Kanuni za Kampuni (Umiliki Manufaa) za mwaka 2023
This section names the regulation as the Companies (Beneficial Ownership) Regulations, 2023, and says it interprets Chapter 212.
AI-assisted research synopsis — verify against the official legal text below.
- Jurisdiction
- Tanzania
- Instrument
- Regulation
- Citation
- Kanuni za Kampuni (Umiliki Manufaa) za mwaka 2023
- Version
- Undated source snapshot
- Language
- sw
- Official source
- View official record ↗
Statute overview
About this statute
This section names the regulation as the Companies (Beneficial Ownership) Regulations, 2023, and says it interprets Chapter 212. This section defines key terms used in the regulations. Kampuni zinapaswa kumjulisha Msajili taarifa za wamiliki manufaa na, katika hali fulani, kufanya hivyo ndani ya siku 30. Watu walioandikishwa kama wamiliki wa hisa lakini si wamiliki halisi wa manufaa, pamoja na wamiliki manufaa, lazima watoe tamko kwa kampuni ndani ya siku 30; kampuni pia lazima iandike na kuwasilisha taarifa husika kwa Msajili baada ya kupokea tamko. Kampuni lazima iwasilishe taarifa ya mabadiliko ya umiliki manufaa kwa Msajili, kwa Fomu Na. 14f na ndani ya siku 30 baada ya mabadiliko; pia nyaraka za utambulisho wa kila mmiliki manufaa na sahihi husika zinahitajika.
Search within this statute
Search all stored provisions in this version.
Legal text
Provisions of Kanuni za Kampuni (Umiliki Manufaa) za mwaka 2023
Showing 13 of 13
- 1 Verify source ↗
Jina
AI-assisted research summary: This section names the regulation as the Companies (Beneficial Ownership) Regulations, 2023, and says it interprets Chapter 212.
1. Kanuni hizi zinajulikana kama Kanuni za Kampuni (Umiliki Manufaa) za mwaka 2023. Tafsiri Sura ya 212 - 2 Verify source ↗
Tafsiri
AI-assisted research summary: This section defines key terms used in the regulations.
2. Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama muktadha utahitajika vinginevyo- “Sheria” maana yake ni Sheria ya Kampuni; “maslahi ya manufaa” maana yake ni maslahi makubwa ya kiuchumi au faida au uwezo mkubwa wa kufanya maamuzi katika kampuni; “mmiliki manufaa” itakuwa na maana kama ilivyoainishwa kwenye Sheria; “mmiliki manufaa halisi” maana yake ni mtu asilia mwenye kumiliki au anayemiliki maslahi ya manufaa katika kampuni na jina lake kusajiliwa katika rejesta ya wamiliki wa kampuni; “mmiliki manufaa asiye halisi” maana yake ni mtu asilia mwenye kumiliki au atakayemiliki maslahi ya manufaa katika kampuni ambaye hajasajiliwa katika rejesta ya wamiliki wa kampuni; "umiliki wa moja kwa moja" maana yake ni umiliki manufaa halisi; "umiliki usio wa moja kwa moja" maana yake ni umiliki manufaa usio halisi; “mmiliki aliyesajiliwa” maana yake ni mtu yeyote ambaye majina yake yameorodheshwa katika rejesta ya 3 Tangazo la Serikali Na. 494 (Linaendelea.) Kanuni Za Kampuni Za Umiliki Manufaa Taarifa za mmiliki manufaa T.S. Na. 41 la 2005 T.S Na 126 la 2014 wamiliki wa kampuni; “Msajili” maana yake ni Msajili wa Kampuni aliyeteuliwa chini ya kifungu cha 450 cha Sheria. SEHEMU PILI TAARIFA ZA WAMILIKI MANUFAA
Part
SEHEMU PILI
- 3 Verify source ↗
Taarifa za wamiliki manufaa
AI-assisted research summary: Kampuni zinapaswa kumjulisha Msajili taarifa za wamiliki manufaa na, katika hali fulani, kufanya hivyo ndani ya siku 30.
