KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MANISPAA YA SONGEA ZA MWAKA, 2016
Section heading for definitions used in Part II on council meetings.
AI-assisted research synopsis — verify against the official legal text below.
- Jurisdiction
- Tanzania
- Instrument
- Regulation
- Citation
- KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MANISPAA YA SONGEA ZA MWAKA, 2016
- Version
- Undated source snapshot
- Language
- sw
- Official source
- View official record ↗
Statute overview
About this statute
Section heading for definitions used in Part II on council meetings. Sehemu hii ina kichwa cha “Mkutano wa Bajeti” wa Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea. This provision is a section heading about conduct in council meetings. This section is about the election of the Mayor and Deputy Mayor of a council. Section title: Governance of council meetings.
Search within this statute
Search all stored provisions in this version.
Legal text
Provisions of KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MANISPAA YA SONGEA ZA MWAKA, 2016
Showing 140 of 140
- 2 Verify source ↗
Tafsiri ya misamiati iliyotumika
AI-assisted research summary: Section heading for definitions used in Part II on council meetings.
2. Tafsiri ya misamiati iliyotumika SEHEMU YA II MIKUTANO YA HALMASHAURI
Part
SEHEMU YA II
- 6 Verify source ↗
Mkutano wa Bajeti
AI-assisted research summary: Sehemu hii ina kichwa cha “Mkutano wa Bajeti” wa Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea.
6. Mkutano wa Bajeti 1 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) - 9 Verify source ↗
Akidi katika mikutano ya Halmashauri
AI-assisted research summary: This provision is a section heading about conduct in council meetings.
9. Akidi katika mikutano ya Halmashauri. SEHEMU YA III TARATIBU ZA MIKUTANO - 3 Verify source ↗
(1) Mikutano ya Kawaida ya Halmashauri itafanyika mara moja
AI-assisted research summary: The council must hold ordinary meetings every three months, and the first ordinary meeting must be convened after election results are announced.
3.-(1) Mikutano ya Kawaida ya Halmashauri itafanyika mara moja kila baada ya miezi mitatu, na itafanyika mahali, tarehe na katika muda kama utakavyokua umepangwa katika kalenda ya Mikutano ya Halmashauri. (2) (a) Mkutano wa kwanza wa kawaida wa Halmashauri utafanyika baada ya Tume ya Uchaguzi kutangaza matokeo ya uchaguzi wa Madiwani wa Kata na uteuzi wa Madiwani wa Viti maalumu, na utafanyika mahali, siku na katika muda utakaopangwa na Mkurugenzi, ilimradi Mkurugenzi atapaswa kuitisha Mkutano huo ndani ya siku thelathini kuanzia tarehe ya matokeo ya uchaguzi wa Madiwani wa Kata na Uteuzi wa Madiwani Viti Maalum yanapotangazwa na Tume ya Uchaguzi ambapo moja ya ajenda za Mkutano huo ni kumchagua Meya/Mwenyekiti, Naibu Meya/Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamati za Kudumu za Halmashauri. (b) Katika Mkutano huo Mkurugenzi wa Halmashauri atawasilisha Taarifa ya kumbukumbu ya maamuzi ya utekelezaji wa shughuli za Halmashauri zilizofanyika katika kipindi ambacho Baraza la madiwani lilivunjwa. Wajumbe wa baraza watapokea na kujadili bila kubatilisha maamuzi yaliyokwisha amuliwa. Mikutano ya Kawaida ya Halma- shauri Mkutano wa Kwanza wa Halma- shauri. Utaratibu wa uchaguzi - 4 Verify source ↗
Uchaguzi wa Meya na Naibu Meya utafanyika kwa kupiga
AI-assisted research summary: Uchaguzi wa Meya na Naibu Meya utafanywa kwa kura za siri, na mpiga kura atachukua karatasi ya kupiga kura kutoka kwa Msimamizi wa Uchaguzi.
4. Uchaguzi wa Meya na Naibu Meya utafanyika kwa kupiga Kura za siri na upigaji wa kura utafanyikia sehemu ya faragha umbali usiopungua mita (5) kutoka kwa Msimamizi wa Uchaguzi na mpiga kura atachukua karatasi ya kupiga kura kutoka kwa Msimamizi wa Uchaguzi. 7 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) Mkutano maalum wa Halma- shauri - 5 Verify source ↗
(1) Mkutano Maalum wa Halmashauri unaweza kuitishwa na
AI-assisted research summary: This section sets the procedure and deadlines for calling a special council meeting, including cases involving removal of the mayor or chairperson.
5.-(1) Mkutano Maalum wa Halmashauri unaweza kuitishwa na Meya ndani ya siku ishirini na moja baada ya kupokea maombi ya maandishi yaliyosainiwa na si pungufu ya theluthi moja ya Wajumbe wote kutaka Mkutano huo ufanyike na maombi hayo yaeleze wazi madhumuni ya kuitishwa kwa Mkutano Maalum huo. (2) Endapo ajenda ya Mkutano huo itahusu kumuondoa madarakani Mwenyekiti, Mkutano huo utaitishwa na Mkurugenzi baada ya kupokea maombi yaliyosainiwa na Wajumbe wa Halmashauri wasiopungua theluthi mbili ya Wajumbe wote. (3) Baada ya Mkurugenzi kupokea maombi kutaka kufanyika kwa Mkutano wa kujadili ajenda ya kumuondoa madarakani Meya, tuhuma na sababu za kutaka Mkurugenzi atamtaarifu Meya kuondolewa Umeya na kumtaka aandae majibu ya tuhuma ndani ya siku tano (5) baada ya kupokea tuhuma hizo. (4) Mkurugenzi katika muda wa siku Tatu (3) baada ya kupokea maelezo ya utetezi kutoka kwa Meya, atawasilisha kwa Mkuu wa Mkoa tuhuma pamoja na maelezo ya utetezi. (5) Mkuu wa Mkoa baada ya kupokea taarifa ya Mkurugenzi ndani ya muda wa siku tano (5) ataunda Timu ya Uchunguzi ambayo itakuwa na wajumbe wasiopungua watatu (3) na wasiozidi watano (5). (6) Timu ya Uchunguzi itatakiwa kukamilisha Uchunguzi katika muda wa siku kumi na nne (14) na kuwasilisha taarifa hiyo kwa Mkuu wa Mkoa. (7) Baada ya Mkuu wa Mkoa kupata taarifa ya Timu ya Uchunguzi atairudisha Taarifa hiyo kwa Mkurugenzi ambaye naye katika muda wa siku kumi na Nne (14) ataiwasilisha kwenye Kikao cha Baraza kwa uamuzi wa tuhuma hizo. Kif.cha 25(5) Sura 288 Utaratibu wa kuwasilish a rufaa (8) Endapo Meya hataridhika na uamuzi wa Baraza, atakata rufaa kwa Waziri kuhusu tu utaratibu uliotumika kumuondoa madarakani na sio vinginevyo. (9) Utaratibu utakaotumika kuwasilisha na kushughulikia rufaa iliyowasilishwa na Meya ni ule ulioelezwa kwenye Taratibu za Kumuondoa Madarakani Meya wa Halmashauri. (10) Iwapo Meya anakataa kuitisha Mkutano maalum wa Halmashauri baada ya kupokea maombi ya kutakiwa kufanya hivyo, 8 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) maombi yaliyosainiwa na Wajumbe wa Halmashauri wasiopungua theluthi moja ya Wajumbe wote wakionyesha sababu ya kuitisha Mkutano huo maalum na kuwasilishwa kwake, au iwapo bila kukataa, Meya, ndani ya kipindi cha siku saba ataendelea kutoitisha Mkutano huo maalum baada ya kupokea ombi la kuitisha Mkutano huo maalum, basi theluthi mbili ya Wajumbe waliotia saini na kuwasilisha kwa Mkurugenzi wanaweza kuitisha Mkutano huo maalum mara moja. (11) Taarifa ya Mkutano maalum itatolewa angalau saa ishirini na nne kabla ya Mkutano. (12) Hakuna shughuli nyingine yoyote itakayojadiliwa katika Mkutano maalum wa Halmashauri isipokuwa ile tu iliyoelezwa kwenye taarifa ya kuitishwa kwa Mkutano huo. Mkutano wa Bajeti - 6 Verify source ↗
Kutakuwepo na Mkutano wa Halmashauri wa Bajeti
AI-assisted research summary: Mkutano wa Halmashauri wa Bajeti ufanyike kwa siku mbili mfululizo, miezi miwili kabla ya mwaka wa fedha kumalizika, na ujadili utekelezaji wa bajeti ya mwaka uliopita pamoja na mipango na bajeti ya mwaka unaofuata.
6. Kutakuwepo na Mkutano wa Halmashauri wa Bajeti utakaofanyika kwa muda wa siku mbili mfululizo na utafanyika miezi miwili kabla ya mwaka wa fedha kumalizika na utajadili mambo yafuatayo:- (a) Utekelezaji wa Mipango na Bajeti ya mwaka uliopita. (b) Mipango na Bajeti ya mwaka unaofuata. Mkutano wa Mwaka - 7 Verify source ↗
(1) (i) Mkutano wa Mwaka wa Halmashauri utafanyika tarehe,
AI-assisted research summary: Halmashauri na maafisa wake lazima wapange na kuendesha mikutano ya mwaka na mikutano mingine kwa kufuata ratiba ya Bunge inapohusika.
7.-(1) (i) Mkutano wa Mwaka wa Halmashauri utafanyika tarehe, mahali na muda utakaopangwa na Halmashauri katika kalenda ya Mikutano na utaitishwa na Mkurugenzi baada ya kuwasiliana na Meya wa Halmashauri. (ii) Mikutano yote ya Baraza itapangwa na Baraza la Madiwani kwa kuzingatia ratiba ya Vikao vya Bunge ili kuwezesha Wabunge kuhudhuria Mikutano ya Baraza la Madiwani. Endapo italazimika kuitishwa kwa Mkutano wa Baraza wakati wa Vikao vya Bunge, Mkurugenzi atamjulisha au kuwajulisha Wabunge husika kuhusu kikao hicho ili wahudhurie. (2) Mkutano wa Kwanza wa Uchaguzi wa Meya, Naibu Meya na Wajumbe wa Kamati utaongozwa na Katibu Tawala wa Wilaya na Mkurugenzi wa Halmashauri atakuwa Katibu. (3) Katika Mkutano wa kawaida wa mwaka, Halmashauri itajadili mambo yafuatayo:- (a) Kumchagua Naibu Meya, (b) Kuteua Wajumbe wa Kamati za Kudumu; (c) Kujadili taarifa ya utendaji na uwajibikaji wa Halmashauri kwa mwaka uliopita. 9 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (d) Kupitisha ratiba ya vikao vya Halmashauri na Kamati za Halmashauri. Taarifa za Mkutano - 8 Verify source ↗
(1) Mkurugenzi atatoa taarifa ya Mkutano kwa maandishi
AI-assisted research summary: Mkurugenzi lazima atume taarifa ya Mkutano kwa maandishi kwa kila Mjumbe angalau siku 7 kabla, na aeleze mahali, siku, saa na mada za mkutano.
8.-(1) Mkurugenzi atatoa taarifa ya Mkutano kwa maandishi kwa kila Mjumbe katika muda usiopungua siku saba akieleza mahali, siku na saa ya Mkutano unaokusudiwa na mambo yatakayojadiliwa katika Mkutano huo. (2) Taarifa ya Mkutano itaambatana na nyaraka au kumbukumbu muhimu zitakazotumika katika Mkutano huo. (3) Isipokuwa kwa idhini ya Meya na au ya idadi ya Wajumbe isiyopungua robo tatu ya Wajumbe waliohudhuria Mkutano, hakuna shughuli yoyote itakayofanywa katika Mkutano wa Halmashauri mbali na shughuli zilizotajwa katika mwaliko wa Mkutano huo. Akidi katika Mikutano ya Halma- shauri - 9 Verify source ↗
(1) Hakuna Mkutano wa kawaida wa Halmashauri utakaofanyika
AI-assisted research summary: Mikutano ya kawaida ya Halmashauri haziwezi kufanyika bila akidi; Mkurugenzi lazima aahirishe na kuitisha tena mkutano usiofikia akidi ndani ya siku 7, na amtaarifu Waziri ikiwa akidi bado haijapatikana.
9.-(1) Hakuna Mkutano wa kawaida wa Halmashauri utakaofanyika isipokuwa kama kutakuwepo idadi ya Wajumbe isiyopungua nusu ya Wajumbe wote waliohudhuria na kujiandikisha kwenye daftari la mahudhurio. (2) Akidi katika Mikutano maalum ya Halmashauri itakuwa ni theluthi mbili ya Wajumbe wote wa Halmashauri na itahesabiwa wakati wa ufunguzi wa Mkutano. (3) Akidi katika Mkutano wa kawaida wa mwaka na Mkutano wa kwanza wa Halmashauri itakuwa theluthi mbili ya Wajumbe wote wa Halmashauri. (4) Endapo Wajumbe waliohudhuria Mkutano hawatafikia akidi ya Mkutano, Mkurugenzi atauahirisha Mkutano huo na kuitisha tena ndani ya siku saba (7) na endapo akidi haitatimia tena, idadi yoyote ya Wajumbe waliohudhuria itatengeneza akidi ya Mkutano na Mkurugenzi atamjulisha Waziri kuwepo kwa hali hiyo. (3) Akidi katika Mikutano maalum ya Halmashauri itakuwa ni theluthi mbili ya Wajumbe wote waHalmashauri na itahesabiwa wakati wa ufunguzi wa Mkutano. (4) Akidi katika Mkutano wa kawaida wa mwaka na Mkutano wa kwanza wa Halmashauri itakuwa theluthi mbili ya Wajumbe wote wa Halmashauri. 10 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) Uchaguzi wa Meya/Mw enyekiti na Naibu Meya/Mak amu Mwenyeiti wa Halma- shauri SEHEMU YA III TARATIBU ZA MIKUTANO
Part
SEHEMU YA III
- 10 Verify source ↗
Uchaguzi wa Meya/ Naibu Meya wa Halmashauri
AI-assisted research summary: This section is about the election of the Mayor and Deputy Mayor of a council.
10. Uchaguzi wa Meya/ Naibu Meya wa Halmashauri - 11 Verify source ↗
Uongozaji wa Mikutano ya Halmashauri
AI-assisted research summary: Section title: Governance of council meetings.
11. Uongozaji wa Mikutano ya Halmashauri - 13 Verify source ↗
Kuruhusu watu na Vyombo vya Habari kwenye Mikutano ya
AI-assisted research summary: Kichwa cha kifungu kinahusu kuruhusu watu na vyombo vya habari kwenye mikutano ya halmashauri.
13. Kuruhusu watu na Vyombo vya Habari kwenye Mikutano ya Halmashauri - 21 Verify source ↗
Hoja zinazoweza kutolewa bila taarifa
AI-assisted research summary: This section is titled “Forms that may be issued without notice.”
21. Hoja zinazoweza kutolewa bila taarifa. - 27 Verify source ↗
Uhuru wa Kutoa mawazo wakati wa majadiliano
AI-assisted research summary: Kichwa cha kifungu kinahusu uhuru wa kutoa mawazo wakati wa majadiliano.
27. Uhuru wa Kutoa mawazo wakati wa majadiliano - 30 Verify source ↗
Mwaliko kwa wasiokuwa Wajumbe kushiriki na kuzungumza
AI-assisted research summary: Section 30 concerns inviting non-members to participate and speak at council meetings.
30. Mwaliko kwa wasiokuwa Wajumbe kushiriki na kuzungumza kwenye vikao vya Halmashauri - 31 Verify source ↗
Mihtasari ya Kata na ya Vijiji/Mitaa
AI-assisted research summary: Section 31 is titled “Mihtasari ya Kata na ya Vijiji/Mitaa” (ward and village/street summaries).
31. Mihtasari ya Kata na ya Vijiji/Mitaa - 32 Verify source ↗
Mihutasari kupelekwa kwa Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa
AI-assisted research summary: This section says Mihutasari is to be taken to the District Commissioner and the Regional Commissioner.
32. Mihutasari kupelekwa kwa Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa - 36 Verify source ↗
Uhalali wa majadiliano ya Halmashauri
AI-assisted research summary: Section about the legality of council deliberations.
36. Uhalali wa majadiliano ya Halmashauri - 37 Verify source ↗
Uwezo wa Halmashauri kujigeuza kuwa Kamati ya Halmashauri nzima
AI-assisted research summary: Section heading about the council’s power to turn itself into the full council committee.
37. Uwezo wa Halmashauri kujigeuza kuwa Kamati ya Halmashauri nzima. - 38 Verify source ↗
Hoja zinazohusu watumishi wa Halmashauri
AI-assisted research summary: Section heading about matters concerning municipal employees.
38. Hoja zinazohusu watumishi wa Halmashauri - 40 Verify source ↗
Uahirishaji wa Vikao
AI-assisted research summary: Section title only: “Uahirishaji wa Vikao” (postponement of meetings).
40. Uahirishaji wa Vikao 2 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) SEHEMU YA IV KAMATI - 10 Verify source ↗
(1) Meya na Naibu Meya watachaguliwa na Wajumbe,
AI-assisted research summary: Wajumbe humchagua Meya na Naibu Meya kwa kura ya siri, na Halmashauri lazima ichague ndani ya siku 60 kama nafasi itaachwa wazi.
10.-(1) Meya na Naibu Meya watachaguliwa na Wajumbe, kutokana na Wajumbe wa Halmashauri kwa kura ya siri itakayopigwa na Mjumbe mmoja mmoja kwenye eneo la faragha litakalotengwa umbali usiopungua mita 5 kutoka mahali alipoketi Msimamizi wa Uchaguzi. (2) Mjumbe kabla ya kwenda sehemu ya faragha kwa ajili ya kupiga kura, atapatiwa na Msimamizi wa Uchaguzi karatasi ya kupigia kura kutoka kwenye chombo maalum kitakachowekwa mbele ya Msimamizi wa Uchaguzi, na atakwenda moja kwa moja kupiga kura yake kwenye sehemu ya faragha. (3) Mtu atatangazwa kuchaguliwa kuwa Meya au Naibu Meya iwapo atapata ingu ya nusu ya kura zilizopigwa. (4) Iwapo wakati wa kumchagua Meya au Naibu Meya, jina moja tu limependekezwa, Wajumbe watapiga kura za siri za “ndiyo” au “hapana”na endapo kura za “ndiyo” zitazidi asilimia hamsini ya kura zote zilizopigwa basi mgombea atatangazwa kuwa Meya au Naibu Meya. (5) Iwapo kura za “Hapana” zitazidi asilimia hamsini ya kura zote zilizopigwa, jina la mgombea mwingine litapendekezwa kwa njia na utaratibu uliotumika hapo awali. (6) Iwapo kura zitafanana, uchaguzi utarudiwa kwa mara ya pili na endapo hata baada ya kurudia uchaguzi kura zimefanana, Baraza litaamua kugawana muda wa kuwa madarakani kwa wagombea hao ambao kura zao zimefanana. (7) Kama itatokea nafasi wazi ya Meya au Naibu Meya, Halmashauri itamchagua Meya au Naibu Meya katika muda wa siku zisizozidi sitini tangu nafasi hiyo ilipotokea. Uongozaji wa Mikutano ya Halma- shauri - 11 Verify source ↗
(1) Mkutano wa Halmashauri utaongozwa na
AI-assisted research summary: This section sets who chairs council meetings, requires councillors to wear approved attire in meetings, bars certain clothing at meetings, and requires the council to set aside two days each week for the mayor’s office duties.
11.-(1) Mkutano wa Halmashauri utaongozwa na:- (a) Meya; au (b) Kama Meya hayupo, Naibu Meya; au (c) Kama Meya na Naibu Meya wote hawapo, au kama Meya na Naibu Meya wote hawawezi kuongoza Mkutano, Mjumbe yeyote atachaguliwa na Wajumbe kutoka miongoni 11 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) mwa Wajumbe waliohudhuria kwa ajili ya kuongoza Mkutano huo, (d) Wajumbe wawapo ndani ya ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri watavaa mavazi maalum yaliyochaguliwa na kushonwa maalum kwa ajili hiyo, (e) Endapo vazi maalum lililochaguliwa na Halmashauri ni joho basi litavaliwa juu ya vazi la Mjumbe, na Endapo Halmashauri haina joho basi Mjumbe atavaa vazi la heshima, na mavazi kama jeans, kofia zinazohusiana na dini na sare za Chama hazitaruhusiwa kuvaliwa wakati wa Mikutano ya Halmashauri na vikao vya Kamati za Kudumu za Halmashauri, (f) Vazi rasmi la Meya, Mkurugenzi na Naibu Meya litakuwa lenye kuonyesha rangi za Bendera ya Taifa na mazao yanayolimwa kwa wingi katika eneo la Halmashauri kadri Halmashauri itakavyoona inafaa. Hata hivyo, Kanuni hii haitaathiri majoho ambayo yanatumika kabla ya Kanuni hii, (g) Endapo katika Mkutano huo Halmashauri itajigeuza kuwa Kamati, Wajumbe watavua majoho. (h) Endapo Baraza taratibu za kuendesha Vikao vya Kamati zitatumika na kikao hicho kitakua cha siri. litajigeuza kuwa Kamati (2) Madaraka au jukumu lolote la Meya kuhusiana na uendeshaji wa Mikutano yanaweza kutekelezwa na mtu anayeongoza Mkutano huo. (3) Halmashauri itatenga siku mbili kila wiki kwa ajili ya Meya kufika ofisini na kutekeleza majukumu yafuatayo; (a) Kusikiliza matatizo ya Wananchi; (b) Kupata maelezo toka kwa Mkurugenzi kuhusu uendeshaji wa shughuli za Halmashauri ikiwa ni pamoja na masuala ya manunuzi; (c) Kusaini mikataba mbalimbali ya Halmashauri; (d) Kushughulikia jambo ambalo Mkurugenzi ataona linahitaji kushughulikiwa au kutekelezwa na Meya. Kumbu- kumbu ya mahudhurio - 12 Verify source ↗
(1) Kila Mjumbe anayehudhuria Mkutano wa Halmashauri
AI-assisted research summary: Members attending council or committee meetings must sign the attendance register before they may attend. The register is kept by the Director for that purpose.
