SHERIA NDOGO YA AFYA NA USAFI WA MAZINGIRA YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IKUNGI YA MWAKA 2022
Sheria Ndogo hii inaitwa Sheria Ndogo ya Afya na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya Ikungi ya Mwaka 2021, na itaanza kutumika baada ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali.
AI-assisted research synopsis — verify against the official legal text below.
- Jurisdiction
- Tanzania
- Instrument
- Regulation
- Citation
- SHERIA NDOGO YA AFYA NA USAFI WA MAZINGIRA YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IKUNGI YA MWAKA 2022
- Version
- Undated source snapshot
- Language
- sw
- Official source
- View official record ↗
Statute overview
About this statute
Sheria Ndogo hii inaitwa Sheria Ndogo ya Afya na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya Ikungi ya Mwaka 2021, na itaanza kutumika baada ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali. This section defines several terms used in the by-law, including officer, food, council, household, wastewater, resident, director, and agent. Wamiliki na wakazi lazima wasafishe maeneo yao, waondoe uchafu kwenye mifereji ya maji, na washiriki usafi wa mazingira kila jumamosi ya mwisho ya mwezi au siku itakayowekwa na Halmashauri. Wamiliki wa nyumba au maeneo ya biashara lazima waweke taa yenye mwanga nje ya jengo na waiwashe usiku. Property owners must keep their premises free of stagnant water, wastewater, garbage, and other matter that could create mosquito or harmful-insect breeding sites.
Search within this statute
Search all stored provisions in this version.
Legal text
Provisions of SHERIA NDOGO YA AFYA NA USAFI WA MAZINGIRA YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IKUNGI YA MWAKA 2022
Showing 24 of 24
- 1 Verify source ↗
Sheria Ndogo hii itajulikana kama Sheria Ndogo
AI-assisted research summary: Sheria Ndogo hii inaitwa Sheria Ndogo ya Afya na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya Ikungi ya Mwaka 2021, na itaanza kutumika baada ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali.
1. Sheria Ndogo hii itajulikana kama Sheria Ndogo ya Afya na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya Ikungi ya Mwaka 2021 na itaanza kutumika baada ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali. Tafsiri - 2 Verify source ↗
Katika Sheria Ndogo hii
AI-assisted research summary: This section defines several terms used in the by-law, including officer, food, council, household, wastewater, resident, director, and agent.
2. Katika Sheria Ndogo hii isipokuwa pale itakavyoelekezwa vinginevyo; “Afisa Mwidhiniwa” maana yake ni Afisa yeyote kusimamia na Halmashauri atakayeteuliwa utekelezaji wa Sheria Ndogo hii; “chakula” maana yake ni kitu chochote kinacholiwa au kunywewa na binadamu isipokuwa dawa, hii ni pamoja na- (a) kitu chochote kinachotumika katika matengenezo ya chakula; (b) kitu chochote kinachoongeza ladha ya chakula; au 1 Sheria Ndogo ya Afya Na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Tangazo la Serikali Na. 216 (Linaendelea.) (c) kitu chochote kinachobadili rangi ya chakula; “Halmashauri” maana yake ni Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi; “kaya” maana yake ni familia inayojumuisha baba, mama, mtoto au watoto na mtu mwingine yeyote anayeishi na familia hiyo au watu wanaokaa katika nyumba moja na kuishi kama familia au mtu yeyote anayeishi peke yake katika chumba au nyumba; “maji taka” maana yake ni kinyesi au mkojo na uchafu mwingine kama maji ya kuoga na maji ya kupigia deki, kuosha vyombo, maji yanayotokana na uchafu kutoka vituo vya mafuta, vituo vya kuoshea magari na viwandani ambapo yana kemikali au yasiyokuwa na kemikali na ambayo hayajasafishwa; “mkazi” maana yake ni mtu yeyote anayeishi katika eneo la Halmashauri na ambaye ana kaya au anaishi katika kaya au taasisi iliyopo katika eneo la Halmashauri au anafanya biashara katika eneo la Halmashauri; “Mkurugenzi” maana yake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri pamoja na Afisa yeyote atakayeteuliwa kutekeleza majukumu ya Mkurugenzi; “Wakala” maana yake ni mtu binafsi au kikundi cha watu, kampuni, taasisi au shirika aliyeteuliwa kusimamia utekelezaji wa Sheria Ndogo hii. - 3 Verify source ↗
(1) Kila mkazi anayemiliki eneo la nyumba,
AI-assisted research summary: Wamiliki na wakazi lazima wasafishe maeneo yao, waondoe uchafu kwenye mifereji ya maji, na washiriki usafi wa mazingira kila jumamosi ya mwisho ya mwezi au siku itakayowekwa na Halmashauri.