3.-(1) Kampuni iliyoanzishwa chini ya Sheria itawasilisha kwa Msajili taarifa za wamiliki manufaa wake. (2) Kampuni itahakikisha inachukua hatua stahiki za kutambua wamiliki manufaa wake na kuingiza taarifa zao katika rejesta yake ya wamiliki manufaa kama ilivyoelekezwa katika kifungu cha 14(2)(b) cha Sheria. (3) Kampuni yenye mmiliki manufaa halisi itawasilisha kwa Msajili taarifa za mmiliki manufaa kwa kuzingatia utaratibu ulioelekezwa kwenye mfumo wa upokeaji wa taarifa za umiliki manufaa ndani ya siku thelathini kuanzia tarehe ambayo jina lake limeingizwa kwenye rejesta ya wamiliki na wamiliki manufaa. (4) Kampuni yenye mmiliki manufaa asiye halisi itawasilisha kwa Msajili taarifa za mmiliki manufaa huyo kwa kujaza Fomu Na. 14b iliyoainishwa kwenye Kanuni za Fomu za Kampuni ndani ya siku thelathini kuanzia tarehe ambayo jina lake limeingizwa kwenye rejesta ya wamiliki na wamiliki manufaa. (5) Pale ambapo mmiliki manufaa asiye halisi anapokoma kuwa mmiliki manufaa, kampuni itatakiwa, baada ya kulipa ada kama zilivyobainishwa kwenye Kanuni za Ada, kuwasilisha notisi kwa Msajili kuhusu mabadiliko hayo kwa kujaza Fomu Na. 14c iliyoainishwa kwenye Kanuni za Fomu za Kampuni ndani ya siku thelathini kuanzia tarehe ya kukoma kuwa mmiliki manufaa. (6) Kampuni itakayoshindwa kuwasilisha fomu ndani ya muda uliobainishwa itawajibika kulipa ada ya ucheleweshaji kwa Msajili kama ilivyoainishwa kwenye Kanuni za Ada. 4 Tangazo la Serikali Na. 494 (Linaendelea.) Kanuni Za Kampuni Za Umiliki Manufaa Tamko la maslahi ya manufaa. T.S. Na. 41 la mwaka 2005 T.S. Na. 41 la mwaka 2005 T.S Na. 126 la 2014 - 4 Verify source ↗
Tamko la maslahi ya manufaa
AI-assisted research summary: Watu walioandikishwa kama wamiliki wa hisa lakini si wamiliki halisi wa manufaa, pamoja na wamiliki manufaa, lazima watoe tamko kwa kampuni ndani ya siku 30; kampuni pia lazima iandike na kuwasilisha taarifa husika kwa Msajili baada ya kupokea tamko.
4.-(1) Mtu ambaye jina lake limeingizwa katika rejesta ya wamiliki na wamiliki manufaa wa kampuni kama mmiliki wa hisa wa kampuni hiyo lakini si mmiliki halisi wa manufaa, atawasilisha kwenye kampuni tamko kuhusu umiliki halisi wa manufaa kwa kujaza Fomu Na. 14d iliyoainishwa kwenye Kanuni za Fomu za Kampuni ndani ya muda wa siku thelathini kuanzia tarehe ambayo jina lake limeingizwa kwenye rejesta ya wamiliki na wamiliki manufaa: Isipokuwa kwamba, pale ambapo kuna mabadiliko kuhusu maslahi ya manufaa, mmiliki aliyesajiliwa katika rejesta ya wamiliki wa kampuni ambaye si mmiliki halisi wa manufaa, atalazimika ndani ya siku thelathini kuanzia tarehe ya mabadiliko, kutoa tamko kuhusu mabadiliko hayo kwenye kampuni kwa kujaza Fomu Na. 14d iliyoainishwa kwenye Kanuni za Fomu za Kampuni. tamko kampuni (2) Mmiliki manufaa asiye halisi atawasilisha kwenye litakalobainisha maslahi aliyonayo kwa kujaza Fomu Na. 14e iliyoainishwa kwenye Kanuni za Fomu za Kampuni ndani ya muda wa siku thelathini kuanzia tarehe ya kupata maslahi ya manufaa katika kampuni: Isipokuwa kwamba, pale ambapo kuna mabadiliko kuhusu maslahi ya manufaa, mmiliki manufaa atalazimika ndani ya siku thelathini kuanzia tarehe ya mabadiliko, kutoa tamko kuhusu mabadiliko hayo kwenye kampuni kwa kujaza Fomu Na. 14e iliyoainishwa kwenye Kanuni za Fomu za Kampuni. (3) Pale ambapo tamko chini ya kanuni hii limepokelewa na kampuni, kampuni itaingiza taarifa za tamko hilo kwenye rejesta ya wamiliki na wamiliki manufaa wa kampuni, na baada ya kulipa ada kama zilivyobainishwa kwenye Kanuni za Ada zinazolipwa kwa Msajili, itawasilisha kwa Msajili taarifa hizo kwa kujaza Fomu Na. 14b ndani ya muda wa siku thelathini baaada ya kupokea tamko hilo. Mabadiliko ya wamiliki manufaa T.S Na. - 5 Verify source ↗
Mabadiliko ya wamiliki manufaa
AI-assisted research summary: Kampuni lazima iwasilishe taarifa ya mabadiliko ya umiliki manufaa kwa Msajili, kwa Fomu Na. 14f na ndani ya siku 30 baada ya mabadiliko; pia nyaraka za utambulisho wa kila mmiliki manufaa na sahihi husika zinahitajika.