12.-(1) Kila Mjumbe anayehudhuria Mkutano wa Halmashauri au Kamati yoyote ya Halmashauri ambamo yeye ni Mjumbe hatahudhuria Mkutano huo mpaka awe ameweka saini yake kwenye Rejesta ya mahudhurio inayotunzwa na Mkurugenzi kwa ajili hiyo. (2) Isipokuwa siku ya kufanyika kwa Mikutano ya Baraza au Kamati ambayo Diwani ni Mjumbe au pale atakapoitwa kutekeleza 12 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) majukumu ya Serikali, si ruhusa kwa Diwani kuwa katika Ofisi za shughuli ambazo hazihusiani na Halmashauri na kufanya Halmashauri au Serikali. Kuruhusu watu na vyombo vya habari kwenye Mikutano ya Halma- shauri - 13 Verify source ↗
(1) Mikutano ya Halmashauri itakuwa wazi kwa watu wote
AI-assisted research summary: Council meetings are open to the public and the media.
13.-(1) Mikutano ya Halmashauri itakuwa wazi kwa watu wote pamoja na vyombo vya habari. (2) Halmashauri itapaswa kuutangazia Umma kuhusu muda, wakati na mahali pa Mkutano na italiweka tangazo hilo mahali panapoonekana kwa urahisi katika eneo la Halmashauri siku zisizopungua tatu kabla ya Mkutano, na kama Mkutano umeitishwa katika muda mfupi ingu basi wakati wa kuitisha Mkutano huo. Utaratibu wa shughuli za Mikutano - 14 Verify source ↗
(1) Isipokuwa kama Halmashauri, kutokana na sababu za
AI-assisted research summary: This section sets the order of business for regular council meetings and lets the council change that order in emergencies, except for certain items that must keep their position.
14.-(1) Isipokuwa kama Halmashauri, kutokana na sababu za dharura, itaamua kubadili utaratibu wa shughuli za Mikutano, utaratibu wa shughuli katika kila Mkutano wa kawaida wa Halmashauri utakuwa kama ifuatavyo:- (a) Meya akiongozwa na Katibu ataingia ukumbini baada ya Mratibu wa vikao kutoa ishara maalum kuashiria Meya kuingia ukumbini na Wajumbe watasimama na kukaa kimya mpaka pale Meya atakaporuhusu Wajumbe kukaa (b) Mkutano utaanza kwa Sala au Dua itakayosomwa na Meya, (c) Endapo Meya au Naibu Meya hawatakuwepo, Wajumbe watachagua mtu wa kuongoza kikao, (d) Baada ya Sala/Dua kusomwa Mkurugenzi na Meya/ watajibu maswali ya papo kwa papo kutoka kwa Wajumbe wa Baraza la madiwani kwa utaratibu na mpangilio kama ilivyooneshwa kwenye Kanuni hizi, (e) Kupokea na kujadili taarifa za kwenye Kata kutoka kwa Madiwani wa Kata husika, (f) Kujadili jambo lolote linalotakiwa kwa mujibu wa Sheria kushughulikiwa kabla ya shughuli nyingine yoyote, (g) Kupokea taarifa yoyote inayopaswa kupokelewa kisheria kabla ya shughuli nyingine yoyote, (h) Kusoma au kuthibitisha muhtasari wa Mkutano wa kawaida wa Halmashauri uliopita na Mikutano yoyote maalum ya Halmashauri iliyofanyika baada ya Mkutano huo wa kawaida. Hata hivyo iwapo nakala za mihtasari zimesambazwa kwa kila Mjumbe kabla au wakati wa kupeleka taarifa ya kuhudhuria Mkutano, mihtasari hiyo itachukuliwa kuwa imesomwa, (i) kupokea taarifa yoyote ambayo Meya atapenda itolewe kwa Halmashauri, 13 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (j) Kujibu maswali kufuatana na Kanuni ya 23 ya Kanuni hizi, (k) Kumalizia shughuli yoyote iliyobaki katika Mkutano wa kawaida uliopita, (l) Kupokea na kufikiria taarifa za Kamati za Halmashauri, kutoka kwa Wenyeviti wa Kamati ambao watahusika kujibu maswali ya Wajumbe kuhusiana na kazi za Kamati husika, (m) Kupokea na kujadili taarifa kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri, (n) Kuidhinisha utiaji lakiri katika hati, (o) Kufikiria hoja binafsi kufuatana na jinsi zilivyopokelewa, na, (p) Kushughulikia mambo mengine yaliyoonyeshwa katika taarifa ya Mkutano. (2) Halmashauri inaweza, katika Mkutano wowote wa kawaida, kubadili utaratibu wa hoja za mazungumzo ili kutoa kipaumbele kwa shughuli yoyote ambayo kwa maoni ya Meya na uharaka wa pekee, lakini mabadiliko hayo hayatabadilisha mpangilio wa shughuli zilizotajwa katika aya (c), (f) na (g) za Kanuni ya 14(1) ya Kanuni hii. Kuthibitisha muhtasari - 15 Verify source ↗
(1) Katibu ataandika muhtasari wa mazungumzo ya kikao
AI-assisted research summary: Katibu must prepare minutes of the meeting; the chair must read, correct, confirm, and sign them; and the minutes must be available for inspection, with copies or parts available on request and subject to a fee approved by the Council.
15.-(1) Katibu ataandika muhtasari wa mazungumzo ya kikao unaozingatia majina ya Wajumbe waliohudhuria na wasiohudhuria, jina la mtoa hoja, aliyeunga mkono hoja, mabadiliko ya hoja kwa ufupi, ushauri uliotolewa na azimio lililofikiwa. Muhtasari huo utasomwa, kurekebishwa, kuthibitishwa na kusainiwa na Mwenyekiti wa Mkutano na kutunzwa katika rejesta maalum ya mihtasari. (2) Mara baada ya kusoma Muhtasari, au kama itachukuliwa kama umesomwa Mwenyekiti atauliza swali “Je Muhtasari wa Mkutano wa Halmashauri wa ya mwezi…………. Mwaka……..utiwe saini kama kumbukumbu sahihi?.” tarehe…………… (3) Hakuna hoja au majadiliano yatakayofanywa kuhusiana na muhtasari isipokuwa kuhusiana na usahihi wa muhtasari, kama hakuna swali lililoulizwa, basi mara baada ya kuthibitishwa Meya atatia saini katika muhtasari huo. (4) Muhtasari ambao utakuwa umesainiwa vilivyo na kama hakuna ushahidi wa kuwepo kwa makosa utakuwa kumbukumbu sahihi na Mkutano utahesabika kuwa umeitishwa na kufanyika 14 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) vilivyo na Wajumbe waliohudhuria watahesabika halali. (5) Mihtasari ya Halmashauri itakuwa wazi kwa ukaguzi na Wajumbe na kwa umma kwa wakati unaofaa na kwa utaratibu utakaokubaliwa na Halmashauri na kwamba mtu yeyote anaweza kupewa sehemu ya muhtasari huo kama akiomba na baada ya kulipa ada kama itakavyoidhinishwa na Halmashauri. Hoja za Meya/Mw enyekiti - 16 Verify source ↗
Hoja zinazowasilishwa na Meya hazitazidi hoja tatu, bila
AI-assisted research summary: Meya anaweza kuwasilisha hoja, lakini hoja zake hazipaswi kuzidi tatu.
16. Hoja zinazowasilishwa na Meya hazitazidi hoja tatu, bila kuathiri haki yake, kama Mjumbe ya kuwasilisha hoja katika taratibu za kawaida. Taratibu za majadiliano - 17 Verify source ↗
(1) Isipokuwa kwa idhini ya Halmashauri mtoa hoja
AI-assisted research summary: Kanuni hii inaweka muda na utaratibu wa kuzungumza katika Mkutano wa Halmashauri, pamoja na mamlaka ya Meya kusimamia nidhamu na utaratibu.
17.-(1) Isipokuwa kwa idhini ya Halmashauri mtoa hoja atahutubia Mkutano wa Halmashauri kwa dakika zisizozidi kumi. Wajumbe wengine ikiwa ni pamoja na mtoa hoja watazungumza kwa muda usiozidi dakika tano kila mmoja; (2) Mjumbe anaruhusiwa kuzungumza mara moja katika hoja yoyote ile isipokuwa hoja inayowasilishwa bila mjadala; (3) Mtoa hoja atakuwa na haki ya kuzungumza kwa muda usiozidi dakika tano katika kujibu majadiliano na muda huo utaanza kuhesabika mara atakapoanza kuchangia au kujibu. Mratibu wa vikao atatoa ishara maalum kumjulisha mtoa hoja kuwa muda wake umeisha na mjadala juu ya hoja hiyo utafungwa. Utaratibu huu wa kuhesabu muda utatumika pia kwa Mjumbe yeyote atakayepewa muda wa kuchangia hojana mara tu baada ya kujibu, mjadala juu ya hoja utafungwa; (4) Mjumbe yeyote aliyekwishachangia kwenye hoja hawezi kutoa au kuunga mkono marekebisho, ila marekebisho yakitolewa na kuungwa mkono, Mjumbe aliyekwishazungumza katika hoja ya awali anaweza kuzungumza kwenye hoja iliyorekebishwa kwa muda usiozidi dakika tatu; (5) Iwapo Wajumbe wawili au ingu watasimama wakati mmoja kuzungumza, Mjumbe atakayetamkwa na Meya ndiye atakayepewa nafasi kwanza; (6) Bila kuathiri masharti ya Kanuni Ndogo ya (5) ya Kanuni hii, Meya atahakikisha kuwa, nafasi ya kuchangia inatolewa kwa za uwakilishi wa uwiano unaofaa miongoni mwa inguine Madiwani walioomba kuchangia hoja hiyo; 15 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (7) Mjumbe anapozungumza ataelekeza mazungumzo yake kwa Meya tu na atapaswa kusimama; (8) Mjumbe anapozungumza hatakatizwa, isipokuwa kwa suala la utaratibu, lakini anaweza kutoa nafasi kwa Mjumbe anayetaka kujieleza; (9) Mjumbe anaposimama kutoa taarifa kuhusu utaratibu, Mjumbe anayezungumza ataketi na atabaki ameketi hadi hoja ya utaratibu itakapokuwa imeamuliwa na Meya, isipokuwa kama anasimama kumweleza Meya kuhusu suala la utaratibu; (10) Meya ndiye pekee mwenye uamuzi kuhusu utaratibu katika Mikutano ya Halmashauri, na anayo madaraka ya kuzuia fujo na kuhakikisha kuwa maamuzi yake katika kusimamia usalama yanatekelezwa mara moja. Wakati wa majadiliano Meya akisimama, Mjumbe anayezungumza au aliyesimama ataketi na hakuna Mjumbe atakayesimama hadi Meya aketi; (11) Hakuna Mjumbe atakayebaki amesimama wakati Mjumbe mwingine anaelekeza mazungumzo yake kwa Meya; (12) Mkurugenzi wa Halmashauri atajibu swali lolote atakaloulizwa na Meya kutokana na shughuli zinazoendelea kwenye Mkutano isipokuwa kama atadai haki ya kukataa kujibu swali kwa msingi ya kwamba jibu linaweza kumweka hatiani au kuvunja uaminifu wake au linamhusisha yeye kama mtetezi mahakamani; (13) Hakuna mtu kwa niaba yake mwenyewe, au kwa niaba ya watu wengine walio kwenye ujumbe wa watu, atakayeruhusiwa kuzungumza katika Mkutano wa Halmashauri isipokuwa kwa idhini ya Halmashauri iliyotolewa kwa njia ya azimio. Idhini ya namna hiyo haitatolewa isipokuwa kama mtu huyo au watu hao wanaotaka kuihutubia Halmashauri watakuwa wamempatia Mkurugenzi au Afisa aliyeruhusiwa naye, taarifa ya muda usiopungua siku tisa kabla ya Mkutano wa Halmashauri ambamo wangetaka maombi yao yafikiriwe kupewa idhini, maombi ya kimaandishi ikieleza jambo linalotarajiwa kujadiliwa, na mpaka taarifa ya kupokelewa kwa maoni hayo itakapokuwa imebandikwa kwenye mbao za matangazo za Halmashauri; (14) Hakuna ingu ya watu wawili watakaokuwa na haki ya kuhutubia Halmashauri kwa niaba ya uwakilishi; na wala hakuna ujumbe utakaozidi idadi ya watu watano watakaoruhusiwa; 16 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (15) Kiwango cha juu cha muda wa kuzungumza na Halmashauri ikiwa ni pamoja na muda wa kusoma risala hakitazidi dakika kumi; Fujo zinazosaba bishwa na Wajumbe - 18 Verify source ↗
(1) Katika Mkutano wowote wa Halmashauri kama Mjumbe
AI-assisted research summary: The Mayor may control a council meeting, name a member who is disrespectful or obstructive, and in serious disorder may adjourn or suspend the meeting.
18.-(1) Katika Mkutano wowote wa Halmashauri kama Mjumbe wa Halmashauri ataonyesha kukosa heshima kwa madaraka aliyonayo Meya au kudharau Kanuni za Kudumu za Halmashauri kwa kuzuia kwa makusudi shughuli za Halmashauri zisiendelee au vinginevyo, Meya ataelekeza Mkutano kwa tukio hilo kwa kumtaja jina mtu anayehusika. (2) Endapo baada ya kutajwa jina mjumbe ataendelea kudharau madaraka ya Meya, basi Meya ataliomba Baraza kuahirisha shughuli za Mkutano na Meya atatafakari jambo hilo na kuagiza yafuatayo; (41) Mjumbe atolewe nje ya Mkutano kama mjumbe wa Halmashauri na kumzuia kuhudhuria vikao vitatu mfululizo pamoja na haki zake zote. (41) Mjumbe kuzuiliwa kuhudhuria vikao vitatu mfululizo na kupoteza haki zake zinazohusiana na vikao hivyo. (3) Iwapo kutatokea fujo kubwa katika Mkutano wowote wa Halmashauri, Meya anaweza kama ataona ni muhimu kufanya hivyo, kuahirisha Mkutano bila majadiliano au swali, au kusimamisha Mkutano kwa muda atakaoona unafaa. Fujo zinazosaba bishwa na umma - 19 Verify source ↗
(1) Iwapo mtu yeyote kati ya umma unaohudhuria
AI-assisted research summary: If a member of the public disrupts a Council meeting, the Mayor must warn them to stop and may order them removed; if disorder continues or spreads in the public meeting area, the Mayor must order removal.
19.-(1) Iwapo mtu yeyote kati ya umma unaohudhuria Mkutano wa Halmashauri atavuruga Mkutano wa Halmashauri, Meya atamuonya mtu huyo aache kufanya hivyo. Endapo mtu huyo ataendelea kuvuruga Mkutano, Meya ataamuru mtu huyo atolewe kwenye chumba cha Mkutano. (2) Endapo kutakuwa na vurugu katika sehemu yoyote ya chumba cha Mkutano kinachotumika na umma, Meya ataamuru kuondolewa kwa watu wote walio katika eneo hilo. Hoja na marekebis ho ya hoja - 20 Verify source ↗
(1) Taarifa ya kila hoja, isipokuwa hoja iliyowasilishwa
AI-assisted research summary: Motions must be submitted in signed writing to the Director at least four days before the next council meeting, and several rules govern how motions and amendments are listed, moved, withdrawn, and decided.
20.-(1) Taarifa ya kila hoja, isipokuwa hoja iliyowasilishwa chini ya Kanuni ya 21, itawasilishwa kwa maandishi yaliyowekwa saini na Diwani au Madiwani waliotoa taarifa, na itapelekwa kwa 17 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) Mkurugenzi angalau siku nne kabla ya Mkutano wa Halmashauri unaofuata na akishaipokea, Mkurugenzi atagonga tarehe na kuipa namba na kuiingiza kwenye daftari kadri hoja zilivyowasilishwa, na daftari hiyo itakuwa wazi kukaguliwa na Mjumbe yeyote wa Halmashauri. (2) Mkurugenzi ataonyesha katika taarifa ya kila Mkutano wa Halmashauri hoja zilizowasilishwa na kwa kadri zilivyopokelewa isipokuwa kama Diwani aliyetoa hoja hiyo ameeleza kwa maandishi wakati alipoleta hoja hiyo, kwamba anataka kuitoa katika Mkutano utakaofanyika baadaye, au baada ya kuwasilisha ameifuta hoja hiyo kwa maandishi. (3) Iwapo hoja ambayo imeonyeshwa katika taarifa ya Mkutano haiwezi kutolewa na Mjumbe aliyewasilisha taarifa; au na Mjumbe mwingine yeyote kwa niaba yake, basi hoja hiyo, isipokuwa kama imeahirishwa kwa idhini ya Halmashauri, itachukuliwa kama imeondolewa na haitawasilishwa tena bila ya kutoa taarifa upya. (4) Iwapo hoja itahusu jambo linalohusu Kamati au Kamati mbalimbali baada ya kupendekezwa na kuungwa mkono, hoja hiyo itapelekwa bila majadiliano kwenye Kamati ambayo Halmashauri itaelekeza ili iweze kufikiriwa na kutayarishiwa taarifa. (5) Ni lazima kila hoja ihusu jambo ambalo Halmashauri ina uwezo na wajibu nalo, au iwe inahusu Halmashauri ya husika. (6) Marekebisho ya hoja yaliyopendekezwa na kuungwa mkono yanaweza kuondolewa tu kwa ridhaa ya Wajumbe wa Halmashauri walio wengi waliopo katika Mkutano. (7) Marekebisho ya hoja yanapokuwa yamethibitishwa, hoja ya msingi kama ilivyorekebishwa itatolewa na Meya kama ndiyo hoja ya msingi ambayo nayo inaweza kufanyiwa marekebisho. Kama marekebisho ya hoja hayakukubaliwa, rekebisho lingine linaweza kupendekezwa. (8) Kwa idhini ya Meya, ingu ya rekebisho moja linaweza kutolewa kwa wakati mmoja mbele ya Mkutano wa Halmashauri, lakini kila rekebisho la namna hii litatolewa moja baada ya jingine kufuatana na jinsi mapendekezo hayo yalivyotolewa. (9) Rekebisho halitachukuliwa kuwa sahihi kama litakuwa sawa na kuikataa hoja moja kwa moja au kama si rekebisho la hoja ya 18 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) msingi linalokusudiwa kurekebisha. (10) Rekebisho ambalo halikutolewa taarifa, halitapendekezwa baada ya mjadala wa hoja inayozungumzwa kuendelea kwa nusu saa, ila kwa mujibu wa sharti hili, taarifa ya idadi yoyote ya marekebisho inaweza kutolewa. (11) Hoja ya kufuta azimio itapitishwa na Wajumbe wasiopungua theluthi mbili ya Wajumbe wote. (12) Hoja ya kuzingatia taarifa ya Kamati au kuidhinisha majadiliano au mapendekezo ya Kamati inaweza kutolewa na Mwenyekiti wa Kamati husika, au na Mjumbe yeyote wa Kamati husika kwa niaba yake. (13) Mjumbe yeyote ambaye hajachangia katika mjadala wa hoja, au hajaitolea marekebisho, anaweza kupendekeza “kwamba Halmashauri iendelee na shughuli inayofuata”. Hoja ya aina hiyo inaweza tu kuzingatiwa baada ya hoja kupendekezwa na kuungwa mkono. Hoja inapotolewa, itaamuliwa bila marekebisho au mjadala, na kama iliyokatizwa na azimio hilo haitaendelea kujadiliwa katika kikao hicho. Hoja ya kupendekeza kuendelea na shughuli inayofuata haitatolewa ingu ya mara moja katika mjadala wa jambo lolote. ikikubaliwa, shughuli (14) Baada ya mjadala kuhusu hoja kuendelea kwa muda usiopungua nusu saa, Mjumbe ambaye hajachangia katika majadiliano anaweza kuomba idhini ya kutoa hoja “kwamba suala lililo mbele yetu sasa liamuliwe” na kama idhini hiyo itatolewa kwa kukubaliwa na si chini ya Wajumbe watano, hoja “kwamba suala lililo mbele yetu sasa liamuliwe” itawasilishwa mara moja, na kama ikiafikiwa, mtoa hoja ya msingi anaweza kuzungumza kwa dakika zisizozidi tano, na baada ya hapo swali au maswali yaliyo mbele ya Halmashauri yatafanyiwa uamuzi. (15) Hoja “kwamba suala lililo mbele yetu sasa liamuliwe” haitatolewa ingu ya mara moja katika mjadala unaoendelea kuhusu jambo lolote mpaka hapo mjadala utakapokuwa umeendelea kwa angalau nusu saa tangu kuwekwa mbele ya Mkutano hoja ya aina hiyo ilipopendekezwa awali. Hoja zinazowez - 21 Verify source ↗
Hoja zifuatazo zinaweza kutolewa bila taarifa
AI-assisted research summary: This section lists motions that may be brought without notice and notes a right to reply.
