyowatendea wagombea katika uandishi wa habari na kwa kiwango cha nafasi kitakachotengwa kwa ajili ya wagombea. kuepuka ubaguzi kwa na (4) Kwa madhumuni ya utekelezaji wa kifungu hiki, Tume inaweza kutoa maelekezo kwa maandishi ambayo yatapaswa kuzingatiwa na chombo chochote cha habari kinachomilikiwa na Serikali. SEHEMU YA NNE UTARATIBU WA UCHAGUZI Siku na muda wa kupiga kura - 147 Verify source ↗
Kupinga matokeo ya uchaguzi kwa njia ya mashauri ya uchaguzi
AI-assisted research summary: Uchaguzi wa mgombea Udiwani unaweza kubatilishwa tu kwa shauri la uchaguzi, na chini ya hali fulani za rushwa, vitendo haramu, ukiukaji wa sheria, au kutokidhi sifa za kuchaguliwa.
147.-(1) Uchaguzi wa mgombea Udiwani hautahojiwa isipokuwa kwa shauri la uchaguzi. (2) Uchaguzi wa mgombea Udiwani utatangazwa kuwa batili kutokana na mojawapo kati ya sababu zifuatazo ikiwa zitathibitishwa kwa kiwango cha kuiridhisha Mahakama: 115 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 (a) kwamba kwa sababu ya vitendo vya rushwa au vitendo haramu vilivyotendwa kuhusiana na uchaguzi, au mazingira mengine ambayo yanafanana na hayo yaliyotajwa au yasiyotajwa, wapiga kura walio wengi walizuiwa au wanaweza kuwa walizuiwa kumchagua mgombea ambaye walimtaka; (b) kwamba, wakati wa kampeni za uchaguzi, maelezo yaliyotolewa na mgombea, au kwa niaba yake na kwa ufahamu wake na ridhaa au idhini yake, kwa nia ya kutumia hoja za tofauti ukabila, zinazohusu uchaguzi au kuhusu yeyote kati ya wagombea au iwapo wagombea si wa jinsi moja, kwa nia ya kutumia tofauti hizo; (c) kutozingatia masharti ya Sheria hii kuhusu uchaguzi, iwapo itajitokeza kuwa uchaguzi haukufanyika kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa katika masharti hayo na kuwa kutozingatia huko kumeathiri matokeo ya uchaguzi; au udini rangi au (d) kwamba kitendo cha rushwa au kitendo haramu kilitendwa kuhusiana na uchaguzi na mgombea au kwa ufahamu na kwa ridhaa au idhini ya mgombea au kwa ufahamu na ridhaa au idhini ya mmoja wa mawakala wake; au (e) kwamba mgombea wakati wa kuchaguliwa kwake hakuwa mtu mwenye sifa ya kuchaguliwa kuwa Diwani. (3) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (2), pale ambapo wakati wa usikilizaji wa shauri la uchaguzi kuhusu uchaguzi chini ya Sheria hii, mahakama inabaini kuwa kitendo cha rushwa au kitendo haramu kuhusu uchaguzi kimetendwa na au kwa ufahamu na ridhaa au idhini ya wakala yeyote wa mgombea, na mahakama ikabaini zaidi baada ya kumpa Mwanasheria Mkuu wa Serikali nafasi ya kusikilizwa, ameithibitishia mahakama kwamba- kwamba mgombea 116 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Kusamehewa kwa kutenda au kutokutenda matendo fulani (a) hakuna kitendo cha rushwa au kitendo haramu na mgombea mwenyewe au kwa ufahamu na ridhaa au idhini ya mgombea au wakala wake; kilichotendwa (b) mgombea alichukua hatua zote zinazostahili kuzuia kufanyika kwa vitendo vya rushwa au vitendo haramu katika uchaguzi huo; na (c) kwa namna nyingine yoyote uchaguzi haukuwa na kitendo chochote haramu kwa upande wa mgombea na wakala wake, ikiwa mahakama itaamua hivyo, kuchaguliwa kwa mgombea huyo hakutakuwa batili kwa sababu ya kitendo chochote kile. - 148 Verify source ↗
Kusamehewa kwa kutenda au kutokutenda matendo fulani
AI-assisted research summary: Mahakama inaweza kuondoa athari za Sheria hii kwa kitendo au kutokutenda kwa mgombea, wakala, au mtu mwingine, ikiwa kilifanyika kwa nia njema au kwa kosa la bahati mbaya na mazingira yanaonyesha ni vema kufanya hivyo.
148. Endapo mahakama itaona ama kwa ombi au kwa shauri la uchaguzi- (a) kwamba kitendo chochote au kutotenda kwa mgombea katika uchaguzi wowote au wakala wake au mtu mwingine yeyote ambacho isipokuwa kwa kifungu hiki kingekuwa ni kitendo cha rushwa au kitendo haramu, kimetendeka au kilifanyika kwa nia njema kwa kughafilika au kukosea kwa bahati mbaya au kwa sababu nyingine yoyote inayofanana na hizo; na (b) kwamba kwa sababu ya mazingira itakuwa vema kwa mgombea huyo au wakala wake au mtu mwingine yeyote, au yeyote kati yao, asihusishwe na athari zozote chini ya Sheria hii kwa kutenda au kutotenda, mahakama inaweza kutoa amri kuruhusu kitendo au kutotenda jambo hilo kutofungwa na masharti ya Sheria hii ambapo vinginevyo kungefanya kutenda au kutotenda kuwa ni kitendo cha rushwa au kitendo haramu, na mgombea, wakala au mtu mwingine yeyote hatahusishwa na athari yoyote chini ya Sheria hii kwa kutenda au kutotenda. Mashauri yanayosikilizwa na Mahakama ya - 149 Verify source ↗
Mashauri yanayosikilizwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi
AI-assisted research summary: Mashauri ya uchaguzi wa udiwani na maombi chini ya Sehemu hii husikilizwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi, na rufaa husikilizwa na Mahakama Kuu.
149.-(1) Kila shauri la uchaguzi wa udiwani na maombi chini ya Sehemu hii yatasikilizwa na 117 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Hakimu Mkazi mahakama ya Hakimu Mkazi, ambayo itajulikana kama “mahakama”. (2) Upande wa shauri ambao hautaridhika na uamuzi wa mahakama ya Hakimu Mkazi chini ya kifungu kidogo cha (2) unaweza kukata rufaa ndani ya siku arobaini na tano kutoka tarehe ya uamuzi. zote chini ya Sehemu hii (3) Rufaa zitasikilizwa na Mahakama Kuu. Mashauri na kuweka dhamana ya gharama - 150 Verify source ↗
Mashauri na kuweka dhamana ya gharama
AI-assisted research summary: Shauri la uchaguzi linaweza kuwasilishwa na watu fulani, lakini mlalamikaji lazima alipe dhamana ya gharama na afuate muda uliowekwa kabla ya shauri kusikilizwa.
150.-(1) Shauri la uchaguzi linaweza kuwasilishwa na mmoja au zaidi ya watu wafuatao: (a) mtu aliyepiga kura kihalali au alikuwa na haki ya kupiga kura katika uchaguzi ambao shauri linahusika; (b) mtu anayedai kuwa alikuwa na haki ya kuteuliwa au kuchaguliwa katika uchaguzi; alikuwa anadai kuwa mgombea katika uchaguzi huo; au ambaye (c) mtu (d) Mwanasheria Mkuu wa Serikali. (2) Msajili wa mahakama hatapanga tarehe ya kusikilizwa isipokuwa kama mlalamikaji amelipa mahakamani dhamana ya gharama, kiasi kisichozidi shilingi laki tano kwa kila mlalamikiwa. shauri (3) Mlalamikaji atatakiwa ndani ya siku kumi na nne baada ya kuwasilisha shauri, kufanya maombi kwa ajili ya uamuzi wa kiasi kitakacholipwa kama dhamana ya gharama na mahakama itaamua maombi hayo ndani ya siku kumi na nne zinazofuata baada ya tarehe ya kuwasilisha maombi yake kwa ajili ya uamuzi wa kiasi kinachopaswa kulipwa kama dhamana ya gharama. (4) Endapo mtu ameunganishwa kama mlalamikiwa kwa mujibu wa amri ya mahakama, mlalamikaji ndani ya siku kumi na nne tangu tarehe ambayo ikielekeza mtu huyo kuunganishwa kuwa mlalamikiwa, atalipa mahakamani kiasi kingine kisichozidi shilingi laki mbili, kama itakavyoelekezwa na mahakama kuhusiana na mtu huyo. ilitolewa amri (5) Endapo kwa maombi yatakayofanywa na 118 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 mlalamikaji, mahakama imeridhika kuwa utekelezaji wa masharti ya kifungu kidogo cha (2) au (4) utasababisha ugumu kwa mlalamikaji, inaweza kuelekeza kwamba- (a) mlalamikaji atoe aina nyingine ya dhamana ambayo thamani yake haizidi shilingi laki tano, kama ambavyo mahakama itaona inafaa; (b) mlalamikaji asamehewe kulipa malipo ya aina yoyote ya dhamana. (6) Amri haitatolewa chini ya kifungu kidogo cha (3), (4) na (5) mpaka nafasi imetolewa kwa mlalamikiwa, au endapo kuna walalamikiwa wawili au zaidi, kwa kila mlalamikiwa kujieleza kwa madhumuni hayo. (7) Ikiwa dhamana ya gharama haitalipwa mahakamani ndani ya siku kumi na nne kutoka tarehe ya uamuzi wa mahakama kuhusu kiasi cha malipo ya la dhamana ya gharama, mwenendo wa shauri uchaguzi hautaendelea kusikilizwa na shauri hilo litafutwa. ile kwa yoyote (8) Masharti ya kifungu kidogo cha (2) na (3) ikiwa, namna hayatatumika Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni mlalamikaji au ni mmoja wa walalamikaji. (9) Kiasi cha fedha kilichowekwa kama dhamana ya gharama au salio la dhamana hiyo kitarejeshwa kwa mlalamikaji mapema iwezekanavyo, endapo mlalamikaji atashinda katika shauri au rufaa na iwapo hakuna amri iliyotolewa dhidi ya mlalamikaji kulipa gharama. Nafuu zinazoweza kuombwa - 151 Verify source ↗
Nafuu zinazoweza kuombwa
AI-assisted research summary: Mlalamikaji anaweza kuomba nafuu fulani katika shauri la uchaguzi.
151. Nafuu zote au yoyote kati ya zifuatazo ambazo mlalamikaji anaweza kustahili, zinaweza kuombwa katika shauri la uchaguzi: (a) tamko kwamba uchaguzi ni batili; (b) tamko kwamba aliyechaguliwa haukuwa halali; uteuzi wa mtu (c) endapo kiti kinadaiwa na mgombea ambaye hakushinda kwa madai kwamba alikuwa 119 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Uthibitisho wa mahakama juu ya uhalali wa uchaguzi Muda wa kuwasilisha na kuamuliwa kwa shauri la uchaguzi amepata kura nyingi zaidi halali, kufanyika uchunguzi wa kura. - 152 Verify source ↗
Uthibitisho wa mahakama juu ya uhalali wa uchaguzi
AI-assisted research summary: Mahakama ikimaliza kusikiliza shauri la uchaguzi huamua kama uchaguzi au uteuzi uliopingwa ni batili, kisha hutuma uamuzi huo kwa Tume; baada ya uthibitisho, uamuzi huwa wa mwisho na uchaguzi huthibitishwa au kurudiwa kulingana na hilo.
152. Wakati wa kuhitimisha usikilizaji wa shauri la uchaguzi, mahakama itaamua iwapo mjumbe ambaye uteuzi au uchaguzi wake unalalamikiwa au mtu mwingine yeyote au mtu aliteuliwa au ipasavyo, au uchaguzi ni batili, na alichaguliwa itathibitisha uamuzi huo kwa Tume na baada ya uthibitisho kutolewa uamuzi utakuwa ni wa mwisho, na uchaguzi utathibitishwa au uchaguzi utafanyika upya kama itakavyohitajika kwa mujibu wa uthibitisho huo. shauri Isipokuwa kwamba, - 153 Verify source ↗
Muda wa kuwasilisha na kuamuliwa kwa shauri la uchaguzi
AI-assisted research summary: Election petitions must be filed within 30 days of results being declared, with a special 28-day window for corruption-based complaints; the court must decide petitions within 12 months, and the Chief Justice may extend that period by up to 6 months if needed.