3.-(1) Kila mkazi anayemiliki eneo la nyumba, kiwanja au biashara atakuwa na wajibu wa kuhakikisha kwamba anafanya usafi wa mazingira yanayozunguka makazi au eneo lake hadi mwanzo wa mipaka ya barabara ya mbele ya nyumba yake. (2) Kila mmiliki wa nyumba, kiwanja au eneo la biashara atakuwa na wajibu wa kuondoa uchafu kama vile mchanga, majani, nyasi au vitu vingine vinavyofanana na hivyo kwenye mifereji ya kupitisha maji inayozunguka au kupita kando ya nyumba, kiwanja au eneo la biashara yake. (3) Bila kuathiri masharti ya kifungu kidogo cha (1), na cha (2) kila mkazi atakuwa na wajibu wa kushiriki katika shughuli za usafi wa mazingira kila jumamosi ya mwisho 2 Wajibu wa kufanya usafi wa mazingira Sheria Ndogo ya Afya Na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Tangazo la Serikali Na. 216 (Linaendelea.) Uwekaji taa za nje ya nyumba na upakaji rangi Wajibu wa kuondoa na kudhibiti mazalia ya mbu wa mwezi au katika siku itakayopangwa na Halmashauri. (4) Mtu yeyote atakayekiuka masharti ya kifungu atakuwa ametenda kosa. - 4 Verify source ↗
(1) Kila mmiliki wa nyumba au eneo la biashara
AI-assisted research summary: Wamiliki wa nyumba au maeneo ya biashara lazima waweke taa yenye mwanga nje ya jengo na waiwashe usiku.
4.-(1) Kila mmiliki wa nyumba au eneo la biashara atakuwa na wajibu wa kuweka taa yenye mwanga nje ya jengo analoishi au analolitumia kwa shughuli za biashara na atatakiwa kuiwasha wakati wa usiku. (2) Mtu yeyote ambaye, bila sababu za msingi atakiuka masharti ya kifungu kidogo cha (1) atakuwa ametenda kosa. - 5 Verify source ↗
(1) Mmiliki wa nyumba, kiwanja au eneo la
AI-assisted research summary: Property owners must keep their premises free of stagnant water, wastewater, garbage, and other matter that could create mosquito or harmful-insect breeding sites.
5.-(1) Mmiliki wa nyumba, kiwanja au eneo la biashara atakuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa katika eneo lake hakuna mkusanyiko wa maji, maji machafu, takataka au kitu chochote cha majimaji au kigumu ambacho kinaweza kuruhusu kuwepo kwa mazalia ya mbu au wadudu wengine wenye madhara kwa afya ya binadamu. (2) Mtu yeyote ambaye bila sababu za msingi, atakiuka masharti ya kifungu kidogo cha (1) atakuwa ametenda kosa. Upulizaji dawa - 6 Verify source ↗
(1) Mtu yeyote anayeendesha biashara ya
AI-assisted research summary: A person operating a pest-spraying business in a council area must have a government-recognized professional certificate, a valid council license, and be supervised by a Health Officer during spraying; breaking these conditions is an offence.
