Kanuni za Utaratibu wa Usafirishaji wa Venia Kwenda Nje ya Nchi za Mwaka 2024
This provision gives the name of the regulations.
AI-assisted research synopsis — verify against the official legal text below.
- Jurisdiction
- Tanzania
- Instrument
- Regulation
- Citation
- Kanuni za Utaratibu wa Usafirishaji wa Venia Kwenda Nje ya Nchi za Mwaka 2024
- Version
- Undated source snapshot
- Language
- sw
- Official source
- View official record ↗
Statute overview
About this statute
This provision gives the name of the regulations. This section defines several terms used in the regulations, including “Kamishna wa Uhifadhi,” “Sheria,” “venia,” “Wakala,” and “Waziri.” Mtu haruhusiwi kusafirisha venia kwenda nje ya nchi bila kibali cha Kamishna wa Uhifadhi, na kibali hicho hutolewa baada ya ridhaa ya Waziri. Mtu anayetaka kusafirisha venia nje ya nchi lazima aombe kibali kwa Kamishna wa Uhifadhi kwa kutumia Fomu 1 na kuonyesha kiasi anachoomba. The Conservation Commissioner must process applications, assess whether the applicant meets the rules in regulation 4, and then send recommendations to the Minister. The Minister may approve or رفض the permit in writing, and if approved the Commissioner must issue the export permit in Form 3.
Search within this statute
Search all stored provisions in this version.
Legal text
Provisions of Kanuni za Utaratibu wa Usafirishaji wa Venia Kwenda Nje ya Nchi za Mwaka 2024
Showing 15 of 15
- 1 Verify source ↗
Kanuni hizi zitajulikana kama Kanuni za
AI-assisted research summary: This provision gives the name of the regulations.
1. Kanuni hizi zitajulikana kama Kanuni za Utaratibu wa Usafirishaji wa Venia Kwenda Nje ya Nchi za Mwaka 2024. Tafsiri - 2 Verify source ↗
Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama muktadha
AI-assisted research summary: This section defines several terms used in the regulations, including “Kamishna wa Uhifadhi,” “Sheria,” “venia,” “Wakala,” and “Waziri.”
2. Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama muktadha utahitaji vinginevyo- “Kamishna wa Uhifadhi” maana yake ni Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania; Sura ya 323 TS. Na. 269 la 2010 “Sheria” maana yake ni Sheria ya Misitu; kipande “venia” maana yake chembamba kilichomenywa kutoka kwenye gogo ambacho hutumika kuzalisha bidhaa mbalimbali; ni “Wakala” maana yake ni Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania ulioanzishwa chini ya Amri ya Uanzishwaji wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania; na “Waziri” ina maana iliyotolewa katika Sheria. 1 Kanuni za Utaratibu wa Usafirishaji wa Venia kwenda Nje ya Nchi Tangazo la Serikali Na. 807 (Linaendelea) SEHEMU YA PILI UTARATIBU WA USAFIRISHAJI WA VENIA KWENDA NJE YA NCHI Katazo la kusafirisha venia
Part
SEHEMU YA PILI
- 3 Verify source ↗
Mtu hatasafirisha venia kwenda nje ya nchi
AI-assisted research summary: Mtu haruhusiwi kusafirisha venia kwenda nje ya nchi bila kibali cha Kamishna wa Uhifadhi, na kibali hicho hutolewa baada ya ridhaa ya Waziri.
3. Mtu hatasafirisha venia kwenda nje ya nchi bila kupata kibali kutoka kwa Kamishna wa Uhifadhi kitakachotolewa baada ya kupata ridhaa ya Waziri. Utaratibu wa maombi ya kibali cha kusafirisha venia - 4 Verify source ↗
(1) Mtu anayekusudia kusafirisha venia
AI-assisted research summary: Mtu anayetaka kusafirisha venia nje ya nchi lazima aombe kibali kwa Kamishna wa Uhifadhi kwa kutumia Fomu 1 na kuonyesha kiasi anachoomba.