21. Hoja zifuatazo zinaweza kutolewa bila taarifa. (a) Kumchagua Mwenyekiti wa Mkutano ambamo hoja 19 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) a kutolewa bila taarifa imetolewa. (b) Hoja kuhusu usahihi wa muhtasari, kufunga Mkutano, kuahirisha Mkutano, utaratibu wa Mkutano, au suala linalofuata. (c) Kuteua Kamati au Wajumbe wa Kamati, au wawakilishi katika taasisi za nje, unaotokana na jambo lililotaarifiwa katika wito wa Mkutano. (d) Kukubali taarifa na mapendekezo ya Kamati na maazimio yote yanayotokana na taarifa au mapendekezo hayo; (e) Kwamba idhini itatolewa kuiondoa hoja. (f) Kusahihisha hoja. (g) Kuongeza muda wa hotuba. (h) Kuwa, jambo lililotajwa katika taarifa ya kuitisha Mkutano litangulie. (i) Kusimamisha Kanuni za kudumu; (j) Kwamba Mjumbe asisikilizwe tena au aondoke katika Mkutano. (k) Kumwomba Mjumbe abakie Mkutanoni, na (l) Kutoa idhini ya Halmashauri pale ambapo idhini inatakiwa kwa mujibu wa Kanuni za kudumu hizi. Haki ya kujibu - 22 Verify source ↗
(1) Mtoa hoja atakuwa na haki ya kujibu maswali wakati wa
AI-assisted research summary: Mtoa hoja ana haki ya kujibu maswali wakati wa kufunga mjadala kabla ya kura au kabla ya hoja ya kuahirisha kikao.
22.-(1) Mtoa hoja atakuwa na haki ya kujibu maswali wakati wa kufunga mjadala juu ya hoja; kabla ya hoja kupigiwa kura au kabla ya hoja kutolewa “kwamba kikao kiahirishwe, (2) Mjumbe anayetumia haki yake ya kujibu hataanzisha hoja nyingine mpya, (3) Baada ya kutolewa kwa jibu ambalo linahusiana na Kanuni hizi, uamuzi utafikiwa bila majadiliano zaidi. Maswali - 23 Verify source ↗
(1) Mjumbe anaweza kumuuliza Mwenyekiti wa Kamati
AI-assisted research summary: Mjumbe anaweza kuuliza Mwenyekiti wa Kamati maswali kuhusu muhtasari uliowasilishwa, na maswali hayo yajibiwe mara moja bila majadiliano.
23.-(1) Mjumbe anaweza kumuuliza Mwenyekiti wa Kamati swali lolote kuhusu muhtasari wa Kamati uliofikishwa mbele ya Halmashauri, (2) Kila swali litaulizwa na kujibiwa bila majadiliano, 20 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (3) Swali au maswali yatajibiwa na Mwenyekiti wa Kamati mara moja, na Mjumbe anayeuliza maswali hayo hatanyimwa haki yake ya kujadili hoja ambayo maswali hayo yanarejewa au kutoa hoja ya marekebisho, la maandishi (4) Pale ambapo swali limeelekezwa kwa Mwenyekiti wa Kamati, au Mkutano na taarifa inayotakiwa imo katika mojawapo ya mihtasari ya Halmashauri, kuonyesha sehemu ya muhtasari ambapo habari hiyo imeonyeshwa, kutachukuliwa ni jibu la kutosha. Maswali ya papo kwa papo’ - 24 Verify source ↗
(1) Halmashauri itatenga muda wa angalau dakika thelathini
AI-assisted research summary: The council must set aside at least 30 minutes in each ordinary meeting for instant questions before normal business starts.
24.-(1) Halmashauri itatenga muda wa angalau dakika thelathini katika kila Mkutano wa Kawaida wa Halmashauri ambapo Meya na Mkurugenzi wa Halmashauri watajibu maswali ya papo kwa papo kutoka kwa Wajumbe kabla ya kuanza kwa shughuli ya kawaida za Mkutano wa Halmashauri. (2) Wajumbe ambao watataka kuuliza maswali ya papo kwa papo kwa Meya na Mkurugenzi watatakiwa kujiorodhesha kwanza kwa Meya angalau masaa ishirini na nne (24) kabala ya Mkutano wa Halmashauri kuanza. (3) Mjumbe yoyote ambae hatajiorodhesha kwa Meya ndani ya masaa ishirini na nne atahesabika kuwa amechelewa na hataruhusiwa kumuuliza Mkurugenzi au Mwenyekiti swali la papo kwa papo. (4) Kabla ya kuanza kwa kipindi cha maswali ya papo kwa papo Mwenyekiti au Meya atataja majina ya Wajumbe waliojiorodhesha kuuliza maswali ya papo kwa papo na idadi ya maswali, (5) Meya ataweka utaratibu ambao ataona unafaa na kuridhiwa na Wajumbe wa namna bora ya kuendesha kipindi cha swali la papo kwa papo. (6) Mjumbe hataruhusiwa kuuliza zaidi ya swali moja la papo kwa papo. 21 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (7) Maeneo ya muhimu ambayo Wajumbe watatakiwa kuuliza maswali ya papo kwa papo:- (a) Uendeshaji wa jumla wa Halmashauri; (b) Utekelezaji wa miradi ya Maendeleo; (c) Mipango ya kimkakati ya Halmashauri kuwaondolea wananchi umaskini; (d) Mipango ya baadaye ya maendeleo ya Halmashauri; (e) Usimamizi na utekelezaji wa Mipango na Bajeti kwa mwaka husika; (f) Utoaji wa huduma za jamii kama vile elimu, afya, maji, barabara na madaraja; (g) Hifadhi ya mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji; (h) Usalama wa Chakula, Raia na Mali zao; (i) Utawala Bora na utatuzi wa kero za wananchi. (8) Baada ya kujibiwa kwa swali, Mjumbe aliyeuliza swali atapewa fursa ya kuuliza swali moja tu la ufafanuzi na maswali yatajibiwa bila mjadala. (9) Meya atakua na uwezo wa kuruhusu au kukataa swali lolote la papo kwa papo ambalo litaonekana linahitaji takwimu au utafiti zaidi au swali ambalo linalenga kumdhalilisha Meya au mjumbe yeyote wa Baraza na uamuzi wake utakuwa wa mwisho. (10) Mara baada ya muda wa nusu saa kumalizika,kipindi cha maswali ya papo kwa papo kitamalizika na kuruhusu shughuli zingine za kikao kuendelea Taarifa za Kamati - 25 Verify source ↗
(1) Kila Kamati au Kamati ya pamoja iliyoteuliwa chini ya
AI-assisted research summary: Kamati lazima iwasilishe taarifa ya majadiliano kuhusu utekelezaji wa majukumu iliyopewa, na baadhi ya muhtasari unaohitaji idhini ya Halmashauri upelekwe kwa wajumbe angalau siku 7 kabla ya mkutano.
25.-(1) Kila Kamati au Kamati ya pamoja iliyoteuliwa chini ya itatoa, katika mojawapo ya vikao viwili vya Kanuni hizi Halmashauri iliyoteua Kamati, Kamati ya pamoja au Kamati Ndogo, taarifa ya majadiliano yanayohusiana na utekelezaji majukumu iliyokasimiwa, kwa ujulisho wa Halmashauri. (2) Muhtasari wa Kamati unaohitaji idhini ya Halmashauri, na taarifa zozote zinazohusiana na muhtasari huo, na ambazo zinaonekana kwa Kamati kuwa zinastahili, zitapelekwa kwa kila Mjumbe wa Halmashauri angalau siku saba kabla ya Mkutano wa Halmashauri ambamo utafikiriwa. (3) Mwenyekiti wa Kamati, au Mjumbe mwingine wa Kamati kwa niaba yake, wakati wa kupendekeza kuidhinishwa kwa muhtasari wa Kamati, anaweza kusema kuwa hakusudii kuwasilisha kipengele au vipengele fulani vya muhtasari huo kwa lengo la 22 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) kupata idhini ya Halmashauri. Katika hali hiyo Mjumbe yeyote hataweza kukizungumzia kipengele au vipengele hivyo na muhtasari utawasilishwa bila vipengele hivyo. Kuondolewa kwa kipengele cha aina hiyo kutatolewa taarifa kwenye Mkutano unaofuata. (4) Taarifa ya Kamati inapokuwa imepokelewa na Halmashauri itamaanisha kuwa hatua zilizochukuliwa na Kamati husika zimekubaliwa na mapendekezo yaliyo kwenye taarifa hiyo yatatekelezwa na kwamba Mkurugenzi atakuwa ameelekezwa ipasavyo. Taarifa za kutoka kwenye Kata - 26 Verify source ↗
(1) Kila Kata itatakiwa kuwasilisha taarifa za utekelezaji
AI-assisted research summary: Kila Kata lazima iwasilishe taarifa za utekelezaji kwenye Mkutano wa Halmashauri, na taarifa hiyo inaweza kuwasilishwa na diwani husika au mbadala aliyeelezwa ikiwa diwani hayupo.
26.-(1) Kila Kata itatakiwa kuwasilisha taarifa za utekelezaji katika Mkutano wa Halmashauri ulioitishwa chini ya Kanuni ya 3(1) ya Kanuni hizi; (2) Taarifa za utekelezaji kutoka katika Kata zitawasilishwa na Diwani wa Kata husika, au kama diwani hayupo, taarifa hiyo itawasilishwa na Diwani wa Viti Maalum anayeishi katika Kata hiyo na kama Diwani Viti Maalum hayupo, Meya atamtaarifu mapema Diwani yeyote ili ajiandae kuwasilisha taarifa hiyo; (3) Kutakuwa na aina tatu za taarifa zitakazowasilishwa:- (41) Taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Kata ambayo itajumuisha ujenzi wa Madarasa, Nyumba za Walimu, Matundu ya Vyoo, Maabara, Viwanja vya Michezo, Vituo vya Afya, Zahanati, Madaraja, Barabara, Mashamba darasa, Ofisi za Vijiji, Mitaa, Kata na Tarafa; Idadi ya watu na vizazi (b) Taarifa zinazohusu hali ya Kata ambazo zitajumuisha- (i) Maendeleo ya Elimu katika Kata kuhusiana na uandikishaji wa watoto wenye umri wa kwenda shule, ufundishaji, utoro, hali ya mahudhurio, mimba mashuleni, ukaguzi na uratibu wa shule. (ii) Hali ya majanga kama vile magonjwa ya mlipuko, mafuriko, njaa, na hali ya uhalifu na vifo. (iii) Maendeleo ya Kilimo, mifugo na uvuvi ambayo itajumuisha upatikanaji wa wataalamu, zana za kisasa na pembejeo za kilimo, mifugo na uvuvi. (iv) Uimarishaji wa dhana ya uzalendo na utaifa kwa kuhamasisha vijana kuanzisha na kujiunga na vikundi vya 23 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) Vijana Wagani kazi na mafunzo ya Jeshi la Mgambo, ulinzi shirikishi na polisi jamii. (c) Taarifa ya utekelezaji wa miradi ya Maendeleo na taarifa ya hali ya Kata sharti ijumuishe pia taarifa za shughuli za kiuchumi, taarifa ya mavuno ya mazao ya chakula na biashara pamoja na taarifa ya utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji. (4) Mkurugenzi wa Halmashauri atahakikisha taarifa kutoka kwenye Kata, zinaandaliwa na kuwasilishwa na Diwani wa Kata hiyo kwenye Baraza la Madiwani ili ipitiwe na kuchambuliwa kwa nia ya kupata hoja zitakazowasilishwa katika Vikao vya Kamati husika na kutoa mrejesho. Mafanikio na changamoto (5) Mwasilishaji wa taarifa atatakiwa kuelezea mafanikio yaliyopatikana, changamoto zilizo jitokeza na mbinu za kukabiliana nazo. (6) Mbinu za kukabiliana na changamoto sharti ziwekewe malengo na muda maalum wa kuzitatua. (7) Taarifa za mapokeo ya fedha na matumizi yake zitakazokuwa zimeandaliwa na Afisa Mtendaji wa Kata, zitawasilishwa sanjari na miradi iliyotekelezwa na gharama zake. (8) Baada ya taarifa kutoka kwenye Kata kupokelewa na Halmashauri, itamaanisha kuwa taarifa hizo zimeidhinishwa na mapendekezo yaliyomo kwenye taarifa yatatekelezwa na Halmashauri, na Kata kupewa taarifa ya utekelezaji wa majukumu hayo. Uhuru wa kutoa mawazo wakati wa majadiliano - 27 Verify source ↗
Kutakuwepo na uhuru wa kutoa mawazo wakati wa
AI-assisted research summary: Watu wanaojadiliana katika Mikutano ya Halmashauri wana uhuru wa kutoa mawazo wakati wa majadiliano, na uhuru huo hauhojiwi mahakamani au nje ya mkutano huo.
27. Kutakuwepo na uhuru wa kutoa mawazo wakati wa majadiliano katika Mikutano ya Halmashauri na uhuru huo hautaweza kuhojiwa katika mahakama yoyote au mahali popote nje ya Mkutano wa Halmashauri. Kauli zenye kashfa - 28 Verify source ↗
(1) Inapotokea, kulingana na maoni ya Mwenyekiti au mtu
AI-assisted research summary: If a member makes a defamatory statement, the Chair must require a written retraction and apology within seven days; if the member refuses, the Meeting Mayor suspends the member for three consecutive council meetings.
28.-(1) Inapotokea, kulingana na maoni ya Mwenyekiti au mtu yeyote anayeongoza Mkutano, kuwa kauli iliyotolewa na Mjumbe inakashifu mtu yeyote, Mwenyekiti atamtaka Mjumbe aliyetoa kauli hiyo kufuta kauli yake na kumwomba msamaha mtu aliyekashifiwa kwa maandishi ndani ya muda wa siku saba tangu kauli hiyo ya kashfa ilipotamkwa. 24 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (2) Endapo Mjumbe aliyetoa kauli za kashfa atakataa kufuta kauli yake na kuomba msamaha kwa maandishi kama inavyoelekezwa katika Kanuni Ndogo (1) ya Kanuni hii. Meya wa Mkutano, atamsimamisha Mjumbe huyo kuhudhuria vikao vitatu mfululizo vya Halmashauri. (3) Mjumbe aliyesimamishwa kwa mujibu wa kanuni Ndogo(2) ya Kanuni hii atapoteza haki zake zote ikiwa ni pamoja na posho,nauli na upendeleo na kinga kwa muda wote wa kusimamishwa kwake; Maamuzi ya Mikutano ya Halma- shauri - 29 Verify source ↗
(1) Masuala yote yaliyojadiliwa na kupendekeza katika
AI-assisted research summary: Council matters are decided by a majority of the members present; if there is a tie, the chair has a casting vote. Some votes must be secret, including votes on removing the Mayor or no confidence in the Mayor, and any other matter the Council decides.
29.-(1) Masuala yote yaliyojadiliwa na kupendekeza katika Mkutano wowote wa Halmashauri yataamuliwa kulingana na wingi wa kura za Wajumbe waliohudhuria Mkutano huo, na ikitokea kura za Wajumbe zikalingana, basi Meya au Mjumbe yeyote mwingine anayeongoza Mkutano, atapiga kura ya turufu mbali ya kura ya kawaida. (2) Iwapo suala linalopigiwa kura linahusu kutokuwa na ingu au kumwondoa Meya madarakani, au jambo lolote inguine kama itakavyoamuliwa na Halmashauri, kura zitapigwa kwa siri. - 30 Verify source ↗
(1) Meya, baada yakushauriana na Wajumbe, anaweza
AI-assisted research summary: Meya anaweza kumwalika mtu yeyote kuhudhuria, kuzungumza, au kushiriki katika mkutano wa Halmashauri; walioalikwa hawana haki ya kupiga kura. Wakuu wa Idara za Halmashauri na Maafisa Tarafa wanapaswa kuhudhuria mikutano yote lakini hawana haki ya kupiga kura.
30.-(1) Meya, baada yakushauriana na Wajumbe, anaweza kumwalika mtu yeyote kuhudhuria na kuzungumzia jambo lolote, au kushiriki kwa njia yoyote, katika Mkutano wowote wa Halmashauri lakini mwalikwa huyo hatakuwa na haki ya kupiga kura katika Mkutano huo. (2) Wakuu wa Idara za Halmashauri na Maafisa Tarafa wanapaswa kuhudhuria Mikutano yote ya Halmashauri lakini hawatakuwa na haki ya kupiga kura katika Mikutano hiyo. - 31 Verify source ↗
Mkurugenzi wa Halmashauri atahakikisha mihtasari yote ya
AI-assisted research summary: The Council Director must make sure all summaries from Ward Development Committees and street general meetings are reviewed and that feedback is given as appropriate.
31. Mkurugenzi wa Halmashauri atahakikisha mihtasari yote ya Kamati za Maendeleo za Kata, na Mikutano Mikuu ya Mitaa inapitiwa hoja zitakazowasilishwa katika vikao vya Kamati husika na kutoa mrejesho inavyopaswa. kuchambuliwa kupata kwa nia na ya - 32 Verify source ↗
(1) Mihtasari ya Halmashauri itatolewa na kupelekwa kwa
AI-assisted research summary: Halmashauri lazima itoe na kupeleka kwa taarifa mihtasari yake kwa Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa ndani ya siku 7 baada ya kuthibitishwa.
32.-(1) Mihtasari ya Halmashauri itatolewa na kupelekwa kwa taarifa, kwa Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa ambamo Halmashauri imo katika muda wa siku 7 baada ya kuthibitishwa kwa mihutasari hiyo. 25 Mwaliko kwa wasiokuwa Wajumbe kushiriki na kuzungumza kwenye vikao vya Halma- shauri Mihtasari ya Kamati ya Maendeleo ya Kata, Mitaa/ Vijiji Mihtasari ya Halma- shauri kupelekwa kwa Mkuu wa Wilaya Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) na Mkuu wa Mkoa Hoja kuhusu matumizi Kupokelewa kwa taarifa za Kamati (2) Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa wanaweza kupewa, wakiomba, nakala ya mihutasari au sehemu ya mihtasari ya Kamati za Kudumu na Kamati nyingine. (3) Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa hawatabadilisha au kubatilisha au kuagiza kubadilisha au kubatilisha uamuzi wa Halmashauri. - 33 Verify source ↗
Hoja yoyote isiyotokana na mapendekezo au taarifa ya
AI-assisted research summary: Non-finance motions that would raise spending or cut revenue are postponed without debate until the next ordinary Council meeting, and the relevant committee must consider the proposal’s financial impact.
33. Hoja yoyote isiyotokana na mapendekezo au taarifa ya Kamati ya Fedha na Utawala, na ambayo, kama ikikubaliwa, itaongeza matumizi au kupunguza mapato yaliyo chini ya usimamizi wa Kamati yoyote, au itasababisha matumizi ya Kamati ya Kudumu, baada ya kupendekezwa au kuungwa mkono, itaahirishwa bila majadiliano mpaka Mkutano wa kawaida wa Halmashauri unaofuata, na Kamati yoyote inayohusika na hoja hiyo itafikiria iwapo ingependa kutoa taarifa kuhusu athari za kifedha za pendekezo hilo. ya Kamati - 34 Verify source ↗
(1) Taarifa
AI-assisted research summary: The motion is that the report be received, and once accepted it is discussed clause by clause; proposed amendments are voted on if any member wants that, and the full report is then presented to the meeting for receipt with or without amendments.
34.-(1) Taarifa kwenye Halmashauri, hoja itakuwa “kwamba taarifa ipokelewe”na baada ya kukubaliwa na Wajumbe taarifa itaanza kujadiliwa kipengele kimoja baada ya kingine. inapowasilishwa (2) Mapendekezo yoyote yaliyomo katika taarifa hiyo yatapigiwa kura iwapo Mjumbe yeyote atapenda iwe hivyo. Baada ya hapo taarifa nzima itawasilishwa mbele ya Mkutano kwa kupokelewa ikiwa na au bila marekebisho. Kuidhini- shwa kwa taarifa ya Kamati - 35 Verify source ↗
Taarifa ya Kamati inapokuwa imepokelewa na Halmashauri
AI-assisted research summary: When the Council receives a committee report, the report’s actions are treated as approved and the report’s recommendations will be carried out.
35. Taarifa ya Kamati inapokuwa imepokelewa na Halmashauri itamaanisha kuwa hatua zilizochukuliwa na Kamati iliyowasilisha taarifa hiyo zimeidhinisha na mapendekezo yaliyo kwenye taarifa yatatekelezwa na kwamba Mkurugenzi wa Halmashauri atakuwa ameelekezwa kama inavyotakiwa. Uhalali wa majadiliano ya Halmashauri - 36 Verify source ↗
Uhalali wa majadiliano kwenye Halmashauri hautaathiriwa
AI-assisted research summary: The validity of council deliberations is not affected by a vacant seat or defects in the election or appointment of committee members or officers.