6.-(1) Mtu yeyote anayeendesha biashara ya upuliziaji dawa ya kuuwa wadudu au wanyama waharibifu katika eneo la Halmashauri atatakiwa: (a) kuwa na cheti cha taaluma kinachotambuliwa na Serikali na leseni hai kutoka Halmashauri; (b) kusimamiwa na Afisa Afya wakati wa upulizaji; na (c) kutoa ya kilichosainiwa na Afisa afya. baada cheti kupuliza dawa (2) Mtu yeyote atakayekiuka masharti ya kifungu kidogo cha (1) atakuwa ametenda kosa. Matengenez o na maegesho ya magari, pikipiki na mitambo - 7 Verify source ↗
(1) Matengenezo ya magari, pikipiki na mitambo
AI-assisted research summary: Matengenezo ya magari, pikipiki na mitambo lazima yafanyike katika karakana, gereji au maeneo yaliyoruhusiwa baada ya kibali cha Halmashauri, na hairuhusiwi kutengeneza au kuegesha gari bovu mahali palipozuiwa.
7.-(1) Matengenezo ya magari, pikipiki na mitambo yatatakiwa kufanyika kwenye karakana, gereji au maeneo yaliyoruhusiwa baada ya kupata kibali rasmi kutoka Halmashauri. (2) Mtu yeyote: 3 Sheria Ndogo ya Afya Na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Tangazo la Serikali Na. 216 (Linaendelea.) (a) hatoruhusiwa kutengeneza gari, pikipiki au mtambo wowote katika eneo la makazi, eneo la wazi au eneo ambalo halikutengwa kwa shughuli hiyo; au (b) kuegesha gari bovu kwenye njia ya miguu, mtaa, uchochoro, mtaro, maeneo ya wazi au barabarani. (3) Mtu yeyote atakayekiuka, bila sababu za msingi, masharti ya kifungu kidogo cha (2) atakuwa ametenda kosa. Utengenezaj i, na uuzaji vyakula. - 8 Verify source ↗
(1) Mtu yeyote anayetengeneza, kuchoma, kupika,
AI-assisted research summary: Watu wanaotengeneza, kuchoma, kupika, kuchemsha au kuuza chakula katika eneo la Halmashauri lazima watii masharti ya afya na wawe na kibali cha Afisa Afya wa Halmashauri.
8.-(1) Mtu yeyote anayetengeneza, kuchoma, kupika, kuchemsha au kuuza chakula cha aina yoyote katika eneo la Halmashauri atatakiwa: (a) kutimiza masharti na kanuni za afya; na (b) kuwa na kibali kutoka kwa Afisa Afya wa Halmashauri. (2) Mtu yeyote atakayekiuka, bila sababu za msingi, masharti ya kifungu kidogo cha (1) atakuwa ametenda kosa. Machinjio na maduka ya nyama - 9 Verify source ↗
(1) Mtu yeyote hatoruhusiwa
AI-assisted research summary: Haramu kuchinja, kuuza, au kusafirisha nyama kwa masharti yaliyopigwa marufuku hapa; pia mmiliki wa duka la nyama lazima ahakikishe duka linatimiza viwango vilivyoorodheshwa.
9.-(1) Mtu yeyote hatoruhusiwa: (a) kwa madhumuni ya kibiashara kuchinja mifugo katika maeneo yasiyokuwa machinjio; (b) kuuza nyama ya aina yoyote katika maeneo yasiyokuwa maduka ya nyama au katika maeneo yasiyoruhusiwa na Halmashauri; (c) kuuza nyama isiyokaguliwa na mtaalamu wa mifugo au mtaalamu wa afya; na (d) kusafirisha nyama kwa madhumuni ya kibiashara kutoka machinjioni bila kutumia gari maalumu nyama lililoidhinishwa na Halmashauri. (2) Kila mmiliki wa duka la kuuzia nyama atatakiwa kuhakikisha yafuatayo: kusafirishia la (a) duka lake ni jengo la kudumu lililosakafiwa kwa marumaru nyeupe hadi urefu wa futi sita kutoka usawa wa sakafu; (b) duka lake lina maji safi, misumeno ya kukatia nyama na vyuma vya kutundikia nyama; (c) duka lake lina kabati la vioo na jokofu la 4 Sheria Ndogo ya Afya Na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Tangazo la Serikali Na. 216 (Linaendelea.) kuhifadhia nyama na mizani ya kupimia nyama; (d) duka lake lina pipa au kifaa cha kuhifadhia takataka; (e) muuzaji ana vazi jeupe pamoja na aproni nyeupe na kofia nyeupe; (f) muuzaji anapima afya kila baada ya miezi sita; na (g) duka lake lina karo la maji machafu. (3) Mtu yeyote atakayekiuka masharti ya kifungu kidogo cha (1) na (2) atakuwa ametenda kosa. Uendeshaji wa biashara ya hoteli na hosteli - 10 Verify source ↗
(1) Kila mmiliki wa nyumba ya kulala wageni,
AI-assisted research summary: Before starting business, owners of guest houses, hostels, schools, health-service premises, or business houses must ensure the building has been inspected by a health officer and has a council permit.