4.-(1) Mtu anayekusudia kusafirisha venia kwenda nje ya nchi atatakiwa kuomba kibali kwa Kamishna wa Uhifadhi kwa kujaza Fomu Namba 1 iliyoainishwa katika Jedwali akiainisha kiasi cha mita za ujazo anazoomba. (2) Maombi ya kibali cha kusafirisha venia kwenda nje ya nchi yaliyoainishwa katika kanuni ndogo ya (1) yatatakiwa kuambatana na nyaraka zifuatazo: (a) cheti cha usajili wa kampuni; (b) cheti cha usajili wa namba ya Utambulisho ya Mlipa Kodi; (c) cheti cha usajili wa biashara ya mazao ya misitu; (d) leseni ya biashara kwa ajili ya kusafirisha mazao ya misitu kwenda nje ya nchi kutoka kwenye Mamlaka husika; (e) cheti cha uthibitisho wa mlipakodi; (f) hati ya usajili wa kiwanda cha kuzalisha venia; (g) iwapo ni mwombaji wa mara ya kwanza, mpango wa uwekezaji unaoainisha namna ya kubadili teknolojia kwa ajili ya kuzalisha mazao na ya misitu utekelezaji wake; na yaliyohandisiwa (h) iwapo ni mwombaji wa mara ya pili na kuendelea, taarifa ya utekelezaji wa mpango wa uwekezaji ulioainishwa katika aya ya (g). Uchakataji wa maombi - 5 Verify source ↗
(1) Kamishna wa Uhifadhi atachakata maombi
AI-assisted research summary: The Conservation Commissioner must process applications, assess whether the applicant meets the rules in regulation 4, and then send recommendations to the Minister. The Minister may approve or رفض the permit in writing, and if approved the Commissioner must issue the export permit in Form 3.
5.-(1) Kamishna wa Uhifadhi atachakata maombi yaliyowasilishwa chini ya kanuni ya 4 kwa lengo la kujiridhisha endapo mwombaji amekidhi masharti yaliyoainishwa katika kanuni ya 4. (2) Bila kuathiri masharti ya kanuni ndogo ya (1) 2 Kanuni za Utaratibu wa Usafirishaji wa Venia kwenda Nje ya Nchi Tangazo la Serikali Na. 807 (Linaendelea) Kamishna wa Uhifadhi atajiridhisha endapo taarifa ya utekelezaji iliyowasilishwa kwa mujibu wa kanuni ya 4(2)(g) inaakisi maendeleo ya utekelezaji wa mpango wa uwekezaji. (3) Kamishna wa Uhifadhi baada ya kuchakata maombi atawasilisha mapendekezo yake kwa Waziri kwa ajili ya kupata ridhaa. (4) Baada ya Waziri kupokea mapendekezo ya kutolewa kibali chini ya kanuni ndogo ya (1), anaweza kwa maandishi- (a) kuridhia kutolewa kwa kibali; au (b) kutoridhia kutolewa kwa kibali na kueleza sababu za uamuzi huo. (5) Baada ya Waziri kuridhia kutolewa kwa kibali cha usafirishaji wa venia kwenda nje ya nchi, Kamishna wa Uhifadhi, atatoa kibali cha kusafirisha venia kwenda nje ya nchi katika Fomu Namba 3 iliyoainishwa katika Jedwali. (6) Endapo Waziri hataridhia kutolewa kwa kibali cha usafirishaji wa venia kwenda nje ya nchi, atamjulisha mwombaji Kamishna wa Uhifadhi, kutoridhiwa kwa maombi yake akiainisha sababu zilizobainishwa na Waziri. - 6 Verify source ↗
(1) Mtu mwenye kibali cha kusafirisha venia
AI-assisted research summary: Holders of a permit to transport venia must apply for an export transportation and inspection certificate, and the Commissioner of Conservation must inspect the shipment and then issue the inspection and transport certificates if satisfied.