153.-(1) Kila shauri la uchaguzi litawasilishwa ndani ya siku thelathini kuanzia tarehe ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi na msimamizi wa uchaguzi: la uchaguzi linalohoji uchaguzi kwa msingi wa kitendo cha rushwa na hasa tuhuma ya malipo ya fedha au kitendo kingine kuwa kimefanywa au kilitendwa tangu tarehe ya kutangazwa kwa matokeo na msimamizi wa uchaguzi au kwa ufahamu na ridhaa au idhini ya mjumbe ambaye uchaguzi wake unalalamikiwa au kwa ufahamu na ridhaa au idhini ya wakala wa mjumbe kwa kutekeleza au kuendeleza kitendo hicho cha rushwa malalamiko hayo yanaweza kuwasilishwa wakati wowote ndani ya siku ishirini na nane baada ya tarehe ya malipo au kitendo. la uchaguzi (2) Bila kuathiri masharti ya kanuni zozote za Mahakama zilizotungwa chini ya kifungu cha 155, shauri lililowasilishwa kwa muda unaostahili linaweza, kwa madhumuni ya kuhoji uchaguzi kuhusu tuhuma za kitendo cha rushwa au kitendo haramu, kurekebishwa kwa ruhusa ya mahakama ndani ya muda ambao shauri linalohoji matokeo ya uchaguzi kwa kigezo hicho linaweza kuwasilishwa. (3) Mahakama itasikiliza na kuamua kila shauri la uchaguzi ndani ya miezi kumi na mbili tangu tarehe 120 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 ya kuwasilishwa kwa shauri la uchaguzi. (4) Endapo hakuna uwezekano wa kuamuliwa kwa shauri la uchaguzi ndani ya kipindi cha miezi kumi na mbili, Jaji Mkuu na kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, anaweza kuongeza muda kwa kipindi kingine kisichozidi miezi sita, kadiri atakavyoamua. Kura zinazoweza kuondolewa wakati wa uchunguzi - 154 Verify source ↗
Kura zinazoweza kuondolewa wakati wa uchunguzi
AI-assisted research summary: During an election petition hearing, votes described in the section must be removed, including votes linked to registration problems, bribery-linked influence, impersonation, multiple voting, and certain disqualifications.
154.-(1) Wakati wa uchunguzi katika kusikiliza shauri la uchaguzi, kura zifuatazo zitaondolewa: (a) kura ya mtu yeyote ambaye jina lake la kata halikuwepo kwenye Daftari alikopigia kura; (b) kura ya mtu yeyote ambaye kura yake au takrima hongo, kwa ilipatikana kushawishiwa; (c) kura ya mtu yeyote ambaye ametenda kosa au amewezesha kutenda kosa la kujifanya mtu mwingine katika uchaguzi; (d) kura ya mtu yeyote ambaye amethibitika kuwa amepiga kura zaidi ya mara moja katika uchaguzi; (e) kura ya mtu yeyote ambaye kwa sababu ya kutiwa hatiani kwa kosa la kitendo cha rushwa au kitendo haramu au kwa sababu ya taarifa ya Mahakama, au kwa sababu ya kutiwa hatiani kwa kosa lolote kinyume cha Sheria hii au Sheria nyingine yoyote aliondolewa sifa ya kupiga kura katika uchaguzi. (2) Kura ya mpiga kura aliyeandikishwa haitaondolewa wakati wa uchunguzi kwa sababu mpiga kura hakuwa na sifa au hana sifa ya jina lake isipokuwa kwa sababu kuingizwa katika Daftari zilizoainishwa katika kifungu kidogo cha (1)(e). Kanuni za Mahakama - 155 Verify source ↗
Kanuni za mahakama
AI-assisted research summary: Jaji Mkuu anaweza, baada ya kushauriana na Tume, kutunga kanuni za mahakama za taratibu na mwenendo wa kufuatwa na kuweka ada zinazolipwa kwa mashauri ya uchaguzi na maombi chini ya Sehemu hii.
155. Jaji Mkuu kwa kushauriana na Tume anaweza kutunga kanuni za mahakama kusimamia taratibu na mwenendo wa kuzingatiwa na kuweka ada itakayolipwa kuhusiana na mashauri ya uchaguzi na 121 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 maombi chini ya Sehemu hii. SURA YA TISA MASHARTI YA JUMLA Maelezo yasiyo sahihi Mamlaka ya Mkurugenzi wa Uchaguzi na wasimamizi wa uchaguzi kutaka taarifa taarifa - 156 Verify source ↗
Maelezo yasiyo sahihi
AI-assisted research summary: A wrong name or description in a register made under this law does not affect how the law applies to the person or place concerned.
156. Kasoro ya jina au maelezo yasiyo sahihi ya mtu yeyote au sehemu iliyotajwa au kuelezwa nyingine, katika Daftari, iliyoandaliwa au kutolewa chini au kwa madhumuni ya Sheria hii, haitaathiri kwa namna yoyote matumizi ya Sheria hii kuhusu mtu huyo au sehemu hiyo, kama mtu huyo au sehemu hiyo inaelezwa hivyo katika Daftari, taarifa au nyaraka kama itakavyotambuliwa. nyaraka au - 157 Verify source ↗
Mamlaka ya Mkurugenzi wa Uchaguzi na wasimamizi wa uchaguzi
AI-assisted research summary: Election officials may ask anyone for information needed to check candidate or voter eligibility and to identify a person or their residence. A person who is legally required to provide that information and fails or delays without good reason commits an offence and may be fined 200,000 shillings on conviction.
157.-(1) Katika kutekeleza majukumu yao chini ya Sheria hii, Mkurugenzi wa Uchaguzi na wasimamizi wa uchaguzi au mtu mwingine yeyote anayehusika na uendeshaji wa upigaji kura au uandikishaji wa wapiga kura, wakati wote, watakuwa na uwezo wa kutaka taarifa kutoka kwa mtu yeyote muhimu ili kuhakikisha kama mtu ana sifa ya kuwa mgombea na kumtambua mtu yeyote au mahali anapoishi mtu yeyote, na kuhakikisha iwapo mtu yeyote amepoteza sifa za kupiga kura au kuwa mgombea. anashindwa (2) Mtu ambaye, baada ya kutakiwa kisheria kutoa taarifa chini ya masharti ya kifungu kidogo cha (1), ambazo anazifahamu au anazimiliki au bila sababu za msingi anachelewa kutoa taarifa hizo, anatenda kosa na isiyozidi akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini shilingi laki mbili. taarifa kutoa hizo Malipo ya watendaji - 158 Verify source ↗
Malipo ya watendaji
AI-assisted research summary: Watu walioajiriwa kwa madhumuni ya Sheria hii hupaswa kulipwa malipo yanayostahili kwa kazi hiyo, isipokuwa walio katika utumishi wa umma, na Tume ndiyo inayoidhinisha malipo hayo kama itavyoona inafaa.
158. Mtu yeyote aliyeajiriwa kwa madhumuni ya Sheria hii, ikiwa hajaajiriwa katika utumishi wa umma, atapokea malipo yanayostahili kwa kazi hiyo kadiri Tume itakavyoona inafaa kuidhinisha. Gharama kulipwa kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali - 159 Verify source ↗
Gharama kulipwa kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali
AI-assisted research summary: Gharama za shughuli za uchaguzi zilizotajwa hapa hulipwa kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali.
159. Gharama zote zitakazotumika- (a) katika kuandaa Daftari, kutoa kadi ya mpiga kura na kufanya mambo mengine au 122 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 vitu vingine vinavyohitajika kufanywa kwa madhumuni ya kutekeleza masharti ya Sheria hii; (b) na Tume, Mkurugenzi wa Uchaguzi, wasimamizi wa uchaguzi na mtu mwingine yeyote aliyeajiriwa kutekeleza majukumu ya uchaguzi; (c) kwa malipo ya maafisa walioainishwa katika kifungu cha 158; na (d) kwa afisa yeyote wa umma kuhusu shughuli rasmi zinazohusiana au zinazotokana na uchaguzi, zitatozwa na kulipwa kutoka kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali. Utoaji wa taarifa - 160 Verify source ↗
Utoaji wa taarifa
AI-assisted research summary: A notice under this law is treated as delivered or given to a person if it is personally delivered, left at the person’s last known address, or sent by post to the last known address.
160. Taarifa chini ya Sheria hii itachukuliwa kuwa imefikishwa au kutolewa kwa mtu yeyote- (a) ikiwa imefikishwa kwake binafsi; (b) iwapo imeachwa kwa ajili yake kwenye anwani yake ya mwisho inayofahamika; au (c) iwapo imetumwa kwake kwa njia ya posta ya mwisho anwani yake katika inayofahamika. Kanuni - 161 Verify source ↗
Kanuni
AI-assisted research summary: The Commission may make regulations to better implement the Act and to specify matters, document forms, and declarations under the Act.
161.-(1) Tume inaweza kutengeneza kanuni kwa ajili ya utekelezaji bora wa masharti ya Sheria hii na bila kuathiri ujumla wa yaliyotangulia, inaweza kutengeneza kanuni zinazoainisha- (a) kitu chochote ambacho chini ya masharti ya Sheria hii kinaweza kuainishwa; na (b) muundo wa nyaraka na matamko kwa madhumuni ya Sheria hii. (2) Endapo fomu zozote zimeandaliwa chini ya kifungu hiki, fomu hizo zitatumika kwa madhumuni ambayo zinahusika au kwa namna ambayo zinaweza kutumika au kuweza kurekebishwa na zinaweza kutafsiriwa na kutumika katika lugha yoyote kama Tume itakavyoelekeza. Kanuni za Maadili ya Uchaguzi - 162 Verify source ↗
Kanuni za Maadili ya Uchaguzi
AI-assisted research summary: Tume must prepare and publish election ethics rules after consulting political parties and the Government.
162.-(1) Kwa madhumuni ya kusimamia 123 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 uchaguzi wa haki, huru na amani, na baada ya kushauriana na vyama vyote vya siasa na Serikali, Tume itaandaa na kuchapisha katika Gazeti la Serikali Kanuni za Maadili ya Uchaguzi zitakazoainisha maadili ya vyama vya siasa, Serikali na Tume wakati wa kampeni za uchaguzi na uchaguzi na utaratibu wa utekelezaji wake. (2) Kanuni za Maadili ya Uchaguzi zitasainiwa na- (a) kila chama cha siasa; (b) kila mgombea kabla hajawasilisha fomu ya uteuzi; (c) Serikali; na (d) Tume, zitapaswa kuzingatiwa na wahusika wote na waliosaini. (3) Mtu ambaye atakiuka masharti ya Kanuni za Maadili ya Uchaguzi ataadhibiwa kwa mujibu wa Kanuni hizo. - 163 Verify source ↗
Msamaha wa ushuru wa stempu
AI-assisted research summary: Nyaraka zilizotolewa kwa kiapo au uthibitisho, zikiwa katika fomu iliyoainishwa na kwa mujibu wa masharti ya Sheria hii, hazitozwi ushuru wa stempu.
163. Hati yoyote itakayotolewa kwa kiapo au uthibitisho kwa mujibu wa masharti ya Sheria hii katika fomu itakayoainishwa itasamehewa kodi ya ushuru wa stempu chini ya sheria yoyote inayotumika kuhusu ushuru wa stempu. - 164 Verify source ↗
Maelekezo
AI-assisted research summary: Tume inaweza kutoa maelekezo ya jumla au mahususi kuhusu majukumu ya wasimamizi wa uchaguzi, wasimamizi wa vituo na watu wengine walioajiriwa, lakini maelekezo hayo lazima yafuate Sheria hii na yasipingane na Sheria au kanuni zake.
164. Tume inaweza, kwa kuzingatia masharti ya Sheria hii, kutoa maelekezo ya jumla au mahususi kuhusu majukumu ya wasimamizi wa uchaguzi, wasimamizi wa vituo na watu wengine walioajiriwa au kwa madhumuni mengine yoyote ya Sheria hii: kwamba, maelekezo hayo hayatakinzana na masharti yoyote ya Sheria hii au kanuni zilizotungwa chini ya Sheria hii. Isipokuwa Msamaha wa ushuru wa stempu Maelekezo Kubadilishwa Daftari - 165 Verify source ↗
Kubadilishwa Daftari
AI-assisted research summary: Mkurugenzi wa Uchaguzi anaweza kuagiza Daftari libadilishwe na daftari jipya ikiwa, kwa maoni yake, ni lazima kufanya hivyo kwa sababu yoyote ile.
165. Endapo, kwa maoni ya Mkurugenzi wa Uchaguzi, itakuwa ni lazima kubadilisha Daftari kwa sababu yoyote ile, itakuwa ni halali kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi kuelekeza Daftari hilo kubadilishwa na daftari jipya. 124 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Matumizi ya teknolojia - 166 Verify source ↗
Matumizi ya teknolojia
AI-assisted research summary: Tume inaweza kutumia teknolojia wakati inatekeleza majukumu yake chini ya Sheria hii.
166. Tume inaweza kutumia teknolojia katika utekelezaji wa majukumu yake chini ya Sheria hii. SURA YA KUMI KUFUTWA KWA SHERIA NA MASHARTI YA MWENDELEZO Kufutwa kwa Sheria Na. 1 ya 1985 na 4 ya 1979 Masharti ya mwendelezo - 167 Verify source ↗
Kufutwa kwa Sheria
AI-assisted research summary: This section repeals the National Election Act of 1985 and the Local Government Election Act of 1979.