10.-(1) Kila mmiliki wa nyumba ya kulala wageni, hosteli, shule, kituo cha kutolea huduma za afya au nyumba ya biashara kabla ya kuanza biashara atakuwa na wajibu wa kuhakikisha: (a) jengo lake limekaguliwa na Afisa Afya; na (b) amepata kibali cha Halmashauri cha kufanya shughuli husika. (2) Kibali cha kuendesha biashara ya nyumba ya kulala wageni, hosteli, shule, kituo cha kutolea huduma za afya au nyumba ya biashara kitatolewa baada ya Halmashauri yafuatayo yamezingatiwa: - kuwa mahitaji kujiridhisha (a) jengo lina mwanga na hewa ya kutosha; (b) jengo lina nafasi na vifaa vya kutosha; (c) uimara wa jengo; (d) jengo lina mfumo imara wa uondoshaji wa maji taka, miminika na taka ngumu; (e) usafi wa jumla wa jengo na vifaa vyake; (f) jengo lina vyoo na mabafu ya kutosha kwa jinsia zote; (g) jengo lina vifaa vya zima moto; (h) tanki la kuhifadhia maji safi; (i) vyoo na bafu vimesakafiwa kwa vigae au marumaru na kuta zake zimewekwa vigae kiasi cha futi sita kutoka usawa wa sakafu; (j) kwa nyumba za kulala wageni na hosteli, uwepo wa vyandarua. 5 Sheria Ndogo ya Afya Na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Tangazo la Serikali Na. 216 (Linaendelea.) Ukaguzi wa afya. Eneo la kutupa taka Vikundi vya wazoa taka Magari ya abiria kuwa na vyombo vya kuhifadhia takataka (3) Mtu yeyote atakayekiuka masharti ya kifungu cha (1) atakuwa ametenda kosa. (4) Bila kuathiri masharti ya kifungu cha (3), wakati wowote Halmashauri ikijiridhisha kuwa mmiliki hajakidhi masharti ya afya inaweza kuzuia utoaji wa huduma husika mpaka hapo mmiliki atakapokuwa amekidhi masharti ya kiafya yaliyotolewa na Halmashauri. - 11 Verify source ↗
Halmashauri itatoza ada ya ukaguzi wa afya
AI-assisted research summary: Halmashauri lazima itoeza ada ya ukaguzi wa afya kabla ya kutoa au kuhuisha leseni ya biashara.
11. Halmashauri itatoza ada ya ukaguzi wa afya kabla ya kutoa au kuhuisha leseni ya biashara. - 12 Verify source ↗
(1) Halmashauri itakuwa na wajibu wa
AI-assisted research summary: The council must set aside a waste disposal area, place special waste containers in its areas, and provide waste collection services for a fee. Anyone who dumps or leaves waste or dirt in unauthorized places commits an offence.
12.-(1) Halmashauri itakuwa na wajibu wa: - (a) kutenga eneo maalum kwa ajili ya kutupia taka; (b) kuweka vyombo maalum vya kutunzia taka katika maeneo ya Halmashauri; na (c) kutoa huduma ya uzoaji taka kwa malipo kutoka kwa wazalishaji wa taka hadi kwenye dampo. (2) Mtu yeyote atakayetupa taka au uchafu wowote au kuacha takataka au uchafu kwenye nyumba, uchochoro, kiwanja, mfereji wa maji ya mvua, barabara au mahali popote pasipotengwa kwa shughuli hiyo atakuwa ametenda kosa. - 13 Verify source ↗
Halmashauri itahamasisha uundaji wa vikundi
AI-assisted research summary: Halmashauri lazima ihamasishe uundaji na utambuzi wa vikundi vya jamii ili viweze kufanya udhibiti wa taka ngumu na usafi wa mazingira mitaani, baada ya mkataba na Halmashauri.