36. Uhalali wa majadiliano kwenye Halmashauri hautaathiriwa na nafasi yoyote wazi ya Mjumbe, dosari zozote zilizo katika uchaguzi au uteuzi wa Wajumbe wa Kamati au zile za maafisa wake. Uwezo wa Halma- shauri kujigeuza - 37 Verify source ↗
Halmashauri
AI-assisted research summary: Halmashauri inaweza kujigeuza kuwa Kamati ya Halmashauri.
37. Halmashauri inaweza kujigeuza kuwa Kamati ya Halmashauri, na mara baada ya kujigeuza, taratibu za kuendesha vikao vya Kamati za Kudumu zitatumika. 26 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) kuwa Kamati ya Halma- shauri nzima Hoja zinazohusu Watumishi wa Halma- shauri Kushiriki kwa Umma litajitokeza - 38 Verify source ↗
Kama
AI-assisted research summary: Mambo yanayomhusu mtumishi wa Halmashauri kuhusu uteuzi, kupandishwa cheo, kufukuzwa kazi, mishahara, mazingira ya kazi au utendaji kwa jumla yanapaswa kujadiliwa na Kamati ya Halmashauri nzima.
38. Kama lolote katika kikao cha jambo Halmashauri linalomhusu Mtumishi yeyote wa Halmashauri kuhusu Uteuzi, kupandishwa cheo, kufukuzwa kazi, mishahara, mazingira ya kazi au utendaji kazi kwa jumla wake, jambo hilo litajadiliwa katika Kamati ya Halmashauri nzima. - 39 Verify source ↗
(1) Mtu yeyote ambaye ni mkazi katika eneo
AI-assisted research summary: A resident in the Council area may attend a Council meeting to present a motion if written notice is given to the Director and the Director approves. A resident may also be invited to attend a committee or subcommittee meeting before a decision is made on matters on which the resident has specific views.
39.-(1) Mtu yeyote ambaye ni mkazi katika eneo la Halmashauri anaweza kuhudhuria kikao cha Halmashauri kwa nia ya kuwasilisha hoja mbele ya Halmashauri, baada ya kutoa taarifa kwa maandishi kwa Mkurugenzi, na Mkurugenzi akamkubali kufanya hivyo. (2) Mtu yeyote ambaye ni mkazi katika eneo la Halmashauri anaweza kualikwa kuhudhuria kikao cha Kamati au Kamati Ndogo kabla uamuzi haujafanyika kuhusu masuala ambayo ana maoni mahsusi. Uahirishaji wa vikao - 40 Verify source ↗
(1) Kwa kuzingatia masharti ya Kanuni Ndogo ya (2) ya
AI-assisted research summary: The council must not adjourn a meeting until all agenda items have been discussed and decided, and if quorum is not met the members present must adjourn the meeting and follow the rules for calling another meeting.
40.-(1) Kwa kuzingatia masharti ya Kanuni Ndogo ya (2) ya Kanuni 18 na Kanuni Ndogo ya 2 ya Kanuni hii, Halmashauri haitaahirisha Mkutano wake hadi dondoo zote za agenda ya Mkutano huo zitakapojadiliwa na kutolewa uamuzi. (2) Pale ambapo katika Mkutano wowote wa Halmashauri akidi haikutimia, Wajumbe waliopo wataahirisha Mkutano na utaratibu wa kuitisha Mkutano mwingine utafanyika kwa kuzingatia maelekezo ya Kanuni hizi. SEHEMU YA IV KAMATI Kamati za Kudumu
Part
SEHEMU YA IV
- 42 Verify source ↗
Meya/Mwenyekiti kuwa Mjumbe wa Kamati zote
AI-assisted research summary: The mayor/chairperson must be a member of all committees.
42. Meya/Mwenyekiti kuwa Mjumbe wa Kamati zote. - 51 Verify source ↗
Mahudhurio katika Mikutano ya Kamati
AI-assisted research summary: Section title on attendance in committee meetings.
51. Mahudhurio katika Mikutano ya Kamati - 52 Verify source ↗
Mtoa hoja kualikwa kwenye Mkutano wa Kamati
AI-assisted research summary: This section concerns inviting the person who moved a proposal to a committee meeting.
52. Mtoa hoja kualikwa kwenye Mkutano wa Kamati - 53 Verify source ↗
Waalikwa wasiokuwa Wajumbe kuhudhuria na kushiriki katika
AI-assisted research summary: This section concerns guests who are not members attending and taking part in committee meetings.
53. Waalikwa wasiokuwa Wajumbe kuhudhuria na kushiriki katika Mikutano ya Kamati - 54 Verify source ↗
Mahudhurio ya Umma na Vyombo vya Habari kwenye Mikutano ya
AI-assisted research summary: Section heading about public attendance and media at committee and subcommittee meetings.
54. Mahudhurio ya Umma na Vyombo vya Habari kwenye Mikutano ya Kamati na Kamati Ndogo - 57 Verify source ↗
Kanuni za kudumu kutumika katika Mikutano ya Kamati
AI-assisted research summary: This section is titled “Permanent rules to apply in committee meetings.”
57. Kanuni za kudumu kutumika katika Mikutano ya Kamati - 58 Verify source ↗
Upigaji kura kwenye Mikutano ya Kamati
AI-assisted research summary: Section title: Voting at committee meetings.
58. Upigaji kura kwenye Mikutano ya Kamati - 61 Verify source ↗
Kutunza siri za majadiliano ya Kamati na Kamati Ndogo
AI-assisted research summary: Provision kuhusu kutunza siri za majadiliano ya Kamati na Kamati Ndogo.
61. Kutunza siri za majadiliano ya Kamati na Kamati Ndogo - 62 Verify source ↗
Kujiuzulu wadhifa wa Mwenyekiti wa Kamati
AI-assisted research summary: Section 62 concerns resignation from the position of Committee Chairperson.
62. Kujiuzulu wadhifa wa Mwenyekiti wa Kamati - 63 Verify source ↗
Kujiuzulu ujumbe wa Kamati na kujazwa kwa nafasi iliyoachwa wazi
AI-assisted research summary: This section is titled about resignation of a committee member and filling a vacant seat.
63. Kujiuzulu ujumbe wa Kamati na kujazwa kwa nafasi iliyoachwa wazi. SEHEMU YA V UNUNUZI WA VIFAA, UPATIKANAJI WA HUDUMA NA UJENZI - 41 Verify source ↗
(1) Halmashauri katika Mkutano wake wa mwaka itateua
AI-assisted research summary: The council must appoint standing committees at its annual meeting and each council member must belong to at least one standing committee.
41.-(1) Halmashauri katika Mkutano wake wa mwaka itateua Wajumbe wa Kamati za Kudumu zifuatazo ambazo zitakuwa na idadi ya Wajumbe (ukimwondoa Meya au Mwenyekiti wa Halmashauri isipokuwa katika Kamati ya Fedha na Utawala) kama inavyoonyesha hapa chini au kama itakavyorekebishwa na Halmashauri mara kwa mara.Isipokuwa katika kuteua Wajumbe wa Kamati ya Fedha na Utawala, Meya na Mkurugenzi watazingatia uwiano wa uwakilishi wa vyama katika Halmashauri. 27 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) Kamati (a) Kamati ya Fedha na Utawala (b) Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu. (c) Kamati ya Mipango Miji na Mazingira. (d) Kamati ya Maadili (c) ya Madiwani Kamati UKIMWI ya Idadi ya Wajumbe 7 13 13 4 4 Akidi 4 7 7 2 2 (2) Kila Mjumbe wa Halmashauri atakuwa Mjumbe wa angalau Kamati moja ya Kudumu. Kamati ya Fedha na Utawala itakuwa na Wajumbe wafuatao; (a) Meya ambaye atakuwa Mwenyekiti. (b) Naibu Meya. (c) Mbunge au Wabunge wa Majimbo wanaowakilisha Majimbo katika eneo la Halmashauri. (d) Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Halmashauri. (e) Wajumbe wawili (2) watakaopendekezwa na Mwenyekiti au Meya na kupigiwa kura na Baraza la Halmashauri mmoja kati yao awe mwanamke. wasiozidi wengine (3) Halmashauri yenye Madiwani wasiozidi ishirini(20), idadi ya wajumbe wa Kamati wa Fedha itakuwa kama ilivyoonyeshwa kwenye Kanuni ya 41(2) ya Kanuni hizi. (4) Bila kuathiri masharti ya Kanuni Ndogo ya (2) ya Kanuni hii, Halmashauri yenye idadi ya Madiwani wanaozidi ishirini (20) na wasiozidi thelathini na tano (35) Wajumbe wa Kamati ya Fedha watakuwa kama ilivyoonyeshwa kwenye Kanuni ya 41(2) pamoja na wajumbe wengine wawili (2) watakaotokana na orodha itakayopendekezwa na Mwenyekiti au Meya na kupigiwa kura na Baraza la Halmashauri mmoja kati yao awe wanawake. (5) Bila kuathiri masharti ya Kanuni Ndogo ya (2)(3) na (4) ya Kanuni hii, Halmashauri yenye idadi ya Madiwani wanaozidi thelathini na tano(35) na zaidi Wajumbe wa Kamati ya Fedha 28 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) watakuwa kama ilivyoonyeshwa kwenye Kanuni ya 41(2) pamoja na wajumbe wengine wanne(4) watakaotokana na orodha itakayopendekezwa na Mwenyekiti au Meya na kupigiwa kura na Baraza la Halmashauri wawili kati yao wawe wanawake. (5) Wajumbe wa Kamati za Kudumu watashika nyadhifa zao kwa muda wa mwaka mmoja na wataendelea kushika nyadhifa hizo mpaka Mkutano wa mwaka wa Halmashauri unaofuata. Isipokuwa Wajumbe waliochaguliwa kwenye Mkutano wa kwanza baada Uchaguzi Mkuu watashika nyadhifa zao kwa muda uliobaki kumaliza Mwaka wa Fedha ambapo Uchaguzi utafanyika tena. (6) Halmashauri inaweza wakati wowote kuvunja na kuunda upya Kamati ya Kudumu iliyoteuliwa kwa mujibu wa Kanuni hii ya kudumu, endapo kufanya hivyo kutakuwa ni kwa manufaa ya Halmashauri. (7) Hakuna Halmashauri itakayounda Kamati ya Kudumu mpya zaidi ya Kamati zilizotajwa kwenye Kanuni ya 41(1) hapo juu, isipokuwa baada ya kuomba na kupata idhini ya maandishi kutoka kwa Waziri. (8) Maombi ya Halmashauri ya kuanzisha Kamati mpya ya Kudumu lazima yakidhi na yawe na maelezo yafuatayo; (a) Upekee wa majukumu yanayoombewa kuundwa kwa Kamati ya Kudumu mpya na majukumu hayo yawe ambayo hayawezi kutekelezwa na Kamati za Kudumu zilizopo na zilizotajwa kwenye Kanuni ya 41(1) hapo juu, (b) Gharama za uendeshaji wa Kamati hiyo kwa mwaka, (c) Kuundwa kwa Kamati ya Kudumu hiyo mpya ni hitaji la lazima na ni kipaumbele cha Halmashauri na jamii kwa ujumla. (9) Kamati yoyote itakayoundwa na Halmashauri bila idhini ya Waziri itakuwa batili na maamuzi yake yote yatakua batili. - 42 Verify source ↗
Meya atakuwa Mjumbe wa Kamati zote za kudumu za
AI-assisted research summary: Meya must be a member of all standing committees of the Halmashauri.
42. Meya atakuwa Mjumbe wa Kamati zote za kudumu za Halmashauri. - 43 Verify source ↗
Kamati zote za Halmashauri zitawasilisha taarifa zao kwa
AI-assisted research summary: Kamati zote za Halmashauri lazima ziwasilishe taarifa zao kwa Halmashauri, na hatua haziwezi kuchukuliwa kutekeleza uamuzi mpaka taarifa ya kamati husika ikubaliwe, isipokuwa kama mamlaka ya kuchukua hatua imekasimiwa kwa Kamati.
43. Kamati zote za Halmashauri zitawasilisha taarifa zao kwa Halmashauri, na hakuna hatua itakayochukuliwa kutekeleza uamuzi 29 Meya kuwa Mjumbe wa Kamati moja Uwezo wa Kamati Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) Kamati za pamoja wowote wa Kamati yoyote mpaka hapo taarifa ya Kamati husika itakapokuwa imekubaliwa na Halmashauri, isipokuwa pale ambapo idhini ya kuchukua hatua imekasimiwa kwa Kamati. - 44 Verify source ↗
(1) Halmashauri inaweza kukubaliana na Halmashauri
AI-assisted research summary: Halmashauri zinaweza kukubaliana kuunda Kamati ya pamoja na zinaweza kukasimu kwake madaraka au kazi fulani, kwa masharti na mipaka waliyojiwekea, isipokuwa shughuli ambazo haziruhusiwi kukasimu.
44.-(1) Halmashauri inaweza kukubaliana na Halmashauri nyingine kuteua Kamati ya pamoja kutokana na Wajumbe wao kwa madhumuni yoyote yale ambayo wana maslahi ya pamoja, na Halmashauri hizo zinaweza kukasimu kwa Kamati hiyo ya pamoja, kutegemea na masharti na mipaka zitakazoweka kama inafaa, madaraka au kazi ya Halmashauri watakavyoona zinazohusiana na madhumuni yaliyozifanya ziunde Kamati hiyo, isipokuwa shughuli zile ambazo Halmashauri haziruhusiwi kukasimu. (2) Muundo na muda wa kazi wa Wajumbe wake na mipaka ya eneo ambamo Kamati hiyo ya pamoja itafanya kazi, itapangwa na Halmashauri zinazoiteua. (3) Kamati ya pamoja haitaingia katika gharama zozote zaidi ya zile ambazo zimeidhishwa na mamlaka iliyoteua Kamati hiyo. Kukasimu madaraka kwenye Kamati - 45 Verify source ↗
(1) Kufuatana na Kanuni Ndogo ya (2) ya Kanuni hii
AI-assisted research summary: Halmashauri inaweza kukasimu baadhi ya kazi kwa Kamati, lakini haiwezi kukasimu baadhi ya mamlaka muhimu kama kutunga sheria ndogo, kutoza kodi, au kuidhinisha bajeti.
45.-(1) Kufuatana na Kanuni Ndogo ya (2) ya Kanuni hii pamoja na masharti mengine ambayo Halmashauri itaona inafaa, Halmashauri inaweza kukasimu kwa Kamati uwezo wa kutekeleza kazi yoyote kwa niaba yake. (2) Halmashauri haitakasimu kwa Kamati yoyote uwezo wa:- (a) Kutunga Sheria Ndogo; (b) Kuweka na kutoza kodi; (c) Kuidhinisha makadirio ya mapato na matumizi ya Halmashauri; (d) Kutoza ada na ushuru; (e) Kuidhinisha mpango na Bajeti ya Halmashauri; (f) Kuingia mikataba mbalimbali ikiwa ni pamoja na mikataba ya kukopa, (g) Kupitisha mpango wa utoaji huduma. (3) Kazi za kila Kamati ya Kudumu ya Halmashauri ni kama zilivyoonyeshwa katika jedwali la Kanuni za kudumu hizi. (4) Halmashauri inaweza kusitisha au kurekebisha uamuzi wa kukasimu madaraka yoyote kwa Kamati, lakini usitishaji au urekebishaji huo hautaathiri jambo lolote lililofanywa kutokana na uamuzi wowote uliochukuliwa kihalali na Kamati. 30 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (5) Shughuli yoyote iliyotekelezwa na Kamati kutokana na kukasimiwa kwa mujibu wa Kanuni hii itatambuliwa kuwa imefanywa au kutekelezwa na Halmashauri. Kamati Ndogo - 46 Verify source ↗
(1) Kamati yoyote au Kamati ya pamoja inaweza kuteua
AI-assisted research summary: Kamati au Kamati ya pamoja inaweza kuteua Kamati Ndogo kwa ajili ya kuchunguza na kutoa taarifa, lakini haiwezi kukasimu madaraka yake ya kiutendaji kwa Kamati Ndogo.
46.-(1) Kamati yoyote au Kamati ya pamoja inaweza kuteua Kamati Ndogo kutokana na Wajumbe wake kadri itakavyoona inafaa kwa ajili ya kuchunguza na kutoa taarifa kuhusu jambo lolote, lakini Kamati haitakasimu madaraka yake ya kiutendaji kwa Kamati Ndogo yoyote. (2) Idadi ya Wajumbe wa Kamati Ndogo pamoja na muda watakaotumikia vitaamuliwa na Kamati iliyoteua Kamati Ndogo hiyo. (3) Mwenyekiti wa Kamati atakuwa Mjumbe wa Kamati Ndogo yoyote kwa mujibu wa wadhifa wake isipokuwa kama atamfahamisha Mkurugenzi kwa maandishi kuwa hatakuwa Mjumbe wa Kamati hiyo. (4) Kila Kamati Ndogo inaweza kumteua mmoja wa Wajumbe wake kuwa Mwenyekiti wa Kamati Ndogo husika. Mikutano ya Kamati - 47 Verify source ↗
(1) Mkutano wa kwanza wa Kamati utaitishwa na
AI-assisted research summary: Mkurugenzi must convene the Committee’s first meeting within one month of appointment, meeting schedules after that need Council approval, members must get at least 24 hours’ notice with the agenda, and the Committee size cannot exceed the Minister-set limit.
47.-(1) Mkutano wa kwanza wa Kamati utaitishwa na Mkurugenzi ndani ya mwezi mmoja baada ya Kamati kuteuliwa na ratiba ya Mikutano kama baada ya hapo kulingana na itakavyoidhinishwa na Halmashauri. (2) Taarifa ya angalau saa ishirini na nne yenye ajenda za kikao itabidi kutolewa kwa Wajumbe kabla ya Mkutano wa Kamati. (3) Idadi ya Kamati haitazidi idadi ambayo itawekwa na Waziri kutokana na uwezo aliopewa chini ya kifungu cha 75(3) cha Sheria. Mwenyekiti wa Kamati - 48 Verify source ↗
(1) Katika kikao chake cha kwanza baada ya Mkutano wa
AI-assisted research summary: Kila Kamati lazima ichague Mwenyekiti wake katika kikao cha kwanza baada ya Mkutano wa mwaka, kabla ya shughuli nyingine kuendelea.
48.-(1) Katika kikao chake cha kwanza baada ya Mkutano wa mwaka wa Halmashauri na kabla ya kuendelea na shughuli yoyote nyingine, kila Kamati itamchagua Mwenyekiti wa Kamati kwa mwaka unaohusika. (2) Mwenyekiti wa Kamati, isipokuwa Kamati ya Fedha na Utawala, atachaguliwa kwa kura ya siri ya Wajumbe walio wengi kwa kupiga kura ya siri kwenye eneo la faragha litakalotengwa na Mkurugenzi kwa ajili hiyo. (3) Meya atakuwa pia Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na 31 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) Utawala. (4) Endapo nafasi ya Mwenyekiti wa Kamati itakuwa wazi katika kipindi cha mwaka husika, Mkurugenzi atatoa taarifa kwa Wajumbe wote wa Kamati kuwa katika kikao kijacho cha kawaida cha Kamati husika dondoo ya kumchagua Mwenyekiti wa Kamati kwa kipindi cha mwaka kilichosalia itakuwa ya kwanza katika agenda. Mkutano maalum wa Kamati - 49 Verify source ↗
(1) Mkutano Maalum wa Kamati utaitishwa baada ya
AI-assisted research summary: Wajumbe wawili theluthi ya Kamati wanaweza kuomba kwa maandishi mkutano maalum ufanyike na waeleze sababu; taarifa ya mkutano lazima ionyeshe tu shughuli itakayofanyika.
49.-(1) Mkutano Maalum wa Kamati utaitishwa baada ya theluthi mbili ya Wajumbe wa Kamati kuomba kwa maandishi kuwa Mkutano huo ufanyike na kueleza sababu. (2) Taarifa ya Mkutano Maalum wa Kamati itaonyesha shughuli itakayofanyika katika Mkutano huo Maalum huo na hakuna jambo jingine lolote litakalojadiliwa katika Mkutano huo. Ajenda za Kamati - 50 Verify source ↗
Mjumbe wa Kamati atakuwa na haki ya hoja zake
AI-assisted research summary: A Committee member is entitled to have their matter placed on the Committee agenda if they give notice at least four days before the meeting date.
50. Mjumbe wa Kamati atakuwa na haki ya hoja zake kuwekwa katika ajenda ya Kamati kama atatoa taarifa ya angalau siku nne kabla ya tarehe ya kikao. Mahudhurio katika Mikutano ya Kamati - 51 Verify source ↗
(1) Mjumbe wa Kamati ya Kudumu au Kamati Ndogo,
AI-assisted research summary: A committee member who missed a subcommittee meeting may not send someone else to represent them, and a council member may only attend another committee’s meeting if invited.