6.-(1) Mtu mwenye kibali cha kusafirisha venia atapaswa kuwasilisha maombi ya kupatiwa cheti cha usafirishaji na ukaguzi wa kila shehena ya venia inayokusudiwa kusafirishwa kwenda nje ya nchi kutoka kwa Kamishna wa Uhifadhi kwa kutumia Fomu Namba 2 iliyoainishwa katika Jedwali. (2) Kamishna wa Uhifadhi, baada ya kupokea maombi yaliyowasilishwa katika kanuni ndogo ya (1), atafanya ukaguzi wa shehena ya venia inayokusudiwa kusafirishwa kwenda nje ya nchi ili kujiridhisha na taarifa zilizotolewa na mwombaji. (3) Baada ya kujiridhisha na taarifa za shehena ya venia inayokusudiwa kusafirishwa kwenda nje ya nchi, Kamishna wa Uhifadhi atatoa Cheti cha Ukaguzi na Cheti cha Kusafirisha venia kwenda nje ya nchi kwa kutumia Fomu Namba 4 na 5 kama zilivyoainishwa katika Jedwali. 3 Cheti cha usafirishaji wa venia na ukaguzi wa shehena Kanuni za Utaratibu wa Usafirishaji wa Venia kwenda Nje ya Nchi Tangazo la Serikali Na. 807 (Linaendelea) Ada ya usafirishaji wa venia kwenda nje ya nchi - 7 Verify source ↗
Mtu anayesafirisha venia kwenda nje ya nchi
AI-assisted research summary: Mtu anayesafirisha venia kwenda nje ya nchi lazima alipe kwa Wakala ada ya usafirishaji ya asilimia 5 ya thamani ya shehena.
7. Mtu anayesafirisha venia kwenda nje ya nchi atatakiwa kulipa kwa Wakala ada ya usafirishaji wa venia kwenda nje ya nchi ambayo ni asilimia tano ya thamani ya shehena ya venia inayosafirishwa kwenda nje ya nchi. SEHEMU YA TATU MASHARTI MENGINEYO Taarifa ya utekelezaji
Part
SEHEMU YA TATU
- 8 Verify source ↗
Kamishna wa Uhifadhi kila baada ya miezi
AI-assisted research summary: The Commissioner of Conservation must submit a detailed report to the Minister every three months.
8. Kamishna wa Uhifadhi kila baada ya miezi mitatu, atawasilisha kwa Waziri taarifa ya kina ya utekelezaji wa Kanuni hizi ikiainisha- (a) idadi ya vibali vilivyotolewa; (b) utekelezaji wa mpango wa uwekezaji wa namna ya kubadili teknolojia kwa ajili ya kuzalisha mazao ya misitu yaliyohandisiwa kwa wote waliopatiwa vibali vya kusafirisha venia kwenda nje ya nchi; (c) ujazo wa iliyotolewa venia kusafirishwa kwenda nje ya nchi; na iliyotolewa venia (d) thamani ya kibali kibali kusafirishwa kwenda nje ya nchi. Muda wa matumizi ya Kanuni hizi - 9 Verify source ↗
(1) Kanuni hizi zitatumika kwa kipindi cha
AI-assisted research summary: Kanuni hizi zinatumika kwa miaka miwili kuanzia tarehe ya kuchapishwa gazettini, na baada ya muda huo mtu yeyote haruhusiwi kusafirisha venia kwenda nje ya nchi.
9.-(1) Kanuni hizi zitatumika kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia tarehe ya kuchapishwa katika Gazeti la Serikali. (2) Baada ya muda wa matumizi ya Kanuni hizi kufika ukomo, mtu yeyote hataruhusiwa kusafirisha venia kwenda nje ya nchi. ________ JEDWALI ________ (Limetengenezwa chini ya kanuni za 4(1), 5(5), 6(1) na 6(3)) FOMU NAMBA 1 FOMU YA MAOMBI YA KIBALI CHA USAFIRISHAJI WA VENIA KWENDA NJE YA NCHI 4 Kanuni za Utaratibu wa Usafirishaji wa Venia kwenda Nje ya Nchi Tangazo la Serikali Na. 807 (Linaendelea) Mimi/Sisi ninaomba/tunaomba kibali cha kusafirisha Venia kwenda nje ya Nchi. Jina la Kampuni: ………………………………………
Part
JEDWALI
- 2 Verify source ↗
Anuani: ……………………… Namba ya simu: …………………
AI-assisted research summary: This section asks for an address and a phone number.
2. Anuani: ……………………… Namba ya simu: …………………. - 4 Verify source ↗
Kiwango kwa Mita za Ujazo
AI-assisted research summary: This text is part of an application form for a certificate to ship/inspect venia for export outside the country.