5.-(1) Kampuni itatakiwa, baada ya kulipa ada kama zilivyoanishwa kwenye Kanuni za Ada zinazolipwa taarifa za kwa Msajili, kuwasilisha kwa Msajili 5 Tangazo la Serikali Na. 494 (Linaendelea.) Kanuni Za Kampuni Za Umiliki Manufaa 126 la 2014 T.S Na. 41 la 2005 T.S Na. 41 la 2005 Kutokutoa taarifa za wamiliki manufaa. mabadiliko ya mmiliki manufaa asiye halisi kupitia Fomu Na. 14f iliyoainishwa kwenye Kanuni za Fomu za Kampuni ndani ya siku thelathini kuanzia tarehe ya mabadiliko. (2) Endapo kutatokea hamisho la hisa au ongezeko au punguzo la mtaji wa kampuni au badiliko la muundo wa mtaji wa hisa za kampuni au mabadiliko ya haki za kupiga kura yatakayosababisha mabadiliko ya maslahi ya manufaa, kampuni pamoja na taratibu zilizowekwa kwenye Sheria, itawasilisha kwa Msajili notisi kupitia Fomu Na. 14f iliyoainishwa kwenye Kanuni za Fomu za Kampuni ikionesha mabadiliko ya umiliki manufaa katika kampuni. (3) Msajili hatasajili notisi ya upatikanaji wa hisa inayohusu mabadiliko ya hisa au nyaraka yoyote zilizogawiwa au haki ya kupiga kura hadi pale matakwa ya kanuni ndogo ya (2) yatakapokuwa yametekelezwa. (4) Notisi ya mabadiliko ya umiliki manufaa iliyorejewa katika kanuni hii itasainiwa na angalau mkurugenzi mmoja wa kampuni au katibu wa kampuni na nakala halisi iliyothibitishwa ya nyaraka rasmi ya utambulisho wa kila mmiliki manufaa itawasilishwa kwa Msajili. - 6 Verify source ↗
Zuio la utoaji taarifa za wamiliki manufaa
AI-assisted research summary: Kampuni hairuhusiwi kutumia au kutoa taarifa kuhusu mmiliki manufaa wake, isipokuwa kwa sababu zilizoorodheshwa katika kifungu hiki.
6. Kampuni haitatumia au kutoa taarifa yoyote kuhusu mmiliki manufaa wake isipokuwa kwa ajili ya- (a) mawasiliano na mmiliki manufaa husika; (b) kutekeleza matakwa ya Sheria; (c) kutekeleza amri ya mahakama; (d) kutekeleza maelekezo ya mmiliki manufaa husika; au (e) kutekeleza matakwa ya sheria nyingine yoyote. SEHEMU TATU REJESTA YA WAMILIKI MANUFAA Rejesta ya wamiliki manufaa
Part
SEHEMU TATU
- 7 Verify source ↗
Rejesta ya wamiliki manufaa
AI-assisted research summary: Msajili lazima aingize na atunze taarifa za wamiliki manufaa wa kila kampuni kwenye rejesta ya wamiliki manufaa.
7.-(1) Kwa kuzingatia kifungu cha 451A cha Sheria, taarifa za wamiliki manufaa wa kila kampuni zilizowasilishwa kwa Msajili kwa mujibu wa Kanuni hizi zitaingizwa na kutunzwa na Msajili kwenye rejesta ya wamiliki manufaa. 6 Tangazo la Serikali Na. 494 (Linaendelea.) Kanuni Za Kampuni Za Umiliki Manufaa (2) Taarifa za wamiliki manufaa wa kampuni zitakazotunzwa na Msajili kwenye rejesta ya wamiliki manufaa idhinishwa zilizoainishwa katika kifungu cha 451B cha Sheria baada ya maombi ya maandishi kuwasilishwa kwa Msajili. kwa mamlaka zitatolewa Kukataliwa usajili - 8 Verify source ↗
Kukataliwa usajili
AI-assisted research summary: Msajili anaweza kukataa kusajili nyaraka za kampuni zenye kusajiliwa chini ya Sheria ikiwa taarifa za mmiliki manufaa hazijawasilishwa au ikiwa hashawishiki kwamba kampuni imewasilisha taarifa sahihi na za wakati kuhusu wamiliki manufaa. Akikataa, lazima awajulishe wahusika.