13. Halmashauri itahamasisha uundaji wa vikundi jamii na kuvitambua ili kuviwezesha kufanya shughuli za udhibiti wa taka ngumu pamoja na usafi wa mazingira katika mitaa baada ya kuingia mkataba na Halmashauri. - 14 Verify source ↗
(1) Kila mmiliki wa gari la abiria litakaloingia
AI-assisted research summary: Wamiliki wa magari ya abiria yanayoingia katika eneo la Halmashauri lazima wawe na chombo cha kuhifadhia taka na wahakikishe abiria wanakitumia.
14.-(1) Kila mmiliki wa gari la abiria litakaloingia katika eneo la Halmashauri atatakiwa kuwa na chombo cha kuhifadhi taka na kuhakikisha kwamba kila abiria anatupa taka kwenye chombo hicho. (2) Wamiliki wa magari ya abiria au madereva wao au makondakta watawajulisha abiria wao juu ya uwepo wa chombo cha kutupia taka katika magari yao ili abiria wasitupe taka kupitia madirishani. (3) Endapo abiria atatupa takataka nje ya chombo cha usafiri, mmiliki au dereva au kondakta atachukuliwa kuwa ametenda kosa na atawajibika kulipa faini ya kiasi 6 Sheria Ndogo ya Afya Na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Tangazo la Serikali Na. 216 (Linaendelea.) kisichozidi shilingi elfu hamsini chini ya utaratibu wa kufifilisha kosa au kushtakiwa mahakamani chini ya Sheria Ndogo hii Uhifadhi maji taka - 15 Verify source ↗
(1) Kila mmiliki wa nyumba, kiwanda au eneo la
AI-assisted research summary: Owners of houses, factories, or business premises must keep a wastewater storage pit/tank, empty it when full, and must not discharge wastewater onto roads, alleys, rivers, water sources, open areas, storm drains, or other unapproved places.
15.-(1) Kila mmiliki wa nyumba, kiwanda au eneo la biashara anatakiwa- (a) kuhakikisha kuwa analo karo la kuhifadhi maji taka; 7 Sheria Ndogo ya Afya Na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Tangazo la Serikali Na. 216 (Linaendelea.) (b) kunyonya maji taka pale karo linapojaa; na (c) kutotiririsha au kutoelekeza maji kutoka vyooni, bafuni, karoni au viwandani kwenda barabarani, uchochoroni, mtoni, kwenye vyanzo vya maji, maeneo ya wazi, kwenye mfereji wa maji ya mvua au sehemu yoyote isiyotengwa kuhifadhia maji taka. (2) Mtu yeyote atakayekiuka masharti ya kifungu kidogo cha (1) atakuwa ametenda kosa. - 16 Verify source ↗
Kila mmiliki wa jengo la makazi au la biashara
AI-assisted research summary: Mmiliki wa jengo la makazi au la biashara lazima ahakikishe jengo lina choo safi, imara na madhubuti, na kwamba kinatumika wakati wote.
16. Kila mmiliki wa jengo la makazi au la biashara atakuwa na wajibu wa kuhakikisha kwamba jengo lake lina choo safi, imara na madhubuti na kuhakikisha kuwa kinatumika wakati wote. - 17 Verify source ↗
Halmashauri inaweza kujenga vyoo vya umma
AI-assisted research summary: Halmashauri inaweza kujenga vyoo vya umma au kuwaruhusu watu binafsi, vikundi au taasisi kuvijenga kwa malipo katika maeneo ambako Halmashauri itaona kuna haja.