51.-(1) Mjumbe wa Kamati ya Kudumu au Kamati Ndogo, ambaye ameshindwa kuhudhuria Mkutano wa Kamati Ndogo, hataruhusiwa kutuma mtu mwingine kumwakilisha kwenye Mkutano wa Kamati au Kamati Ndogo. (2) Mjumbe wa Halmashauri hatakuwa na haki ya kuhudhuria kikao chochote cha Kamati au Kamati Ndogo ambamo yeye si Mjumbe, isipokuwa kama Kamati au Kamati Ndogo inayohusika imemwalika kuhudhuria, na hata hivyo hatakuwa na haki ya kupiga kura au kudai posho kwa kuhudhuria Mkutano huo wa Kamati au Kamati Ndogo. - 52 Verify source ↗
Mjumbe wa Halmashauri anayewasilisha hoja ambayo
AI-assisted research summary: A council member who submits a motion sent to committee must be notified of the committee meeting, and if they attend, they must be allowed to speak on the motion.
52. Mjumbe wa Halmashauri anayewasilisha hoja ambayo imepelekwa kwenye Kamati atapewa taarifa ya Mkutano wa Kamati ambamo hoja yake imepagwa kuzungumzwa na kama atahudhuria atapewa nafasi ya kuizungumzia. - 53 Verify source ↗
Mwenyekiti wa Kamati, Kamati ya pamoja au Kamati
AI-assisted research summary: A committee chair, joint committee, or subcommittee chair may invite any person to attend and speak at a meeting, after consulting members.
53. Mwenyekiti wa Kamati, Kamati ya pamoja au Kamati Ndogo baada ya kushauriana na Wajumbe wa Kamati, Kamati ya pamoja na Kamati Ndogo, anaweza kumwalika mtu yeyote kuhudhuria na kuzungumza kwenye Mkutano kuhusu suala lolote au 32 Mjenga hoja kualikwa kwenye Mkutano wa Kamati Waalikwa wasiokuwa Wajumbe kuhudhuria na Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) kushiriki katika Mikutano ya Kamati Mahudhurio ya umma na vyombo vya habari kwenye Mikutano ya Kamati na Kamati Ndogo Athari za nafasi wazi kwenye Kamati kushiriki kwa namna yoyote kwenye kikao cha Kamati, lakini mtu huyo atakayealikwa hatakuwa na haki ya kupiga kura kwenye Mkutano huo. - 54 Verify source ↗
Majadiliano katika Kamati, Kamati ya pamoja au Kamati
AI-assisted research summary: Committee, joint committee, and subcommittee proceedings are not open to the public or the media unless the Council resolves to allow attendance.
54. Majadiliano katika Kamati, Kamati ya pamoja au Kamati Ndogo hayatakuwa wazi kwa umma na vyombo vya habari, isipokuwa kwa kutokana na azimio la Halmashauri linaloruhusu kuwa umma na vyombo vya habari vihudhurie. - 55 Verify source ↗
(1) Kunapotokea nafasi wazi kwenye Kamati, Kamati ya
AI-assisted research summary: Kamati inaweza kuendelea kufanya kazi hata kama kuna nafasi wazi, hadi nafasi hizo zijazwe kwa uchaguzi au uteuzi.
55.-(1) Kunapotokea nafasi wazi kwenye Kamati, Kamati ya pamoja au Kamati Ndogo, Kamati itaendelea kutekeleza shughuli zake licha ya kuwepo kwa nafasi wazi hiyo au hizo au mpaka nafasi hiyo au hizo zitakapojazwa kwa njia ya uchaguzi au uteuzi. Mjumbe atakayejaza nafasi hiyo atashika nafasi wazi hiyo kwa kipindi kilichosalia cha Mjumbe ambaye nafasi yake imekuwa wazi. (2) Uhalali wa tendo lolote au maamuzi ya Mkutano wowote wa Kamati hautaathiriwa kutokana na hitilafu katika uteuzi wa Mjumbe aliyeshika nafasi hiyo au nafasi hizo kuachwa wazi na Mjumbe, au Wajumbe au Mjumbe au Wajumbe kuamua kutoka kwenye kikao kwa lengo la kukwamisha jambo linalotaka kutolewa maamuzi na Kamati hiyo. Akidi kwenye Mikutano ya Kamati Kanuni za kudumu katika Mikutano ya Kamati - 56 Verify source ↗
Endapo Wajumbe waliohudhuria Mkutano hawatafikia
AI-assisted research summary: If meeting attendees do not make quorum, the Director must adjourn the meeting and call it again within seven days; if quorum still is not met, any attending members make quorum and the meeting may continue as valid.
56. Endapo Wajumbe waliohudhuria Mkutano hawatafikia akidi ya Mkutano, Mkurugenzi ataahirisha Mkutano huo na kuuitisha tena ndani ya siku saba (7) na endapo akidi haitatimia tena, idadi yoyote ya Wajumbe waliohudhuria itatengeneza akidi ya Mkutano ambapo mkutano huo utaendelea na utakuwa halali na Mkurugenzi atamjulisha Waziri kuwepo kwa hali hiyo. - 57 Verify source ↗
(1) Kanuni ya 17 ya Kanuni hizi za Kudumu
AI-assisted research summary: Rule 17 applies, with necessary modifications, to council committee meetings. A member speaking at a committee meeting must be seated and may speak more than twice on the matter being discussed.
57.-(1) Kanuni ya 17 ya Kanuni hizi za Kudumu itatumika,baada ya kufanya marekebisho yanayostahili, kwenye Mikutano ya Kamati za Halmashauri. (2) Mjumbe anapozungumza katika Mkutano wa Kamati atakuwa ameketi na anaweza kuzungumza zaidi ya mara mbili juu ya jambo linalojadiliwa. 33 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) Upigaji kura kwenye Mikutano ya Kamati Mihtasari ya Kamati - 58 Verify source ↗
Masuala yote yanayoletwa mbele ya Kamati yataamuliwa
AI-assisted research summary: Masuala yanayoletwa mbele ya Kamati yanaamuliwa kwa kura nyingi za wajumbe waliohudhuria na kupiga kura; ikitokea kura mlingano, mwenyekiti ana kura ya turufu.
58. Masuala yote yanayoletwa mbele ya Kamati yataamuliwa kwa wingi wa kura za Wajumbe waliohudhuria na kupiga kura kwenye Mkutano husika. Endapo kunatokea kura mlingano mtu anayeongoza kikao hicho atakuwa na kura ya turufu. - 59 Verify source ↗
(1) Muhtasari wa kila Kamati, Kamati ya pamoja na Kamati
AI-assisted research summary: Muhtasari wa Kamati lazima usainiwe kwenye mkutano unaofuata na mwenyekiti wa mkutano huo.
59.-(1) Muhtasari wa kila Kamati, Kamati ya pamoja na Kamati Ndogo, utajumuisha majina ya Wajumbe waliohudhuria na wasiohudhuria, na utasainiwa kwenye Mkutano unaofuata na mtu aliyeongoza Mkutano na muhtasari uliosainiwa hivyo, kama hakuna ushahidi wa kuwa una makosa, utapokelewa kwa ushahidi bila uthibitisho zaidi. (2) Hakuna hoja au mjadala utakaoendeshwa kuhusiana na muhtasari wa Kamati isipokuwa kuhusu usahihi wa suala lolote linalohusu usahihi litatolewa kwa hoja. Kufikiriwa upya maamuzi - 60 Verify source ↗
Pale ambapo suala lililowasilishwa limeamuliwa kwa
AI-assisted research summary: A matter decided under rule 58 may not be discussed again in the same committee meeting unless a motion is supported by two-thirds of the members present and voting.
60. Pale ambapo suala lililowasilishwa limeamuliwa kwa mujibu wa Kanuni ya 58, suala hilo halitaanza kujadiliwa upya katika Mkutano huo wa Kamati isipokuwa kama hoja hiyo inaungwa mkono na theluthi mbili ya Wajumbe waliohudhuria na kupiga kura. Kutunza siri za majadiliano ya Kamati na Kamati Ndogo - 61 Verify source ↗
Mjumbe wa Kamati au Kamati Ndogo hatatoa nje jambo
AI-assisted research summary: A committee or subcommittee member must not disclose or discuss committee matters outside the committee without permission, and may not speak in the subcommittee until the committee or subcommittee has reported to the council or finished implementing the matter.
61. Mjumbe wa Kamati au Kamati Ndogo hatatoa nje jambo lolote lililoletwa au kuzungumzwa kwenye Kamati au Kamati Ndogo bila ruhusa ya Kamati hiyo, au kuzungumza kwenye Kamati Ndogo mpaka hapo Kamati hiyo au Kamati Ndogo hiyo itakapokuwa imetoa taarifa kwenye Halmashauri au itakapokuwa imekamilisha utekelezaji wa jambo hilo. Kujiuzulu wadhifa wa Mwenyekiti wa Kamati Kujiuzulu ujumbe wa Kamati na kujazwa kwa nafasi iliyowazi - 62 Verify source ↗
Mwenyekiti wa Kamati anaweza kujiuzulu wadhifa wake
AI-assisted research summary: Mwenyekiti wa Kamati anaweza kujiuzulu wadhifa wake kwa kutoa taarifa ya maandishi iliyo saini na kutumwa kwa Mkurugenzi.
62. Mwenyekiti wa Kamati anaweza kujiuzulu wadhifa wake kwa kutoa taarifa ya maandishi aliyoisaini na kutuma kwa Mkurugenzi. - 63 Verify source ↗
(1) Mjumbe yeyote wa Kamati anaweza kujiuzulu wadhifa
AI-assisted research summary: A committee member may resign by sending a signed written notice to the Director.
63.-(1) Mjumbe yeyote wa Kamati anaweza kujiuzulu wadhifa wake kwa kutoa taarifa ya maandishi aliyoisaini na kuituma kwa Mkurugenzi. (2) Nafasi inayotokana na kujiuzulu kwa Mjumbe itajazwa na Halmashauri katika kikao chake cha kawaida baada ya tarehe ya kujiuzulu kwa Mjumbe. 34 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) SEHEMU YA V UNUNUZI WA VIFAA, UPATIKANAJI WA HUDUMA NA UJENZI Taratibu za uagizaji Sura ya 290
Part
SEHEMU YA V
- 65 Verify source ↗
Kumbukumbu za majadiliano yanayohusu uagizaji
AI-assisted research summary: Kifungu hiki kinataja kumbukumbu za majadiliano yanayohusu uagizaji.
65. Kumbukumbu za majadiliano yanayohusu uagizaji - 70 Verify source ↗
Diwani au Afisa kutokuwa na maslahi kwenye Mikataba
AI-assisted research summary: Section title about a public officer not having an interest in contracts.
70. Diwani au Afisa kutokuwa na maslahi kwenye Mikataba SEHEMU YA VI MASUALA MENGINE - 64 Verify source ↗
(1) Uagizaji wa mali, huduma na ujenzi katika Halmashauri
AI-assisted research summary: Manunuzi ya mali, huduma na ujenzi katika Halmashauri lazima yafuate kanuni za manunuzi, na Bodi ya Zabuni isimamie shughuli zote za uagizaji.
64.-(1) Uagizaji wa mali, huduma na ujenzi katika Halmashauri utazingatia Kanuni za Manunuzi zilizotungwa chini ya kifungu cha 68 cha Sheria za Fedha za Serikali za Mitaa,Sura ya 290 na Sheria ya Manunuzi ya mwaka 2011. Kumbu- kumbu za majadiliano yanayohusu uagizaji (2) Kutakuwepo na Bodi ya Zabuni ambayo imeanzishwa kwa mujibu wa Kanuni za Bodi ya Zabuni (Uanzishwaji na Mwenendo) za Serikali za Mitaa na ambayo itasimamia shughuli zote za uagizaji katika Halmashauri. (3) Muhtasari wa Bodi ya Zabuni utapaswa kuwasilishwa kwenye kikao kifuatacho cha Halmashauribaada ya muhtasari huo kujadiliwa na kupitishwa kwanza na Kamati ya Fedha na Utawala. - 65 Verify source ↗
Bodi ya Zabuni ya Halmashauri itaweka kumbukumbu ya
AI-assisted research summary: Bodi ya Zabuni ya Halmashauri lazima iandae na ihifadhi kumbukumbu za mchakato wa ununuzi, itoe sehemu fulani za kumbukumbu inapoombwa chini ya masharti yaliyotajwa, na isitoe taarifa fulani za tathmini ya zabuni isipokuwa ikiwa mahakama itaelekeza hivyo.
65. Bodi ya Zabuni ya Halmashauri itaweka kumbukumbu ya majadiliano yanayohusu taratibu za ununuzi zikiwa na angalau taarifa zifuatazo:- (a) Maelezo mafupi kuhusu vitu, ujenzi au huduma iliyosababisha Bodi zinazotarajiwa kutolewa na haja kuitisha zabuni. (b) Majina na anuani ya Wazabuni waliowasilisha zabuni, maelezo kuhusu sifa au ukosefu wa sifa za wazabuni waliowasilisha zabuhi zao. (c) Bei au msingi wa upangaji wa bei na muhtasari wa masharti mengine muhimu ya kila zabuni na ya kila mkataba wa uagizaji wa mali, huduma na ujenzi. (d) Muhtasari wa tathmini na mlinganisho wa zabuni pamoja na upendeleo uliokuwepo katika tathmini hiyo. (e) Kama zabuni zilikataliwa tamko kuhusu uamuzi huo na sababu za uamuzi huo. (f) Kama utaratibu mwingine wa kupata vitu au huduma mbalimbali ya utaratibu wa zabuni ndio uliotumika, basi tamko kuhusu sababu zilizoifanya Bodi iamue kutumia utaratibu huo mwingine. (g) Kama zabuni ilikataliwa kwa kuwa mzabuni alitoa, alikubali kutoa moja kwa moja au kwa njia isiyo ya moja kwa moja, kwa mtumishi wa sasa au wa zamani wa Halmashauri, bakshishi ya aina yoyote, ahadi ya kumwajiri au kitu chochote kinachohusiana na ajira au chenye thamani, kama 35 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) hamasisho kwa utendaji au uamuzi au utaratibu wa kutumia, tamko kuhusu jambo hilo. (h) Katika upataji wa huduma, sababu na hali iliyoifanya Bodi kuchagua utaratibu wa kutumia katika upataji huo wa huduma. (i) Katika upataji wa vitu au huduma ambao Bodi imeamua kudhibiti ushiriki kwa misingi ya Taifa, Mkoa au Wilaya, tamko kuhusu sababu na hali iliyofanya Bodi kudhibiti ushiriki huo. (j) Katika upataji wa vifaa na huduma kwa kuwaomba watoaji kutoa mapendekezo yao moja kwa moja tamko la sababu na hali iliyofanya Bodi kuamua kutumia utaratibu huo, na (k) Muhtasari wa maombi yoyote ya ufafanuzi kuhusu mchujo wa zabuni au nyaraka za zabuni na majibu yaliyotolewa pamoja na muhtasari wa marekebisho yoyote yaliyofanywa katika nyaraka hizo. (2) Sehemu ya kumbukumbu zilizotajwa kwenye Kanuni Ndogo ya (1) (a) na (b) ya Kanuni hii zitatolewa, kama zikiombwa, kwa mtu yeyote baada ya zabuni kutangazwa, kufunguliwa na kukubaliwa, au baada ya kusimamishwa kwa taratibu za uagizaji bila ya kuingia katika mkataba wa uagizaji. (3) Sehemu ya kumbukumbu zilizoelekezwa katika Kanuni Ndogo ya (1) (c) hadi (g) ya Kanuni hii kama itaombwa, itatolewa kwa wazabuni waliowasilisha zabuni baada ya zabuni kukubaliwa au baada ya kusitishwa bila ya kuingia kwenye mkataba wa utoaji wa vitu au huduma. (4) Isipokuwa kama itaelekezwa hivyo na mahakama yenye mamlaka na kutegemeana na masharti ya maelekezo hayo, Bodi haitatoa habari- (a) kama utoaji huo wa habari utakuwa kinyume cha Sheria; utazuia utekelezaji wa Sheria; hautakuwa na maslahi kwa umma; utahatarisha maslahi halali ya kibiashara ya wahusika au utazuia ushindani halali; na; (b) habari zinazohusu uchambuzi, tathmini na ulinganisho wa zabuni pamoja na bei mbali ya muhtasari ulioelezwa kwenye Kanuni Ndogo ya (1) (e) ya Kanuni hizi. 36 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (5) Mara baada ya zabuni kujadiliwa na Bodi, Katibu atamjulisha Mzabuni aliyefanikiwa ili makubaliano ya nyaraka za mkataba yaweze kufikiwa. (6) Nakala za muhtasari zitapelekwa kwa siri kwa kila Mjumbe wa Bodi, Mkurugenzi, Mweka Hazina, Mkaguzi wa Ndani na Mkuu wa Idara husika kwa taarifa na kumbukumbu. (7) Kila mzabuni ambaye hakufanikiwa atajulishwa na akiomba sababu za kutokubaliwa kwa zabuni yake atapaswa kupewa sababu. (8) Bodi ya Zabuni kwa kuzingatia masharti ya Kanuni za uagizaji itaandaa taarifa ya mwenendo na maamuzi ya zabuni zilizoitishwa na kuwasilishwa kwenye Mkutano wa kawaida wa Halmashauri kupitia Kamati ya Kudumu husika. - 66 Verify source ↗
Katika mkataba wowote wa kimaandishi, yatawekwa
AI-assisted research summary: In any written contract, terms must be included giving Halmashauri the right to end the contract and claim compensation if the contractor engages in bribery-related conduct.
66. Katika mkataba wowote wa kimaandishi, yatawekwa maneno ambayo yataonyesha kuwa Halmashauri itakuwana haki kusitisha mkataba na kumdai Mkandarasi malipo ya fidia kutokana na kusimamishwa kwa mkataba huo endapo Mkandarasi atabainika kuwa ameahidi kutoa au ametoa, au amekubali kutoa kwa mtu yeyote zawadi yoyote au upendeleo wa aina yoyote kama kishawishi au zawadi kwa kufanya au kumpendelea au kutomkubali mtu yeyote kuhusiana na mkataba na Halmashauri au kama vitendo hivyo vitakuwa vimefanywa na mtumishi yeyote aliyeajiriwa naye au kwa niaba yake iwe Mkandarasi anafahamu au hafahamu atakuwa ametenda kosa chini ya Sheria ya Kuzuia na Kudhibiti Rushwa ya mwaka 2007. Uzuiaji wa rushwa Usimamiaji wa mikataba - 67 Verify source ↗
(1) Mkurugenzi wa Halmashauri atawajibika katika
AI-assisted research summary: The Municipal Director must properly supervise and monitor contracts, and contract changes and payments are restricted until stated conditions are met.
67.-(1) Mkurugenzi wa Halmashauri atawajibika katika usimamiaji na ufuatiliaji mzuri wa Mikataba. (2) Mkataba wa upataji vitu hautabadilishwa kwa namna yoyote ile baada ya kutiwa saini na pande zonazohusika isipokuwa kama mabadiliko hayo ni- (a) kwa faida ya Halmashauri na hayailetei hasara Halmashauri; (b) yamethibitishwa na Bodi ya zabuni ya Halmashauri; na (c) Upande mwingine unaafiki. (3) Malipo ya mwisho hayatafanywa mpaka mkataba mzima utakapokuwa umekamilika kutokana na kuridhika kwa Halmashauri na kulingana na vipengele vya mkataba unaohusika. 37 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) Uvunjaji wa mkataba Rejesta ya mikataba (4) Malipo ya fedha za salio hayatalipwa mpaka upite muda wa miezi sita na kazi iwe haina kasoro. - 68 Verify source ↗
Pale ambapo mkataba uliotiwa
AI-assisted research summary: If the contractor has not complied with the council-sealed contract, the Director must consult the Finance and Administration Committee as soon as possible and then inform the contractor of the decision.
68. Pale ambapo mkataba uliotiwa lakiri/muhuri na Halmashauri haukufuatwa na mkandarasi, ikiwa ni pamoja na ucheleweshaji usiokuwa wa kimsingi, Mkurugenzi atashauriana mapema iwezekanavyo na Kamati ya Fedha na Utawala kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa kwenye mkataba, itaamua hatua muafaka za kuchukua na kumfahamisha Mkandarasi juu ya uamuzi. - 69 Verify source ↗
(1) Mkurugenzi atatunza maelezo yote ya mikataba kwenye
AI-assisted research summary: Mkurugenzi lazima atunze rejesta ya mikataba na kulinganisha malipo halisi na malipo yaliyoidhinishwa.
69.-(1) Mkurugenzi atatunza maelezo yote ya mikataba kwenye rejesta ya mikataba na atafanya ulinganifu wa malipo halisi na yale yaliyoidhinishwa. (2) Taarifa ya matumizi yote ya ziada lazima yapelekwe kwenye Bodi ya Zabuni yakiambatana na maelezo kutoka kwa Mkurugenzi. Diwani/ Afisa kutokuwa na maslahi katika mikataba - 70 Verify source ↗
(1) Endapo Diwani au Afisa wa Halmashauri ana maslahi
AI-assisted research summary: Diwani au Afisa wa Halmashauri mwenye maslahi ya kifedha katika mkataba au jambo analojadiliwa lazima atangaze maslahi hayo na asishiriki katika majadiliano au kupiga kura.