167. Sheria ya Taifa ya Uchaguzi ya Mwaka 1985 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1979 zinafutwa. vyote shughuli (a) vitendo - 168 Verify source ↗
Masharti ya mwendelezo
AI-assisted research summary: Vitu vilivyofanywa na Tume chini ya sheria zilizofutwa vinaendelea kuwa halali hadi vibatilishwe; fomu zilizoidhinishwa nazo zinachukuliwa kuwa zimeidhinishwa chini ya Sheria hii, na sheria ndogo zilizoendelea kutumika zinachukuliwa kuwa zimetengenezwa chini ya Sheria hii hadi zifutwe au zibadilishwe.
168. Bila kujali kufutwa kwa Sheria ya Taifa ya Uchaguzi ya Mwaka 1985 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1979- zote na zilizotekelezwa na Tume chini ya Sheria hizo zitaendelea kuwa halali hadi pale zitakapobatilishwa chini ya Sheria hii; (b) fomu zote zilizoidhinishwa na Tume kwa madhumuni ya Sheria hizo zitachukuliwa kuwa fomu zilizoidhinishwa chini ya Sheria hii hadi pale zitakapofutwa na Sheria hii au sheria ndogo zitakazotengenezwa chini ya Sheria hii; na (c) sheria ndogo zote zilizotengenezwa chini ya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi ya Mwaka 1985 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1979 ambazo bado zinatumika, kuwa zimetengenezwa chini ya Sheria hii hadi pale zitakapofutwa na Sheria hii au sheria ndogo zitakazotengenezwa chini ya Sheria hii. zitachukuliwa Imetungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 02 Februari, 2024. NENELWA JOYCE MWIHAMBI Katibu wa Bunge 125
Part
SEHEMU YA NNE
- 30 Verify source ↗
Rufaa kwenda Mahakama ya Mwanzo
AI-assisted research summary: Mahakama ya Mwanzo husikiliza rufaa hizi kwa wazi, taarifa ikitolewa kwa wahusika; uamuzi wake ni wa mwisho. Uamuzi unaweza kuathiri marekebisho ya Daftari la Awali la Wapiga Kura na utoaji wa kadi ya mpiga kura, na baadhi ya hali huruhusu au kuzuia kadi mbadala kutolewa.
30.-(1) Kila rufaa chini ya kifungu cha 23 au 29 itaeleza kwa kifupi sababu za rufaa, na itaambatishwa na kiasi cha fedha ambacho Tume, kupitia notisi katika Gazeti la Serikali, itaainisha kiwe dhamana. (2) Mahakama ya Mwanzo itasikiliza kila rufaa katika sehemu ya wazi kwa kutoa taarifa ya muda, tarehe na mahali rufaa itakaposikilizwa kwa pande zinazohusika na itakuwa na hiari ya kusikiliza au kutosikiliza ushahidi wowote, na uamuzi wa rufaa itakaoutoa utakuwa ni wa mwisho na hautahojiwa na mahakama yoyote. (3) Endapo Mahakama ya Mwanzo itaamua rufaa ambayo imekatwa kuhusiana na Daftari la Awali la Wapiga Kura kuhusu kadi ya mpiga kura, itampa afisa mwandikishaji maelezo yaliyotiwa saini na hakimu yenye majina ambayo Mahakama imeamua yafutwe kutoka katika Daftari la Awali la Wapiga Kura au maelezo ya jina la mtu yeyote atakayepewa kadi ya mpiga kura, na afisa mwandikishaji atamtaarifu Mkurugenzi wa Uchaguzi kuhusu matokeo ya rufaa, na Mkurugenzi wa Uchaguzi atafanya marekebisho au ataelekeza kufanywa marekebisho katika Daftari la Awali la Wapiga Kura na kutoa kadi ya mpiga kura ipasavyo: iliyotolewa Isipokuwa kwamba- (a) Mahakama ya Mwanzo haitamtaka afisa mwandikishaji kutoa kadi nyingine ya mpiga kura pale ambapo kadi ya mpiga kura au imeharibika, hadi pale mtu huyo atakapotoa tamko kwa afisa mwandikishaji kama inavyohitajika chini ya kifungu cha 22; na (b) katika hali yoyote ile ambayo kifungu cha 19, 20 au 21 kinatumika na ikiwa hakuna tamko lililotolewa kwa mujibu wa kifungu cha 22, afisa mwandikishaji anaweza imepotea awali 34 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kukataa kuelekeza kutolewa kwa kadi nyingine ya mpiga kura mpaka kadi ya mpiga kura iliyotolewa awali kwa mhusika iwe imerejeshwa. rufaa (4) Endapo imetupiliwa mbali, na Mahakama ya Mwanzo ina maoni kuwa rufaa ilikatwa bila sababu za msingi inaweza kuamuru kuwa dhamana ya kiasi cha fedha ambacho Tume itaainisha kwa notisi katika Gazeti la Serikali, itaifishwe kwa Serikali au kama hakuna amri hiyo dhamana hiyo itarejeshwa. (5) Wadaawa katika rufaa hawatastahili kulipwa gharama za kesi au fidia: Isipokuwa kwamba, kama rufaa imekatwa na kukubaliwa na Mahakama ya Mwanzo na endapo Mahakama itaona kuwa rufaa hiyo imekatwa bila sababu za msingi, Mahakama inaweza, kama itaona inafaa, kuamuru mrufani kulipa fidia ya kiasi cha fedha ambacho Tume itaainisha kwa notisi katika Gazeti la Serikali, na kiasi chochote kitakachoamriwa kitapatikana kana kwamba amri hiyo ni amri ya kukaza hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Mwanzo kwa ajili ya urejeshwaji wa fedha. cha fedha chochote kilicholipwa (6) Endapo rufaa imekatwa chini ya kifungu hiki, Mahakama ya Mwanzo, iwe ilikubali au kukataa inaweza kuamuru kuwa dhamana yoyote rufaa, iliyotaifishwa au itakayotaifishwa kwa Serikali au kiasi au kitakacholipwa kama fidia kwa mujibu wa amri ya afisa mwandikishaji chini ya kifungu cha 28, au kiasi chochote cha dhamana au kiasi cha fedha ambacho Mahakama ya Mwanzo inaweza kuainisha kisilipwe au kutaifishwa, au kurudishwa kwa mweka pingamizi, chochote kadiri kitakachoamriwa kurudishwa kitarejeshwa kana kwamba amri hiyo ilikuwa ni amri ya kukaza hukumu ya Mahakama ya Mwanzo kwa ajili ya urejeshwaji wa fedha. itakavyokuwa, kiasi na (7) Shahidi anaweza kuitwa na kuapishwa wakati wa kusikiliza rufaa chini ya masharti ya 35 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kifungu hiki kwa utaratibu unaofanana kwa karibu na mazingira ya uendeshaji wa kesi katika Mahakama ya Mwanzo pale inapotekeleza mamlaka yake ya kuendesha kesi za jinai, na bila kuathiri masharti ya sheria nyingine yoyote, anaweza kuwajibishwa kwa adhabu sawa na inayotolewa kwa kutoa ushahidi wa uongo au kutohudhuria. (8) Mtu anayestahili kuhudhuria kama mdaawa katika rufaa iliyowekwa chini ya masharti ya kifungu hiki anaweza kuhudhuria mwenyewe au kuwakilishwa na wakili. ujumla wa masharti (9) Taratibu na mwenendo wa usikilizaji wa rufaa chini ya kifungu hiki zitakuwa kwa namna ambayo Mahakama ya Mwanzo itaamua, na bila yaliyotangulia, kuathiri Mahakama ya Mwanzo, ikiwa itaridhika kuwa rufaa mbili au zaidi zinahusu hoja inayofanana, inaweza kutamka kuwa uamuzi rufaa iliyosikilizwa awali itapaswa kuzingatiwa na wadaawa wa rufaa hiyo nyingine au rufaa hizo kwa kadiri itakavyoelekeza. iliyoutoa katika Masharti yatokanayo na jina kuongezwa au kufutwa katika Daftari la Awali la Wapiga Kura - 31 Verify source ↗
Masharti yatokanayo na jina kuongezwa au kufutwa katika Daftari
AI-assisted research summary: When a person’s name is added to or removed from the preliminary voters’ register, the registrar must act accordingly, and a person whose name is removed may be required to return any voter card or file a declaration within at least 10 days.
31.-(1) Endapo jina la mtu yeyote limeongezwa katika Daftari la Awali la Wapiga Kura kwa mujibu wa kifungu cha 28, au kadi yoyote ya mpiga kura imetolewa kwa mtu yeyote kwa kuzingatia kifungu hicho, afisa mwandikishaji atachukua hatua kuhusu mtu huyo kana kwamba hakukataa maombi yanayohusika na rufaa hiyo. (2) Endapo jina la mtu yeyote limefutwa kutoka katika Daftari la Awali la Wapiga Kura kwa mujibu wa kifungu cha 28, afisa mwandikishaji atamtaka mtu huyo- (a) kurejesha kadi yoyote ya mpiga kura ambayo imetolewa kwake chini ya Sheria hii; au (b) kutoa na kuwasilisha tamko kwa afisa mwandikishaji kama ilivyoainishwa katika kifungu cha 22, ndani ya kipindi kisichopungua siku kumi, kama afisa 36 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 afisa atakavyoelekeza, mwandikishaji mwandikishaji ataelekeza kufutwa kwa kadi yoyote iliyorejeshwa. na SURA YA TATU UCHAGUZI WA RAIS SEHEMU YA KWANZA UTEUZI WA WAGOMBEA WA KITI CHA RAIS NA MAKAMU WA RAIS Uteuzi wa wagombea wa kiti cha Rais na Makamu wa Rais - 75 Verify source ↗
Siku na muda wa kupiga kura
AI-assisted research summary: In a contested election, voting must take place in each electoral area on the scheduled voting day, following the procedure set out in this section.
75. Katika uchaguzi unaoshindaniwa, upigaji kura utafanyika katika kila eneo la uchaguzi kwa utaratibu ulioelekezwa katika Sehemu hii, katika siku iliyopangwa kwa ajili ya kupiga kura katika eneo hilo la uchaguzi kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha - 69 Verify source ↗
Tangazo la uchaguzi
AI-assisted research summary: Kichwa cha kifungu hiki ni “Tangazo la uchaguzi” na kinaonekana kurejea mpangilio wa chaguzi zinazoshindaniwa.
69. 68 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Mpangilio wa chaguzi zinazoshindaniwa - 76 Verify source ↗
Mpangilio wa chaguzi zinazoshindaniwa
AI-assisted research summary: Msimamizi wa uchaguzi lazima aandae vituo vya kupigia kura, ateue wasimamizi wasaidizi na msimamizi wa kituo, asambaze vifaa na masanduku ya kura, na aweke taarifa na nakala ya Daftari kama Tume itaelekeza.
76. Msimamizi wa uchaguzi- (a) ataandaa idadi ya kutosha ya vituo vya kupigia kura katika kila eneo la uchaguzi kwa mujibu wa masharti ya tangazo lolote lililotolewa chini ya kifungu cha 69; (b) atateua kwa kila eneo la uchaguzi idadi ya watu watakaojulikana kama wasimamizi wasaidizi wa vituo, kama atakavyoona inafaa kumsaidia msimamizi wa kituo wakati wa kupiga kura katika uchaguzi; (c) atateua kutoka miongoni mwa wasimamizi wasaidizi wa vituo, mtu atakayekuwa kiongozi wa kituo ambaye atajulikana kama msimamizi wa kituo; (d) atagawa kwa kila kituo cha kupigia kura vituturi kwa idadi ambayo kwa maoni ya ataona wa msimamizi vinahitajika, kura ambamo wapiga wanaweza kupiga kura zao kwa siri; uchaguzi tangazo (e) atabandika au kuwezesha kubandikwa nje ya kila kituo cha kupigia kura katika sehemu ya wazi linaloonesha majina kwa mpangilio wa alfabeti za majina ya ukoo au kwa mpangilio mwingine kama Tume la imepigwa mgombea, karibuni ndani ya miezi mitatu na finyanzo au siasa chama kinachomdhamini mgombea; itakavyoelekeza, picha jina kamili ambayo nembo cha ya (f) ataweka ndani na nje ya kila kituo cha kupigia kura, taarifa zenye maelekezo ya utaratibu wa kufuatwa wakati wa kupiga kura; (g) atagawa kwa kila msimamizi wa kituo idadi ya masanduku ya kupigia kura na karatasi za kura ambazo kwa maoni ya msimamizi wa uchaguzi ataona zinahitajika; (h) atagawa kwa kila kituo cha kupigia kura vifaa vya kuandikia ambavyo wapiga kura watatumia kuweka alama katika karatasi ya 69 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Mawakala wa upigaji kura kura na zana zitakazotumika kuweka alama rasmi katika karatasi za kura; (i) kwa kuzingatia maelekezo yoyote ambayo Tume inaweza kutoa kwa madhumuni hayo, atagawa kwa kila kituo nakala ya Daftari katika eneo la uchaguzi au sehemu ya Daftari hilo ambayo itakuwa na majina ya wapiga kura walioruhusiwa kupiga kura katika kituo hicho; na (j) atafanya jambo lingine lolote au kutekeleza majukumu mengine yoyote kama Tume itakavyoelekeza.