8.-(1) Msajili anaweza kukataa kusajili nyaraka yoyote ya kampuni inayopaswa kusajiliwa chini ya Sheria ikiwa- (a) taarifa za mmiliki manufaa hazikuwasilishwa; au (b) hakuridhika kwamba kampuni imewasilisha taarifa sahihi na za wakati kuhusu wamiliki manufaa wa kampuni. (2) Endapo Msajili atakataa kusajili nyaraka kwa mujibu wa kanuni hii, atapaswa kuwajulisha wahusika ipasavyo kuhusu uamuzi huo. Uwasilishaji wa nyaraka - 9 Verify source ↗
Uwasilishaji wa nyaraka
AI-assisted research summary: Msajili anaweza kuamua namna na utaratibu wa kuwasilisha nyaraka, ikijumuisha kuwasilisha kwa njia ya kielektroniki.
9. Nyaraka yoyote inayopaswa kuwasilishwa kwa Msajili chini ya Kanuni hizi inaweza kuwasilishwa katika muundo na kwa utaratibu utakaojumuisha muundo wa kielektroniki na mawasiliano kwa njia ya kielektroniki kama Msajili atakavyoona inafaa. SEHEMU YA NNE MASHARTI YA JUMLA Makosa na adhabu
Part
SEHEMU YA NNE
- 10 Verify source ↗
Makosa na adhabu
AI-assisted research summary: A person who fails to keep beneficial ownership records, file required changes or declarations with the Registrar, or otherwise breach these Regulations commits an offence and may be fined.
10. Mtu ambaye- (a) atashindwa kutunza kumbukumbu za wamiliki manufaa; (b) atashindwa kuwasilisha kwa Msajili taarifa kuhusu mabadiliko ya umiliki manufaa wa kampuni; (c) atashindwa kuwasilisha kwa Msajili tamko taarifa za wamiliki manufaa wa lenye kampuni; au (d) atakiuka masharti yoyote ya Kanuni hizi, atakuwa ametenda kosa na endapo akitiwa hatiani, atawajibika kulipa faini isiyopungua shilingi milioni tano lakini isiyozidi shilingi milioni kumi. Kutokutoa taarifa za siri - 11 Verify source ↗
Usiri wa taarifa
AI-assisted research summary: Watu walioorodheshwa hawaruhusiwi kufichua au kutoa taarifa za siri zilizopatikana chini ya Kanuni hizi kwa mtu ambaye hajaidhinishwa.
11. Msajili, afisa aliyeidhinishwa, mamlaka au 7 Tangazo la Serikali Na. 494 (Linaendelea.) Kanuni Za Kampuni Za Umiliki Manufaa Nyongeza ya muda vitengo vilivyoainishwa chini ya kifungu cha 451B cha Sheria hawataruhusiwa, hata baada ya ukomo wa ajira zao, kuweka wazi au kutoa taarifa za siri zilizopatikana kwa mujibu wa Kanuni hizi kwa mtu yeyote ambaye hajaidhinishwa. - 12 Verify source ↗
Kuongeza muda
AI-assisted research summary: A company that misses a filing deadline may ask the Registrar for more time, and the Registrar may grant up to 30 days.
12.-(1) Endapo muda wa kuwasilisha taarifa umeainishwa katika Kanuni hizi na endapo kampuni imeshindwa kuwasilisha taarifa hizo ndani ya muda ulioainishwa, kampuni hiyo inaweza kuwasilisha kwa Msajili maombi ya nyongeza ya muda kwa ajili ya kuwasilisha taarifa hizo. (2) Baada ya kujiridhisha na sababu zilizotolewa, Msajili anaweza kuongeza muda wa kuwasilisha nyaraka kwa kipindi kisichozidi siku thelethini. Kufutwa kwa kanuni TS. Na. 391 la 2021 - 13 Verify source ↗
Kufutwa kwa Kanuni
AI-assisted research summary: The 2021 Company (Beneficial Ownership) Regulations are repealed.
13. Kanuni za Kampuni (Umiliki Manufaa) za mwaka 2021 zinafutwa. Dodoma, 23rd June, 2023 ASHATU K. KIJAJI, Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara 8
Provision text is displayed from LexChat’s stored statute record. Use the official source links to verify amendments, commencement, and current legal force.
Ask AI about this statute
Kanuni za Kampuni (Umiliki Manufaa) za mwaka 2023
Sign in to ask AI about this statute
Sign in to start authenticated, citation-grounded statute research.
Sign in