17. Halmashauri inaweza kujenga vyoo vya umma au kumruhusu mtu binafsi, vikundi vya watu au taasisi kujenga vyoo vya umma vitakavyotoa huduma kwa malipo katika maeneo ambayo Halmashauri itaona kuwa kuna haja ya kufanya hivyo. - 18 Verify source ↗
(1) Mtu, kikundi au taasisi yenye lengo la
AI-assisted research summary: Mtu, kikundi au taasisi inayokusanya watu kwa muda maalum kwenye eneo lisilo na choo cha kudumu lazima ijenge vyoo vya muda kwa idhini na usimamizi wa Halmashauri.
18.-(1) Mtu, kikundi au taasisi yenye lengo la kukutanisha watu kwa muda maalum katika eneo ambalo halina choo cha kudumu itatakiwa kujenga vyoo kwa matumizi ya wakati huo kwa idhini na usimamizi wa Halmashauri. (2) Mtu, kikundi au taasisi itakayokiuka masharti ya kifungu kidogo cha (1) itakuwa imetenda kosa. - 19 Verify source ↗
(1) Endapo katika ukaguzi wa afya itagundulika
AI-assisted research summary: If a health inspection finds a house has no toilet, a full toilet, or an unsafe toilet, the authorized officer must give the house owner a 30-day notice to fix it.
19.-(1) Endapo katika ukaguzi wa afya itagundulika kuwa nyumba yoyote haina choo au choo kilichopo kimejaa au hakifai kwa matumizi ya binadamu, Afisa Mwidhiniwa atatoa ilani ya siku thelathini kwa mmiliki wa nyumba akiainisha masharti ya kurekebisha hali hiyo. (2) Mmiliki wa nyumba atakayeshindwa kutekeleza masharti ya Ilani iliyotolewa chini ya kifungu kidogo cha (1) atakuwa ametenda kosa. (3) Bila kuathiri masharti ya kifungu kidogo cha (1), 8 Wajibu wa kuwa na choo na kukitumia Vyoo vya umma Vyoo vya muda katika mkusanyiko Ilani ya kujenga choo Sheria Ndogo ya Afya Na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Tangazo la Serikali Na. 216 (Linaendelea.) Ilani ya kuondoa kero Upimaji wa afya Halmashauri inaweza kuamuru nyumba au jengo hilo lisitumike kwa shughuli za makazi au biashara hadi hapo hali hiyo itakaporekebishwa. - 20 Verify source ↗
(1) Endapo Afisa Mwidhiniwa atabaini kuwa
AI-assisted research summary: Afisa Mwidhiniwa akibaini kero kwenye eneo alilokagua, atatoa ilani ya siku saba kwa mhusika kuiondoa. Halmashauri inaweza kuamuru nyumba au jengo lisitumike kwa makazi au biashara hadi hali irejeshwe. Asiyetii masharti ya ilani ndani ya muda huenda ametenda kosa.
20.-(1) Endapo Afisa Mwidhiniwa atabaini kuwa eneo alilokagua lina kero yoyote atatoa ilani ya siku saba kwa mmiliki wa nyumba, mpangaji, mtumiaji au mtu yeyote anayehusika akimtaka kuondoa kero hiyo. (2) Halmashauri inaweza kuamuru nyumba au jengo hilo lisitumike kwa makazi au biashara hadi hapo hali itakapokuwa imerekebishwa. (3) Mtu yeyote atakayeshindwa kutekeleza masharti ya Ilani aliyopewa ndani ya muda ulioainishwa kwenye Ilani atakuwa ametenda kosa. - 21 Verify source ↗
(1) Kila mmiliki wa sehemu inayotoa huduma ya
AI-assisted research summary: Owners of listed food- and hospitality-related businesses must make sure their workers have a health check every six months.
21.-(1) Kila mmiliki wa sehemu inayotoa huduma ya hoteli, mgahawa, baa, bucha, sehemu za kuokea mikate, nyumba za kulala wageni, grosari au mtu yeyote anayetengeneza chakula kwa ajili kuuza atatakiwa kuhakikisha kuwa wahudumu wake wanapima afya kila baada ya miezi sita. 9 Sheria Ndogo ya Afya Na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Tangazo la Serikali Na. 216 (Linaendelea.) Uteuzi wa wakala Adhabu Kufifilisha kosa (2) Mmiliki yeyote atakayekiuka masharti ya kifungu kidogo cha (1) atakuwa ametenda kosa. - 22 Verify source ↗
Mkurugenzi anaweza kuteua kampuni,kikundi au
AI-assisted research summary: Mkurugenzi anaweza kuteua kampuni, kikundi, au mtu binafsi ili kutekeleza majukumu yake chini ya Sheria Ndogo hii.