Part
sehemu ya wazi
- 77 Verify source ↗
Mawakala wa upigaji kura
AI-assisted research summary: Political parties may appoint polling agents for polling stations with candidates, but must give written notice and the station supervisor handles complaints at the station.
77.-(1) Kila chama cha siasa kinaweza, baada ya kupata ridhaa ya wagombea, kuteua mtu mmoja atakayejulikana kama wakala wa upigaji kura kwa kila kituo ndani ya jimbo au kata ambayo ina mgombea au wagombea kwa madhumuni ya- (a) kuwabaini watu wanaodanganya kuwa wanastahili kupiga kura; (b) kumwakilisha na kulinda maslahi ya mgombea au wagombea katika kituo cha kupigia kura; (c) kushirikiana na msimamizi wa kituo na wasimamizi wasaidizi wa ili kuhakikisha sheria na taratibu zinazohusu upigaji kura na chaguzi zinazingatiwa katika kituo. kituo (2) Taarifa ya maandishi ya uteuzi, inayotaja jina na anwani ya kituo cha kupigia kura ambacho wakala amepangiwa, kwa kadiri itakavyowezekana, itatolewa kwa msimamizi wa uchaguzi si chini ya siku saba kabla ya siku ya uchaguzi au ndani ya muda mfupi zaidi kama Tume itakavyoruhusu: Isipokuwa kwamba, chama cha siasa kinaweza, kwa taarifa iliyotolewa chini ya kifungu kidogo hiki, kuteua wakala mbadala wa upigaji kura, ambaye anaweza kuwepo na kutekeleza majukumu yoyote ya wakala wa upigaji kura pale ambapo wakala wa upigaji kura anayehusika hatakuwepo katika kituo, ama kwa 70 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kudumu au kwa muda. (3) Endapo wakala yeyote wa upigaji kura atafariki au kushindwa kutekeleza majukumu yake, chama cha siasa kinachohusika kinaweza kumteua wakala wa upigaji kura mwingine badala yake na mapema iwezekanavyo kitatoa taarifa kwa maandishi kwa msimamizi wa uchaguzi anayehusika kuhusu jina na anwani ya wakala wa upigaji kura aliyeteuliwa na kituo cha kupigia kura alichopangiwa. (4) Msimamizi wa kituo, kwa kusaidiana na kushirikiana na wakala wa upigaji kura, atatatua au vinginevyo atashughulikia malalamiko katika kituo mara yatakapotokea na kuletwa kwake na mgombea, wakala wa kituo cha kupigia kura, mpiga kura au mtu yeyote aliyeandikishwa na anayestahili kupiga kura katika kituo husika. Masanduku ya kura - 78 Verify source ↗
Masanduku ya kura
AI-assisted research summary: Kila sanduku la kura lazima litengenezwe ili kuruhusu kura kuingizwa bila kuweza kutolewa, na msimamizi wa kituo lazima alioneshe kuwa tupu, alifunge kwa lakiri, na alihifadhi limefungwa kabla ya kupiga kura.
78.-(1) Kila sanduku la kura litatengenezwa kwa namna ambayo itaruhusu wapiga kura kuweka karatasi za kura ndani yake bila kuweza kuzitoa karatasi za kura. tupu sanduku (2) Mapema kabla ya kuanza kupiga kura, msimamizi wa kituo katika kila kituo cha kupigia kura ataonesha la kura kwa watu watakaokuwepo kihalali ili waweze kuona kwamba liko tupu, na atalifunga na kuweka lakiri kwa namna itakayozuia kufunguliwa bila kuvunja lakiri na ataliweka lionekane ili kuweka karatasi za kura na ataendelea kuliweka likiwa limefungwa na kuwekwa lakiri. Muundo wa karatasi za kura - 79 Verify source ↗
Muundo wa karatasi za kura
AI-assisted research summary: Kila karatasi ya kura lazima iwe na picha ya hivi karibuni ya mgombea, jina kamili la mgombea, na alama au nembo ya chama kinachomdhamini ikiwa ipo; pia iwe inaweza kukunjwa, iwe katika muundo unaotumika na watu wenye mahitaji maalumu, na ishikizwe kwenye kishina chenye namba zinazofuatana.
79. Kila karatasi ya kura- (a) itakuwa na- (i) (ii) picha iliyopigwa karibuni ndani ya jina kamili la mgombea; miezi mitatu; na (iii) finyanzo au nembo ya chama cha siasa kinachomdhamini mgombea, ikiwa ipo; (b) iwe inaweza kukunjwa; 71 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Katazo la kuweka wazi kura (c) itakuwa katika muundo unaowezesha kutumika na watu wenye mahitaji maalumu; na (d) itashikizwa katika kishina chenye namba zinazofuatana. - 80 Verify source ↗
Katazo la kuweka wazi kura
AI-assisted research summary: Mpiga kura hawezi kulazimishwa kusema alimmpigia nani kura katika shauri la kupinga matokeo ya uchaguzi.
80. Mtu aliyepiga kura katika uchaguzi hatatakiwa, katika mwenendo wowote wa mashauri ya kuhoji matokeo ya uchaguzi, kueleza ni mgombea yupi alimpigia kura: Isipokuwa kwamba, kifungu hiki hakitatumika lolote ambalo hoja katika mwenendo wa shauri inayobishaniwa ni iwapo msimamizi wa kituo katika kutekeleza majukumu chini ya masharti ya kifungu cha 84(3)(b), (c) na (i) alitenda hivyo kwa nia njema. SEHEMU YA TANO UTARATIBU WA KUPIGA NA KUHESABU KURA Watu wanaostahili kupiga kura Kupoteza sifa za kupiga kura
Part
SEHEMU YA TANO
- 81 Verify source ↗
Watu wanaostahili kupiga kura
AI-assisted research summary: Mtu aliye raia na aliyeandikishwa kama mpiga kura anaweza kupiga kura, lakini lazima ajitambulishe kwa msimamizi wa uchaguzi na hapaswi kupiga kura zaidi ya mara moja katika uchaguzi huo.
81.-(1) Kwa mujibu wa masharti ya Sheria hii, kila mtu, ambaye ni raia wa Jamhuri ya Muungano na ambaye wakati uchaguzi wowote unafanyika katika chini ya Sheria hii jimbo ameandikishwa katika jimbo au kata hiyo kuwa mpiga kura, atastahili kupiga kura katika uchaguzi huo katika au ambayo jimbo aliandikishwa. au kata yoyote ameandikishwa kata au (2) Kila mtu, anapotaka kupiga kura katika uchaguzi chini ya Sheria hii, atajitambulisha kwa msimamizi wa uchaguzi kwa namna ambayo itaelekezwa na mtu hatastahili kupiga kura zaidi ya mara moja katika uchaguzi huo. - 82 Verify source ↗
Kupoteza sifa za kupiga kura
AI-assisted research summary: Mtu aliyeandikishwa kuwa mpiga kura haruhusiwi kupiga kura katika uchaguzi wowote ikiwa hali zinazomhusu zingemfanya apoteze sifa za kuandikishwa kama mpiga kura.
82. Bila kujali masharti ya kifungu cha 81, mtu ambaye ameandikishwa kuwa mpiga kura hatastahili kupiga kura katika uchaguzi wowote iwapo mazingira yatajitokeza kuhusiana na mtu huyo, kama angekuwa hajaandikishwa, yangesababisha mtu huyo kupoteza sifa za kuandikishwa kama mpiga kura. 72 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Mahali pa kupigia kura - 83 Verify source ↗
Mahali pa kupigia kura
AI-assisted research summary: Mtu anayestahili kupiga kura chini ya kifungu cha 81 lazima apige kura katika jimbo au kata aliyoandikishwa, si mahali pengine.
83. Kila mtu anayestahilli kupiga kura chini ya masharti ya kifungu cha 81 atapiga kura katika jimbo au kata ambayo ameandikishwa kuwa mpiga kura kwa madhumuni ya uchaguzi, na si mahali pengine. Utaratibu wa kupiga kura - 84 Verify source ↗
Utaratibu wa kupiga kura
AI-assisted research summary: Section 84 sets out how voting at a polling station must be carried out, including voter identification, ballot secrecy, assistance for some voters, and how complaints are handled.
84.-(1) Bila kuathiri masharti ya kifungu cha 77(3) na 109, kila wakala wa kituo cha kupigia kura atakuwepo wakati wa ufunguzi wa upigaji kura katika kituo ambacho ameteuliwa kuwa wakala wa upigaji kura. (2) Kabla ya kuanza kupiga kura katika kituo cha kupigia kura, wakala wa upigaji kura atatakiwa na msimamizi wa kituo cha kupigia kura kwa namna itakayoainishwa kuwasilisha kwake malalamiko yoyote aliyonayo au aliyoyapokea, au maelezo yoyote ya kuridhika kwake namna mpangilio wa upigaji kura katika kituo cha kupigia kura ulivyowekwa. (3) Upigaji kura katika uchaguzi utafanyika kwa namna ifuatayo: ambalo ameandikishwa, (a) kila mpiga kura anayetaka kupiga kura atakwenda mwenyewe katika kituo cha kupigia kura alichopangiwa katika eneo la na uchaguzi atamridhisha msimamizi wa kituo au msimamizi msaidizi wa kituo hicho cha kupigia kura, kuwa yeye ni mpiga kura kama anavyodai na kuwa hajapiga kura katika kituo hicho cha kupigia kura au mahali pengine popote, na mtu huyo anaweza kumridhisha msimamizi wa kituo au msimamizi msaidizi wa kituo kuwa yeye ni mpiga kura kama anavyodai kwa kuonesha kwa afisa huyo au msimamizi msaidizi wa kituo kadi ya mpiga kura au ushahidi wowote wa maandishi kama Mkurugenzi wa Uchaguzi atakavyoelekeza; (b) ikiwa mpiga kura hawezi kupiga kura kwa sababu ya ulemavu wa kutoona au sababu nyingine ya kimaumbile au hawezi kusoma, mpiga kura huyo anaweza kumuomba mtu 73 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 atakayemchagua isipokuwa msimamizi wa kituo, msimamizi msaidizi wa kituo, karani mwongozaji, mlinzi wa kituo au wakala wa upigaji kura kumsaidia kupiga kura kwa mujibu wa aya (c) mpaka (k) ya kifungu hiki kidogo na mtu huyo aliyechaguliwa chini ya aya hii atamsaidia mpiga kura asiyezidi mmoja: kwamba, Isipokuwa pale ambapo katika kaya kutakuwa na mtu zaidi ya mmoja ambao wanahitaji msaada chini ya aya hii, itakubalika kisheria kwa watu wa kaya hiyo kumchagua mtu mmoja wa kuwasaidia; (c) baada ya kuridhishwa na utambulisho wa mpiga kura na kuwa jina la mpiga kura huyo lipo katika Daftari la eneo hilo la uchaguzi na mpiga kura amepangiwa kupiga kura katika kituo hicho cha kupigia kura, msimamizi wa kituo au msimamizi msaidizi wa kituo atampa mpiga kura husika karatasi ya kura; (d) kabla ya msimamizi wa kituo au msimamizi msaidizi wa kituo kutoa karatasi ya kura kwa mtu yeyote- (i) karatasi ya kura itagongwa muhuri wenye alama rasmi; (ii) namba na taarifa za mpiga kura, kama zilivyoainishwa katika nakala ya Daftari au sehemu ya Daftari linalotunzwa katika kituo cha kupigia kura, zitatajwa; (iii) namba ya mpiga kura katika nakala ya Daftari au sehemu ya Daftari itawekwa alama katika kishina; na (iv) alama itawekwa mkabala na namba ya mpiga kura katika nakala ya Daftari au sehemu ya Daftari kuonesha kuwa mpiga kura huyo 74 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 amepokea karatasi ya kura; (e) kwa kuzingatia masharti ya aya (h), mpiga kura baada ya kupokea karatasi ya kura atakwenda mara moja kwenye moja ya vituturi vya kupigia kura katika kituo cha kupigia kura na kupiga kura yake kwa siri kwa utaratibu uliolekezwa katika aya (f), atakunja karatasi ya kura ili kuficha kura yake na atakwenda katika sanduku la kura kumuonesha msimamizi msaidizi wa kituo alama rasmi iliyo nyuma ya karatasi ya kura kura na iliyokunjwa ndani ya sanduku la kupigia kura; atatumbukiza karatasi ya (f) mpiga kura atapiga kura yake kwa kuweka alama katika jina la mgombea anayetaka kumchagua; (g) mpiga kura hataweka maandishi au alama yoyote inayoweza kumtambulisha katika karatasi ya kura; (h) mpiga kura atapiga kura bila ya kuchelewa; (i) iwapo mpiga kura hajui kusoma au haelewi jinsi ya kupiga kura msimamizi wa kituo anaweza, mbele ya wakala wa upigaji kura, kumuelekeza utaratibu wa kupiga kura; (j) kwa kuzingatia masharti ya aya (b) na (i), mpiga kura hataonesha alama aliyoweka katika karatasi yake ya kura kwa mtu yeyote, na kama atafanya hivyo karatasi ya kura itachukuliwa kuwa imeharibika: Isipokuwa kwamba, masharti ya aya hii hayatatumika ikiwa karatasi ya kura imeoneshwa na mpiga kura kwa msimamizi wa kituo kwa madhumuni tu ya kuhakikisha kama mpiga kura ametimiza wajibu wake kwa usahihi; (k) mpiga kura ambaye kwa bahati mbaya ametumia karatasi yake ya kura kwa namna kama ambayo ya karatasi kuhesabika ya kura, baada haitaweza halali 75 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kuwasilisha karatasi hiyo kwa msimamizi wa kituo, na kumridhisha msimamizi wa kituo kwamba karatasi hiyo ya kura imeharibika kwa bahati mbaya, atapewa karatasi nyingine badala ya ile iliyoharibika na mara moja karatasi ya kura iliyoharibika na kishina chake kitawekwa alama kuwa imefutwa. (4) Kabla ya mchakato wowote wa upigaji kura kuanza, msimamizi wa kituo atamtaka wakala wa upigaji kura wa kila mgombea kujaza kwenye fomu itakayoainishwa na kuwasilisha kwa msimamizi wa kituo- (a) malalamiko yoyote aliyonayo, kuhusu maandalizi ya kupiga kura; (b) kuridhishwa kwake na maandalizi ya utaratibu wa upigaji kura katika eneo linalohusika; au (c) malalamiko yoyote yaliyowasilishwa na mpiga kura yeyote kuhusiana na maandalizi ya upigaji kura katika eneo linalohusika. (5) Endapo mpiga kura ana malalamiko yoyote kuhusu mwenendo wa uchaguzi katika kituo cha kupigia kura au kata ambayo ameandikishwa kupiga kura, anaweza kuandika malalamiko yake kwenye fomu itakayoainishwa na kuiwasilisha fomu hiyo kwa msimamizi wa kituo cha kupigia kura kabla mpiga kura hajaondoka katika kituo cha kupigia kura. (6) Endapo malalamiko uchaguzi yaliyorejewa katika kifungu kidogo cha (5) yanamhusu msimamizi wa kituo cha kupigia kura, mpiga kura atawasilisha fomu ya malalamiko mbele ya mawakala wa upigaji kura wa wagombea. ya Kuruhusiwa kuingia katika kituo cha kupigia kura - 85 Verify source ↗
Kuruhusiwa kuingia katika kituo cha kupigia kura
AI-assisted research summary: A person may vote only at the polling station assigned to them, and entry to a polling station is limited to listed authorized people or those later allowed by the station supervisor.