4. Kiwango kwa Mita za Ujazo: .............................................................. Jina la Mwombaji: ……………………………. Wadhifa: ……………………….. Saini: ……………………………… Tarehe: ……………………………. Muhuri wa Kampuni: ……………………………. 5 Kanuni za Utaratibu wa Usafirishaji wa Venia kwenda Nje ya Nchi Tangazo la Serikali Na. 807 (Linaendelea) FOMU NAMBA 2 FOMU YA MAOMBI YA CHETI CHA USAFIRISHAJI/UKAGUZI WA VENIA KWENDA NJE YA NCHI Mimi/Sisi ninaomba/tunaomba cheti cha usafirishaji/ukaguzi wa venia kwenda nje ya Nchi. - 2 Verify source ↗
Anuani: ……………………Namba ya simu: …………………………
AI-assisted research summary: This section asks for an address and phone number.
2. Anuani: ……………………Namba ya simu: …………………………. - 4 Verify source ↗
Nchi ambako venia inapelekwa: …………………………………………
AI-assisted research summary: Section 4 is a heading about the country where the permit is taken to be sent.
4. Nchi ambako venia inapelekwa: ………………………………………… - 5 Verify source ↗
Sehemu (kituo cha forodha) shehena ya venia inapopita
AI-assisted research summary: This section appears to name a customs checkpoint related to cargo in transit.
5. Sehemu (kituo cha forodha) shehena ya venia inapopita: …………………… - 6 Verify source ↗
Kiwango kwa Mita za Ujazo
AI-assisted research summary: This provision shows forms for a permit, inspection certificate, and shipping certificate for exporting venia outside the country.
6. Kiwango kwa Mita za Ujazo: .................................................................. Jina la Mwombaji: …………………………………………………………… Wadhifa: ………………………………….. Saini: ……………………………………………………………………….. Tarehe: ……………………………………………………………………….. Muhuri wa Kampuni: …………………………………………………… KIBALI CHA USAFIRISHAJI WA VENIA KWENDA NJE YA NCHI FOMU NAMBA 3 kimetolewa sanduku Kibali kwa kwenda …………………...........cha ..................................kupitia wa cha……………………………………………………………. ................................wa kusafirisha bandari/uwanja venia posta la ya nchi ndege/kituo (i) Spishi ya venia: ………………..……………… (ii) Mita za Ujazo: ………………………………… (iii) Tarehe ya kutolewa kibali: …………………… Jina: ………………………… Saini: ……………………………. Kamishna wa Uhifadhi Tarehe: ........................................ 6 Kanuni za Utaratibu wa Usafirishaji wa Venia kwenda Nje ya Nchi Tangazo la Serikali Na. 807 (Linaendelea) FOMU NAMBA 4 CHETI CHA UKAGUZI WA VENIA KWENDA NJE YA NCHI Mimi………………………………………………Nathibitisha kuwa nimekagua shehena ya venia inayomilikiwa na ………………………………………………. iliyopo…………………….na kubaini kuwa imekidhi masharti yaliyotolewa chini ya Sheria za Misitu, Sura ya 323. Leo tarehe ……………………………Mwezi………………….20………………. ………………………. Saini ya Afisa Mkaguzi FOMU NAMBA 5 CHETI CHA KUSAFIRISHA VENIA NJE YA NCHI Cheti hiki kimetolewa kwa................................... wa sanduku la posta ..................................... kusafirisha Venia kutoka bandari/uwanja wa ndege/kituo cha ………………………kwenda nchi ya………………………kama ifuatavyo: (a) Spishi ya venia: ............................................................... (b). Mita za Ujazo: ................................................................. Jina: …………………………………… Saini: ………………………………… Kamishna wa Uhifadhi Tarehe: …………………………… Dodoma, 3 Septemba, 2024 PINDI HAZARA CHANA Waziri wa Maliasili na Utalii 7
Provision text is displayed from LexChat’s stored statute record. Use the official source links to verify amendments, commencement, and current legal force.
Ask AI about this statute
Kanuni za Utaratibu wa Usafirishaji wa Venia Kwenda Nje ya Nchi za Mwaka 2024
Sign in to ask AI about this statute
Sign in to start authenticated, citation-grounded statute research.
Sign in