22. Mkurugenzi anaweza kuteua kampuni,kikundi au mtu binafsi kutekeleza majukumu yake chini ya Sheria Ndogo hii. - 23 Verify source ↗
Mtu yeyote atakayetiwa hatiani kwa kosa lolote
AI-assisted research summary: If a person is convicted of any offence under this bylaw, they must pay a fine, go to prison, or both.
23. Mtu yeyote atakayetiwa hatiani kwa kosa lolote chini ya Sheria Ndogo hii atawajibika kulipa faini isiyozidi shilingi laki tatu au kifungo kisichozidi miezi kumi na mbili au vyote viwili kwa pamoja. - 24 Verify source ↗
Mkurugenzi anaweza kumtoza mtu yeyote
AI-assisted research summary: Mkurugenzi anaweza kumtoza mtu aliyefanya kosa chini ya Sheria Ndogo hii shilingi 200,000 ikiwa mkosaji anakiri kosa kwa hiari na kukubali kujaza fomu maalum.
24. Mkurugenzi anaweza kumtoza mtu yeyote aliyetenda kosa chini ya Sheria Ndogo hii kiasi cha shilingi laki mbili iwapo mkosaji atakiri kosa kwa hiyari na kuwa tayari kujaza fomu maalum iliyoambatishwa katika Jedwali la Sheria Ndogo hii. 10 Sheria Ndogo ya Afya Na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Tangazo la Serikali Na. 216 (Linaendelea.) ______ JEDWALI ________ (Limetengenezwa chini ya kifungu cha 24) ________ HATI YA KUFIFILISHA KOSA Mimi……………………………………………….………. nakiri kwa hiari yangu mwenyewe mbele ya …………………………ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi/Afisa mwidhiniwa kwa niaba ya Mkurugenzi, kwamba Tarehe ………Mwezi………. Mwaka………. nilikutwa na kosa la kukiuka masharti ya Sheria Ndogo ya Afya na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi ya Mwaka 2022, nipo tayari kulipa kiasi cha shilingi………………….na kutimiza wajibu wangu chini ya Sheria Ndogo hiyo badala ya kushtakiwa Mahakamani. Nathibitisha kwamba maelezo hapo juu ni kweli na nimeyatoa kwa hiari yangu kadri ya ufahamu wangu Leo Tarehe………………………………. ya Mwezi…………………. Mwaka………………… Jina…………………………………………Saini……………………………………… Mbele ya: Jina………………………………………... Cheo……………………………………. Saini……………………………………… Tarehe…………………………………… 11 Sheria Ndogo ya Afya Na Usafi wa Mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Tangazo la Serikali Na. 216 (Linaendelea.) Nembo na muhuri wa Halmashauri ya Wilaya ya IKUNGI umebandikwa kwenye Sheria Ndogo hizi kwa Azimio lililopitishwa na mkutano wa Baraza la madiwani ulioitishwa Tarehe 22/1/2021 na ubandikwaji huo kushuhudiwa na:- JUSTICE L. KIJAZI, Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya , Wilaya ya Ikungi ALLY J. MWANGA, Mwenyekiti Halmashauri ya Wilaya ya IKUNGI L.S NAKUBALI, Dodoma, 9 Machi, 2022 UMMY A MWALIMU Waziri wa Nchi-OR-TAMISEMI 12
Provision text is displayed from LexChat’s stored statute record. Use the official source links to verify amendments, commencement, and current legal force.
Ask AI about this statute
SHERIA NDOGO YA AFYA NA USAFI WA MAZINGIRA YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IKUNGI YA MWAKA 2022
Sign in to ask AI about this statute
Sign in to start authenticated, citation-grounded statute research.
Sign in