85.-(1) Mtu hataruhusiwa kupiga kura katika kituo chochote cha kupigia kura isipokuwa katika kituo la cha kupigia kura alichopangiwa katika eneo uchaguzi ambalo amejiandikisha kama mpiga kura. (2) Mtu hataruhusiwa kuingia katika kituo cha kupigia kura isipokuwa wafuatao: 76 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 (a) msimamizi wa kituo; (b) msimamizi msaidizi wa kituo; (c) wakala wa upigaji kura; (d) mpiga kura; (e) mtu anayemsaidia mpiga kura asiyeweza kupiga kura, kwa mujibu wa kifungu cha 84(3)(b); (f) mwangalizi aliyeidhinishwa na Tume kwa maandishi; (g) mgombea; (h) mjumbe wa Tume; (i) Mkurugenzi wa Uchaguzi; (j) afisa wa Tume; (k) mratibu wa uchaguzi wa Mkoa; (l) afisa anayeshughulikia uchaguzi; (m) afisa wa polisi au mtu mwingine yeyote anayehusika na usalama katika kituo cha kupigia kura; na (n) msimamizi wa uchaguzi na msimamizi msaidizi wa uchaguzi. (3) Msimamizi wa kituo anaweza kwa hiari yake kuwaruhusu angalau waangalizi wasiopungua wawili kama wapo kuingia katika kituo cha kupigia kura. (4) Tume inaweza kualika waangalizi wa ndani na wa kimataifa na kuandaa mwongozo kwa ajili ya kusimamia mwenendo wa waangalizi. (5) Endapo mtu yeyote ataonesha utovu wa nidhamu ndani ya kituo cha kupigia kura au atashindwa kutii amri halali ya msimamizi wa kituo, anaweza mapema iwezekanavyo, kwa amri ya msimamizi wa kituo kuondolewa katika kituo cha kupigia kura na afisa wa polisi yeyote aliyepo ndani au karibu na kituo au na mtu mwingine yeyote aliyeidhinishwa kwa maandishi na msimamizi wa kituo au msimamizi wa uchaguzi, na mtu huyo aliyeondolewa hataruhusiwa kuingia katika kituo cha kupigia kura isipokuwa kwa ruhusa ya msimamizi wa kituo. (6) Mtu aliyeondolewa kwa mujibu wa kifungu 77 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Tuhuma za ukiukwaji wa taratibu kidogo cha (5), iwapo atashtakiwa kwa kutenda kosa lolote katika kituo hicho cha kupigia kura, anaweza kuwekwa chini ya ulinzi mpaka atakapofikishwa mbele ya hakimu na mamlaka yaliyotolewa na kifungu hiki hayatatumika kwa lengo la kumzuia mpiga kura yeyote, ambaye kwa namna yoyote anastahili kupiga kura katika kituo chochote cha kupigia kura, kutumia nafasi ya kupiga kura katika kituo hicho cha kupigia kura. - 86 Verify source ↗
Tuhuma za ukiukwaji wa taratibu
AI-assisted research summary: A polling station manager must warn a person suspected of not being a qualified voter, explain the reasons, and, if the person later proves eligibility and signs the required declaration, give that person a ballot paper and allow voting.
86.-(1) Endapo msimamizi wa kituo chochote cha kupigia kura atakuwa na sababu za kuamini, au pale ambapo mgombea au wakala wa upigaji kura aliyepo katika kituo chochote cha kupigia kura anatuhumu kuwa, mtu yeyote anayetaka kupiga kura katika kituo hicho, si mpiga kura anayestahili kupiga kura katika kituo hicho cha kupigia kura, msimamizi wa kituo atamuonya mtu huyo kuwa kama atapiga kura atakuwa ametenda kosa kwa mujibu wa Sheria hii. (2) Iwapo, bila kujali onyo hilo, mtu huyo atasisitiza kutaka kupiga kura na- (a) akatoa ushahidi wowote kuonesha kuwa anastahili kupiga kura katika kituo cha kupigia kura kinachohusika; na (b) baada ya kutakiwa kutoa na kusaini tamko kama ilivyoelekezwa na kifungu cha 87, atatoa na kutia saini tamko moja au matamko yote ambayo kifungu hicho kimeyaainisha, msimamizi wa kituo atampa karatasi ya kura mtu huyo na kumruhusu kupiga kura katika kituo hicho. (3) Msimamizi wa kituo atanakili jina na anwani kamili ya mtu aliyeonywa chini ya kifungu kidogo cha (1) ambavyo mtu huyo ametoa kama jina na anwani yake, na ikiwa mtu huyo amepiga kura, msimamizi wa kituo ataeleza suala hilo katika kumbukumbu. (4) Kabla ya kumuonya mtu kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (1), msimamizi wa kituo atamueleza mtu huyo sababu za kuamini kwake 78 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Tamko la kupiga kura Kuahirishwa kwa upigaji kura kwamba mtu huyo si mpiga kura anayestahili kupiga kura katika kituo husika cha kupigia kura au, kama tuhuma zinazotajwa katika kifungu kidogo cha (1) zimetolewa na mgombea au wakala wa upigaji kura aliye katika kituo husika cha kupigia kura, atamtaka mgombea au wakala kueleza mbele yake na mbele ya mtu anayetaka kupiga kura sababu za tuhuma, na ikiwa mgombea au wakala atakataa kutekeleza sharti hilo, msimamizi wa kituo atapuuza tuhuma zilizotolewa. - 87 Verify source ↗
Tamko la kupiga kura
AI-assisted research summary: The polling station supervisor may require a voter to prove identity and sign one or more declarations before receiving a ballot paper, and may refuse the ballot if the person cannot prove identity or refuses to make a declaration.
87.-(1) Msimamizi wa kituo katika kituo chochote cha kupigia kura anaweza, kwa ridhaa yake, na kwa maombi ya mgombea aliye katika kituo cha kupigia kura au wakala wa upigaji kura, kumtaka mtu yeyote anayetaka kupiga kura kabla ya kupewa karatasi ya kura, kutoa ushahidi ambao utamtambulisha kwamba mtu huyo ndiye aliyeelezwa katika kadi ya mpiga kura ambayo ameitoa, kama msimamizi wa kituo ataona ni lazima na kumtaka kutoa na kusaini tamko moja au matamko yote yaliyotolewa. (2) Endapo mtu yeyote atashindwa kutoa ushahidi wa utambulisho wake au atakataa kutoa tamko lolote, msimamizi wa kituo anaweza kukataa kumpa karatasi ya kura. - 88 Verify source ↗
Kuahirishwa kwa upigaji kura
AI-assisted research summary: If voting at a polling station is stopped or blocked for riots, violence, disasters, or another valid reason while some voters are still waiting, the station manager must postpone voting to the next day and notify the election manager as soon as possible.
88.-(1) Endapo mwenendo wa upigaji kura katika kituo chochote unakatizwa au kuzuiliwa kwa ghasia au vurugu, majanga au kwa sababu nyingine yoyote ya msingi wakati kuna wapiga kura waliobaki ambao hawajamaliza utaratibu wa kupiga kura, msimamizi wa kituo ataahirisha zoezi mpaka siku inayofuata na mapema iwezekanavyo atampa taarifa msimamizi wa uchaguzi. (2) Endapo upigaji kura unaahirishwa katika kituo chochote cha kupigia kura- (a) saa za kupiga kura katika siku ambayo upigaji kura umeahirishwa zitakuwa sawa na siku ya awali ya kupiga kura; na (b) rejea katika Sheria hii kuhusu kufunga upigaji kura itatafsiriwa ipasavyo. 79 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Kufunga zoezi la upigaji kura Utaratibu wa kufunga upigaji kura - 89 Verify source ↗
Kufunga zoezi la upigaji kura
AI-assisted research summary: If voting time has ended and some voters are still present but have not voted, the polling station must stay open long enough for them to vote.
89. Endapo muda wa kupiga kura umeisha katika kituo chochote cha kupigia kura na kuna wapiga kura waliopo ambao hawajapata nafasi ya kupiga kura, kituo cha kupigia kura kitakuwa wazi kwa muda wa kutosha kuwawezesha wapiga kura hao kupiga kura. - 90 Verify source ↗
Utaratibu wa kufunga upigaji kura
AI-assisted research summary: Before the polling station is closed after voting ends, the polling agent gets a final chance to make a prescribed-form statement about satisfaction, dissatisfaction, or complaints about how the vote was conducted.
90.-(1) Kabla ya kufunga kituo cha kupigia kura baada ya upigaji kura kumalizika, wakala wa upigaji kura atapewa nafasi ya mwisho kuwasilisha katika fomu itakayoainishwa kama ameridhika au hajaridhika na mwenendo wa upigaji kura au ana malalamiko kura ulivyoendeshwa katika kituo cha kupigia kura na malalamiko yoyote yaliyowasilishwa yatatatuliwa au yatashughulikiwa kadiri iwezekanavyo. kuhusu upigaji namna namna bora kwa (2) Wakati wa kuhitimisha upigaji kura, msimamizi wa kituo ataandaa taarifa akieleza kwa kina malalamiko yote yaliyotolewa wakati na baada ya kumalizika kwa upigaji kura na hatua zilizochukuliwa kwa kila malalamiko na taarifa hiyo itasomwa mbele ya na kuthibitishwa na kusainiwa na wakala wa upigaji kura, msimamizi wa kituo na msimamizi msaidizi wa kituo, na itawasilishwa kwa msimamizi wa uchaguzi kwa mujibu wa kifungu cha 102. Wakala wa upigaji kura kuwa wakala wa kuhesabu kura - 91 Verify source ↗
Wakala wa upigaji kura kuwa wakala wa kuhesabu kura
AI-assisted research summary: Mawakala wa upigaji kura au wa mbadala walioteuliwa na chama cha siasa huwa mawakala wa kuhesabu kura wakati wa kuhesabu kura. Mgombea wa urais, ubunge au udiwani anaweza kumteua wakala wa kuhesabu kura kumwakilisha wakati wa majumuisho ya matokeo ya uchaguzi.