70.-(1) Endapo Diwani au Afisa wa Halmashauri ana maslahi ya kifedha ya moja kwa moja au vinginevyo katika mkataba wowote, mkataba unaopendekezwa au jambo lolote, na yupo kwenye Mkutano wa Halmashauri au Kamati ambapo mkataba huo, au mkataba unaopendekezwa au jambo lingine lolote linajadiliwa, atatangaza jambo hilo mara Mkutano utakapokuwa umeanza na hatashiriki wala kuwepo katika majadiliano au kupiga kura kuhusu jambo linalohusu mkataba au mkataba unaopendekezwa au jambo lingine lolote ambalo ana maslahi nalo. (2) Kanuni hii haitatumika kuhusiana na maslahi katika mkataba au suala lingine ambalo Mjumbe au Afisa wa Halmashauri ana maslahi nalo kama mlipa kodi au mkazi katika eneo lililo katika himaya ya Halmashauri. (3) Diwani atahesabika kuwa na maslahi ya moja kwa moja katika mkataba au jambo jingine endapo- (a) (b) yeye au mtu aliyemchagua ni Mjumbe wa kampuni au chombo kingine au anayo hati ya hisa katika kampuni ambayo itaingia, au imependekezwa iingie katika mkataba, au anao uhusiano wa kifedha katika jambo linalojadiliwa; au yeye ni mbia au ameajiriwa na mtu ambaye mkataba unafanywa naye, au utakuwa chini yake, au anao uhusiano wa kifedha wa moja kwa moja katika suala linalojadiliwa au kuzungumzwa. 38 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (4) Katika Kanuni hii maslahi ya moja kwa moja na yasiyo ya moja kwa moja ya mwanandoa au ndugu wa familia kama inafahamika kwa Mjumbe wa Halmashauri itachukuliwa kuwa ni maslahi ya moja kwa moja au yasiyo ya moja kwa moja. (5) Taarifa ya jumla itakayotolewa kwa Mkurugenzi na Diwani au Afisa wa Halmashauri kuhusiana na yeye, mkewe, mumewe au ndugu yake kwamba ana maslahi ya moja kwa moja au yasiyo ya moja kwa moja katika mkataba unaokusudiwa au jambo lingine na akieleza aina ya maslahi itachukuliwa, isipokuwa pale atakapoondoa taarifa hiyo, kuwa ametoa taarifa ya kutosha ya maslahi yake kuhusiana na suala ambalo limo katika mjadala. (6) Mkurugenzi ataandika taarifa za watu wenye maslahi waliotoa taarifa chini ya Kanuni Ndogo ya (1) na taarifa yoyote iliyomo katika Kanuni Ndogo ya (5) itakuwa wazi kwa ukaguzi wakati wa saa za kazi. (7) Halmashauri inaweza baada ya kupata kibali cha Waziri, kuondoa kizuizi chini ya Kanuni hii kinachoifanya ishindwe wakati wowote kufanya Mkutano pale ambapo idadi ya Wajumbe wenye maslahi ni kubwa mno kiasi cha kukwamisha shughuli za Halmashauri au itakuwa ni kwa maslahi ya wakazi wa Halmashauri kuondoa kikwazo hicho. (8) Katika Kanuni za Kudumu hizi ,ndugu wa familia itachukuliwa kuwa ni pamoja na baba, mama, mtoto, kaka, au dada na wanandoa wao. SEHEMU YA VI MASUALA MENGINE Kiapo na kukubali wadhifa
Part
SEHEMU YA VI
- 72 Verify source ↗
Majukumu ya Diwani
AI-assisted research summary: Section 72 is titled “Majukumu ya Diwani” (councilor duties).
72. Majukumu ya Diwani 3 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) - 78 Verify source ↗
Diwani kutembelea maeneo, shughuli mbalimbali za ujenzi
AI-assisted research summary: Section title about councillor visits to areas and various construction activities.
78. Diwani kutembelea maeneo, shughuli mbalimbali za ujenzi - 82 Verify source ↗
Uteuzi wa Wajumbe kwenye Taasisi za nje
AI-assisted research summary: This section concerns the appointment of members to external institutions.
82. Uteuzi wa Wajumbe kwenye Taasisi za nje - 83 Verify source ↗
Kumwondoa Meya/Mwenyekiti madarakani
AI-assisted research summary: This section is titled “Kumwondoa Meya/Mwenyekiti madarakani” and appears in Part VII on allowances for members.
83. Kumwondoa Meya/Mwenyekiti madarakani SEHEMU YA VII POSHO KWA WAJUMBE - 71 Verify source ↗
Kila Diwani kabla ya kushika wadhifa wake kama Diwani
AI-assisted research summary: Before taking office and before the first council meeting, each councillor must take an oath and give a written declaration to the Director.
71. Kila Diwani kabla ya kushika wadhifa wake kama Diwani na kabla ya Mkutano wa kwanza wa Halmashauri:- (a) atakula kiapo kama kilivyoonyeshwa kwenye nyongeza ya kwanza ya Kanuni hizi za kudumu kitakachosimamiwa na Hakimu Mkazi au Hakimu wa Wilaya; na (b) atatoa tamko la kimaandishi lililoandikwa kwa Mkurugenzi akiahidi kutekeleza jambo linalohusiana na tamko la maslahi katika shughuli za kibiashara, mali, na kadhalika na kuzifuata Kanuni za Maadili ya Madiwani. 39 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) Majukumu ya Diwani - 72 Verify source ↗
(1) Diwani atakuwa na majukumu yafuatayo
AI-assisted research summary: The councilor must stay close to voters, attend council and committee meetings, meet residents at least one day each month, report council decisions to voters, contribute expertise in discussions, join local development activities, and follow public interest, law, and ethics rules while doing these duties.
72.-(1) Diwani atakuwa na majukumu yafuatayo:- (a) kuwa karibu na wapiga kura na kupata ushauri wa Wananchi katika mambo yanayotarajiwa kujadiliwa kwenye Halmashauri. (b) kutoa maoni na mapendekezo ya wananchi kwa (c) (d) (e) Halmashauri. kuhudhuria Mikutano ya Halmashauri na ya Kamati au Kamati Ndogo ambamo yeye ni Mjumbe. kutenga angalau siku moja kila mwezi kukutana na wananchi katika eneo lake la uchaguzi. kutoa taarifa kwa wapiga kura kuhusu maamuzi ya jumla ya Halmashauri na hatua zilizochukuliwa na Halmashauri kuondoa matatizo yaliyowahi kuelezwa na wakazi wa eneo lake la uchaguzi. (f) kuchangia ujuzi na uzoefu wake katika majadiliano yanayofanyika katika Mikutano ya Halmashauri na Kamati za Halmashauri, na (g) kushiriki katika shughuli za pamoja za maendeleo katika eneo lake la uchaguzi na katika eneo zima la Halmashauri. (2) Katika kutekeleza wajibu wake diwani atazingatia- (a) Maslahi ya Taifa na maslahi ya Wananchi katika eneo la Halmashauri; (b) Katiba, Sheria na Kanuni; (c) Kanuni za Maadili ya Madiwani, Mwongozo juu ya mahusiano ya Madiwani na Watumishi na miiko mingine. Nafasi wazi - 73 Verify source ↗
(1) Kiti cha Mjumbe wa Halmashauri kitakuwa wazi
AI-assisted research summary: Kiti cha Mjumbe wa Halmashauri huwa wazi ikiwa kuna sababu zilizoorodheshwa, na Waziri anatangaza uwazi wa kiti baada ya kupokea taarifa ya maandishi kutoka kwa Meya.
73.-(1) Kiti cha Mjumbe wa Halmashauri kitakuwa wazi endapo Mjumbe- (a) (b) (c) (d) (e) (f) amefariki; anakubali ajira kama mtumishi wa Halmashauri; kwa mujibu wa Sheria yoyote anatangazwa kuwa hana akili timamu; yuko chini ya hukumu ya kifo au kifungo kinachozidi miezi sita kilichotolewa kwake na mahakama; kwa mujibu wa Sheria yoyote anatamkwa kuwa anapoteza sifa za kuendelea kuwa Mjumbe; atakoma kuwa mwanachama wa chama cha siasa 40 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (g) (h) kilichompendekeza kuwa mgombea wa kiti cha udiwani; anapokuwa amepatikana na kosa kutokana na Kanuni za Maadili ya Madiwani na adhabu ya kosa alilotenda ni pamoja na kumwondoa Mjumbe madarakani; na anapoteza ujumbe kwa mujibu wa Kanuni ya 71 (2) ya Kanuni hizi za kudumu; anahukumiwa kwa kosa la kutotaja maslahi yake. amejiuzulu kutoka kiti chake; (i) (j) (k) Halmashauri imevunjwa na kuathiri mipaka ya majimbo ya uchaguzi; uchaguzi wa Mjumbe umetangazwa kuwa batili;au (l) (m) bila sababu ya kuridhisha au bila idhini au kibali cha maandishi cha Mwenyekiti, Mjumbe anakosa kuhudhuria Mikutano mitatu ya kawaida inayofuatana ya Halmashauri au Kamati ambamo yeye ni Mjumbe. (2) Waziri atatangaza kiti kuwa wazi pale atakapojulishwa na Meya kwa maandishi kwamba kiti kiko wazi kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 42 (1) cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Sura ya 288. Kutokuwe po kwa Wajumbe - 74 Verify source ↗
(1) Halmashauri yaweza kutoa idhini ya kutokuwepo katika
AI-assisted research summary: Halmashauri inaweza kuidhinisha Mjumbe asihudhurie Mikutano yake kwa muda usiozidi miezi kumi ikiwa anataka kwenda nje ya Tanzania; akikaa nje ya nchi zaidi ya miezi kumi, kiti chake cha udiwani huchukuliwa kuwa wazi.
74.-(1) Halmashauri yaweza kutoa idhini ya kutokuwepo katika Mikutano yake kwa muda usiozidi miezi kumi kwa Mjumbe yeyote anayetaka kwenda nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (2) Pale ambapo Mjumbe kwa sababu yoyote ile amekuwa nje ya nchi kwa muda unaozidi miezi kumi kiti chake cha udiwani kitachukuliwa kuwa kipo wazi. Taratibu za kutunga Sheria Ndogo - 75 Verify source ↗
(1) Pale ambapo Halmashauri inakusudia kutunga Sheria
AI-assisted research summary: Halmashauri must notify local residents and invite written objections or suggestions before making by-laws; after making them, the by-laws are sent to the Minister for approval and must be published in the Government Gazette before they start to apply.
75.-(1) Pale ambapo Halmashauri inakusudia kutunga Sheria Ndogo itatoa tangazo kwa wakazi wa eneo husika kuhusu kusudio hilo katika namna ambayo itahakikisha kuwa watakaoathirika na Sheria Ndogo inayokusudiwa kutungwa wanafahamu vilivyo na kuwaomba wanaopenda kutoa pingamizi lolote au mapendekezo yao kwa maandishi katika muda uliowekwa. (2) Pale ambapo baada ya muda wa taarifa kumalizika hakuna pingamizi au malalamiko yaliyowasilishwa, au hakuna mtu yeyote aliyetoa kipingamizi kinachokubalika mbele ya Halmashauri, ikizingatia itaendelea kutunga Sheria Ndogo Halmashauri malalamiko na pingamizi zilizotolewa. 41 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (3) Sheria Ndogo zikishatungwa na Halmashauri zitapelekwa kwa Waziri ili aweze kuziidhinisha. (4) Waziri anaweza kuidhinisha, kukubali au kukataa kuidhinisha Sheria Ndogo au kutoa au kusimamisha kibali chake kwa kutoa masharti atakayoyaeleza na anaweza baada ya kutoa idhini yake, kupanga tarehe ya kuanza kutumika kwa Sheria Ndogo hizo. (5) Waziri anaweza, kabla ya kuidhinisha Sheria Ndogo zenye athari kwenye maeneo yaliyotengwa au maeneo maalum au kwa Sheria nyingine yoyote, kushauriana na Waziri anayehusika na Sheria husika au na jambo lililotungiwa Sheria Ndogo kadri itakavyokuwa. (6) Sheria Ndogo yoyote iliyotungwa na Halmashauri lazima itangazwe katika Gazeti la Serikali kabla ya kuanza kutumika. Ukaguzi wa nyaraka - 76 Verify source ↗
(1) Mjumbe ataweza, kwa madhumuni ya kutekeleza
AI-assisted research summary: Mjumbe anaweza kukagua waraka wa Kamati ya Halmashauri kwa ajili ya kutekeleza wajibu wake, na anaweza kupewa nakala ikiwa zinapatikana na akiomba; lakini hapaswi kukagua au kuomba nakala ya waraka unaohusu jambo analo maslahi nalo.
76.-(1) Mjumbe ataweza, kwa madhumuni ya kutekeleza wajibu wake kama Mjumbe, na si vinginevyo, kukagua waraka wowote ambao umejadiliwa na Kamati ya Halmashauri na kama nakala zinapatikana, anaweza kupewa, akiomba, nakala kwa madhumuni hayo hayo. (2) Mjumbe hatakagua kwa makusudi au kutaka apewe nakala ya waraka wowote unaohusu jambo ambalo yeye ana maslahi nalo kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji), Sura ya 288. Hata hivyo Kanuni hii haitamzuia Mkurugenzi kuzuia kukaguliwa kwa waraka wowote ambao umezuiliwa kutolewa kwa mujibu wa Sheria yoyote au Kanuni zilizotungwa chini ya Sheria hizo. Uanzishaji wa Bodi za Huduma - 77 Verify source ↗
(1) Halmashauri inaweza, kwa mujibu wa kifungu 88 cha
AI-assisted research summary: Halmashauri inaweza kuunda Bodi za Huduma kwa hati rasmi iliyotangazwa kwenye Gazeti la Serikali, ikiwa inaona inafaa na kwa mujibu wa kifungu 88 kilichotajwa.
77.-(1) Halmashauri inaweza, kwa mujibu wa kifungu 88 cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji), Sura ya 288 kwa madhumuni ya kutekeleza kazi zake katika eneo lililo chini ya mamlaka yake, kuunda Bodi za Huduma kwa hati rasmi iliyotangazwa kwenye Gazeti la Serikali, kama itakavyoona inafaa kufanya hivyo. (2) Bodi ya Huduma iliyotajwa katika Kanuni Ndogo ya (1) ya Kanuni hizi itawajibika moja kwa moja kwenye Halmashauri kupitia itatekeleza kazi zake kama Kamati ya Kudumu husika na ilivyofafanuliwa katika hati inayoianzisha. 42 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) Diwani kutembelea maeneo, shughuli mbalimbali za ujenzi n.k - 78 Verify source ↗
(1) Mjumbe wa Halmashauri anaweza kutembelea eneo,
AI-assisted research summary: A council member may visit certain sites and report to the Director, but may not give technical instructions on site.
78.-(1) Mjumbe wa Halmashauri anaweza kutembelea eneo, jengo au shughuli za ujenzi zinazotekelezwa na au kwa niaba ya Halmashauri na anaweza kutuma taarifa kwa Mkurugenzi akieleza sababu za matembezi yakeili aweze kupangiwa Wataalam wa mradi au shughuli husika kwa ajili kupata maelekezo ya kitaalam. (2) Mjumbe wa Halmashauri anapotembelea shughuli au miradi ya maendeleo inayotekelezwa na au kwa niaba ya Halmashauri hataruhusiwa kutoa maelekezo au maagizo ya kitaalam awapo kwenye eneo la mradi. (3) Baada ya diwani kutembelea maeneo au majengo kama ilivyoainishwa kwenye Kanuni Ndogo ya (1) ya Kanuni hii anaona kuna umuhimu wa kutoa maoni au mang’amuzi yake juu ya matembezi hayo atafanya hivyo kwa kuwasilisha maoni au mang’amuzi yake kwa Mkurugenzi ambaye atafanyia kazi au kuyapeleka kwa afisa anayesimamia kazi husika kwa utekelezaji; (4) Endapo maoni au mang’amuzi ya Diwani hayawezi kufanyiwa kazi na Mkurugenzi au Afisa mhusika, basi atamshauri diwani kupeleka maoni na mang’amuzi yake kwa Kamati inayohusika ili yachunguzwe zaidi na kuamuliwa. (5) Kamati za Kudumu za Halmashauri zinaweza kutembelea miradi ya maendeleo au shughuli yoyote inayotekelezwa na au kwa niaba ya Halmashauri ili mradi katika kutembelea miradi hiyo Kamati itaongozana na Wataalam wa mradi au shughuli husika ili kupata maelekezo ya kitaalam. Uhifadhi wa Lakiri ya Halma- shauri Utiaji muhuri kwenye nyaraka (6) Kamati ya Kudumu itatembelea miradi au shughuli za maendeleo kabla ya Kikao cha Kamati ambacho kitajadili mradi au shughuli hiyo. - 79 Verify source ↗
Lakiri ya Halmashauri
AI-assisted research summary: Lakiri ya Halmashauri lazima itunzwe kwa usalama na kuwekwa chini ya kufuli katika Kasiki kwenye ofisi ya Mkurugenzi.
79. Lakiri ya Halmashauri itatunzwa kwa usalama na kufungiwa katika Kasiki kwenye Ofisi ya Mkurugenzi mwenyewe. - 80 Verify source ↗
(1) Lakiri ya Halmashauri haitabandikwa katika Hati
AI-assisted research summary: Lakiri ya Halmashauri haiwezi kuwekwa kwenye hati yoyote mpaka iwe imeidhinishwa na azimio la Halmashauri.
80.-(1) Lakiri ya Halmashauri haitabandikwa katika Hati yoyote mpaka ubandikaji huo umeidhinishwa na azimio la Halmashauri likiidhinisha kukubaliwa kwa zabuni, ununuzi, uuzaji au upangishaji au kuchukua mali yoyote, utoaji wa Hati yoyote ya ukopeshaji fedha, uwasilishaji wa madai yoyote, uwekaji wa viwango vya kodi, uingiaji kwenye mkataba, kutunga Sheria Ndogo, 43 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) au hati yotote iliyo rasmi ambayo kwa mujibu wa Sheria au Kanuni yoyote inahitaji kuwekwa lakiri ya Halmashauri. (2) Lakiri itashuhudiwa au kuthibitishwa na Meya au Naibu Meya na Mkurugenzi, na hati zilizowekwa lakiri zitasainiwa na Meya au Naibu Meya, kama hali itakavyokuwa. Uandiki- shaji wa anuani - 81 Verify source ↗
(1) Itakuwa wajibu wa kila Mjumbe katika kikao cha
AI-assisted research summary: Members must give the Director a written notice of their permanent address at the first Council meeting after election.
81.-(1) Itakuwa wajibu wa kila Mjumbe katika kikao cha kwanza cha Halmashauri, baada ya uchaguzi kutoa taarifa ya maandishi kwa Mkurugenzi juu ya anuani yake ya kudumu ya kupokelea taarifa. Taarifa zilizopelekwa kwa kutumia anuani iliyoandikishwa itachukuliwa kama ndiyo sahihi na inatosheleza kwa matumizi yote. (2) Iwapo Mjumbe atatoa taarifa ya maandishi kwa Mkurugenzi kuwa angependa taarifa ya Mikutano ya Halmashauri iwe inatumwa kwake kwa kutumia anuani atakayoitaja kwenye taarifa hiyo ambayo ni tofauti na ile katika Kanuni Ndogo ya (1), taarifa yoyote itakayoachwa au itakayotumwa kwa njia ya posta kwa kutumia anwani hiyo itachukuliwa kuwa inatosha kwa ajili ya kutoa taarifa inayotakiwa kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu hizi. Uteuzi wa Wajumbe kwenye taasisi za nje - 82 Verify source ↗
(1) Katika Mkutano wake wa kwanza, Halmashauri itateua
AI-assisted research summary: Halmashauri lazima katika mkutano wake wa kwanza iteue wawakilishi wake kwenye Bodi na taasisi za nje, na wawakilishi hao lazima watoe taarifa kwa Mkurugenzi kuhusu shughuli zinazoathiri sera na maslahi ya Halmashauri na wakazi wake; Mkurugenzi achukue hatua zifaazo.
82.-(1) Katika Mkutano wake wa kwanza, Halmashauri itateua wawakilishi wake kwenye Bodi na Taasisi za nje ambazo Halmashauri inastahili kuwakilishwa. (2) Mjumbe au Wajumbe, wanaoiwakilisha Halmashauri kwenye Bodi na Taasisi za nje, watatakiwa kuwasilisha kwa Mkurugenzi taarifa kuhusu shughuli za Bodi au Taasisi zinazogusa Sera na maslahi ya Halmashauri na wakazi wake kijumla na Mkurugenzi atachukua hatua zifaazo. Kumwondoa Meya madarakani - 83 Verify source ↗
(1) Halmashauri inaweza kumwondoa Meya madarakani
AI-assisted research summary: Halmashauri inaweza kumwondoa Meya madarakani ikiwa azimio linaungwa mkono na theluthi mbili ya Wajumbe na kuna sababu zilizoainishwa.
83.-(1) Halmashauri inaweza kumwondoa Meya madarakani kwa azimio linaloungwa mkono na theluthi mbili ya Wajumbe kutokana na hoja au sababu yoyote kati ya sababu zifuatazo:- (a) Kutumia nafasi yake vibaya; (b) Kushiriki katika vitendo vya rushwa; (c) Kushindwa kutekeleza majukumu yake (d) Mwenendo mbaya au ukosefu wa adabu; au (e) Ulemavu wa kimwili au kiakili kwa kiasi cha kumfanya kushindwa kutekeleza majukumu yake kama Meya. (2) Hoja au sababu zitakazotolewa lazima iwe imetimizamasharti yafuatayo: 44 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (i) Iwe na tuhuma mahsusi yenye ushahidi wa kutosha (ii) Iwe imetolewa maelezo kamili na yenye kueleweka kuhusu tuhuma zinazohusika. (3) Kwa madhumuni ya kumwondoa Meya madarakani, kwa sababu zozote zilizotamkwa chini ya Kanuni Ndogo ya (1) ya Kanuni hii, Halmashauri itatumia taratibu zilizotolewa katika Taratibu za Kumwondoa Meya zilizotangazwa kwenye gazeti la Serikali na Waziri kwa mujibu wa Sheria. SEHEMU YA VII POSHO KWA WAJUMBE Aina za posho
Part
SEHEMU YA VII
- 85 Verify source ↗
Posho endapo Mkutano utaahirishwa
AI-assisted research summary: This section is about what happens if a meeting is adjourned.
85. Posho endapo Mkutano utaahirishwa SEHEMU YA VIII MABADILIKO KWENYE KANUNI ZA KUDUMU - 84 Verify source ↗
(1) Wajumbe wa Halmashauri watalipwa posho mbalimbali
AI-assisted research summary: Council members are to be paid allowances approved by the Minister, and the Council must pay a member’s medical costs if the member falls ill or is injured while doing work assigned by the Council.
84.-(1) Wajumbe wa Halmashauri watalipwa posho mbalimbali kama itakavyopendekezwa na Halmashauri na kuidhinishwa na Waziri. (2) Posho zitakazolipwa kwa Wajumbe wa Halmashauri zitakuwa za aina zifuatazo- (a) Posho ya usafiri; (b) Posho ya kuhudhuria kikao; (c) Posho ya madaraka; (d) Posho ya kujikimu; (e) Posho ya mwezi. (f)Kiinua mgongo (3) Endapo Mjumbe wa Halmashauri ataugua au ataumia wakati akifanya kazi aliyotumwa na Halmashauri, gharama za matibabu yake zitalipwa na Halmashauri. Posho endapo Mkutano utaahiri- shwa - 85 Verify source ↗
Endapo Mkutano wa Halmashauri au Kamati utaahirishwa
AI-assisted research summary: If a council or committee meeting is adjourned for lack of quorum, attending members may be paid the amounts set out in rule 84(2)(a) and (d), but no sitting allowance is paid in that case.
85. Endapo Mkutano wa Halmashauri au Kamati utaahirishwa kwa sababu ya kukosekana kwa akidi, Mjumbe au Wajumbe waliofika kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano huo ulioahirishwa watastahili malipo yaliyotajwa katika Kanuni ya 84 (2) (a) na (d) iwapo wamelazimika, bila kukusudia, kulala njiani au kwenye Makao makuu ya Halmashauri. Hakuna malipo ya posho ya kuhudhuria kikao yatakayofanywa katika hali ya namna hiyo. SEHEMU YA VIII MABADILIKO KWENYE KANUNI ZA KUDUMU Kusitisha utumiaji wa Kanuni za
Part
SEHEMU YA VIII
- 86 Verify source ↗
Kusitisha utumiaji wa Kanuni za kudumu
AI-assisted research summary: Sehemu hii ina kichwa cha ‘Kusitisha utumiaji wa Kanuni za kudumu’.
86. Kusitisha utumiaji wa Kanuni za kudumu - 87 Verify source ↗
Marekebisho na mabadiliko ya Kanuni za Kudumu
AI-assisted research summary: Section title about amendments and changes to the Permanent Regulations.
87. Marekebisho na mabadiliko ya Kanuni za Kudumu - 88 Verify source ↗
Kanuni za Kudumu kutolewa kwa Wajumbe
AI-assisted research summary: This section is titled as rules to be issued to members.
88. Kanuni za Kudumu kutolewa kwa Wajumbe - 91 Verify source ↗
Wimbo wa Taifa,Dua na sala ya kuiombea Halmashauri
AI-assisted research summary: Section heading on the national anthem, prayers, and a prayer for the council.
91. Wimbo wa Taifa,Dua na sala ya kuiombea Halmashauri - 92 Verify source ↗
Kufuta Kanuni zilizopo
AI-assisted research summary: Sehemu hii inaeleza sababu na msingi wa Kanuni hizi za kudumu, na kwamba zinaweka utaratibu wa Halmashauri kuendesha mikutano na shughuli zake.
92. Kufuta Kanuni zilizopo. 4 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) SEHEMU YA I MASHARTI YA MWANZO KWA KUWA kauli-mbiu ya Halmashauri ni kuendesha shughuli kwa namna inayozingatia demokrasia, ufanisi, tija, ushirikishwaji, uwazi na uwajibikaji; jukumu NA KWA KUWA la Halmashauri ni kuimarisha demokrasia katika ngazi zote na kutoa huduma kwa wananchi kwa kuzingatia ufanisi, usawa, haki na kwa namna inayochochea maendeleo ya maeneo yaliyo chini ya mamlaka ya Halmashauri kwa kuwashirikisha wananchi; NA KWA KUWA madhumuni ya Kanuni hizi za kudumu ni kuweka utaratibu wa namna Halmashauri itakavyoendesha Mikutano na shughuli zake kwa kuzingatia misingi ya utawala bora; SASA BASI, Kanuni hizi za kudumu zinaelekeza ifuatavyo; Jina na tarehe ya Kuanza kutumika - 86 Verify source ↗
(1) Kanuni yoyote
AI-assisted research summary: Halmashauri inaweza kusitisha Kanuni kwa azimio la theluthi mbili ya Wajumbe waliopo, kwa hoja bila taarifa ya siku 45, ili kurahisisha shughuli za dharura au zenye manufaa; lakini haiwezi kufanya hivyo kama kusitisha kutasababisha ukiukaji wa sheria au kushindwa kutimiza wajibu wa kisheria.
86.-(1) Kanuni yoyote inaweza kusitishwa kwa azimio lililoungwa mkono na theluthi mbili za Wajumbe waliohudhuria Mkutano wa Halmashauri kwa hoja iliyopendekezwa bila taarifa 45 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) Kudumu kwa madhumuni ya kuwezesha shughuli yoyote iliyofafanuliwa ili ishughulikiwe na Halmashauri kama jambo la dharura au lenye manufaa. Marekebi- sho na mabadiliko ya Kanuni za Kudumu Kanuni za Kudumu kutolewa kwa Wajumbe Kutafsiri Kanuni za Kudumu Ziara za Wajumbe (2) Halmashauri haitasitisha matumizi ya Kanuni yoyote kama kusitisha huko kutasababisha kufanya jambo ambalo limezuiliwa na Sheria au kutofanya jambo linalotakiwa kufanywa chini ya Sheria yoyote. - 87 Verify source ↗
Halmashauri inaweza kubadilisha, kuongeza, kurekebisha
AI-assisted research summary: Halmashauri inaweza kubadilisha, kuongeza, kurekebisha au kutengua Kanuni hizi za kudumu kwa kuunga mkono azimio kwa kura zisizopungua theluthi mbili na kwa kupata idhini ya Waziri.
87. Halmashauri inaweza kubadilisha, kuongeza, kurekebisha au kutengua Kanuni hizi za kudumu kwa azimio lililoungwa mkono kwa wingi usiopungua theluthi mbili ya kura na baada ya kupata idhini ya Waziri. - 88 Verify source ↗
Nakala
AI-assisted research summary: Mkurugenzi lazima atoe nakala iliyochapishwa ya Kanuni hizi kwa kila Mjumbe.
88. Nakala iliyochapishwa ya Kanuni za Kudumu hizi zitatolewa na Mkurugenzi kwa kila Mjumbe. - 89 Verify source ↗
Uamuzi wa Meya kuhusu maana ya matumizi ya Kanuni
AI-assisted research summary: The Mayor’s decision on the meaning of these Regulations or on the conduct of a Council Meeting cannot be challenged during any Council Meeting.
89. Uamuzi wa Meya kuhusu maana ya matumizi ya Kanuni hizi au mwenendo wa Mkutano wa Halmashauri hautapingwa wakati wa Mkutano wowote wa Halmashauri. SEHEMU YA IX ZIARA ZA WAJUMBE
Part
SEHEMU YA I
- 1 Verify source ↗
Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya
AI-assisted research summary: Kanuni hizi zinaitwa Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea za Mwaka 2016, na huanza kutumika mara baada ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali.
1. Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea za Mwaka 2016 na zitaanza kutumika mara baada ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali; Tafsiri - 2 Verify source ↗
Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama maelezo haya yatahitajika
AI-assisted research summary: Section 2 defines the key terms used in these Rules, including local officials, quorum, council bodies, voting terms, and officeholders.
2. Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama maelezo haya yatahitajika vinginevyo; “Afisa wa Serikali za Mitaa” maana yake ni mtu ambaye ameajiriwa na au ambaye yumo katika Utumishi wa Mamlaka ya Serikali za Mitaa na ambaye anashika au anakaimu katika nafasi ya menejimenti; “Akidi” ni idadi ya Madiwani itakayokamilika baada ya kujiorodhesha katika rejesta ya Mahudhurio ya Mkutano ambayo itaruhusu kufanya maamuzi ya Mkutano kwa mujibu wa Kanuni za 9, 49 na 56; “Chama” ni chama cha siasa chenye uwakilishi katika Baraza la Madiwani; “Diwani” maana yake ni Mjumbe wa Halmashauri aliyetajwa kwa mujibu wa kifungu 24(2) cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Sura ya 288; 5 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) “Fujo” maana yake ni kitendo chochote kinachoweza kufanywa na Mjumbe au Mshiriki wa Vikao vyaHalmashauri au Kamati ya Kudumu ambacho ni kinyume na taratibu za uendeshaji wa vikao, kinachoweza kuvuruga kikao. Mfano kuongea bila ruhusa ya Mwenyekiti, kutoa lugha isiyofaa, kutoa kauli yenye maudhi, kuingia kwenye kikao akiwa umelewa, kuingia na silaha na kutoa lugha ya kashfa, kukaidi amri ya Mwenyekiti, kukaidi kutoka nje pale anapoamriwa kutoka kutokana na fujo alizosababisha; “Halmashauri” maana yake ni Halmashauri ya Manispaa ya Songea; “Kamati” (a) Inapotumika kuhusiana na Halmashauri ya Manispaa ina iliyoteuliwa na iliyoanzishwa au maana ya Kamati Halmashauri Manispaa chini ya Sheria; (b) Inapotumika kuhusiana na Kamati ya Maendeleo ya Kata ina maana ya Kamati hiyo; (c) Inapotumika kuhusiana na Kamati Ndogo maana yake ni Kamati Ndogo hiyo iliyoteuliwa na Kamati; (d) Inapotumika kuhusiana na Kamati nyingine ina maana ya Kamati hiyo; (e) Kwa maana ya Bodi ya Zabuni ni Katibu wa Bodi ya Zabuni. “Kura ya siri” Maana yake ni Kura itakayopigwa katika eneo la faragha lililotengwa kwa madhumuni ya kupiga kura, eneo ambalo halitapungua umbali wa mita tano (5) kutoka kwa Msimamizi wa kura; “Mkurugenzi” maana yake ni Mkurugenzi wa Manispaa wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea pamoja na Afisa yeyote aliyeteuliwa kutekeleza majukumu ya Mkurugenzi; “Mjumbe” maana yake ni Mjumbe wa Halmashauri kama ilivyoainishwa na kifungu cha 27(1) cha Sheria; “Meya” Kwa madhumuni ya Halmashauri maana yake ni Meya wa Manispaa ya Songea, na inajumuisha Naibu Meya wakati anapotekeleza majukumu ya Meya kwa mujibu wa kanuni hizi. “Mwenyekiti” 6 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) a) Kwa madhumuni ya Halmashauri maana yake ni Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea, na inajumuisha Naibu Meya wakati anapotekeleza majukumu ya Umeya kwa mujibu wa Kanuni hizi. b) Kwa madhumuni ya Kamati, Bodi au Kamati Ndogo maana yake ni Mwenyekiti wa Kamati, Bodi au Kamati Ndogo. c) Kwa maana ya Bodi ya Zabuni ni Mwenyekiti wa Bodi ya Zabuni “Sheria” maana yake ni Sheria ya Serikali za Mitaa(Mamlaka za Miji) Sura ya 288; “Waziri” maana yake ni Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa; SEHEMU YA II MIKUTANO YA HALMASHAURI
Part
SEHEMU YA IX
- 90 Verify source ↗
(1) Wajumbe wa Halmashauri wanaweza kwenda ziara
AI-assisted research summary: Council members may go on training trips if the trips are included in the council plan and budget, and the council must check several conditions before allowing a trip.
90.-(1) Wajumbe wa Halmashauri wanaweza kwenda ziara mbalimbali za mafunzo ili mradi ziara hizo ziwe zimeainishwa kwenye mpango na Bajeti ya Halmashauri. Isipokuwa kwa ziara ambazo gharama zake hazihusiani na Bajeti ya Halmashauri, Wajumbe watafanya ziara hizo kwa mujibu wa ratiba ya mpango huo. (2) Bila kuathiri masharti ya Kanuni Ndogo ya (1) ya kanuni hii Halmashauri kabla ya kuruhusu kufanyika kwa ziara itahaikikisha kwamba- (a) shughuli ya ziara hiyo inafanana na shughuli zinazofanywa na Halmashauri; ziara hiyo inapata kwanza kibali cha Mkuu wa Mkoa; cha (b) (c) Wajumbe wanakitu kwenda kuonyesha kule wanakokwenda kujifunza; ziara zinazofanyika nje ya Mkoa zihusishe wadau (d) 46 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) mbalimbali wa Halmashauri kutegemeana na ziara husika. ziara iwe na matunda yanayoonekana; (e) (f) Wajumbe walioshiriki kwenye ziara warejeapo wanatakiwa kuandaa na kuwasilisha ripoti ya maandishi kwa Halmashauri kuhusu mambo mapya na ya msingi waliyojifunza na kuweka utaratibu mzuri wa kuyatekeleza kwenye Kata zao na kwenye Halmashauri; (g) Ziara zinafanywa kwa vikundi vya Wajumbe wachache kadri itakavyokubalika na Halmashauri. - 91 Verify source ↗
Kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Halmashauri,utaimbwa
AI-assisted research summary: Before the Halmashauri meeting starts, the national anthem is sung and then a prayer is said.
91. Kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Halmashauri,utaimbwa wimbo wa Taifa na kufuatiwa na Dua au Sala ya kuiombea Halmashauri ifuatayo; “Ewe MWENYEZI MUNGU Mtukufu, Muumba wa Mbingu na Dunia umeweka katika Dunia Serikali za Wanadamu ili haki yako itendeke. Twakuomba, uibariki Manispaa yetu ya Songea idumishe uhuru, umoja, haki na amani. Uwajalie viongozi wetu wa Manispaa hekima, afya njema na maisha marefu ili pamoja na wanaowashauri wadumishe utawala bora. Utuongezee hekima na busara sisi Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea na utupe uwezo wa kujadili kwa dhati, mambo yatakayoletwa mbele yetu leo, ili tufanye maamuzi sahihi yenye manufaa kwa watu wote na ustawi wa Manispaa yetu. Amina”. - 92 Verify source ↗
Kanuni hizi zinafuta Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya
AI-assisted research summary: These regulations repeal the Songea Municipal Council Standing Orders of 2003.
92. Kanuni hizi zinafuta Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea za mwaka 2003. Wimbo wa Taifa, Dua/ Sala ya kuiombea Halma- shauri Tangazo la Serikali Namba 205 47 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) JEDWALI Chini ya Kanuni ya 42(3) HADIDU ZA REJEA ZA KAMATI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI ZA MIJI. Madhumuni ya jumla:
Part
JEDWALI
- 1 Verify source ↗
Kuishauri Halmashauri kutengeneza malengo yanayozingatia matakwa ya Miji na kuchukua
AI-assisted research summary: Halmashauri ihimizwe kuweka malengo yanayozingatia matakwa ya Miji na kuchukua hatua zinazofaa ili kuyafikia.
1. Kuishauri Halmashauri kutengeneza malengo yanayozingatia matakwa ya Miji na kuchukua hatua ambazo zitaonekana zinafaa ili kufikia malengo yaliyokusudiwa. - 2 Verify source ↗
Kuishauri Halmashauri kufanya maamuzi juu ya Sera muhimu
AI-assisted research summary: This section says to advise the council on making decisions about important policy matters.
2. Kuishauri Halmashauri kufanya maamuzi juu ya Sera muhimu. - 3 Verify source ↗
Kuishauri Halmashauri kufanya maamuzi juu ya utoaji wa huduma kulingana na rasilimali
AI-assisted research summary: This provision says the council should be advised to make decisions about providing services according to the resources it has.
3. Kuishauri Halmashauri kufanya maamuzi juu ya utoaji wa huduma kulingana na rasilimali walizo nazo. - 4 Verify source ↗
Kuiwezesha Halmashauri kutengeneza taratibu zitakazoongoza utendaji wa Kamati, Kamati
AI-assisted research summary: Halmashauri inawezeshwa kutengeneza taratibu za kuongoza utendaji wa Kamati, Kamati Ndogo, na watumishi ili watimize wajibu wao.
4. Kuiwezesha Halmashauri kutengeneza taratibu zitakazoongoza utendaji wa Kamati, Kamati Ndogo, na ule wa watumishi ili watimize wajibu wao. - 5 Verify source ↗
Kufanya mapitio yatakayowezesha Halmashauri kuamua juu ya kuongeza, kupunguza,
AI-assisted research summary: Halmashauri inawezeshwa kupitia mapitio kuamua kuongeza, kupunguza, kubinafsisha, au kuwashirikisha wadau katika utoaji wa huduma.
5. Kufanya mapitio yatakayowezesha Halmashauri kuamua juu ya kuongeza, kupunguza, kubinafsisha au kuwashirikisha wadau katika utoaji wa huduma. - 6 Verify source ↗
Kuhakikisha kuwa miundo na taratibu za utendaji wa Halmashauri zinazingatia ufanisi,
AI-assisted research summary: The Council’s structures and operating procedures should be arranged to support efficiency, stability, and productivity in achieving the Council’s goals.
6. Kuhakikisha kuwa miundo na taratibu za utendaji wa Halmashauri zinazingatia ufanisi, uthabiti na tija katika kufikia malengo ya Halmashauri. - 7 Verify source ↗
Kuiwezesha Halmashauri kujenga mahusiano imara kati yake na Serikali kuu, Serikali
AI-assisted research summary: Kamati ya Fedha na Utawala lazima ikutane kila mwezi, isimamie mapato na mali za Halmashauri, na isifanye kazi za kamati nyingine; pia inawasilisha bajeti na mipango kwa Halmashauri. Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya hushughulikia afya ya jamii, elimu na huduma za maji.