91.-(1) Kila wakala wa upigaji kura au wakala mbadala wa upigaji kura aliyeteuliwa na chama cha siasa kwa mujibu wa kifungu cha 77 cha Sheria hii, wakati wa kuhesabu kura atakuwa wakala wa kuhesabu kura. (2) Kila mgombea katika uchaguzi wa Rais, Wabunge au Madiwani anaweza kumteua wakala wa kuhesabu kura kumwakilisha mgombea huyo mahali na wakati wa majumuisho ya matokeo ya uchaguzi yatakayofanywa na Tume, msimamizi wa uchaguzi au msimamizi msaidizi kadiri itakavyokuwa. uchaguzi, wa 80 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Mahali pa kuhesabia kura - 92 Verify source ↗
Mahali pa kuhesabia kura
AI-assisted research summary: Votes are generally counted at the polling station where they were cast, but election officials may direct nearby or grouped stations to be counted at one place for stated reasons.
92.-(1) Kwa kuzingatia masharti ya kifungu kidogo cha (2), kura zote za uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani zilizopigwa katika kituo cha kupigia kura zitahesabiwa katika kituo hicho cha kupigia kura. (2) Bila kujali masharti ya kifungu kidogo cha (1), Tume, Mkurugenzi wa Uchaguzi au msimamizi wa uchaguzi anaweza, kwa sababu za kiusalama, ufinyu wa nafasi ya kuhesabia au huduma nyingine au kwa sababu nyingine za msingi, kuelekeza kuwa kura za vituo kadhaa vya kupigia kura vilivyo karibu au vituo vyote vya kupigia kura katika eneo la uchaguzi au mchanganyiko wa maeneo ya uchaguzi yaliyo jirani, zitahesabiwa katika sehemu moja. (3) Endapo maelekezo yametolewa kwa kuzingatia kifungu kidogo cha (2), kura kutoka kila kituo kwa kutenganishwa kwa utaratibu kama vile kura zimehesabiwa katika kituo ambacho zimepigwa. zitahesabiwa kupigia kura cha (4) Wakati wa kuhitimisha kuhesabu kura katika kituo cha kupigia kura, msimamizi wa kituo kwa msaada wa msimamizi msaidizi wa kituo atazifunga kura zilizohesabiwa katika vifurushi tofauti vya kura zilizohesabiwa na zilizokataliwa. (5) Wakati wa kuhitimishwa kwa utaratibu chini ya kifungu kidogo cha (4), kila mgombea au wakala wake wa kuhesabu kura ataeleza katika fomu itakayoainishwa iwapo ameridhika au kama ana malalamiko yoyote kuhusu utaratibu huo. (6) Malalamiko yoyote yaliyowasilishwa chini ya kifungu hiki ambayo yanaweza kutatuliwa, yatashughulikiwa mapema na msimamizi wa kituo na tukio hilo litajumuishwa katika kwa msimamizi wa taarifa uchaguzi. itakayowasilishwa iwezekanavyo (7) Endapo mgombea au wakala wake wa kuhesabu kura anakataa kujaza au kusaini fomu yoyote chini ya kifungu hiki, msimamizi wa kituo au msimamizi msaidizi wa kituo atamtaka mgombea huyo au wakala wake kutoa sababu za kukataa kwake kwa 81 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 maandishi na msimamizi huyo wa kituo au msimamizi msaidizi wa kituo ataandika kukataa huko katika taarifa atakayowasilisha kwa msimamizi wa uchaguzi. (8) Mgombea au wakala wake anayekataa kutekeleza masharti ya kifungu kidogo cha (7) atazuiliwa kuhusu mwenendo wa kupiga na kuhesabu kura katika kituo hicho. kutoa malalamiko yoyote Kuhesabu kura katika - 93 Verify source ↗
Kuhesabu kura
AI-assisted research summary: The polling station supervisor must count votes after polling closes and follow the section’s procedure; candidates or counting agents present may state satisfaction or complaints at each stage, and written statements about complaints must be certified, signed, and sent to the election supervisor.
93.-(1) Msimamizi wa kila kituo cha kupigia kura akisaidiwa na msimamizi msaidizi wa kituo hicho, mapema aliyepangiwa iwezekanavyo baada ya kufunga upigaji kura, mbele ya watu waliorejewa katika kifungu cha 94, ikiwa wapo, atahesabu kura kwa kuzingatia utaratibu ulioainishwa katika Sehemu hii hadi hapo kuhesabu kura kutakapomalizika. kituo (2) Katika hitimisho la kila hatua ya mchakato wa kuhesabu kura, wagombea au mawakala wa kuhesabu kura kama wapo, watatakiwa kueleza kwa utaratibu uliowekwa kama wameridhika au wana malalamiko yoyote na kueleza malalamiko hayo ikiwa iliyohitimishwa katika yapo, kuhusu kila hatua kuhesabu kura. yaliyotolewa (3) Malalamiko ambayo yanaweza kutatuliwa au kuamuliwa, yatatatuliwa au yataamuliwa katika hatua ambayo yametolewa na msimamizi wa kituo ataandaa taarifa katika fomu itakayoainishwa, kuhusu malalamiko hayo na jinsi yalivyotatuliwa. (4) Kila maelezo yaliyoandikwa na msimamizi wa kituo kwa mujibu wa kifungu hiki yatathibitishwa na wakala wa upigaji kura, msimamizi wa kituo na msimamizi msaidizi wa kituo na yatasainiwa na kuwasilishwa kwa msimamizi wa uchaguzi. Watu wanaoweza kuwepo wakati wa kuhesabu kura - 94 Verify source ↗
Watu wanaoweza kuwepo wakati wa kuhesabu kura
AI-assisted research summary: Watu hawaruhusiwi kuwepo wakati wa kuhesabu kura, isipokuwa orodha ya watu walioorodheshwa katika kifungu hiki.
94.(1) Mtu hataruhusiwa kuwepo wakati wa kuhesabu kura isipokuwa wafuatao: (a) msimamizi wa kituo; (b) msimamizi msaidizi wa kituo; 82 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 (c) wakala wa kuhesabu kura au wakala mbadala wa kuhesabu kura; (d) mgombea; (e) afisa wa polisi au mtu mwingine anayehusika na usalama katika sehemu ambayo kura zinahesabiwa; (f) msimamizi wa uchaguzi, msimamizi msaidizi wa uchaguzi au mratibu wa uchaguzi wa Mkoa; (g) mjumbe wa Tume; (h) Mkurugenzi wa Uchaguzi au afisa wa Tume; (i) mwangalizi wa uchaguzi aliyeidhinishwa kwa maandishi na Tume; na (j) afisa anayeshughulikia uchaguzi. (2) Mtu yeyote tofauti na aliyetajwa katika kifungu kidogo cha (1) hataruhusiwa kuwepo katika eneo ambalo kura zinahesabiwa. - 95 Verify source ↗
Taratibu za kuhesabu kura
AI-assisted research summary: Kabla kuhesabu kura, msimamizi wa kituo na wasimamizi wasaidizi lazima wahakiki idadi ya waliopiga kura, wahesabu karatasi zisizotumika na zilizoharibika, wakague na wafungue lakiri na sanduku la kura.
95.-(1) Kabla msimamizi wa kituo na wasimamizi wasaidizi wa kituo hawajaanza kuhesabu kura mbele ya watu waliorejewa katika kifungu cha 94, ikiwa wapo- (a) watahakiki na kuandika idadi ya watu wote waliopiga kura katika kituo cha kupigia kura; Taratibu za kuhesabu kura zote (b) watahesabu na kuandika idadi na karatasi za kura hazikutumika, ambazo zikijumuisha karatasi za kura zozote zilizoharibika na kuzifunga katika bahasha maalumu; (c) watakagua lakiri na kuhakikisha kama imefunguliwa au imechezewa; (d) watafungua lakiri; na (e) watafungua sanduku la kura. (2) Kwa madhumuni ya Sehemu ya Pili ya Sura ya Sita ya Sheria hii, neno “lakiri” litajumuisha kufuli na utaratibu mwingine wowote, mfumo au kitu ambacho kimeidhinishwa na Tume kwa ajili ya kutunza usalama wa vitu vilivyomo katika sanduku la 83 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kupigia kura, na maneno lakiri, fungua, funga au fungua lakiri na mabadiliko yake ya kisarufi na misemo inayofanana itakapotumika kwa ajili ya lakiri au sanduku la kura, yatakuwa na maana inayofanana. (3) Baada ya sanduku la kura kufunguliwa, msimamizi wa kituo atatoa na kuhesabu kwa sauti kila karatasi ya kura na kuandika jumla ya kura zilizopatikana ndani ya sanduku la kura. (4) Baada ya kuhakikisha jumla ya karatasi za kura katika sanduku la kura, kura hizo zitahesabiwa kama ifuatavyo: ambazo (b) karatasi imeharibika (a) msimamizi wa kituo atakunjua kila karatasi ya kura, ataionesha kwa watu wote waliopo na atataja kwa sauti mgombea ambaye amepigiwa kura hiyo au kama karatasi ya kura au haikujazwa, vinginevyo si halali; za kura zimetajwa zitawekwa kwa mpangilio na katika mafungu tofauti zikionesha upande wa juu, kulingana na mgombea aliyepigiwa kura hiyo au kura isiyojazwa au isiyo halali; (c) msimamizi wa kituo atahesabu kwa sauti na kuandika idadi ya kura katika kila fungu na kuhakiki jumla yake kwa kulinganisha na idadi ya karatasi za kura jumla ya zilizopatikana ndani ya sanduku la kura na idadi ya wapiga kura waliopiga kura katika kituo cha kupigia kura. - 96 Verify source ↗
Karatasi ya kura ambayo haitahesabika kuwa halali
AI-assisted research summary: A ballot paper is not valid if it lacks an official mark, is marked in a way that could identify the voter, is unmarked, or is unclear; a vote for a withdrawn candidate is treated as a spoiled vote.
96.-(1) Karatasi ya kura haitahesabiwa kuwa halali iwapo- (a) haina alama rasmi; (b) kura iliyopigwa imepigwa kinyume na kifungu cha 84 au inatakiwa chini ya kifungu kuwa imeharibika; kuchukuliwa hicho (c) imeandikwa kitu chochote au kuwekwa alama ambayo inaweza kumtambulisha mpiga kura tofauti na namba iliyochapwa 84 Karatasi ya kura ambayo haitahesabika kuwa halali Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Uthibitisho wa msimamizi wa kituo kwenye karatasi ya kura; au (d) haijawekwa alama au ni batili kwa kutoeleweka. (2) Kura yoyote itakayopigwa kwa mgombea yeyote aliyejitoa ugombea chini ya Sheria hii itachukuliwa kuwa kura iliyoharibika. - 97 Verify source ↗
Uthibitisho wa msimamizi wa kituo
AI-assisted research summary: Msimamizi wa kituo au msimamizi msaidizi wa kituo lazima aandike “imekataliwa” juu ya kura ambayo haijahesabiwa chini ya kifungu cha 96, na aongeze “kukataliwa kumepingwa” ikiwa pingamizi dhidi ya uamuzi wake limetolewa na wakala wa kuhesabu kura.
97.-(1) Msimamizi wa kituo au msimamizi msaidizi wa kituo ataandika neno “imekataliwa” juu ya karatasi ya kura ambayo, chini ya masharti ya kifungu cha 96 haijahesabiwa. (2) Msimamizi wa kituo au msimamizi msaidizi wa kituo ataongeza kwa kuandika maneno “kukataliwa kumepingwa” kama pingamizi dhidi ya uamuzi wake limetolewa na wakala yeyote wa kuhesabu kura. Karatasi za kura zilizokataliwa - 98 Verify source ↗
Karatasi za kura zilizokataliwa
AI-assisted research summary: Msimamizi wa kituo lazima aandae taarifa ya idadi ya karatasi za kura zilizokataliwa na aeleze sababu zake.
98. Msimamizi wa kituo ataandaa maelezo yanayoonesha idadi ya karatasi za kura zilizokataliwa yenye vichwa vya taarifa vifuatavyo: (a) kukosekana kwa alama rasmi; (b) kura imepigwa kinyume na ilivyoelezwa katika kifungu cha 84(3)(c) au ichukuliwe kuwa imeharibika chini ya masharti ya kifungu cha 84(3)(j); (c) maandishi au alama ambayo itamtambulisha mpiga kura; (d) haina alama au batili kwa kutoeleweka; na (e) kura imepigwa kwa wagombea zaidi ya wale anastahili kuwapigia kura chini ya kifungu cha 84(3)(f), ambao mpiga kura na kwa maombi, atamruhusu wakala wa kuhesabu kura yeyote kutoa nakala ya maelezo hayo. Kufungana kwa kura na kurudia kuhesabu katika uchaguzi unaoshindaniwa - 99 Verify source ↗
Kufungana kwa kura na kurudia kuhesabu katika uchaguzi
AI-assisted research summary: Kama kuna tie ya kura katika uchaguzi unaoshindaniwa, msimamizi wa uchaguzi lazima ahesabu upya kura. Iwapo tie itaendelea baada ya kuhesabu upya, Tume inapanga siku nyingine ya kupiga kura ndani ya siku 30 baada ya siku ya uchaguzi. Wagombea au mawakala wao wanaweza kuomba kuhesabiwa upya.