7. Kuiwezesha Halmashauri kujenga mahusiano imara kati yake na Serikali kuu, Serikali zingine za Mitaa na Umma kwa ujumla. A. Kamati ya Fedha na Utawala: Majukumu ya jumla: Kamati hii inawashirikisha Wenyeviti wa Kamati zote za kudumu na inapaswa kukutana kila mwezi mara moja. Aidha, madaraka ya Kamati hii ni kama ya Kamati zingine za kudumu na hivyo hairuhusiwi kisheria kufanya kazi/majukumu ya Kamati zingine za kudumu. Kwa ujumla, majukumu yake ni pamoja na kusimamia na kudhibiti ukusanyaji wa mapato na matumizi ya mali ya Halmashauri kwa kupitia vikao vyake. Majukumu Maalum ya Kamati: (i) (ii) (iii) (iv) (v) (vi) Kuweka mikakati na kupendekeza uongezaji wa mapato Kuwasilisha mapendekezo ya Bajeti na mpango wa Maendeleo kwenye Halmashauri ili kuidhinishwa na Halmashauri. Kusimamia utunzaji wa hesabu za fedha ikiwa ni pamoja na uhakiki wa mali za Halmashauri, ukusanyaji wa mapato, kufuta madeni, na kuomba vibali maalum kwa matumizi yanayohitaji kibali cha Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa. Kufikiria na, pale inapowezekana, kupendekeza kwenye Halmashauri masuala yanayohusu Sheria Ndogo na utendaji katika ngazi za chini za Halmashauri. Kupokea na kuzingatia mapendekezo ya kubadili matumizi ya mafungu ya fedha (re- allocation) yaliyopo katika makisio yaliyoidhinishwa na kuyapeleka kwa Halmashauri. Kuratibu mapendekezo kutoka kwenye Kamati zingine kuhusu matumizi ya kawaida na miradi na kuyawasilisha kwenye Halmashauri. (vii) Kufikiria na kupendekeza kwenye Halmashauri mikopo yote ya Halmashauri. (viii) Kutoa mapendekezo ya vitega uchumi kwa madhumuni ya kuongeza mapato kwa (ix) (x) mujibu wa Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura ya 290. Kupokea na kujadili taarifa za wakaguzi wa fedha na mali ya Halmashauri na kupendekeza hatua za kuchukuliwa kutokana na maelekezo na maoni ya wakaguzi kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Mitaa, Sura ya 290. Kusimamia na kudhibiti matumizi ya fedha za Halmashauri, kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa na Waziri na taratibu nyingine zitakazowekwa na Halmashauri; 48 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (xi) Kupitia marekebisho yote yaliyopendekezwa hususan kuhusu taratibu za fedha, ikiwa ni pamoja na mapitio ya mara kwa mara yanayohusu thamani ya fedha ambapo Kanuni mbalimbali za manunuzi ya mali na vifaa hutumika; (xii) Kufikiria na kupendekeza mabadiliko ya viwango vya kodi, ada na ushuru mbalimbali, vinavyotolewa na Halmashauri; (xiii) Kufikiria mapendekezo ya Bajeti na Mipango ya Maendeleo ya kila Kamati ya Kudumu na kuiwasilisha kwenye Halmashauri ili kupata idhini; (xiv) Kushughulikia tofauti ya mapato na matumizi katika bajeti yote na kupendekeza hatua stahiki ya kuchukua kuondoa mapungufu katika mapato au ziada matumizi; (xv) Kufikiria mapendekezo yote yanayohusu matumizi makubwa ya fedha kabla hayajawasilishwa kwenye Halmashauri ili kupata idhini; (xvi) Kupokea mahesabu ya mwaka ya Halmashauri na kuhakikisha taarifa ya mahesabu ya mwaka inawasilishwa kwa wakati kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali; (xvii) Kupitia na kuidhinisha mpango wa manunuzi wa Halmashauri kwa kuzingatia mpango wa Bajeti uliopitishwa na Halmashauri; (xviii) Kupitia taarifa ya kila robo mwaka kuhusu Manunuzi iliyowasilishwa na Afisa Masuuli; (xix) Kusimamia utekelezaji wa mikataba ya Halmashauri kwa kukagua miradi inayotekelezwa na vifaa vilivyopokelewa; (xx) Kumwelekeza Mkurugenzi kufanya manunuzi au ukaguzi wa huduma au vifaa vilivyonunuliwa ili kupata thamani halisi, itafanyika hivyo endapo itadhihirika kwamba, maelezo yaliyotolewa kuhusu manunuzi ya vifaa au huduma hayaridhishi; (xxi) Kuidhinisha majina ya wajumbe wa Bodi ya zabuni na wa Bodi zingine kwa mujibu wa Sheria husika; (xxii) Kushughulikia orodha ya wadaiwa wote itakayokayowasilishwa kwenye Kamati na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukua; (xxiii) Kupendekeza njia na taratibu za kuondosha vifaa chakavu. Uondoshaji wa vifaa unaweza kufanyika kwa njia ya kuuza au kuviharibu; (xxiv) Kujadili na kupitia taarifa za fedha za kila mwezi na kila robo mwaka; (xxv) Kupendekeza kwa Halmashauri hatua za kuchukua kuhusu kufuta madeni ya Halmashauri; (xxvi) Kushughulikia Sera kuhusu kukopa na uwekezaji, (xxvii) Kubuni na kupendekeza mpango wa kuanzisha na kuendeleza uhusiano na Halmashauri nyingine. (xxviii) Kurekebisha na kusimamia makusanyo na matumizi ya mapato ya vijiji na miji midogo kwa mujibu wa Sheria, (xxix) Kuteua wakaguzi wa fedha/mali za Serikali za Vijiji kwa mujibu wa Sheria, Sura ya 290). (xxx) Kujadili na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa kuhusu mambo yote ya yanayohusu masuala ya ajira na kinidhamu ya wafanyakazi na watumishi. (xxxi) Kujadili na kutoa mapendekezo kuhusu masuala yanayohusu nyumba za Halmashauri. (xxxii) Kupokea na kutoa uamuzi juu ya mapendekezo ya watumishi wanaokwenda masomoni. (xxxiii) Kujadili na kupendekeza masuala yote yanayohusu maslahi ya jumla ya watumishi, ikiwa ni pamoja na mikopo, nyumba, usafiri, matibabu, rambirambi na motisha nyinginezo. (xxxiv) Kupitisha mapendekezo ya kuthibitisha watumishi kazini baada ya kumaliza kipindi cha majaribio kulingana na miundo husika ya utumishi. 49 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) B: Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya: Majukumu ya Jumla Kushughulikia mambo yote yanayohusu afya ya jamii, elimu na huduma za maji. Kamati hii pia itashughulikia mambo yanayohusiana na jitihada za wanannchi vijijini kujiletea maendeleo yao kwa kutumia mbinu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kushauri, kushawishi, kuzindua, kuelimisha na kushirikisha wananchi hao hasa katika kutayarisha, kutekeleza, kusimamia na kutathmini mipango yao ya maendeleo. Majukumu maalum ya Kamati: (i) Kuandaa mipango madhubuti ya maendeleo ya upanuzi na ujenzi wa hospitali, vituo vya afya na zahanati (ii) Kuandaa mipago ya maendeleo ya upanuzi na ujenzi wa shule za awali na msingi na elimu ya watu wazima kwa mujibu wa Sheria ya Elimu ya 1978 kama ilivyorekebishwa mwaka 1995. (iii) Kupendekeza mipango ya ujenzi au upanuzi wa vituo,viwanja, majengo na mazingira ya burudani, starehe, mapumziko na michezo. (iv) Kuamua juu ya mambo yanayohusu uhifadhi wa mambo ya kale na mandhari mbalimbali yenye sura nzuri. (v) Kuandaa na kuratibu njia bora juu ya uhifadhi wa nyaraka muhimu kwa ajili ya kumbukumbu hizo zitahifadhiwa kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa Sura ya 288 (vi) Kupendekeza njia bora juu ya uhifadhi wa sanaa mbalimbali za ufundi na za maonyesho kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa Sura ya 288 (vii) Kupendekeza matumizi mazuri ya lugha ya taifa. (viii) Kupendekeza namna ya malezi ya vijana ili waweze kuwa wazalishaji katika Taifa. (ix) Kusimamia uanzishaji wa uendelezaji wa vikundi vya jamii na vya hiari vya wananchi katika Halmashauri kwa mujibu wa Sera wa maendelo ya jamii. (x) Kusimamia na kuhakiki maeneo ya misitu, mapori, na mbuga zilizotengwa kama hifadhi ya mamlaka ya Serikali za Mitaa. (xi) Kupendekeza na kufanya tathmini ya uendelezaji wa mabonde, mito na mabwawa. (xii) Kubuni na kupendekeza namna ya kudhibiti moto (xiii) Kubuni na kupendekeza mikakati ya utumiaji wa nishati mbadala, kuzuia ukataji miti ovyo, na kuhimiza upandaji miti kwa wingi. (xiv) Kuhakikisha kwamba ukaguzi wa majengo unafanyika mara kwa mara. (xv) Kupendekeza mipango madhubuti ya ujenzi wa barabara vijijini na wilayani kwa ujumla. (xvi) Kupendekeza Sheria Ndogo zinazohusu Kamati hizi. 50 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) D: Kamati ya Kudumu ya Kudhibiti Ukimwi Majukumu ya Kamati: - 1 Verify source ↗
Kushirikisha wadau tofauti katika maeneo husika ili kuongeza uchangiaji wa mawazo
AI-assisted research summary: Provision inahusu kushirikisha wadau tofauti katika maeneo husika ili kuongeza uchangiaji wa mawazo, nyenzo, usimamizi, uratibu na utekelezaji wa kazi za Tume za kudhibiti UKIMWI.
1. Kushirikisha wadau tofauti katika maeneo husika ili kuongeza uchangiaji wa mawazo na/au nyenzo, usimamizi, uratibu na utekelezaji wa kazi za Tume za kudhibiti UKIMWI; - 2 Verify source ↗
Kusimamia uundaji wa Kamati zote za kudhibiti UKIMWI
AI-assisted research summary: Sehemu hii inaeleza kusimamia uundaji wa kamati zote za kudhibiti UKIMWI.
2. Kusimamia uundaji wa Kamati zote za kudhibiti UKIMWI; - 3 Verify source ↗
Kupendekeza na kuchambua hali ya UKIMWI/Mipango na utekelezaji wake na kufikisha
AI-assisted research summary: Consider and analyze HIV/AIDS status, plans, and implementation, then communicate them to the local level for further action.
3. Kupendekeza na kuchambua hali ya UKIMWI/Mipango na utekelezaji wake na kufikisha katika ngazi husuka kwa hatua zaidi; - 4 Verify source ↗
Kutathmini hali ya UKIMWI katika eneo lake
AI-assisted research summary: The committee must handle planning, land use, agriculture, infrastructure, environment, and cooperative matters, and the government must not give funds to a council without solid AIDS-control plans.
4. Kutathmini hali ya UKIMWI katika eneo lake; (i) Idadi ya waathirika: wagonjwa, yatima, wajane, (ii) Kasi ya maambukizo. (iii) Mazingira maalum yanayochangia maambukizo. (iv) Uelewa wa wananchi juu ya janga hili. (v) Serikali haitatoa fedha kwa Halmashauri isiyokuwa na mipango madhubuti ya kudhibiti UKIMWI. (vi) Kuweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha kila mtoto aliyefikia umri wa kwenda shule anafanya hivyo. (vii) Kuweka mikakati ya makusudi juu ya njia bora za kuchangia baadhi ya huduma za Elimu na Afya. (viii) Kubuni na kupendekeza njia bora za kuzuia na kudhibiti magonjwa ya milipuko. (ix) Kupendekeza Sheria Ndogo za Kamati hii. C: Kamati ya Mipango Miji na Mazingira: Majukumu ya jumla Kamati hii itashughulikia masuala ya uzalishaji mali ikiwemo kilimo, mifugo, viwanda, madini, Biashara n.k. Aidha itashughulikia pia miundombinu na suala zima la mendeleo ya Ardhi na hifadhi ya mazingira. Majukumu maalum ya Kamati; (i) Kupendekeza kwa Halmashauri mipango ya kupanua biashara na jinsi ya kukusanya mapato yatokanayo na upanuzi huo. (ii) Kupendekeza mipango ya matumizi ya ardhi katika eneo la Halmashauri. (iii) Kusimamia matumizi ya Sheria ya nguvu kazi. (iv) Kuandaa mipango madhubuti ya maendeleo ya upanuzi wa kilimo katika Halmashauri 51 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) (v) Kusimamia na kuhakiki miradi ya ujenzi wa masoko, minada, majosho na vituo vya mifugo. (vi) Kushughulikia uanzishaji na uendelezaji wa vyama vya ushirika kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Ushirika. 52 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) FAHARASA – HALMASHAURI ZA MANISPAA YA SONGEA Kanuni Na. Kifungu cha Sheria A Ajenda za Kamati Akidi katika Mikutano ya Halmashauri Akidi kwenye Mikutano ya Kamati Athari za nafasi wazi kwenye Kamati B C D Diwani au Afisa kutokuwa na maslahi katika mikataba Diwani kutembelea maeneo, shughuli mbalimbali za ujenzi nk. Wimbo wa Taifa/Dua ya kuiombea Halmashauri E F Fujo zinazosababishwa na umma Fujo zinazosababishwa na Wajumbe wa watumishi zinazohusu G H Haki ya kujibu Hoja kuhusu matumizi Hoja na marekebisho ya hoja Hoja za Mwenyekiti/Meya Hoja Halmashauri Hoja zinazoweza kutolewa bila taarifa I J K Kamati za Kudumu Kamati za pamoja Kanuni za kudumu kutumika katika Mikutano ya Kamati Kanuni Wajumbe Kauli zenye kashfa Kiapo na kukubali wadhifa Kuidhinishwa kwa Taarifa ya Kamati Kufikiriwa upya maamuzi Kufutwa kwa Kanuni zilizopo za kudumu kutolewa kwa Kujiuzulu ujumbe wa Kamati na kujazwa kwa nafasi iliyoachwa wazi. Sura ya 288 kif.36 Sura ya 288 kif.51(2) na (3) Sura ya 288 kif.51(1);51(3) Sura ya 288 kif.43 50 9 56 55 70 78 91 19 18 22 33 20 16 38 21 41 44 57 88 28 71 35 60 92 63 53 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) Kanuni Na. Kifungu cha Sheria Kujiuzulu wadhifa wa Mwenyekiti wa Kamati Kumbukumbu ya mahudhurio. Meya/Mwenyekiti Kumwondoa madarakani Kupokelewa kwa taarifa za Kamati Kuruhusu watu na vyombo vya Habari kwenye Mikutano ya Halmashauri. Kushiriki kwa Umma Kusitisha utumiaji wa Kanuni za kudumu. Kutafsiri Kanuni za kudumu Kuthibitisha muhtasari Kutokuwepo kwa Wajumbe Kutunza siri za Majadiliano ya Kamati na Kamati Ndogo. L M Maamuzi ya Mikutano ya Halmashauri Mahudhurio katika Mikutano ya Kamati Majukumu ya Diwani Marekebisho na mabadiliko ya Kanuni za kudumu Maswali Maswali ya papo kwa papo Mihtasari ya Kamati za maendeleo za Kata na vijiji/Mitaa. Mihtasari kupelekwa kwa Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa. Mihtasari ya Kamati Mikutano ya Kamati Mikutano ya kawaida ya Halmashauri Mtoa hoja kualikwa kwenye Mkutano wa Kamati. Mkutano wa Bajeti Mkutano wa Mwaka Mkutano maalum wa Halmashauri Mkutano maalum wa Kamati Mwaliko wa wasiokuwa Wajumbe N Nafasi wazi P Aina za posho Posho endapo Mkutano utaahirishwa 62 12 83 34 13 39 86 89 15 74 61 29 51 72 87 23 24 31 32 59 47 3 52 6 7 5 49 30 73 84 85 54 Sura ya 288 kif.40 (2) Sura ya 288 kif.25(5) ; GN 263/95 Sura 288 kif.39(1) Taz.pia Sura ya 290 kif.47 Sura ya 288 kif.40(1) Sura ya 288 kif.34(1) Sura ya 288 kif.34(3) Sura ya 288 kif.45, 50 Sura ya 288 kif. 42(2) Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) Kanuni Na. Kifungu cha Sheria Q R Rejesta ya mikataba S T Taarifa za Kamati Taarifa kutoka kwenye kata Taarifa za Mikutano Tafsiri Taratibu za kutunga Sheria Ndogo Taratibu za Majadiliano Taratibu za Uagizaji U Uahirishaji wa vikao Uandikishaji wa Anwani Uandishaji wa Bodi za Huduma Uchaguzi wa Meya/ Mwenyekiti na Naibu Meya/Makamu wa Halmashauri Uhalali wa majadiliano ya Halmashauri Uhuru wa kutoa mawazo wakati wa majadiliano Ukaguzi wa nyaraka Akidi kwenye Mikutano ya Kamati Upigaji kura kwenye Mikutano ya Kamati Usimamiaji wa mikataba Utaratibu wa shughuli za Mikutano Uteuzi wa Wajumbe kwenye Taasisi za nje Utiaji mhuri kwenye Nyaraka Uvunjaji wa mkataba Uwezo wa Halmashauri kujigeuza kuwa Kamati ya Halmashauri nzima. Uwezo wa Kamati Uzuiaji wa Rushwa Mwenyekiti V W Waalikwa Wajumbe wasiokuwa kuhudhuria na kushiriki katika Mikutano ya Kamati. X Y Z Ziara za Wajumbe 69 25 26 8 2 75 17 64 40 81 77 10 36 27 76 56 58 67 14 82 80 68 37 43 66 53 90 55 Sura ya 288 kif.35 Sura ya 288 kif.38 Sura ya 288 kif.45(1) Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KIAPO CHA DIWANI Mimi ……………………………… naapa/natamka kwa dhati kwamba nitaitumikia Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa wadhifa wangu wa Udiwani na kwamba nitahifadhi, nitalinda na kutetea, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria za Tanzania, Maadili ya Madiwani na Kanuni za Kudumu za Halmashauri kama zilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria na kwamba nitaitumikia Halmashauri ya Manispaaa ya Songea kwa uaminifu, kwa uwezo na moyo wangu wote. (Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie) Kiapo/Tamko hili limetolewa hapa; ……………………………………… Na…………………………………………………………………………….. Leo tarehe…………………… Mwezi wa…………………..20………. Mbele ya:……………………………………….. Jina:……………………………………………… Cheo:……………………………………………. Saini:…………………………………………… Anuani………………………………………….………………………………….. HAKIMU/WAKILI WA KUAPISHA 56 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI (Kwa mujibu wa kifungu cha 9 na cha 11 cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma) Mimi…………………………………………………… Anuani; …………………… baada ya kuchaguliwa/kuteuliwa na kuapishwa katika wadhifa wa…….……...tarehe……………………….mwaka 20….Ninatamka rasmi na kwa moyo mnyofu kwamba hadi sasa nina rasilimali na madeni yafuatayo:- (1) Fedha taslimu, Amana katika benki au taasisi ya fedha; taja namba ya akaunti, benki au taasisi ya fedha na kiasi: ……………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………….………… 2) Hawala za Hazina (Treasury Bills) na dhamana nyingine maalum:- ……………………………………………………………………………………………………… ………………………………………………………………………………..…………………… 3) Faida ya akiba, mafungu ya mgawanyo wa faida zinazotokana na hisa n.k. ……………………………………………………………………………………………………… ………………………………………………………………………….…………………………… 4) Nyumba au majengo ya kupangisha, taja mahali yalipo na ukubwa au eneo: ……………………………………………………………………………………………………… ………………………………………………………………………..…………………………… * Rasilimali zinazotakiwa ni pamoja na zifuatazo, ambazo ni zako binafsi, za mume/mke au watoto wadogo wasiooa au kuolewa wa kiongozi wa umma. (a) Fedha taslimu na amana katika benki au taasisi nyingine ya fedha. (b) Hawala za Hazina Treasury Bills) na nyinginezo za dhamana maalum zinazotolewa au kudhaminiwa na Serikali au vyombo vya Serikali. (c) Faida itokanayo na fedha iliyowekwa akiba Benki, Chini ya Ujenzi au taasisi nyingine ya fedha. (d) Mgao wa fedha kutokana na fungu la rasilimali ya kampuni (stocks) au hisa za kiongozi wa umma katika kampuni au shirika lolote. (e) Maslahi katika chombo cha biashara kisichokuwa na mkataba na Serikali, na kisichokuwa na au kisichotawala amana zinazouzwa bayana na vyombo vya umma. (f) Mashamba ya kibiashara. (g) Mali halisi zisizohamishika ambazo si rasilimali zisizotakiwa kutajwa; na (h) Rasilimali zinazoleta faida, ambazo si rasilimali zisizotakiwa kutajwa na ambazo zinamilikiwa kwa mbali. 57 Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na. 162 (linaendelea) ambayo nyinginezo au maslahi (5) Mashamba ya kibiashara, mifugo, madini n.k. ……………………………………………………………………………………………………… ……………………………………………………………………………………………………… (6) Magari na aina nyingine za usafiri wa kibiashara; ……………………………………………………………………………………………………… ……………………………………………………………………………………………………… (7) Mashine za kusaga nafaka, viwanda na shughuli nyingine za kibiashara au mitambo:…………………………………………………………………………………………… ……………………………………………………………………………………………………… ……………………………………………………………....................................………………… (8) Rasilimali anapenda kutaja:……………………………………………………………………………………………… ……………………………………………………………………………………………………… (9)Madeni;……………………………………………………………...…………………………… ………………………………………………………………….…………………………………… Tamko hili linatolewa na kusainiwa mbele yangu ………………………………………………....……......……. na (mtoa tamko)……………………………….............……… ninayemfahamu binafsi, au aliyetambulishwa kwangu na ………………………………………………………………… ….………….. ambaye ninamfahamu leo tarehe ……………......………..…… Mtoa tamko Mwezi wa ………………………………………..……….…… saini…………………………………………….……………… Wadhifa:………………………………………..……………… Anuani:………………………………………...………………. …………………………………………………………………. (Tamko hili lazima litolewe mbele ya Kamishna wa Viapo) kiongozi wa umma KWA: KAMISHINA WA MAADILI, SEKRETARIETI YA MAADILI, S.L.P 13341, DAR ES SALAAM. Nembo ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea imebandikwa katika Kanuni hizi kufuatia Azimio la Halmashauri lililotolewa katika kiako kilichoitishwa na kufanyika tarehe 30 mwezi Januari, 2014 na ilibandikwa mbele ya: ZACHARIA NACHOA, Mkurugenzi Manispaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea CHARLES MHAGAMA, Mstahiki Meya Halmashauri ya Manispaa ya Songea NAKUBALI Dodoma, 20 Mei, 2015 MIZENGO P. PINDA (MB.), Waziri Mkuu 58
Provision text is displayed from LexChat’s stored statute record. Use the official source links to verify amendments, commencement, and current legal force.
Ask AI about this statute
KANUNI ZA KUDUMU ZA HALMASHAURI YA MANISPAA YA SONGEA ZA MWAKA, 2016
Sign in to ask AI about this statute
Sign in to start authenticated, citation-grounded statute research.
Sign in