99.-(1) Endapo kwa mujibu wa kifungu cha 103 au 104 kunatokea kufungana kwa kura baina ya wagombea katika uchaguzi unaoshindaniwa kiasi kwamba nyongeza ya kura moja ingefanya yeyote kati yao kutangazwa kuchaguliwa, msimamizi wa uchaguzi atarudia kuhesabu kura zilizopigwa. 85 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Wagombea au mawakala wa kuhesabu kura wanaweza kuomba kurudia kuhesabu kura Uamuzi wa msimamizi wa kituo (2) Endapo kuna kufungana tena kwa kura kama ilivyothibitishwa kwa kurudia kuhesabu kura, msimamizi wa uchaguzi, kwa kuzingatia masharti ya kifungu hiki atatoa taarifa ya maelezo hayo kwa Tume, ambayo, kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, itapanga siku nyingine inayofaa, si zaidi ya siku thelathini baada ya siku ya uchaguzi, kwa ajili ya kupiga kura kwa wagombea ambao kura zao zilifungana katika upigaji kura wa kwanza. - 100 Verify source ↗
Wagombea au mawakala wa kuhesabu kura wanaweza kuomba
AI-assisted research summary: Mgombea au wakala wake anaweza kuomba kura zihesabiwe upya mara moja au mbili ikiwa yuko hapo wakati wa kuhesabu kuisha; msimamizi wa kituo anaweza kukataa ombi la kuhesabu tena mara ya tatu au zaidi ikiwa matokeo ya marudio mawili ya mwisho yanafanana.
100.-(1) Mgombea au wakala wake wa kuhesabu kura, iwapo atakuwepo wakati wa kuhesabu au kurudia kuhesabu kura kunapomalizika, anaweza, kumtaka msimamizi wa kituo kurudia kuhesabu kura mara moja au mbili lakini msimamizi wa kituo anaweza kukataa kuhesabu mara ya tatu au zaidi kama matokeo ya kurudia kuhesabu kura mara mbili za mwisho yanalingana. (2) Hatua hazitachukuliwa baada ya kumaliza kuhesabiwa au kurudiwa kuhesabiwa kura mpaka wagombea na mawakala wa kuhesabu kura waliopo kituoni wakati wa kura watakapokuwa wamepewa nafasi ya kutosha kutumia haki iliyotolewa katika kifungu kidogo cha (1). kuhesabu kumaliza yoyote kuhusu karatasi ya - 101 Verify source ↗
Uamuzi wa msimamizi wa kituo
AI-assisted research summary: Msimamizi wa kituo lazima aamue hoja yenye mgogoro baada ya kushauriana na wasaidizi au wahusika waliopo.
101. Msimamizi wa kituo, baada kushauriana na msimamizi msadizi wa kituo, mawakala, au wagombea kama wapo, ataamua hoja itakayojitokeza yenye mgogoro, uamuzi utatakiwa kurejewa na msimamizi wa uchaguzi au msimamizi msaidizi wa uchaguzi wakati wa kujumlisha kura kutoka vituo vyote vya kupigia kura katika jimbo au kata, na uamuzi wa msimamizi wa uchaguzi au msimamizi msaidizi wa uchaguzi utakuwa wa mwisho na unaweza tu kuhojiwa kwa kurejewa katika shauri la uchaguzi kwa mujibu wa Sura ya Nane ya Sheria hii. Wajibu wa msimamizi wa - 102 Verify source ↗
Wajibu wa msimamizi wa kituo baada ya kuhesabu kura
AI-assisted research summary: Baada ya kuhesabu kura, msimamizi wa kituo lazima apange, asaini, abatike na akabidhi nyaraka na sanduku la kura kama kifungu kinavyoelekeza.
102.-(1) Baada ya kuhitimisha kuhesabu kura kwa mujibu wa kifungu cha 93, msimamizi wa kituo- 86 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 kituo baada ya kuhesabu kura (a) atafunga katika vifurushi tofauti karatasi za na zenye mgogoro kura halali, zilizokataliwa; (b) ataandaa taarifa tofauti za matokeo kwa ajili ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Tume itakavyoelekeza, ambazo zitasainiwa na msimamizi wa kituo na mawakala, ikiwa wapo; namna kwa (c) atawataka mawakala wa kuhesabu kura, au mgombea kama yupo, kueleza katika fomu au maalumu kuthibitisha kura zilivyohesabiwa; malalamiko kuridhika yoyote namna (d) atabandika katika sehemu ya wazi nakala ya matokeo ya awali ya uchaguzi katika kituo cha kupigia kura; (e) atampa kila wakala wa kuhesabu kura aliyepo katika kituo nakala ya taarifa ya matokeo; (f) ataweka vifurushi vyote vya karatasi za kura ndani ya sanduku la kura na kulifunga kwa lakiri; na (g) akiwa ameongozana na mawakala wa vituo vya kupigia kura waliopo kwa idadi itakayoelekezwa na Tume, atapeleka na kukabidhi kwa msimamizi wa uchaguzi sanduku la kura pamoja na taarifa ya matokeo ya uchaguzi wa kituo cha kupigia kura. (2) Endapo mgombea au wakala wake atakataa kusaini fomu iliyoainishwa chini ya kifungu hiki, msimamizi wa kituo au msimamizi msaidizi wa kituo atamtaka mgombea huyo au wakala kutoa sababu za kukataa kwa maandishi. (3) Endapo mgombea au wakala wake atakataa kutekeleza masharti ya kifungu kidogo cha (2) atazuiliwa kutoa malalamiko yoyote kuhusu utaratibu wa kupiga na kuhesabu kura katika kituo husika. 87 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Majumuisho ya kura katika uchaguzi wa wabunge - 103 Verify source ↗
Majumuisho ya kura katika uchaguzi wa wabunge
AI-assisted research summary: This section sets rules for counting parliamentary election votes, who may be present, and when candidates or agents may ask for verification or a recount.
103.-(1) Masharti ya kifungu cha 45 yatatumika kwa kuzingatia maboresho yatakayohitajika kuhusu kujumlisha kura katika uchaguzi wa wabunge. (2) Watu wafuatao wanaruhusiwa kuwepo katika kituo cha kujumlisha kura: (a) msimamizi wa uchaguzi; (b) msimamizi msaidizi wa uchaguzi; (c) mratibu wa uchaguzi wa Mkoa; (d) mjumbe wa Tume; (e) Mkurugenzi wa Uchaguzi au afisa wa Tume; (f) mgombea; (g) wakala wa kuhesabu kura; (h) afisa wa polisi au mtu mwingine anayehusika na usalama wa mahali pa kuhesabia kura; (i) mwangalizi aliyeidhinishwa kwa maandishi na Tume; au (j) afisa anayeshughulikia uchaguzi. (3) Baada ya taarifa zote za matokeo na masanduku ya kura yenye karatasi za kura zinazotokana na uchaguzi wa Wabunge kupokelewa kutoka kwenye vituo vya kupigia kura katika jimbo, msimamizi wa uchaguzi, baada ya kuamua uhalali wa kura zenye mgogoro na kabla ya kujumlisha kura hizo, atatangaza kwa sauti matokeo ya kila kituo cha kupigia kura katika jimbo kwa kufuatana. (4) Mgombea au wakala wa upigaji kura anaweza uchaguzi kumuomba msimamizi wa kuangalia sehemu yoyote ya majumuisho ili kuhakiki usahihi wake lakini hatastahili kuomba kurudia kuhesabu kura zote au karatasi zote za kura kutoka katika kituo chochote cha kupigia kura, isipokuwa kama usahihi wa taarifa ya matokeo kutoka kituo hicho cha kupigia kura ulipingwa na wakala wa upigaji kura au mgombea aliyekuwepo katika kituo cha kupigia kura. (5) Endapo maombi yatakuwa yamefanywa kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (4), msimamizi wa uchaguzi bila sababu za msingi, hatakataa kuhakiki 88 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Majumuisho ya kura katika uchaguzi wa madiwani majumuisho au kurudia kuhesabu karatasi za kura katika kituo chochote cha kupigia kura. - 104 Verify source ↗
Majumuisho ya kura katika uchaguzi wa madiwani
AI-assisted research summary: Baadhi ya watu wanaruhusiwa kuwepo katika kituo cha kujumlisha kura, na msimamizi wa uchaguzi au msimamizi msaidizi lazima atangaze matokeo na kujumlisha kura kwa utaratibu ulioelezwa.
104.-(1) Watu wafuatao wanaruhusiwa kuwepo katika kituo cha kujumlisha kura: (a) msimamizi wa uchaguzi; (b) msimamizi msaidizi wa uchaguzi; (c) mratibu wa uchaguzi wa Mkoa; (d) mjumbe wa Tume; (e) Mkurugenzi wa Uchaguzi au afisa wa Tume; (f) mgombea; (g) wakala wa kuhesabu kura; (h) afisa wa polisi au mtu mwingine anayehusika na usalama wa mahali pa kuhesabia kura; (i) mwangalizi aliyeidhinishwa kwa maandishi na Tume; au (j) afisa anayeshughulikia uchaguzi. (2) Baada ya taarifa zote za matokeo na masanduku ya kura yenye karatasi za kura zinazotokana na uchaguzi wa madiwani kupokelewa kutoka kwenye vituo vya kupigia kura katika kata, msimamizi wa uchaguzi au msimamizi msaidizi wa uchaguzi, kadiri itakavyokuwa, baada ya kuamua uhalali wa kura zozote zenye mgogoro na kabla ya kujumlisha kura, atatangaza kwa sauti matokeo ya kila kituo cha kupigia kura katika kata kwa kufuatana. (3) Baada ya kuhitimisha utaratibu chini ya kifungu kidogo cha (2), msimamizi wa uchaguzi au msimamizi msaidizi wa ataendelea kujumlisha pamoja idadi ya- uchaguzi (a) kura zote zilizopigwa katika kata; (b) kura zote zilizopigwa kwa kila mgombea; na (c) karatasi za kura zilizokataliwa. Kutangaza matokeo ya ubunge - 105 Verify source ↗
Kutangaza matokeo ya ubunge
AI-assisted research summary: Baada ya matokeo ya uchaguzi kuthibitishwa, msimamizi wa uchaguzi lazima atangaze mshindi, amjulishe mgombea aliyeshinda, abandike taarifa ya matokeo, na apeleke taarifa kwa Tume. Tume pia inaweza kusitisha uchaguzi ikiwa kuna ukiukwaji na kuweka siku nyingine ndani ya siku 30.
105.-(1) Endapo matokeo ya uchaguzi yamehakikiwa, msimamizi wa unaoshindaniwa uchaguzi- 89 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 (a) mapema atatangaza iwezekanavyo kuchaguliwa kwa mgombea aliyepigiwa kura nyingi halali; (b) atamtaarifu mgombea aliyeshinda kuhusu kuchaguliwa kwake; (c) atahakikisha taarifa kamili ya matokeo inabandikwa kwenye makao makuu ya Halmashauri inayohusika; na (d) ataandaa taarifa na kuiwasilisha kwa Tume ikionesha- (i) malalamiko yaliyotolewa katika kila hatua ya uchaguzi na hatua au uamuzi uliochukuliwa kwa kila malalamiko; (ii) maoni ya wagombea kuhusu uchaguzi; na (iii) matokeo ya uchaguzi, na Tume itaelekeza matokeo, pamoja na idadi ya kura jimbo, alizopata kwa kila mgombea katika kila kuchapishwa katika Gazeti la Serikali. chama (2) Endapo itatokea Mbunge mteule hana nia ya kuendelea na ubunge au kufariki kabla ya siasa kinachomdhamini kuapishwa, mwanachama husika, kitaitaarifu Tume kwa maandishi na Tume, kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali, itateua siku nyingine ya uteuzi wa mgombea kwa mujibu wa kifungu cha 49. cha Kutangaza matokeo ya udiwani (3) Tume inaweza kusitisha mchakato wa uchaguzi pale itakapobainika kuwa kuna ukiukwaji wa Sheria na taratibu za uchaguzi, na ndani ya siku thelathini itatangaza siku nyingine ya uchaguzi. - 106 Verify source ↗
Kutangaza matokeo ya udiwani
AI-assisted research summary: After election results are verified, the election supervisor must announce the winning candidate, notify the winner, post the full results notice, and submit a report to the Commission. The Commission may suspend the election process for breaches and must then announce another election day within 30 days.
106.-(1) Endapo matokeo ya uchaguzi yamehakikiwa, msimamizi wa uchaguzi- (a) mapema atatangaza iwezekanavyo kuchaguliwa mgombea aliyepigiwa kura nyingi halali; (b) atamtaarifu mgombea aliyeshinda kuhusu kuchaguliwa kwake; (c) atahakikisha taarifa kamili ya matokeo 90 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 inabandikwa kwenye Ofisi ya Afisa Mtendaji wa Kata na Makao Makuu ya Halmashauri inayohusika; (d) ataandaa taarifa na kuiwasilisha kwa Tume ikionesha- (i) malalamiko yaliyotolewa katika kila hatua ya uchaguzi na hatua au uamuzi uliochukuliwa kwa kila malalamiko; (ii) maoni ya wagombea kuhusu uchaguzi; na (iii) matokeo ya uchaguzi, na Tume itaelekeza matokeo, pamoja na idadi ya kura alizopata kwa kila mgombea katika kila jimbo, kuchapishwa katika Gazeti la Serikali. (2) Endapo itatokea Diwani mteule hana nia ya kuendelea na udiwani au kufariki kabla ya kuapishwa, chama cha siasa kinachomdhamini mwanachama husika, kitaitaarifu Tume kwa maandishi na Tume, kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali itateua siku nyingine ya uteuzi wa mgombea kwa mujibu wa kifungu cha 61. (3) Tume inaweza kusitisha mchakato wa uchaguzi pale itakapobainika kuwa kuna ukiukwaji wa Sheria na taratibu za uchaguzi, na ndani ya siku thelathini itatangaza siku nyingine ya uchaguzi. - 107 Verify source ↗
Utunzaji wa nyaraka
AI-assisted research summary: Msimamizi wa uchaguzi na Tume lazima wahifadhi kwa usalama nyaraka za uchaguzi, kisha waziteketeze baada ya miezi sita tangu siku ya uchaguzi isipokuwa mahakama itaagiza vinginevyo.
107.-(1) Msimamizi wa uchaguzi atahakikisha anatunza kwa usalama nyaraka zote zinazohusu uendeshaji wa uchaguzi. (2) Tume itahakikisha inatunza kwa usalama nyaraka zote zinazohusu uendeshaji wa uchaguzi zilizowasilishwa kwake chini ya masharti ya Sheria hii. (3) Msimamizi wa uchaguzi na Tume watahakikisha nyaraka zote ambazo kifungu hiki kinatumika, zinateketezwa baada ya kupita kipindi cha miezi sita toka siku ya uchaguzi isipokuwa kama itaelekezwa vinginevyo kwa amri ya Mahakama ya wilaya au Mahakama Kuu itakayotolewa kutokana na mwenendo wa mashauri ya uchaguzi ya udiwani au 91 Utunzaji wa nyaraka Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Mamlaka ya wasimamizi wasaidizi wa vituo Mamlaka ya wagombea Kutokuwepo kwa mawakala hakutabatilisha mwenendo ubunge mtawalia. - 108 Verify source ↗
Mamlaka ya wasimamizi wasaidizi wa vituo
AI-assisted research summary: Msimamizi msaidizi wa kituo anaweza kupewa ruhusa na msimamizi wa kituo kufanya kazi ambazo msimamizi wa kituo anaweza kufanya, lakini hawezi kutoa amri ya kukamatwa au kumtenga/kumuondoa mtu katika kituo cha kupigia kura.
108. Msimamizi msaidizi wa kituo anaweza kuruhusiwa na msimamizi wa kituo kufanya jambo lolote au kitu chochote ambacho msimamizi wa kituo ametakiwa kufanya au ameruhusiwa kufanya katika kituo cha kupigia kura na Sheria hii, isipokuwa hawezi kutoa amri ya kukamatwa mtu yeyote, au kumtenga au kumuondoa mtu yeyote katika kituo cha kupigia kura. - 109 Verify source ↗
Mamlaka ya wagombea
AI-assisted research summary: Mgombea anaweza kufanya au kusaidia kufanya kitendo chochote ambacho wakala wa upigaji kura au wakala wa kuhesabu kura ameidhinishwa au ametakiwa kufanya.
109. Mgombea anaweza kutenda kitendo chochote au kitu chochote ambacho wakala wa upigaji kura ameidhinishwa au ametakiwa kufanya, na anaweza kumsaidia wakala wa upigaji kura au wakala wa kuhesabu kura kufanya kitendo au kitu hicho. - 110 Verify source ↗
Kutokuwepo kwa mawakala hakutabatilisha mwenendo
AI-assisted research summary: If something is done properly, it is not invalid just because the polling agent, counting agent, or candidate was absent at the scheduled time and place.
110. Endapo katika Sheria hii, kitendo chochote au kitu chochote kimetakiwa au kimeidhinishwa kufanyika mbele ya wakala wa upigaji kura au wakala wa kuhesabu kura au mgombea, kutokuwepo kwa mawakala hao au mgombea kwa muda na mahali palipopangwa kwa ajili hiyo, kama kitendo au kitu hicho kimefanywa kwa usahihi, hakutabatilisha kitu au kitendo kilichofanywa. Chaguzi zinazofanyika kwa wakati mmoja - 111 Verify source ↗
Chaguzi zilizofanyika kwa wakati mmoja
AI-assisted research summary: When presidential, parliamentary, and council elections are held on the same day in an area, voting happens together at all polling stations and counting is done separately.
111. Endapo katika eneo la uchaguzi inatokea inapangwa kuwa siku ya uchaguzi siku moja unaoshindaniwa wa Rais, Wabunge na Madiwani- (a) upigaji kura katika chaguzi tatu, utafanyika kwa pamoja katika vituo vyote vya kupigia kura katika eneo hilo; kura yaliyotenganishwa (b) msimamizi wa uchaguzi atatoa masanduku ya na yanayotofautiana na kila msimamizi wa kituo ataandaa na kusimamia kituo chake cha kupigia kura na ataweka masanduku ya kupigia kura kwa utaratibu ambao utaepuka mkanganyiko wowote unaoweza kutokea kwa sababu ya upigaji kura wa chaguzi tofauti zinazofanyika kwa pamoja: 92 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Isipokuwa kwamba, kwa kuzingatia maelekezo yoyote ya Tume kwa ajili hiyo, sanduku moja la kura linaweza kutolewa kwa kila kituo cha kupigia kura kwa uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani; (c) karatasi za kura kwa chaguzi hizo zitakuwa ili kuzitofautisha kwa na rangi tofauti urahisi; (d) mpiga kura ambaye ataondoka katika kituo cha kupigia kura baada ya kupiga kura katika mojawapo ya chaguzi hataruhusiwa kuingia tena katika kituo hicho cha kupigia kura kwa ajili ya kupiga kura katika uchaguzi mwingine; (e) matakwa ya aya (c) yatachukuliwa kuwa yamezingatiwa katika chaguzi zote endapo taarifa zilizoainishwa katika aya hiyo zitaitishwa mapema iwezekanavyo kabla ya kumpa mpiga kura karatasi ya kura kwa uchaguzi wowote ambao alipewa kwanza; na (f) kuhesabu kura kwa chaguzi hizo kutafanyika kwa kutenganishwa. tatu SEHEMU YA SITA UTEUZI WA WABUNGE NA MADIWANI WANAWAKE WA VITI MAALUMU Uteuzi wa wabunge wanawake wa viti maalumu
Part
SEHEMU YA SITA
- 112 Verify source ↗
Uteuzi wa wabunge wanawake wa viti maalumu
AI-assisted research summary: Political parties may submit qualified women candidates to the Commission at least 30 days before the election, and the Commission selects and announces the women special-seat MPs.
112.-(1) Kutakuwa na Wabunge wanawake wa viti maalumu katika Bunge kama ilivyoainishwa katika Ibara ya 66 ya Katiba. (2) Chama cha siasa kinachogombea katika uchaguzi wa Wabunge utakaofanyika baada ya kuvunjwa kwa Bunge kinaweza kupendekeza na kuwasilisha kwa Tume majina ya wagombea wanawake wenye sifa kwa ajili ya uteuzi wa viti maalumu vya wanawake si chini ya siku thelathini kabla ya siku ya uchaguzi. (3) Tume itaainisha wanawake watakaoteuliwa na kila chama cha siasa. idadi ya wagombea 93 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 (4) Majina ya wanawake wagombea waliopendekezwa kwa Tume yatakuwa katika mpangilio kwa kuzingatia kipaumbele. mwanamke Kila mgombea aliyependekezwa kwa Tume atatakiwa kujaza fomu ya uteuzi. (5) (6) Masharti ya Ibara ya 67 ya Katiba ambaye kila mwanamke kwa yatatumika amedhaminiwa na chama cha siasa. (7) Kwa kuzingatia Ibara ya 66, 67 na 78 za Katiba na kwa mujibu wa mpangilio wa kipaumbele uliooneshwa katika orodha iliyopendekezwa na kila chama cha siasa, Tume itateua na kutangaza idadi ya wanawake wagombea kutoka katika vyama vya siasa vinavyohusika kuwa Wabunge Wanawake Viti Maalumu. (8) Tume itatuma taarifa ya uteuzi kwa Spika wa Bunge na kwa Makatibu Wakuu wa vyama vya siasa vinavyohusika. (9) Orodha ya majina ya wanawake wagombea waliopendekezwa kwa Tume kwa mujibu wa Ibara ya 78(4) ya Katiba na kila chama cha siasa kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu, kwa kuzingatia Ibara ya 76(3) ya Katiba, itakuwa ndiyo orodha itakayotumiwa na Tume kwa madhumuni ya kujaza nafasi wazi ya ofisi ya Mbunge wa viti maalumu vya wanawake wakati wa kipindi chote cha uhai wa Bunge: Isipokuwa kwamba, inapotokea orodha ya majina iliyowasilishwa kwa Tume imemalizika, Tume itakitaka chama husika kuwasilisha orodha ya nyongeza ya majina ya wagombea wanawake viti maalumu wanaopendekezwa kwa ajili ya uteuzi. - 113 Verify source ↗
Uteuzi wa madiwani wanawake viti maalumu
AI-assisted research summary: Section 113 sets out how women’s special-seat councillor candidates are proposed and selected through the Electoral Commission.
113.-(1) Kutakuwa na viti maalumu vya wanawake katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa kama ilivyoainishwa chini ya Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji). (2) Kila chama cha siasa ambacho kitagombea uchaguzi wa udiwani katika uchaguzi mkuu, chini ya 94 Uteuzi wa madiwani wanawake viti maalumu Sura ya 287 na 288 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) ndani ya Halmashauri, kinaweza kupendekeza kwa Tume, majina ya wanawake ambao wana sifa za kuteuliwa kuwa wagombea wa viti maalumu vya wanawake. (3) Kwa kuzingatia masharti ya Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) au kadiri itakavyokuwa, Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji), Tume idadi ya wagombea itaainisha wanawake watakaoteuliwa na kila chama cha siasa. (4) Kila chama cha siasa kinachowadhamini wagombea wanawake katika uchaguzi kitapendekeza kwa Tume orodha ya wagombea si chini ya siku thelatihini kabla ya siku ya uchaguzi. ya majina ya wanawake wanaopendekezwa kwa Tume yatakuwa katika mpangilio wa kipaumbele. (5) Orodha (6) Kila mgombea aliyependekezwa kwa Tume atatakiwa kujaza fomu ya uteuzi. mwanamke Sura ya 287 na Sura ya 288 (7) Masharti ya kifungu cha 58 yatatumika kwa kila mwanamke aliyedhaminiwa na chama cha siasa kuwa mgombea. (8) Kwa mujibu wa kifungu cha 58, Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) na kwa mujibu wa mpangilio wa kipaumbele ulioainishwa katika orodha iliyopendekezwa na kila chama cha siasa, Tume itatangaza idadi ya wanawake wagombea kutoka siasa vinavyohusika ambao katika vyama vya watachaguliwa kuwa Madiwani Wanawake Viti Maalumu. (9) Tume itapeleka taarifa ya uteuzi kwa Halmashauri na Makatibu Wakuu wa vyama vya siasa vinavyohusika. (10) Orodha ya majina ya wanawake wagombea waliopendekezwa kwa Tume na kila chama cha siasa wakati wa uchaguzi mkuu itakuwa ndiyo orodha itakayotumiwa na Tume kwa madhumuni ya kujaza nafasi wazi ya ofisi ya Diwani wa viti maalumu 95 Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024 wanawake wakati wa kipindi chote cha miaka mitano baada ya uchaguzi mkuu: iliyowasilishwa kwa Tume Isipokuwa kwamba, inapotokea orodha ya majina imemalizika, Tume itakitaka chama husika kuwasilisha orodha ya nyongeza ya majina ya wagombea wanawake viti maalumu wanaopendekezwa kwa ajili ya uteuzi. SURA YA SABA MAKOSA NA ADHABU SEHEMU YA KWANZA MAKOSA YANAYOHUSU UANDIKISHAJI NA UTEUZI Makosa yanayohusu uandikishaji
Provision text is displayed from LexChat’s stored statute record. Use the official source links to verify amendments, commencement, and current legal force.
Ask AI about this statute
Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2024
Sign in to ask AI about this statute
Sign in to start authenticated, citation-grounded statute research.
Sign in